Six Man
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 253
- 893
- Thread starter
- #21
MAANDISHI YA HALFANI SUDY
RED BUTTERFLY (10)
Mawasiliano 0652 212391
Yule mwanamke akamnyanyua kwa nguvu Christopher kwa kutumia mkono wa kulia, sasa walikuwa wamesimama sambamba. Meneja Christopher mbele, yule Mwanamke wa mwenye kasi ya ajabu na shabsha ambaye walikuwa wanamtambua kwa jina la Red butterfly alikuwa nyuma.
"Niseme tena tu uhai wa huyu fala ninao mimi. Hata mkinipiga risasi roho yangu haitoenda motoni kabla sijaichakaza vibaya san shingo ya huyu mjinga. Sasa ombi ni moja tu kwenu, wekeni silaha chini na mnipishe hapo mlangoni. La sivyo nitakufa lakini nitakuwa nimeuwa..." Yule mwanamke alisema kwa kujiamini na woga wote uliomvaa awali ulikuwa umemtoka. Alijua ile ni karata yake pekee ambayo ilimpasa kuitumia vizuri kujiokoa. Maneno aliyoyasema yaliingia vizuri kwa wale askari. Na walijua kwamba mwanamke alikuwa anasema kweli. Alikuwa na uwezo wa kuuwa kabla hajafa. Na dhamira yao kama askari ilikuwa kumlinda meneja Christopher na sio kusababisha kifo chake. Ilikuwa dhima kuu ya askari, kulinda raia.
"Nakuuwaaa mwanaume.." Yule mwanamke alisema kwa sauti ndogo sikioni mwa meneja Christopher.
"Jamani naombeni mnisaidie ataniua huyu..." Meneja Christopher alikuwa anasema huku analia. Aliruhusu mkojo kumtoka mtoto wa kiume.
"We komaa! Sio wakusaidie, wapishe mlangoni tuondoke zetu.." Yule mwanamke alisema kwa ukali.
"Adrian. Nahesabu hadi tatu. Kama hamthamini uhai wa huyu raia mwema kwa sababu ya kunikamata mimi basi sawa" Yule mwanamke aliacha hiyo sentensi iingie kwa wale askari kisha akaanza kuhesabu.
"Moja, Mbi..." Hakumaliza mbili. Askari wote sita wakiongozwa na Adrian waliweka silaha chini. Hawakutaka kuwa sababu ya kifo cha yule raia mwema. Kwa maana yule mwanamke alikuwa anamaanisha, sura na sauti yake zilikuwa shahidi.
"Natoka nje na huyu mwanamme. Silaha yangu itahitaji mguso mdogo sana kuitoa risasi katika chemba na kuitoa roho ya huyu mjinga. Ninachomaanisha sitaki yeyote yule alete ujanja ( akatukana tusi kubwa la nguoni). Kwanza nyote sogeeni kuleee" Yule mwanamke alisema huku akiionesha kona moja pembeni ya ile ofisi. Na wale askari walitii. Yule mwanamke alikuwa ameushika usukani sasa kwa kujiamini.
Yule mwanamke akaanza kumkokota meneja Christopher kwa tahadhari kubwa sana. Mkongojo sasa ukielekezwa kwa zamu kwa wale askari. Akapita naye mlangoni kwa kasi na kutoka nje. Akauvuta ule mlango wa ofisi na kuufunga kwa nje. Akamsukuma yule meneja mlangoni na kukimbilia kwenye pikipiki yake nyuma ya ile ofisi. Aliwasha na kutokomea kwa kasi akiwaacha wakina Adrian wamezubaa ofisini. Ni meneja Christopher ndiye aliyewafungulia mlango dakika tatu baadae baada ya kujitambua. Red butterfly alikuwa ametokomea...
***SURA YA NNE***
Baada ya nusu saa Adrian Kaanan alikuwa pembeni ya kitanda cha Daniel Mwaseba katika hospitali ya Kairuki. Alikuwa amemwelezea kila kitu kilichotokea kule katika kiwanda cha nguo cha Urafiki. Daniel alimwelewa Adrian lakini alikuwa hajamwelewa kabisa.
