Rocket

Rocket

Ziroseventytwo

Platinum Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
9,154
Reaction score
17,028
Eti ile ndege inayopita juu sana na kuacha moshi wa mchirizi inaitwaje? Kuna watu wanasema inaitwa rocket! Ni kweli? Je kwa hapa Africa inatua wapi, nchi gani? Mwenye ufahamu anijuze tafadhali.
 
Eti ile ndege inayopita juu sana na kuacha moshi wa mchirizi inaitwaje? Kuna watu wanasema inaitwa robket! Ni kweli? Je kwa hapa Africa inatua wapi, nchi gani? Mwenye ufahamu anijuze tafadhali.
Ndege_Chombo cha Usafiri.
Robket_Rocket
Umeandika kuwa ni ndege tayari.
 
Rocket ni aircraft lakini sio aeroplane. Aircraft ni chombo chochote chenye uwezo wa kutembea hewani...hata kishada ni aircraft, kwa maana hiyo hata vigagura wetu wa Bongo wanapaa hewani kwa aircraft.

Ule moshi muuonao juu baada ya chombo kupita si moshi wa roketi...zamani wengi tulikuwa tunadanganywa kwamba ni roketi, lakini ilikuwa ni maneno mbofumbofu!!!

Kwa ufupi ule moshi ni moshi wa ndege kubwa za jet za kawaida kama unazoziona JNIA, lakini wakati huo zinakuwa kwenye anga zajuu sana baada ya kufikia mahala pa cruising level(yaani baada ya kitendo cha kuendelea kupanda kufikia mwisho wake.).

Actually kile unachokiona si moshi wa ndege bali ni mgongano 'bombarding' ya hewa hususan baada ya kupashwa joto na gases zinazotoka kwenye eksozi ya ndege inayopita eneo hilo muda huo.

Ndege ile ikipita inaacha low pressure kwenye eneo, kitendo kinachosababisha hewa kutoka sehemu zingine kujaza eneo lilenkwa mgandamizo mkubwa, na hivyo tuonacho sisi ni tabaka la hewa hiyo.

Eksozi ya ndege haiwezi kutoa moshi mwingi vile maana moshi ni dalili ya ubovu katika injini, hivyo ndege hiyo itaanguka baada ya dakika 2 tu baada ya kupaa.
 
Roketi mkuu ni habari ingine kabisa.
Yenyewe inatumika kufanya safari za kisayansi za anga za juu kabisa, ikiwa ni pamoja na kwenda kwrnye mwezi pamoja na kwenye sayari zinginezo.

Tofauti kubwa kabisabya roketi na ndege zingine pia ipo kwenye uondokaji wake inapokwenda kwenye mission. yenyewe huwa inaondoka kama risasi kuelekea 90° kutoka usawa wa ardhi wakati ndege za kawaida zinatumia runway.

Angalia video za take-off ya roketi uone jinsi ilivyo msala mkuu... ni kwamba ngoma inachochewa moto mkali sana ili baadhi ya sehemu zake zilipuke na kuipa lift...na inaendelea kupanda juu kwa kuendelea kuungua na kupungua size yake.

Kwa ufupi ni hivo...roketi huwa zinaenda kwenye 'missions' fulani za kisayansi na kiuchunguzi zilizoandaliwa kwa miaka mingi na si kupeleka abiria, mfano tu ni kupeleka satelite huko hewani ambazo zinatumika kwa mawasiliano huku duniani.
Pia ni nchi kama mbili au tatu tu za dunia hii zilizofanikiwa kurusha roketi kwenda huko angani na si kila nchi, kama ilivyo kwa ndege.
 
Roketi mkuu ni habari ingine kabisa.
Yenyewe inatumika kufanya safari za kisayansi za anga za juu kabisa, ikiwa ni pamoja na kwenda kwrnye mwezi pamoja na kwenye sayari zinginezo.

Tofauti kubwa kabisabya roketi na ndege zingine pia ipo kwenye uondokaji wake inapokwenda kwenye mission. yenyewe huwa inaondoka kama risasi kuelekea 90° kutoka usawa wa ardhi wakati ndege za kawaida zinatumia runway.

Angalia video za take-off ya roketi uone jinsi ilivyo msala mkuu... ni kwamba ngoma inachochewa moto mkali sana ili baadhi ya sehemu zake zilipuke na kuipa lift...na inaendelea kupanda juu kwa kuendelea kuungua na kupungua size yake.

Kwa ufupi ni hivo...roketi huwa zinaenda kwenye 'missions' fulani za kisayansi na kiuchunguzi zilizoandaliwa kwa miaka mingi na si kupeleka abiria, mfano tu ni kupeleka satelite huko hewani ambazo zinatumika kwa mawasiliano huku duniani.
Pia ni nchi kama mbili au tatu tu za dunia hii zilizofanikiwa kurusha roketi kwenda huko angani na si kila nchi, kama ilivyo kwa ndege.

mkuu shukrani kwa maelezo mazuri. Swali lipo pale pale kile tunachokiona(aircraft) kikiruka umbali mrefu bila kusikia muungurumo wake na kinaacha hicho kinachoonekana kama moshi ni nini? Leo nimekiona. Kilienda then kikarudi. Kinaruka/rushwa toka wapi? Na kinaelekea wapi.

