chingaa
Member
- Jun 25, 2017
- 86
- 77
Hatakama ni story.. Ila mimi siwezi kukubaliUPEPO WA USIKU-7
BONIFACE BIRAGE
“Nimetoka nje ya ndoa si mara moja.”kwa kumfichia mumewe kwamba hawana ushirikiano mzuri wa kifaragha hakumsema mbele za watu.Ni jambo lao labda watu wahisi tu nasio kuwa na ushahidi kutoka kwake.Ingebaki siri yake daima!Mengine yabaki siri za sisimizi.
“Nimekuwa nikishiriki kimapenzi ya siri na Masua!”Pigo kali kama ngumi ya za wanamsumbwi!Kwa kweli hungelikabili kama una moyo wa nyama.Lilikuwa pigo la uhakika.Ni kama alimdunga sindano hasa akiwa sio mtu aliyependa kutobolewa na kifaa hicho.Hali ilianza kubadilika.Hiz karata anazocheza alitakiwa kuzipanga kwa umakini kuliko jambo lolote lile.
Bario alitizama chini kwa hasira halafu akauleta uso kwa Masua!Masua aliangalia pembeni kwa aibu!Chakula kikawa kizito kuchota nakutafuna pia!Ilikuwa mtu kati kawekwa!Yaani umenibamba viutamu!Dj Afro angekwambia bumper to bumper…Heri ushikwe kwa namna nyingine lakini si kwa uwazi kiasi hiki huku ni kumvua mtu nguo mbele ya kadamnasi
“Mke wangu kwani unasema nini?”ilibidi amuulize maana bado hakuwa ameshika maelezo ya bibi huyu.
“Ni kweli nimekuwa na uhusiano wa kimapenzi na Masua kwa muda mrefu sasa.”alisema nakumwangalia mumewe kumpima kama bado ana shari zozote.Halafu mtu mwenyewe yupo mezani mwake.Anakula hapohapo?Jamaa alichanganyikiwa kwa sekunde kadhaa.
“Kwani mmefanya nini na nini?”hata hakupanga kuuliza swali kama hilo japo ilikuja tu akajikuta kauliza bila kutegemea.
“Yote ambayo umekuwa huyafanyi!”ilikuwa aibu ya mwaka.Bario alikwepesha macho nakutizama chini.Dah!Wanawake wanajua kuzicheza kete zao.Hili lilikuwa jipya nakumpiga kunako maeneo husika ya shutuma.Yaani alimtandika kwa neno zito hata wote waliokuwa mezani walijikuta wakishikwa na mshtuko uliowakaba kooni.
“Hata juzi nilipotoweka usiku nilikuwa kwake.”Laredo aliendelea kupasua mwamba bila ajizi yeyote ile.
Alitamani kujua nyendo za mkewe lakini hakuwa na wazo kama zingefikia hatua hii.Ilikuwa kali ya mwaka!Pengine hakutwakiwa kujua lolote si chochote.Hii ilikuwa kali ya mwaka!
“Unaweza kunilaumu lakini bado.Safari ni ndefu.Tumekuwa tukifanya mapenzi mara nyingi na yeye.”kwa jinsi alivyoropoka uchafu wake hata usingeamini!Halikuwa jambo la kuzungumzwa mbele ya wanaume hawa.Ni aibu ya mwaka!Pengine hata angemwita mume wake chemba walizungumze jambo hilo labda uwezekano wa suluhu ungefanyika kimyakimya.Aliumwaga mpunga katikati ya kuku wengi tena wakienyeji!Kusema habari kama hii ilihitaji ujasiri wa msemaji na hadhira anayoihutubia.Kwa kawaida hakuna ambaye angevumilia jambo hili nasiajabu zingelika ngumi hapahapo!Lakini Laredo alishawajua waume zake na namna ya kuwadhibiti.Alijua leo kapiga hatua kubwa sana kusema kitu hicho nasio kwamba kingekubaliwa.Alijaribu kete hiyo!
Bario hakuvumilia aliamka nakwenda chumbani.Laredo kidogo alie,akajikaza.Alijua anavunja ndoa japo kichwani alikuwa namahesabu kwamba ni muhimu akilipua jipu palepale kuliko kuja kugundulika baadaye.Akainuka nakumfuata mume wake hadi chumbani.Alimkuta amekaa kitandani kainamisha kichwa chini.Mwingi wa mawazo.Bora aseme jambo kuliko ukimya wa namna ile wa ghafla.Mshtuko upo ila sio kwa kiwango kile.