"Kwanini unahisi huyo mwanamke ni Red butterfly, wakati Red butterfly tunaamini ni mzee au hujivika umbo la kizee. Sasa huyo aliyewafungia nyie katika ofisi ya meneja wa kiwanda cha nguo cha Urafiki mnasema alikuwa ni msichana mrembo?" Daniel Mwaseba alimuuliza Adrian.
" Mimi naamini yule mwanamke ndiye Red butterfly. Wepesi na kasi ulionielezea ni ileile nilioushuhudia kwa macho yangu. Hata Idd amethibitisha yule ni Red butterfly. Alikuwa anajivika tu umbo la bibi kizee, lakini kwa meneja alikwenda kwa umbo lake halisi" Adrian alisema.
"Nimekuelewa Adrian, unafikiri kwanini Red butterfly kama inavyotupasa kuamini kuwa ni huyohuyo alienda katika kiwanda cha nguo cha Urafiki?" Daniel aliuliza.
"Kwa mujibu wa Meneja Christopher, Red butterfly alienda kuulizia kilekile nilichoenda kuulizia mimi. Na kwabahati nzuri ni mimi ndiye niliyefanikiwa kukipata. Sasa ninaamini katika safu hii ya uongozi kuna kitu ambacho Red butterfly alikuwa anakihitaji" Adrian alisema huku akitoa karatasi tano alizopewa na meneja Christopher na kumkabidhi Daniel.
"Uko vizuri sana Adrian. Kwakuwa waliouwawa wote walikuwa viongozi wa kiwanda cha Urafiki miaka hiyo bila shaka kwa kupitia kuangalia viongozi wa kipindi hiko tutapata jibu" Daniel Mwaseba alisema huku akiziangalia zile karatasi kwa umakini.
"Ona, ona Adrian, waliouwawa wote nane walikuwa viongozi wa mwaka 1955 hadi 1957" Daniel alisema kwa wahka mkubwa.
"Nimeliona hilo kaka Daniel ingawa wewe umechukua muda mfupi sana kugundua. Mwaka 1955 mpaka 1957 kiwanda cha Urafiki kilikuwa na viongozi kumi na tano katika kamati yake ya utendaji. Na nane kati ya hao wameuwawa kwa mkongojo wa Red butterfly. Kwa maana walibaki hai viongozi saba tu wa kipindi hiko. Lakini viongozi watano kati ya hao wameuwawa kwa magonjwa mbalimbali kabla ya tukio hili. So walio hai mpaka sasa ni viongozi watatu tu" Adrian alisema kwa kirefu.
"....ambao unapaswa kuwafatilia ili kujua kwanini viongozi wenzao wa kipindi hiko wanasakwa na Red butterfly" Daniel Mwaseba alidakia.
"Ndio kazi iliyopo mbele yangu baada ya kutoka hapa" Adrian alisema.
"Ila kuwa makini sana Adrian. Kwasasa Red butterfly anajua kwamba umemuwahi pale katika kiwanda cha Urafiki kwa kuchukua hizi nyaraka. Sasa atakusaka kwa kujua wewe ni mtu hatari kwake. Hakikisha kila unapoenda wakina Idd wapo nyuma yako wanakulinda, peaneni taarifa mara kwa mara. Unaenda hatua ya mwisho katika kufumbua fumbo la Red butterfly, kuwa makini sana katika hatua hii. Shirikiana na wenzako. Ushirikiano ni kila kitu katika misheni hatari kama hizi" Daniel Mwaseba alisema.
Waliendelea kuongea kama nusu saa kisha wakaagana. Waliongea pia kuhusu kupotea kwa Elizabeth Neville. Adrian alimwambia kuwa bado watu wa China wakiongozwa na Maxi Lee wanaendelea na uchunguzi wao. Mwishowe Adrian aliondoka akiwa na imani kubwa ya kwenda kufumbua fumbo la Red butterfly huku Daniel akiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kwanini Red butterfly anafanya mauaji kwa viongozi wa kiwanda cha urafiki tu wa mwaka 1955 hadi 1957? na swali la wapi alipo mke wake Elizabeth Neville pia liliendelea kuganda katika kichwa cha Daniel Mwaseba...
Nini kitaendelea...kesho nayo ni siku...
RED BUTTERFLY (10)
Mawasiliano 0652 212391
Yule mwanamke akamnyanyua kwa nguvu Christopher kwa kutumia mkono wa kulia, sasa walikuwa wamesimama sambamba. Meneja Christopher mbele, yule Mwanamke wa mwenye kasi ya ajabu na shabsha ambaye walikuwa wanamtambua kwa jina la Red butterfly alikuwa nyuma.
"Niseme tena tu uhai wa huyu fala ninao mimi. Hata mkinipiga risasi roho yangu haitoenda motoni kabla sijaichakaza vibaya san shingo ya huyu mjinga. Sasa ombi ni moja tu kwenu, wekeni silaha chini na mnipishe hapo mlangoni. La sivyo nitakufa lakini nitakuwa nimeuwa..." Yule mwanamke alisema kwa kujiamini na woga wote uliomvaa awali ulikuwa umemtoka. Alijua ile ni karata yake pekee ambayo ilimpasa kuitumia vizuri kujiokoa. Maneno aliyoyasema yaliingia vizuri kwa wale askari. Na walijua kwamba mwanamke alikuwa anasema kweli. Alikuwa na uwezo wa kuuwa kabla hajafa. Na dhamira yao kama askari ilikuwa kumlinda meneja Christopher na sio kusababisha kifo chake. Ilikuwa dhima kuu ya askari, kulinda raia.
"Nakuuwaaa mwanaume.." Yule mwanamke alisema kwa sauti ndogo sikioni mwa meneja Christopher.
"Jamani naombeni mnisaidie ataniua huyu..." Meneja Christopher alikuwa anasema huku analia. Aliruhusu mkojo kumtoka mtoto wa kiume.
"We komaa! Sio wakusaidie, wapishe mlangoni tuondoke zetu.." Yule mwanamke alisema kwa ukali.
"Adrian. Nahesabu hadi tatu. Kama hamthamini uhai wa huyu raia mwema kwa sababu ya kunikamata mimi basi sawa" Yule mwanamke aliacha hiyo sentensi iingie kwa wale askari kisha akaanza kuhesabu.
"Moja, Mbi..." Hakumaliza mbili. Askari wote sita wakiongozwa na Adrian waliweka silaha chini. Hawakutaka kuwa sababu ya kifo cha yule raia mwema. Kwa maana yule mwanamke alikuwa anamaanisha, sura na sauti yake zilikuwa shahidi.
"Natoka nje na huyu mwanamme. Silaha yangu itahitaji mguso mdogo sana kuitoa risasi katika chemba na kuitoa roho ya huyu mjinga. Ninachomaanisha sitaki yeyote yule alete ujanja ( akatukana tusi kubwa la nguoni). Kwanza nyote sogeeni kuleee" Yule mwanamke alisema huku akiionesha kona moja pembeni ya ile ofisi. Na wale askari walitii. Yule mwanamke alikuwa ameushika usukani sasa kwa kujiamini.
Yule mwanamke akaanza kumkokota meneja Christopher kwa tahadhari kubwa sana. Mkongojo sasa ukielekezwa kwa zamu kwa wale askari. Akapita naye mlangoni kwa kasi na kutoka nje. Akauvuta ule mlango wa ofisi na kuufunga kwa nje. Akamsukuma yule meneja mlangoni na kukimbilia kwenye pikipiki yake nyuma ya ile ofisi. Aliwasha na kutokomea kwa kasi akiwaacha wakina Adrian wamezubaa ofisini. Ni meneja Christopher ndiye aliyewafungulia mlango dakika tatu baadae baada ya kujitambua. Red butterfly alikuwa ametokomea...
***SURA YA NNE***
Baada ya nusu saa Adrian Kaanan alikuwa pembeni ya kitanda cha Daniel Mwaseba katika hospitali ya Kairuki. Alikuwa amemwelezea kila kitu kilichotokea kule katika kiwanda cha nguo cha Urafiki. Daniel alimwelewa Adrian lakini alikuwa hajamwelewa kabisa.