Usichoke mkuu jf ni darasa.
 
1. Ule mchirizi sio moshi bali ni artificial clouds (Mawingu yasio halisi) ambapo hutokana na Mvuke unaotoka kwenye exhaust unaganda unapokutana na baridi kali ya huko angani. In chemistry exothermic reaction ina-Generate Joto ambalo husababisha moja husababisha products(CO2 + H2O) za hiyo engine combustion kutoka zikiwa na joto sana, kiasi kwamba H2O hutoka kama mvuke (Vapour) na inapotoka katika engine Ghafla inagandishwa na atmosperic temperature. Hapo ndipo unaona mstari mweupe na baadae unapotea,.

Hali hii hutokea kawaida unapowasha Gari lako asubuhi, utaona maji maji yanatoka katika exhaust, lakini hutaona mawingu kwa sababu hali ya hewa katika sea level ni joto kulinganisha na huko angani.

Eti ile ndege inayopita juu sana na kuacha moshi wa mchirizi inaitwaje? Kuna watu wanasema inaitwa rocket! Ni kweli? Je kwa hapa Africa inatua wapi, nchi gani? Mwenye ufahamu anijuze tafadhali.
 
1. Ule mchirizi sio moshi bali ni artificial clouds (Mawingu yasio halisi) ambapo hutokana na Mvuke unaotoka kwenye exhaust unaganda unapokutana na baridi kali ya huko angani. In chemistry exothermic reaction ina-Generate Joto ambalo husababisha moja husababisha products(CO2 + H2O) za hiyo engine combustion kutoka zikiwa na joto sana, kiasi kwamba H2O hutoka kama mvuke (Vapour) na inapotoka katika engine Ghafla inagandishwa na atmosperic temperature. Hapo ndipo unaona mstari mweupe na baadae unapotea,.

Hali hii hutokea kawaida unapowasha Gari lako asubuhi, utaona maji maji yanatoka katika exhaust, lakini hutaona mawingu kwa sababu hali ya hewa katika sea level ni joto kulinganisha na huko angani.

ahsante! Umezungumzia matokeo. So hicho chombo kinachoruka kinaitwaje? Rocket? Ndege? Au ni nini? Kinaruka au kinarushwa kutokea wapi?

Twende kazi
 
Soyuz_rocket_ASTP.jpg

Hiyo ndio rocket sio ndege kama ilivyoelezwa na PakaJimmy na ymollel hapo ipo kwenye mtambo wa kurushia tayari kwa kurushwa kueleleke anga za juu
 
Last edited by a moderator:
MKUU Zeroseventytwo
Katika post yangu ya kwanza nimeshaeleza jibu la swali lako, labda uko overanxious kujua kinachoendekea.

Nimekwambia kwamba kile kinachotoa ule moshi ni ndege za kawaida kabisa za jet kama unazoziona zimeegesha pale JNIA na wala si kitu ingine. Ni Boeing, Airbus, CRJ, etc, Tena huwa zimepiga abiria full on board.

Unless kama swali lako lina maana nyingine...laakini hilo ndio jibu.
Kama sivyo uliza tena.
 
Last edited by a moderator:
Asante mkuu Suip kwa kuweka kielelezo.

kwa kumuongezea majibu mdau ni kwamba gharama ya kuandaa huo mtambo peke yake bila hata ya rocket ni bajeti za nchi yako kadha, ndiyo maana si nchi zote zinaweza.
Africa hii wala Europe hakuna nchi inayorusha roketi. Ni Waamerika na Warusi, huenda na Korea.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu paka jimmy, Suip, na ymollel nimewapata vizuri kabisa. Ahsanteni kwa majibu mazuri. Tupo pamoja. Kwa kuongeza swali dogo la nyongeza. Vp mbona hatusikii muungurumo wa hiyo ndege? Inaruka umbali kiasi masikio yetu yanashindwa kusense huo muungurumo.?
 
Last edited by a moderator:
Ni hivi. Umbali huo Ambao ndege hizi zinakuwa huwezi kusikia mngurumo hata kidogo. Ni mbali sana Kwa kweli.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Bwana Ziroseventytwo
Hizo ndege cruising level yake iko kwenye umbali wa futi 45,000 na zingine eg. ile ndege maarufu ya Concorde zilienda hadi futi 60,000 juu sawa na wastani wa km 20 kwenda juu...

Sasa imagine kama inawezekana kusikia ndegr kwenye umbali huo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom