Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
RIWAYA: UKURASA WA TISA
NA: BAHATI K MWAMBA
SIMU: 0758573660/0658564341
Sehemu moja maarufu ndani ya jiji la Dodoma kulikuwa na kundi kubwa la watu pembezoni mwa barabara wakiwa wamesimama kimakundimakundi. Watu hao walikuwa wamesimama kwa kuzizunguka baadhi ya meza za kuuzia magazeti zilizoko maeneo hayo maarufu kwa jina la Nyereresquare. Licha ya eneo hilo kuwa linapokea idadi kubwa ya watu kuanzia majira ya ahsubuhi hadi jua lizamapo, lakini ni aghalabu kukuta watu wengi wakiwa mbele ya mabango ya meza za wauza magazeti na vitabu zilizoko sehemu hiyo. Kwa siku za karibuni lile jambo lilianza kuzoeleka miongoni mwa watu waliokuwa wakipita au kuingia ndani ya viwanja vya Nyereresquare.
Miongoni mwa watu waliokuwa wakiwahi ahsubuhi na kuzunguka meza ya mmoja wa muuza magazeti, alikuwa ni Jane Mgale, Mama mwenye watoto wenye umri wa kuzidiana miaka miwili huku mkubwa akiwa na umri wa miaka minne na mdogo miaka miwili. Mama huyu ambae umri wake ulikuwa chini ya miaka ishirini na sita, alijikuta akiwa mtumwa wa kuamka kila jumatano na ijumaa ahsubuhi kwa lengo la kuwahi kununua moja ya jarida lililoanza kujichukulia umaarufu hapa nchini, huku likiwa na siku chache tangu kuanzishwa kwake. Jane alikuwa na sababu mbili kubwa zilizomfanya awe anawahi ahsubuhi sana kwenda kununua jarida hilo, sababu moja wapo ikiwa ni mazingira aliyokuwa akitokea kutokuwa na muuza magazeti ambae alikuwa ni wakala wa lile jarida lililokuwa likimpa safari za lazima kila jumatano na ijumaa, lakini sababu kubwa zaidi ilikuwa ni kile kilichokuwa kikipatikana kwenye ukurasa wa tisa wa jarida la Ngano Zetu lililokuwa likichapishwa na kampuni ya Mwa'se'ma Publishers.
Ukurasa wa tisa wa jarida hilo kulichapishwa simulizi za kweli kutoka kwa watu mbalimbali, kurasa nyingine zilichapishwa riwaya kutoka kwa waandishi wenye uzoefu na wale wanaochipukia. Ngano zetu lilikuwa ni jarida lilijizolea umaarufu kwa muda mfupi tangu lilipoanzishwa, watu wengi walipenda kulinunua kwa sababu ya kusoma riwaya nzuri kutoka kwa waandishi mashuhuri nchini Tanzania, lakini wengi wao walivutiwa na simulizi za kweli zilizokuwa zikichapishwa ukurasa wa tisa, zilikuwa ni simulizi zenye visa na mikasa mizito walizowahi kukutana nazo baadhi ya watu mashuhuri na wasio mashuhuri ilimaradi, walipata nafasi ya kusimulia waliyowahi kuyapitia kwenye maisha yao. Licha ya ukweli kwamba watu walisoma na kuvutiwa sana na mikasa ya ukurasa huo, lakini wakati huo kulikuwa na simulizi nzuri sana iliyokuwa ikivuta hisia za watu wengi sana hata wale ambao hawakuwa wapenzi wa usomaji, walijikuta wakivutiwa na jarida lile hasa ule ukurasa wa tisa hadi kumi na moja, walivutiwa na kisa cha mwandishi Bahati Kisarwa Mwamba ambae alipenda kuandika mikasa ya mhalifu Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku, pia alipenda kuandika visa vya jasusi Honda Makubi, Zedi Wimba na Obimbo Mtei.
