Roho mbaya ya binadamu

Roho mbaya ya binadamu

thebogo055

Member
Joined
Jun 22, 2020
Posts
19
Reaction score
176
Kuna watu tunatofautiana sana kimawazo, fikra, weledi nk.

Wapo binadamu hata umfanyie nini bado hatokuheshimu wala ku appreciate yote uliyomfanyia.. yupo radhi akuue achukue nafasi yako. Sishangai hii ni human nature (ubinafsi) tuna ubinafsi sana ingawa ni ngumu sana kuuonesha lakn deep inside kuna roho ile ya kwanini, sio wote lakini.

Nawapa mfano mmoja kwenye maisha yangu. Binafsi nina roho ya huruma kiasi kwamba kuna baadhi ya ubaya huwa nachukulia poa ukinifanyia. Nina uwezo wa ku- control hasira zangu na maswaiba yanayonipata.. najua hichi ni kipawa pia kwasababu kuna watu hawawezi kuvumilia.

Sasa kwa ufupi ni hivi. nimekutana na mtu mwenye roho mbaya sijawah kuona duniani. dah! Nimebahatika kumsaidia mtu kupata kazi, nikamuamini sana na kumpa nafasi kubwa katika maisha yangu, lakin nimekuja kugundua huyu mtu ni muongo, mnafik, mzandiki, black mailer yaan kila sifa anayo.

Hivi inawezekana vipi nakutuma ufuatilie pesa yangu mahali halafu umeipokea na kwangu huileti. Na bahati mbaya yule mtu alietoa hiyo pesa alipoteza simu so akawa hapatikani. Sasa kila nikimuuliza yule mtu vipi umepewa ile pesa anasema hamuoni na hawajaonana kumbe kashapokea na kula.

Sasa leo natoka safarini kwenye misele yangu ghafla nakutana na yule ambae alikuwa na pesa yangu... tukapeana hi.. then nikakumbushia deni!

Cha ajabu jamaa anasema hela alimpa yule mtu niliemtuma zaidi ya week mbili sasa, ikabidi nipge simu niweke loud speaker, yule mpumbavu akakana hajapokea. Sasa ili kujua nani muongo nikamchukua yule mtu nikaenda kwa jamaa.

Dah ni aibu tupu..kumbe hela kapewa na katumia yote na bado anafanya kazi kwenye sehem ambayo mimi ndio nilimuweka kwa sababu ya kumuonea huruma.

Na mbaya zaidi nimepata taarifa anatangaza ile sehemu ya kazi ni yake. Jamani kuna binadamu wanafanya tusisaidiane.

Nimeamua nimtupe kila mtu ashinde mechi zake. Leo kaja Home kamkuta wife anamwambia ana maongezi naye. Ila kwa kuwa nilimpa maagizo wife kwamba akija amfukuze ikabidi jamaa asepe tu.

Sasa nasikia ananitafuta huko anataka suluhisho.
 
Mkuu, hilo ni jambo la kawaida sana, kuitafuna hiyo pesa haimaanishi ana roho mbaya dhidi yako. Kitendo hicho inawezekan kimesababishwa na uhitaji wa pesa kwa muda huo atakua alitumia akijua atafidia lakini mambo yakawa magumu.

Tafadhali Msamehe mpe nafsi nyingine.
 
Ulikuwa hujui hilo? Mwamini mtu nusu ile iliyobaki ongezea kwako
 
Mkuu, hilo ni jambo la kawaida sana, kuitafuna hiyo pesa haimaanishi ana roho mbaya dhidi yako. Kitendo hicho inawezekan kimesababishwa na uhitaji wa pesa kwa muda huo atakua alitumia akijua atafidia lkn mambo yakawa magumu.
Tafadhali Msamehe mpe nafsi nyingine.
Kwani aliye mwagiza amchukulie yeye hakuwa na shida nayo? Tabia sio kabisa wala si uungwana
 
Kwani mwagiza amchukulie yeye hakuwa na shida nayo? Tabia sio kabisa wala si uungwana
Kwan wewe hujawahi daiwa pesa na mtu!? Ukaipata lakini usiipeleke badala yake ukatatulia matatizo yako kwanza!?
 
Mkuu, hilo ni jambo la kawaida sana, kuitafuna hiyo pesa haimaanishi ana roho mbaya dhidi yako. Kitendo hicho inawezekan kimesababishwa na uhitaji wa pesa kwa muda huo atakua alitumia akijua atafidia lakini mambo yakawa magumu.

Tafadhali Msamehe mpe nafsi nyingine.
I'm really afraid of hela za watu, Ni mlango was ufukara na mikosi
 
Binadamu ni jeur sana cha muhimu kila mtu apambane na hali yake.....
 
Mi pia napenda niwe mwaminifu lkn shida saa nyingine zonanifanya nisiwe mwaminifu.
Ni uamuzi wako tu, ukipewa sasa kazi ya kijumbe si utaushia segerea ?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kitu cha hapana kukifikisha kama kilivyo mkuu ni ujasiri sana.

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom