FANANI MTENZI
Senior Member
- Jul 4, 2017
- 106
- 95
- Thread starter
- #41
UPEPO WA USIKU-15
BONIFACE BIRAGE
Ilikuwa damu ya nini?Mama mkwe bado hakujua.Kuona damu katika mazingira kama yale yalimpa mawazo mengi.Kimuhemuhe kilichomgusa moyo kikamfanya aufungue mlango wa chumbani akaingia.Alianza kukagua kile chumba akifuata pale alipohisi alikanyaga damu.Moyo ulimuenda kmbio kwa hofu!Alipotizama akaufuata mchirizi huo wa damu ambao bado ulikuwa mbichi kabisa.Ilielekea chini ya mvungu.Mama mkwe akasita kidogo nakurudi hadi ukumbini kwa haraka hata kabla hajaangalia chini ya mvungu kuna nini?
Huku maswali yakizidi kupanda.
“Damu za nini?”alijiuliza.
“Tena zinaelekea chini ya mvungu!Au ndo kwasababu anaonekana wa ajabu ajabu kama mtu anayelia?”alijiuliza asipate jibu.Alipokuwa pale alisikia kama simu inayounguruma kwa mtetemeko.Ukimya uliokuwepo ulimpa fursa ya kusikia chochote kinachoendelea mule ndani.Akasogea nakuichukua ile simu.Alikuwa mama wa kisasa hivyo vitu vya kiteknolojia havikumsumbua jambo lolote.Akaikagua aliona namba ngeni lakini hakupokea.Simu ilikata na bila shaka kulikuwa na msururu wa ujumbe mwingi uliokuwa umetumwa kwenye simu pamoja na simu nyingi ambazo zilipigwa bila kujibiwa.Kwenye kioo cha simu aliona picha ya Hamza pamoja na Laredo wakiwa katika pozi la busu ambalo usingesema shemeji atakaa na shemeji mtu!Mama mkwe alikuwa mdadisi alipekua kwenye simu jumbe nyingi alizoona zilikuwa za kawaida hasa lawama kwamba Hamza anapigiwa simu lakini hapokei.Mama akapekua tena kwenye picha za simu.Alifanya hivyo baada ya kuona picha ikiwa imehifadhiwa kwenye kioo cha simu kati ya Laredo na Hamza alitaka kujua kuna picha ngapi nyingine zina utata!Halafu kama Hamza kasafiri kwanini simu ipo hapa tena imewashwa na kuna simu nyingi zimeingia bila kupokelewa?
Alipofika kwenye faili la picha mama mkwe alichanganyikiwa.Alikuta picha nyingi lakini asilimia kubwa za picha zilikuwa kati ya Laredo na Hamza.Mara wakiwa katika maeneo ya faragha.Picha za selfie na nyingine zikionesha Laredo akiwa mtupu bila shaka picha hizi zilichukuliwa wakiwa pamoja maeneo yenye hatari sana.Hilo halikukwepeshs wazo kwamba kuna kitu kati ya Laredo na shemeji yake!Mama mtu akameza jambo hilo akingoja wasaa wakulitapika vilivyo.Aliendelea kukagua picha hilo moja baada ya nyingine.Mazingira ya picha zile yalipigwa ndani ya nyumba ile!Chochote kilichofanyika lazima kilikuwa kwa uwazi mpaka hatua ya kupiga picha ilimpa uhakika kwamba hakuna mzaha kati ya Hamza na mke wa kaka yake!
Mama mkwe akatoka hadi nje ya chumba kile.Alipokuwa anatizama huku na kule alisikia tena simu nyingine ikiita!Moyo ukapiga paa!Alifuata mlio ulitokea dirishani kwenye chumba cha Masua!Kwa kuwa alimjua mpangaji huyo aliamua kwenda hadi dirishani hapo akachungulia lakini hakuona mtu zaid simu ilikuwa kwa dirishani ni kiasi cha kupenyeza mkono nakuitoa!Akaichukua!Alipotizama kwenye kioo akashtuka!Ilibidi akimbie ndani.
Kwenye kioo cha simu kulikuwa na picha ya Laredo na Masua wakiwa katika pozi la mahaba!Katika kukagua picha ile aligundua fika kwamba halikuwa pozi la jirani kwa jirani lilikuwa zaid ya kawaida!Bila kufikiri sana alienda kwenye faili la picha huko nako alikuta vituko!Picha zilikuwepo kibao kati ya Laredo na Masua wakiwa katika pozi zenye kutilia mashaka wala usingewaza mara mbili kwamba watu hawa ni wapenzi!Mama mkwe aliduwaa!Alienda hadi chumbani tena huku akiwa na maswali lukuki.
“Inakuwaje anapiga picha za ajabu na shemeji yake hadi na jirani yake huku sikuutukanisha uke jamani?Huyu msichana si bure anatabia ya ajabu!”
Akiwa pale chumbani alipeleka upekuzi kwenye chumba kile moja ya picha akiwa na Hamza ilikuwa palepale chumbani mashuka na blanketi lilelile bila kubisha.Wasiwasi wa maswali hayo ukamfanya mama apeleke macho kitandani.Lakini ghafla akaona mchirizi wa damu kwenye shuka la pale kitandani ukiwa kwenye kingo za kitanda!Akafuata ni kama alama za mikono ya mtu aliyekuwa ameshika damu na tena ni kama aligusa kitanda bila kutarajia!.Ilibidi aende hadi uvunguni lakini kabla haja gusa kitu alisikia mtu kumsimamia kwa nyuma!
“Mama! “aliita Laredo hali iliyofanya mama mkwe kuinuka ghafla!
“Kuna nini umenishtua!”alisema akiwa kwenye mshtuko wa kukutwa.Laredo nusura moyo umpasuke maana kamkuta mama amechutama anataka kuchungulia uvunguni.Je,kama amesha chungulia?
“Nilikuwa na kwambia uje…eh!...Uje…”kigugumizi kikamshika!Lakini palepale mama akarudi kuchutama akaelekeza macho uvunguni.Akapeleka mkono nakugusa kitu!Moyo ulipigaa paa!Aligusa mguu ulianza kupoa!Ilikuwa ngozi ya mtu!Ilibidi auvute tena kwa nguvu akaona ni mgumu!Akavuta!Alijua bila shaka kuna mwanaume kafichwa huku nini?Hilo lilikuja baada ya kuona picha za ajabu ajabu kwenye simu mbili alizookota!Halafu likaja wazo lakuona damu!Vyote hivi vilikuja kichwani kwa haraka.Akauvuta mguu wote!Akakutana na maiti!Ni jinamizi bay asana kuwahi kumtokea.Lilimtisha na kumfedhehesha maisha yake yote!Mama huyu aliyekuwa na taaluma ya uuguzi ambaye kwa sasa ni mstaafu alijikuta akiinuka kwa haraka!Ulikuwa mwili usio na fahamu maana aliuvuta ukatokeza kutoka miguuni hadi kiunoni!
Laredo katumbua macho!Ilikuwa sadfa!Haikupangwa japo ipo siku mtu angezigundua maiti zile lakini sio kwa haraka vile!Palepale Laredo alijua fika kaumbuka!Atasema nini!
Hakuna mama asiyejua mwili wa mwanaye!Mama mkwe palepale aliutambua mwili ule!Ni wa mwanaye!Hamza!
“Mwananguuu!”alipika kite!Nywele za malaika zikamsimama!Ilibidi bimkubwa huyo ajishike kichwa kwa sekunde kama tano!Halafu akarudi chini nakuuvuta miguu!Akauburuza wote kutoka uvunguni!Alikutana na mwili wa Hamza!Ulikuwa kimya macho kayafumba!Mama aliduwaa!Ilikuwaje?Alienda hadi pale chini akamshika mkono kuhisi kama kulikuwa na mapigo ya mshipa!Balaa!Jambo likazuka palepale.Tumbo la uchungu alilolisikia miaka mingi iliyopita aliukumbuka uchungu huo katika fikra ya saikolojia nakuanza kuyahisi yale maumivu kwenye tumbo lake kwa kasi ya ajabu!Hapa kuna maiti ya mwana wake!Alipigwa na bumbuazi la uhakika!Akadata!Hiki ni kizaazaa!
“Mwanangu maiti!Uuuwii!...Hamza wangu wamekutendaje!..Nipeni shuka jamanii…nipeni shukaaa!...Nipeni shuka niliee uwii!”
Hakika ilikuwa huzuni kubwa sana!Mama alikuwa akilia kwa uchungu wa hali ya juu!Lakini katika kuuangalia mwili wa Hamza kulikuwa hakuna damu zaidi ya kama povu lililoganda kinywani nakuteleza kwenye kuta za shavu!Ile damu ilimfanya mama wa watu akiwa analia aingie chini ya uvungu tena!Akaona miili imerundikwa!Laredo alikuwa amekwisha!
Nguvu za kuvuta ile miili zikaisha pyuu!Alimgeukia Laredo aliyekuwa anatetemeka zaidi ya kifaranga kilicho mwagiwa maji!Alikuwa amefumwa!Hakuweza hata kumtizama mama mkwe wake vizuri!Alikuwa akigusanisha viganja vya mikono kana kwamba ananawa!Hakueleweka!
Mama mkwe alimshika kwa kumkunjanguo ya juu!Lakini mikono ya mama ilikuwa dhaifu sana alijikuta akimwachia huku kilio kikimshinda!Laredo naye alianza kulia ni kama bomba la machozi lilifunguliwa kati yao!Huyu analia kapoteza mwana,huyu analia kapoteza mume!
“Mwanangu kafa na nini?”aliuliza mama mkwe! Lakini ghafla kitu kika mwambia Laredo akimbie na atokomee!Mama kakuta maiti takribani nne katika chumba chake!Hilo tayari ni kosa!Inatakiwa polisi wa aitwe!Asingesema eti hajui miili hiyo kaitoa wapi?Tayari alishajikoroga kwenye majibu kuwa watu hawa wamesafiri wakati wameshauliziwa takribani mara kadhaa!Kwanza na mama mkwe!Pili mama Shully!Hii ni hatari kwa usalama wake!
“Niambiee…niambieeeee!...Wananguu wamekuwaje!...Mjukuu wangu mmefanyajeee!”alipiga kelele mama mkwe.Wote hawakuwa na pumzi.Laredo alitikisa kichwa kana kwamba hajui lolote!Alikumbuka vyema alivyofyetua risasi kwa kujihami lakini ikawa kosa akajikuta kampiga mwanaye!Alijikuta akilia tena!Alikumbuka pia usiku uliopita aliwaacha wanaume hao salama,kuja kuamka asubuhi anakutana na maiti.Bila shaka alishajua chakula kilikuwa na sumu lakini mpishi ni yeye!Wakati akiwaza hayo akakumbuka kauli ya Hamza alivyojaribu kumshawishi amuue Bario iliwabaki wote.Hilo lilimpa njia mpya kwamba aliyeua si yeye bali kuna mkono wa Hamza maana alionesha dalili!
Lakini akiwa hajajipanga alijikuta akisikia hodi ikibishwa!Kutoka mlango wa sebuleni.Bila hata kuwaza alimrukia mama mkwe na kumkwida shingo akaanguka naye hadi chini!Alikuwa anamnyonga!
BONIFACE BIRAGE
Ilikuwa damu ya nini?Mama mkwe bado hakujua.Kuona damu katika mazingira kama yale yalimpa mawazo mengi.Kimuhemuhe kilichomgusa moyo kikamfanya aufungue mlango wa chumbani akaingia.Alianza kukagua kile chumba akifuata pale alipohisi alikanyaga damu.Moyo ulimuenda kmbio kwa hofu!Alipotizama akaufuata mchirizi huo wa damu ambao bado ulikuwa mbichi kabisa.Ilielekea chini ya mvungu.Mama mkwe akasita kidogo nakurudi hadi ukumbini kwa haraka hata kabla hajaangalia chini ya mvungu kuna nini?
Huku maswali yakizidi kupanda.
“Damu za nini?”alijiuliza.
“Tena zinaelekea chini ya mvungu!Au ndo kwasababu anaonekana wa ajabu ajabu kama mtu anayelia?”alijiuliza asipate jibu.Alipokuwa pale alisikia kama simu inayounguruma kwa mtetemeko.Ukimya uliokuwepo ulimpa fursa ya kusikia chochote kinachoendelea mule ndani.Akasogea nakuichukua ile simu.Alikuwa mama wa kisasa hivyo vitu vya kiteknolojia havikumsumbua jambo lolote.Akaikagua aliona namba ngeni lakini hakupokea.Simu ilikata na bila shaka kulikuwa na msururu wa ujumbe mwingi uliokuwa umetumwa kwenye simu pamoja na simu nyingi ambazo zilipigwa bila kujibiwa.Kwenye kioo cha simu aliona picha ya Hamza pamoja na Laredo wakiwa katika pozi la busu ambalo usingesema shemeji atakaa na shemeji mtu!Mama mkwe alikuwa mdadisi alipekua kwenye simu jumbe nyingi alizoona zilikuwa za kawaida hasa lawama kwamba Hamza anapigiwa simu lakini hapokei.Mama akapekua tena kwenye picha za simu.Alifanya hivyo baada ya kuona picha ikiwa imehifadhiwa kwenye kioo cha simu kati ya Laredo na Hamza alitaka kujua kuna picha ngapi nyingine zina utata!Halafu kama Hamza kasafiri kwanini simu ipo hapa tena imewashwa na kuna simu nyingi zimeingia bila kupokelewa?