Kilichowavutia watu kufuatilia mkasa wa mwandishi huyo si matukio aliyokutana nayo pekee bali pia ni kuwakutanisha wahusika anaopenda kuwatumia kwenye riwaya zake kuwa sehemu ya wasimuliaji. Zuki Gadu pamoja na jasusi Honda Makubi nao walijumuika nae kwenye simulizi ile ya kweli, wasomaji hawakuishia kusoma visa na mikasa yake kwenye jambo alilokuwa akilisimulia, walisoma pia mikasa ya watu waliokuwa wakizunguka nae kwenye mkasa wake huo wa kweli uliowahi kumkuta kwenye safari ya maisha yake. Wale waliokuwa wakisoma vitabu vyake na kuwafahamu wahusika hao ambao walidhani ni watu wa kufikirika, kupitia jarida lile walipata uhakika kuwepo Zuki Gadu halisi, Honda Makubi halisi na wengineo, lakini kubwa zaidi waligundua Bahati alikuwa na urafiki na watu hao. Kwa wasomaji hao kwao si burudani tu walioipata kwa kusoma mkasa wa mwandishi wampendae, bali walipata kuufahamu ukweli wa baadhi ya maswali waliojiuliza.
Tofauti na wasomaji wengine ambao walivutiwa na matukio ya kufurahisha na kusikitisha yaliyosimuliwa na wahusika, Jane Mgale alikuwa anafuatilia jambo kwenye mkasa ule, alifuatilia maisha halisi ya Bahati Mwamba aliyoyasimulia, maisha hayo ni mahusiano. Kwa nini? Kwa sababu alikuwa akimfahamu mwanaume huyo na alimfahamu kwa sababu ndiye baba wa watoto wake wawili aliokuwa akiwalea na ndiye aliyekuwa mume wake wa ndoa. Alifuatilia kila toleo jipya kwa sababu aliamini ataendelea kufahamu mengi ambayo hakuwa akiyafahamu kuhusu mume wake, mambo ambayo mume wake hakuwahi kumwambia hata kwa bahati mbaya ijapokuwa, hata kuhusu mkasa huo kuchapishwa gazetini aliyemwambia aufuatilie ni huyohuyo mumewe, bila shaka alitaka amfahamu kupitia jarida hilo.
“Oh! Leo umechelewa kidogo na nakala ya mwisho nimemuuzia huyo dada mliyepishana.” Muuza magazeti alimwambia baada ya kufika na kukosa nakala kwenye meza zilizokuwa zikiuza jarida la Ngano Zetu.
“Mungu wangu!” Alijikuta akiponyokwa na hayo maneno huku akigeuza haraka na kwenda kumfuata mwanamke mmoja aliyepishana nae wakati akienda kwenye ubao wa magazeti.
“Samahani Dada!.” Alisema huku akimvuta bega mwanamke aliyekuwa mbele yake, mwanamama yule akageuka na kumtazama.
“Samahani kama nitakukera kwa ombi langu.” Alianza kuzungumza.
“Usijali, nakusikiliza.” Mwanamke aliyesimamishwa alimjibu.
“Naomba uniuzie hilo jarida uliloshika mkononi.” Alisema huku akitoa noti ya elfu tano na kuipunga hewani.
“Mh! Lakini si yapo kwenye meza za hawa wauzaji?” Yule mwanamke alimwambia huku akionekana kushangazwa na ombi lile.
“Yaani meza zote hazina nakala na bahati mbaya ni kwamba,hapa mjini jarida hilo linauzwa hapa tu.” Alimwambia huku bado akiwa ameshika pesa mkononi mwake.
“Hapana mdogo wangu, siuzi. Siwezi kukosa simulizi ya ukurasa wa tisa.” Yule mwanamke alimwambia kwa kumaanisha.
“Tafadhali sana, naomba uniuzie kwa pesa yote hii.” Alimwambia huku akiwa anamwonesha ile elfu tano iliyokuwa mkononi mwake.
“Hapana! Yaani ulivyo na shida na uhondo huo na mimi nina shida mara nyingi zaidi yako.” Mwanamama alimkatalia.
Jane alivuta mkoba wake na kuufungua, akiingiza mkono na kutoka na noti ya elfu kumi na kuipunga hewani.
“Nalinunua kwa hii pesa.” Alisema huku akimuonesha ile elfu kumi.
Wahenga walisema, pesa maua, pesa sabuni ya roho, mwanamke yule aliishia kujiumauma huku akinyoosha mkono na kuipokea ile pesa na kuliacha jarida la Ngano Zetu likiwa mali halali ya Bi. Jane Mgale.