Alienda nakuketi ubavuni mwake.Ukimya ukapita kati yao!Ukimya uliobeba mengi na siri za utata.
“Nini kilifanyika hapa nilipokuwa hospitali.”alianza Bario akipandisha ujasiri wa mbwa wa kiume asiye na meno!
“Nililala na Masua.”kwanini afiche bora aseme ukweli.Kiwango alichofikia ilibidi aongee tu.Ukimywa wa kula gizani ulishaisha muda.Usaliti wake ulikuwa umepevuka kwa sasa.
“Wapi?”
“Kwenye hiki kitanda.”akaonesha kwa kidole.
Bario akameza mate ambapo sasa mdomo ulianza kuwa mchungu!Ukawa umekauka!Nguvu ni kama zilimwishia!Aliona kama kizunguzungu kilitaka kuja kikapotea!Alihisi mkojo umembana lakini hakuwa na haja ya kwenda chooni!Ndoa zina mambo wakati mwingine siyo zote bali baadhi tu!
“Kwanini ulifanya hivi?”
Laredo alitegemea kuulizwa vile.Akajikohoza kukusanya ujasiri.Hakuwa na sababu kwamba ni jambo gani alitakiwa kulisema ilikumuweka mumewe kwa wazo alilotaka!Wazo la kuwa na mabwana watatu!
“Hata nikwambie hutanielewa,kifupi nilikusaliti na stahili kuachwa.’’ Ni kama alijipa talaka.Alijuafika Bario asingempa talaka bali angemwacha atimbwe na ulimwengu.Ilikuwa kama dhihaka usoni mwa Bario.Tena dharau zenye chembe ya wizi wa makinikia.
“Not well at all.”alisema kwa huzuni.
“Na sio Masua tu.Nina uhusiano na Hamza pia.Nawapenda wote nipo tayari kuishi na nyie wote.Kilichobaki ni ndoa nikiwaongeza Masua na Hamza.Tutaishi mkijua kwamba mimi ni mke wenu.Mambo ya wivu hayatakuwepo.Tutakuwa na raha tukifanya mambo kwa pamoja.Ni wazo zuri mume wangu.Kuliko niendelee kuwasaliti bora wote mnioe tuishi wote hapa.Watu wa nje hawatajua kwamba nyie ni wanaume wangu wote.Watajua kwamba wewe ndo mume hao wengine ni ndugu tu.”
Bario alitumbua macho,’’Hivi unajua unachosema?”
“Nakijua.”alisisitiza binti huyu kwa ustaadi wa hali ya juu.Kama ni kilevi basi alikuwa amevuta au kunywa kile chenyewe.Lakini hakuwa amevuta wala kulewa.Ilikuwa akili tu kama mtu yeyote.Kilicho kichwani mwake nikuingiza utamaduni alioubeba kutoka maeneo ya huko ng’ambo.Vile aliona hajapigwa kofi wala kufokewa alijua fika ana hoja ya kujibu.Ni vile aliukuta moyo wa Bario ni nyama.
“Ni sehemu chache sana wanazo fanya mambo haya.”alisema Bario akimwambia mkewe.Kitu hiki kilisharipotiwa nchi za ng’ambo.Kwa mujibu wa Bario alishasoma utamaduni huo ambao ni wa watu wan je.Hakuwa wakitanzania.Huku usingekubaliwa kabisa.Ni kwamba mwanamke huyu aolewe na hawa watu watatu waishi pamoja wakishiriki mambo yote.
“Hii siyo open relationship yaani nikuruhusu uende na yeyote unayejisikia kwenda naye ilhali tupo pamoja.Hii ni serious ujue?”alisema Bario akikuna kichwa.Papi za midomo yake ilikauka kaukau.
“Sisi tutakuwa sehemu moja ya hiyo.Polyandry sio mbaya bali ni uhakika kwa mwanamke kuwa na waume watatu.Sina haja nakuwa na open relationship?Kuwa nayo open realationship ni hainipi uhakika mimi.Kwanza nitakuwa muhuni zaidi.Bora tufanye polyandry mwanamke mmoja anakuwa na mabwana wa halali zaidi ya mmoja.Mimi nimewachagua nyie watatu.Bario,Masua na Hamza.”alijitetea mwanamke Yule.