"Kwanini unahisi huyo mwanamke ni Red butterfly, wakati Red butterfly tunaamini ni mzee au hujivika umbo la kizee. Sasa huyo aliyewafungia nyie katika ofisi ya meneja wa kiwanda cha nguo cha Urafiki mnasema alikuwa ni msichana mrembo?" Daniel Mwaseba alimuuliza Adrian.
" Mimi naamini yule mwanamke ndiye Red butterfly. Wepesi na kasi ulionielezea ni ileile nilioushuhudia kwa macho yangu. Hata Idd amethibitisha yule ni Red butterfly. Alikuwa anajivika tu umbo la bibi kizee, lakini kwa meneja alikwenda kwa umbo lake halisi" Adrian alisema.
"Nimekuelewa Adrian, unafikiri kwanini Red butterfly kama inavyotupasa kuamini kuwa ni huyohuyo alienda katika kiwanda cha nguo cha Urafiki?" Daniel aliuliza.
"Kwa mujibu wa Meneja Christopher, Red butterfly alienda kuulizia kilekile nilichoenda kuulizia mimi. Na kwabahati nzuri ni mimi ndiye niliyefanikiwa kukipata. Sasa ninaamini katika safu hii ya uongozi kuna kitu ambacho Red butterfly alikuwa anakihitaji" Adrian alisema huku akitoa karatasi tano alizopewa na meneja Christopher na kumkabidhi Daniel.
"Uko vizuri sana Adrian. Kwakuwa waliouwawa wote walikuwa viongozi wa kiwanda cha Urafiki miaka hiyo bila shaka kwa kupitia kuangalia viongozi wa kipindi hiko tutapata jibu" Daniel Mwaseba alisema huku akiziangalia zile karatasi kwa umakini.
"Ona, ona Adrian, waliouwawa wote nane walikuwa viongozi wa mwaka 1955 hadi 1957" Daniel alisema kwa wahka mkubwa.
"Nimeliona hilo kaka Daniel ingawa wewe umechukua muda mfupi sana kugundua. Mwaka 1955 mpaka 1957 kiwanda cha Urafiki kilikuwa na viongozi kumi na tano katika kamati yake ya utendaji. Na nane kati ya hao wameuwawa kwa mkongojo wa Red butterfly. Kwa maana walibaki hai viongozi saba tu wa kipindi hiko. Lakini viongozi watano kati ya hao wameuwawa kwa magonjwa mbalimbali kabla ya tukio hili. So walio hai mpaka sasa ni viongozi watatu tu" Adrian alisema kwa kirefu.
"....ambao unapaswa kuwafatilia ili kujua kwanini viongozi wenzao wa kipindi hiko wanasakwa na Red butterfly" Daniel Mwaseba alidakia.
"Ndio kazi iliyopo mbele yangu baada ya kutoka hapa" Adrian alisema.
"Ila kuwa makini sana Adrian. Kwasasa Red butterfly anajua kwamba umemuwahi pale katika kiwanda cha Urafiki kwa kuchukua hizi nyaraka. Sasa atakusaka kwa kujua wewe ni mtu hatari kwake. Hakikisha kila unapoenda wakina Idd wapo nyuma yako wanakulinda, peaneni taarifa mara kwa mara. Unaenda hatua ya mwisho katika kufumbua fumbo la Red butterfly, kuwa makini sana katika hatua hii. Shirikiana na wenzako. Ushirikiano ni kila kitu katika misheni hatari kama hizi" Daniel Mwaseba alisema.
Waliendelea kuongea kama nusu saa kisha wakaagana. Waliongea pia kuhusu kupotea kwa Elizabeth Neville. Adrian alimwambia kuwa bado watu wa China wakiongozwa na Maxi Lee wanaendelea na uchunguzi wao. Mwishowe Adrian aliondoka akiwa na imani kubwa ya kwenda kufumbua fumbo la Red butterfly huku Daniel akiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kwanini Red butterfly anafanya mauaji kwa viongozi wa kiwanda cha urafiki tu wa mwaka 1955 hadi 1957? na swali la wapi alipo mke wake Elizabeth Neville pia liliendelea kuganda katika kichwa cha Daniel Mwaseba...
Nini kitaendelea...kesho nayo ni siku...

