1979Magufuli
JF-Expert Member
- Feb 20, 2023
- 439
- 1,756
Kuna vijana ambao wameamua kujifanya kumsemea Robertinho kuwa hata Simba isipocheza mpira mzuri lakn inashinda, wengine wanasema hajafungwa hata mechi moja, wengine wanamuita kuwa kiboko ya Yanga, wengine wanasema ametimiza malengo aliyopewa, wengine wanamsifia timu haishindi lakini inaongoza ligi, kusifu sifu kwiiiiiingi.
Wengi wanaomsifu kila nikiwaangalia kwenye YouTube au mitandao ya kijamii sura zao zinaonyesha kuwa wameanza kuipenda Simba hivi karibuni, Hao ni wale ambao wakati Simba inafuzu kwenye makundi kwa kuitoa Zamalek walikuwa na umri wa miaka 5 hadi 10, wengine walikuwa wanasoma, umri wao ni kama Ahmed Ally au Ally Kamwe au Pivadinho.Sijui kama waliwahi kumuona Christopher Alex na ndio walikuwa wanambishia Gentamycine kuwa Alex hakuwahi kucheza beki wakati ukweli ni ukweli Alex aliwahi kucheza beki na marehemu James Siang'a alipenda sana kumchezesha beki wakati fulani.
Simba hatujaanza kuiona leo wengine tangu shamba la bibi enzi za akina marehemu Mansoor Magram, Salum Madadi, marehemu Syllasaid Mziray Abdallah Kibadeni, Patrick Phiri, Dragan Popadic, Kopunovic huyu wa Tabora United marehemu James Siang'a nk.
Siang'a na Phiri kwa nyakati tofauti kama mngeweza kuwaona kipindi kile wakati wanafundisha Simba na mkaiangalia Simba hii ya wazungu sijui Gomes, sjui Pablo, sijui Aussems sijui Sven mtakubaliana na mm kuwa Robertinho ni msanii tu, anapewa sifa za kijinga kabisa.
Marehemu Siang'a alimbadilisha kabisa marehemu Christopher Alex, maana Alex alikuwa akichukiwa sana na mashabiki kama ilivyokuwa awali kwa Kibu Dennis, badaae Alex akakaa sawa sawia na kila mtu akamkubali na rasta zake na hasa pale alipowatungua waarabu kwa penati ya mwisho kule kwao, Siang'a alimbadilisha kabisa Joseph Kaniki Golota akawa tishio hasa na guu lake la mavi, emmanuel Gabriel akawa hashikiki kule mbele, Wilycliff Ketto akitawala dimba la kati na Shekhan Rashid huku chini akiwa seleman matola.
Simba ilikuwa Simba hasa, ukija hovyo unakula mkono kweli, sio hii mikono ya utopolo ya kuongea biashara na Kevin yondani, ukweli ni kuwa tunaipenda Simba na tunakwenda kushangilia lakini ule mpira wetu haupo, wamebaki wajinga wajinga wa kusifia.
Viungo wetu sio flexible, je viungo wetu wanacheza kama alivyokuwa akicheza marehemu Idd Seleman kibode, wanacheza kama alivyo Seleman Matola au wakati fulani Jerry Santo au Christopher Alex, mbona timu inafanya sana makosa, Simba ilikuwa ngumu kuifunga bao, sasa akina Kanoute kwanza hajiamini kabisa raia huyu wa mali, hivi Feisal salum alivyokuwa akicheza namba 6 ndio hivi anavyocheza kanoute.
Hapana, hapana, watu wanapotoa maoni yaheshimiwe, I have the right to freedom of expression, mtu anapotoa maoni asitukanwe, ajibiwe kwa hoja. MIMI nimeweka fact in issue mezani na wengine waweke ili kusifia sio matusi na nn, burudani hatuipati na Ahly wamebadilika sana, tusije kutia aibu, we hadi Leo kocha hajui kama Baleke, Bocco na Phiri nani aanze, hao wote umeshawapa nafasi tumewaona hebu mpe basi Chilunda naye uone vurugu zake, we unamtegemea Bocco ndio awasumbue Al Ahly.Mh.
Wengi wanaomsifu kila nikiwaangalia kwenye YouTube au mitandao ya kijamii sura zao zinaonyesha kuwa wameanza kuipenda Simba hivi karibuni, Hao ni wale ambao wakati Simba inafuzu kwenye makundi kwa kuitoa Zamalek walikuwa na umri wa miaka 5 hadi 10, wengine walikuwa wanasoma, umri wao ni kama Ahmed Ally au Ally Kamwe au Pivadinho.Sijui kama waliwahi kumuona Christopher Alex na ndio walikuwa wanambishia Gentamycine kuwa Alex hakuwahi kucheza beki wakati ukweli ni ukweli Alex aliwahi kucheza beki na marehemu James Siang'a alipenda sana kumchezesha beki wakati fulani.
Simba hatujaanza kuiona leo wengine tangu shamba la bibi enzi za akina marehemu Mansoor Magram, Salum Madadi, marehemu Syllasaid Mziray Abdallah Kibadeni, Patrick Phiri, Dragan Popadic, Kopunovic huyu wa Tabora United marehemu James Siang'a nk.
Siang'a na Phiri kwa nyakati tofauti kama mngeweza kuwaona kipindi kile wakati wanafundisha Simba na mkaiangalia Simba hii ya wazungu sijui Gomes, sjui Pablo, sijui Aussems sijui Sven mtakubaliana na mm kuwa Robertinho ni msanii tu, anapewa sifa za kijinga kabisa.
Marehemu Siang'a alimbadilisha kabisa marehemu Christopher Alex, maana Alex alikuwa akichukiwa sana na mashabiki kama ilivyokuwa awali kwa Kibu Dennis, badaae Alex akakaa sawa sawia na kila mtu akamkubali na rasta zake na hasa pale alipowatungua waarabu kwa penati ya mwisho kule kwao, Siang'a alimbadilisha kabisa Joseph Kaniki Golota akawa tishio hasa na guu lake la mavi, emmanuel Gabriel akawa hashikiki kule mbele, Wilycliff Ketto akitawala dimba la kati na Shekhan Rashid huku chini akiwa seleman matola.
Simba ilikuwa Simba hasa, ukija hovyo unakula mkono kweli, sio hii mikono ya utopolo ya kuongea biashara na Kevin yondani, ukweli ni kuwa tunaipenda Simba na tunakwenda kushangilia lakini ule mpira wetu haupo, wamebaki wajinga wajinga wa kusifia.
Viungo wetu sio flexible, je viungo wetu wanacheza kama alivyokuwa akicheza marehemu Idd Seleman kibode, wanacheza kama alivyo Seleman Matola au wakati fulani Jerry Santo au Christopher Alex, mbona timu inafanya sana makosa, Simba ilikuwa ngumu kuifunga bao, sasa akina Kanoute kwanza hajiamini kabisa raia huyu wa mali, hivi Feisal salum alivyokuwa akicheza namba 6 ndio hivi anavyocheza kanoute.
Hapana, hapana, watu wanapotoa maoni yaheshimiwe, I have the right to freedom of expression, mtu anapotoa maoni asitukanwe, ajibiwe kwa hoja. MIMI nimeweka fact in issue mezani na wengine waweke ili kusifia sio matusi na nn, burudani hatuipati na Ahly wamebadilika sana, tusije kutia aibu, we hadi Leo kocha hajui kama Baleke, Bocco na Phiri nani aanze, hao wote umeshawapa nafasi tumewaona hebu mpe basi Chilunda naye uone vurugu zake, we unamtegemea Bocco ndio awasumbue Al Ahly.Mh.