“Laredo umechanganyikiwa kwa kweli?How can you manage three husbands?”
“I can kwa sababu siku zote nimekuwa nikiweza.Haina haja yakuleta bifu.Tumalize kiistaarabu jambo hili.Mbona nyie wanaume mnaoa wanawake wawili hadi watano kwani mwanamke hana ujasiri huo.”
Kichwa kikacheza kwa mshangao kwa upande wa Bario.Mapya.Huu utamaduni wa ng’ambo una mashaka yake.
“Tatizo waafrika tunambana sana mwanamke hatumpi fursa ya kuridhika kwa kile anachotaka.Binadamu aliumbwa kufurahia maisha.Nikitoka na mwanamke mwanaume mwingine mnasema mimi mzinzi sasa nadai ishu ndogo tu niolewe na nyie watatu.Msiwe na wivu wowote!”
Bario aliinuka nakuja hadi ukumbini.Hamza alitaka kukimbia,”Usikimbie Hamza.We baki.Najua kinachoendelea hadi sasa.Nahitaji ushauri wenu.”
Hamza alirudi nakuketi.Alivuta pumzi ndefu nakuwaza aseme nini kwakuwa alishajua Laredo amemwleza mumewe jambo hilo,”Laredo mimi nakupenda kwa dhati nipo tayari kushare na wenzangu.”
“Hata mimi nashauri jambo hilo.”akaitikia Masua kwa haraka.Hawa walishapangwa tangu kitambo wala hakuna aliye na pingamizi.Ashukuru Mungu hawa walimwelewa lakini wangekuwa wengine ngumi zingelika kwa hatari ya kifo!
“Bario unaona wenzako wanaakili.Utakuwa muunganiko mzuri usio na vikwazo.Hamtakuwa na hofu ya kushare mke kwamba yupo na nani?Tutaishi nyumba moja kwa upendo wa ajabu na tutakuwa na familia moja iliyo na nguvu.”
“Unadhani jamii itatuonaje?”Bario akajikuta akiuliza.Kuambiwa hao wanaakili alihisi kutukanwa.
“Jamii haitajua hii ni siri yetu sisi tu.”
Bario alitulia kwanza akafikiri huku akijiambia haya ni majaribu au ndoto ya kutisha!Kuliko kupinga sana bora kieleweke mara ileile,”Sawa.”aliunga mkono huku akijiambia anataka kuona safari hiyo itaishia wapi.Japo alimpenda mkewe lakini kuna wakati alichoka nakusubiri aone mwishio wake ni nini?Pia alijiuliza ni kweli anampenda mkewe?Au mwanamke huyu ameshachuja.Jambo hilo lilikuwa gumu na hata kubali yake hakuijua imetoka wapi?Wengine wangesema kapuliziwa!
“Kwaanzia leo jueni nyie ni waume zangu na mimi ni mke wenu.”alijikaza nakuwatamkia.Wanaum wote wakatizamana kisha kwa shingo upande wakapeana mikono.Hata hakujua ilikuwaje ikawa rahisi kwa wanaume hao kukubali jambo hilo.Msafara wa ndoa baina ya mwanamke mmoja na wanume watatu ukaanza.
“Tukitaka kuwa na watoto?’’Bario akauliza.
“Hilo nachagua mimi nizae na nani?Lakini kaeni mkijua wote mtahitajika kuwa responsible kwa watoto wetu.Hakuna huyu ni wafulani.Wote ni baba kwa watoto wote sawa!’’maelezo ya Laredo yaliwashtua sana.Yalikuwa mapya kwa muafrika!
“Leo na lala na mume wangu mkubwa nyie hamtaruhusiwa kunigusa hadi tutakapofunga ndoa za kisheria.Hakuna wakutoa ushahidi kwamba nimeolewa nataka wote mnimiliki kisiri.Au sio wapenzi wangu?”
Bario alikuwa namahesabu yake.Alitaka kuona mbio za Laredo zinishia wapi?
USIKOSE TOLEO LIJALO STORY NDO KWANZA INAANZA!
Tears of the sun