“Ahsante sana, ubarikiwe kwa msaada huu ulionipa. Kuipata nakala hii kwangu ni zaidi ya pesa niliyokupa.” Jane aliongea wakati akiagana na yule mwanamke, akageuza na kukamata barabara kuelekea stendi ya daladala ili kurejea nyumbani kwake maeneo ya Msalato.
NA: BAHATI K MWAMBA
SIMU: 0758573660/0658564341
Sehemu moja maarufu ndani ya jiji la Dodoma kulikuwa na kundi kubwa la watu pembezoni mwa barabara wakiwa wamesimama kimakundimakundi. Watu hao walikuwa wamesimama kwa kuzizunguka baadhi ya meza za kuuzia magazeti zilizoko maeneo hayo maarufu kwa jina la Nyereresquare. Licha ya eneo hilo kuwa linapokea idadi kubwa ya watu kuanzia majira ya ahsubuhi hadi jua lizamapo, lakini ni aghalabu kukuta watu wengi wakiwa mbele ya mabango ya meza za wauza magazeti na vitabu zilizoko sehemu hiyo. Kwa siku za karibuni lile jambo lilianza kuzoeleka miongoni mwa watu waliokuwa wakipita au kuingia ndani ya viwanja vya Nyereresquare.
Miongoni mwa watu waliokuwa wakiwahi ahsubuhi na kuzunguka meza ya mmoja wa muuza magazeti, alikuwa ni Jane Mgale, Mama mwenye watoto wenye umri wa kuzidiana miaka miwili huku mkubwa akiwa na umri wa miaka minne na mdogo miaka miwili. Mama huyu ambae umri wake ulikuwa chini ya miaka ishirini na sita, alijikuta akiwa mtumwa wa kuamka kila jumatano na ijumaa ahsubuhi kwa lengo la kuwahi kununua moja ya jarida lililoanza kujichukulia umaarufu hapa nchini, huku likiwa na siku chache tangu kuanzishwa kwake. Jane alikuwa na sababu mbili kubwa zilizomfanya awe anawahi ahsubuhi sana kwenda kununua jarida hilo, sababu moja wapo ikiwa ni mazingira aliyokuwa akitokea kutokuwa na muuza magazeti ambae alikuwa ni wakala wa lile jarida lililokuwa likimpa safari za lazima kila jumatano na ijumaa, lakini sababu kubwa zaidi ilikuwa ni kile kilichokuwa kikipatikana kwenye ukurasa wa tisa wa jarida la Ngano Zetu lililokuwa likichapishwa na kampuni ya Mwa'se'ma Publishers.
Ukurasa wa tisa wa jarida hilo kulichapishwa simulizi za kweli kutoka kwa watu mbalimbali, kurasa nyingine zilichapishwa riwaya kutoka kwa waandishi wenye uzoefu na wale wanaochipukia. Ngano zetu lilikuwa ni jarida lilijizolea umaarufu kwa muda mfupi tangu lilipoanzishwa, watu wengi walipenda kulinunua kwa sababu ya kusoma riwaya nzuri kutoka kwa waandishi mashuhuri nchini Tanzania, lakini wengi wao walivutiwa na simulizi za kweli zilizokuwa zikichapishwa ukurasa wa tisa, zilikuwa ni simulizi zenye visa na mikasa mizito walizowahi kukutana nazo baadhi ya watu mashuhuri na wasio mashuhuri ilimaradi, walipata nafasi ya kusimulia waliyowahi kuyapitia kwenye maisha yao. Licha ya ukweli kwamba watu walisoma na kuvutiwa sana na mikasa ya ukurasa huo, lakini wakati huo kulikuwa na simulizi nzuri sana iliyokuwa ikivuta hisia za watu wengi sana hata wale ambao hawakuwa wapenzi wa usomaji, walijikuta wakivutiwa na jarida lile hasa ule ukurasa wa tisa hadi kumi na moja, walivutiwa na kisa cha mwandishi Bahati Kisarwa Mwamba ambae alipenda kuandika mikasa ya mhalifu Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku, pia alipenda kuandika visa vya jasusi Honda Makubi, Zedi Wimba na Obimbo Mtei.