Alipofika kwenye faili la picha mama mkwe alichanganyikiwa.Alikuta picha nyingi lakini asilimia kubwa za picha zilikuwa kati ya Laredo na Hamza.Mara wakiwa katika maeneo ya faragha.Picha za selfie na nyingine zikionesha Laredo akiwa mtupu bila shaka picha hizi zilichukuliwa wakiwa pamoja maeneo yenye hatari sana.Hilo halikukwepeshs wazo kwamba kuna kitu kati ya Laredo na shemeji yake!Mama mtu akameza jambo hilo akingoja wasaa wakulitapika vilivyo.Aliendelea kukagua picha hilo moja baada ya nyingine.Mazingira ya picha zile yalipigwa ndani ya nyumba ile!Chochote kilichofanyika lazima kilikuwa kwa uwazi mpaka hatua ya kupiga picha ilimpa uhakika kwamba hakuna mzaha kati ya Hamza na mke wa kaka yake!
Mama mkwe akatoka hadi nje ya chumba kile.Alipokuwa anatizama huku na kule alisikia tena simu nyingine ikiita!Moyo ukapiga paa!Alifuata mlio ulitokea dirishani kwenye chumba cha Masua!Kwa kuwa alimjua mpangaji huyo aliamua kwenda hadi dirishani hapo akachungulia lakini hakuona mtu zaid simu ilikuwa kwa dirishani ni kiasi cha kupenyeza mkono nakuitoa!Akaichukua!Alipotizama kwenye kioo akashtuka!Ilibidi akimbie ndani.
Kwenye kioo cha simu kulikuwa na picha ya Laredo na Masua wakiwa katika pozi la mahaba!Katika kukagua picha ile aligundua fika kwamba halikuwa pozi la jirani kwa jirani lilikuwa zaid ya kawaida!Bila kufikiri sana alienda kwenye faili la picha huko nako alikuta vituko!Picha zilikuwepo kibao kati ya Laredo na Masua wakiwa katika pozi zenye kutilia mashaka wala usingewaza mara mbili kwamba watu hawa ni wapenzi!Mama mkwe aliduwaa!Alienda hadi chumbani tena huku akiwa na maswali lukuki.
“Inakuwaje anapiga picha za ajabu na shemeji yake hadi na jirani yake huku sikuutukanisha uke jamani?Huyu msichana si bure anatabia ya ajabu!”
Akiwa pale chumbani alipeleka upekuzi kwenye chumba kile moja ya picha akiwa na Hamza ilikuwa palepale chumbani mashuka na blanketi lilelile bila kubisha.Wasiwasi wa maswali hayo ukamfanya mama apeleke macho kitandani.Lakini ghafla akaona mchirizi wa damu kwenye shuka la pale kitandani ukiwa kwenye kingo za kitanda!Akafuata ni kama alama za mikono ya mtu aliyekuwa ameshika damu na tena ni kama aligusa kitanda bila kutarajia!.Ilibidi aende hadi uvunguni lakini kabla haja gusa kitu alisikia mtu kumsimamia kwa nyuma!
“Mama! “aliita Laredo hali iliyofanya mama mkwe kuinuka ghafla!
“Kuna nini umenishtua!”alisema akiwa kwenye mshtuko wa kukutwa.Laredo nusura moyo umpasuke maana kamkuta mama amechutama anataka kuchungulia uvunguni.Je,kama amesha chungulia?
“Nilikuwa na kwambia uje…eh!...Uje…”kigugumizi kikamshika!Lakini palepale mama akarudi kuchutama akaelekeza macho uvunguni.Akapeleka mkono nakugusa kitu!Moyo ulipigaa paa!Aligusa mguu ulianza kupoa!Ilikuwa ngozi ya mtu!Ilibidi auvute tena kwa nguvu akaona ni mgumu!Akavuta!Alijua bila shaka kuna mwanaume kafichwa huku nini?Hilo lilikuja baada ya kuona picha za ajabu ajabu kwenye simu mbili alizookota!Halafu likaja wazo lakuona damu!Vyote hivi vilikuja kichwani kwa haraka.Akauvuta mguu wote!Akakutana na maiti!Ni jinamizi bay asana kuwahi kumtokea.Lilimtisha na kumfedhehesha maisha yake yote!Mama huyu aliyekuwa na taaluma ya uuguzi ambaye kwa sasa ni mstaafu alijikuta akiinuka kwa haraka!Ulikuwa mwili usio na fahamu maana aliuvuta ukatokeza kutoka miguuni hadi kiunoni!
Laredo katumbua macho!Ilikuwa sadfa!Haikupangwa japo ipo siku mtu angezigundua maiti zile lakini sio kwa haraka vile!Palepale Laredo alijua fika kaumbuka!Atasema nini!
Hakuna mama asiyejua mwili wa mwanaye!Mama mkwe palepale aliutambua mwili ule!Ni wa mwanaye!Hamza!
“Mwananguuu!”alipika kite!Nywele za malaika zikamsimama!Ilibidi bimkubwa huyo ajishike kichwa kwa sekunde kama tano!Halafu akarudi chini nakuuvuta miguu!Akauburuza wote kutoka uvunguni!Alikutana na mwili wa Hamza!Ulikuwa kimya macho kayafumba!Mama aliduwaa!Ilikuwaje?Alienda hadi pale chini akamshika mkono kuhisi kama kulikuwa na mapigo ya mshipa!Balaa!Jambo likazuka palepale.Tumbo la uchungu alilolisikia miaka mingi iliyopita aliukumbuka uchungu huo katika fikra ya saikolojia nakuanza kuyahisi yale maumivu kwenye tumbo lake kwa kasi ya ajabu!Hapa kuna maiti ya mwana wake!Alipigwa na bumbuazi la uhakika!Akadata!Hiki ni kizaazaa!
“Mwanangu maiti!Uuuwii!...Hamza wangu wamekutendaje!..Nipeni shuka jamanii…nipeni shukaaa!...Nipeni shuka niliee uwii!”
Hakika ilikuwa huzuni kubwa sana!Mama alikuwa akilia kwa uchungu wa hali ya juu!Lakini katika kuuangalia mwili wa Hamza kulikuwa hakuna damu zaidi ya kama povu lililoganda kinywani nakuteleza kwenye kuta za shavu!Ile damu ilimfanya mama wa watu akiwa analia aingie chini ya uvungu tena!Akaona miili imerundikwa!Laredo alikuwa amekwisha!
Nguvu za kuvuta ile miili zikaisha pyuu!Alimgeukia Laredo aliyekuwa anatetemeka zaidi ya kifaranga kilicho mwagiwa maji!Alikuwa amefumwa!Hakuweza hata kumtizama mama mkwe wake vizuri!Alikuwa akigusanisha viganja vya mikono kana kwamba ananawa!Hakueleweka!
Mama mkwe alimshika kwa kumkunjanguo ya juu!Lakini mikono ya mama ilikuwa dhaifu sana alijikuta akimwachia huku kilio kikimshinda!Laredo naye alianza kulia ni kama bomba la machozi lilifunguliwa kati yao!Huyu analia kapoteza mwana,huyu analia kapoteza mume!
“Mwanangu kafa na nini?”aliuliza mama mkwe! Lakini ghafla kitu kika mwambia Laredo akimbie na atokomee!Mama kakuta maiti takribani nne katika chumba chake!Hilo tayari ni kosa!Inatakiwa polisi wa aitwe!Asingesema eti hajui miili hiyo kaitoa wapi?Tayari alishajikoroga kwenye majibu kuwa watu hawa wamesafiri wakati wameshauliziwa takribani mara kadhaa!Kwanza na mama mkwe!Pili mama Shully!Hii ni hatari kwa usalama wake!
“Niambiee…niambieeeee!...Wananguu wamekuwaje!...Mjukuu wangu mmefanyajeee!”alipiga kelele mama mkwe.Wote hawakuwa na pumzi.Laredo alitikisa kichwa kana kwamba hajui lolote!Alikumbuka vyema alivyofyetua risasi kwa kujihami lakini ikawa kosa akajikuta kampiga mwanaye!Alijikuta akilia tena!Alikumbuka pia usiku uliopita aliwaacha wanaume hao salama,kuja kuamka asubuhi anakutana na maiti.Bila shaka alishajua chakula kilikuwa na sumu lakini mpishi ni yeye!Wakati akiwaza hayo akakumbuka kauli ya Hamza alivyojaribu kumshawishi amuue Bario iliwabaki wote.Hilo lilimpa njia mpya kwamba aliyeua si yeye bali kuna mkono wa Hamza maana alionesha dalili!
Lakini akiwa hajajipanga alijikuta akisikia hodi ikibishwa!Kutoka mlango wa sebuleni.Bila hata kuwaza alimrukia mama mkwe na kumkwida shingo akaanguka naye hadi chini!Alikuwa anamnyonga!