Kilichowavutia watu kufuatilia mkasa wa mwandishi huyo si matukio aliyokutana nayo pekee bali pia ni kuwakutanisha wahusika anaopenda kuwatumia kwenye riwaya zake kuwa sehemu ya wasimuliaji. Zuki Gadu pamoja na jasusi Honda Makubi nao walijumuika nae kwenye simulizi ile ya kweli, wasomaji hawakuishia kusoma visa na mikasa yake kwenye jambo alilokuwa akilisimulia, walisoma pia mikasa ya watu waliokuwa wakizunguka nae kwenye mkasa wake huo wa kweli uliowahi kumkuta kwenye safari ya maisha yake. Wale waliokuwa wakisoma vitabu vyake na kuwafahamu wahusika hao ambao walidhani ni watu wa kufikirika, kupitia jarida lile walipata uhakika kuwepo Zuki Gadu halisi, Honda Makubi halisi na wengineo, lakini kubwa zaidi waligundua Bahati alikuwa na urafiki na watu hao. Kwa wasomaji hao kwao si burudani tu walioipata kwa kusoma mkasa wa mwandishi wampendae, bali walipata kuufahamu ukweli wa baadhi ya maswali waliojiuliza.
Tofauti na wasomaji wengine ambao walivutiwa na matukio ya kufurahisha na kusikitisha yaliyosimuliwa na wahusika, Jane Mgale alikuwa anafuatilia jambo kwenye mkasa ule, alifuatilia maisha halisi ya Bahati Mwamba aliyoyasimulia, maisha hayo ni mahusiano. Kwa nini? Kwa sababu alikuwa akimfahamu mwanaume huyo na alimfahamu kwa sababu ndiye baba wa watoto wake wawili aliokuwa akiwalea na ndiye aliyekuwa mume wake wa ndoa. Alifuatilia kila toleo jipya kwa sababu aliamini ataendelea kufahamu mengi ambayo hakuwa akiyafahamu kuhusu mume wake, mambo ambayo mume wake hakuwahi kumwambia hata kwa bahati mbaya ijapokuwa, hata kuhusu mkasa huo kuchapishwa gazetini aliyemwambia aufuatilie ni huyohuyo mumewe, bila shaka alitaka amfahamu kupitia jarida hilo.
“Oh! Leo umechelewa kidogo na nakala ya mwisho nimemuuzia huyo dada mliyepishana.” Muuza magazeti alimwambia baada ya kufika na kukosa nakala kwenye meza zilizokuwa zikiuza jarida la Ngano Zetu.
“Mungu wangu!” Alijikuta akiponyokwa na hayo maneno huku akigeuza haraka na kwenda kumfuata mwanamke mmoja aliyepishana nae wakati akienda kwenye ubao wa magazeti.
“Samahani Dada!.” Alisema huku akimvuta bega mwanamke aliyekuwa mbele yake, mwanamama yule akageuka na kumtazama.
“Samahani kama nitakukera kwa ombi langu.” Alianza kuzungumza.
“Usijali, nakusikiliza.” Mwanamke aliyesimamishwa alimjibu.
“Naomba uniuzie hilo jarida uliloshika mkononi.” Alisema huku akitoa noti ya elfu tano na kuipunga hewani.
“Mh! Lakini si yapo kwenye meza za hawa wauzaji?” Yule mwanamke alimwambia huku akionekana kushangazwa na ombi lile.
“Yaani meza zote hazina nakala na bahati mbaya ni kwamba,hapa mjini jarida hilo linauzwa hapa tu.” Alimwambia huku bado akiwa ameshika pesa mkononi mwake.
“Hapana mdogo wangu, siuzi. Siwezi kukosa simulizi ya ukurasa wa tisa.” Yule mwanamke alimwambia kwa kumaanisha.
“Tafadhali sana, naomba uniuzie kwa pesa yote hii.” Alimwambia huku akiwa anamwonesha ile elfu tano iliyokuwa mkononi mwake.
“Hapana! Yaani ulivyo na shida na uhondo huo na mimi nina shida mara nyingi zaidi yako.” Mwanamama alimkatalia.
Jane alivuta mkoba wake na kuufungua, akiingiza mkono na kutoka na noti ya elfu kumi na kuipunga hewani.
“Nalinunua kwa hii pesa.” Alisema huku akimuonesha ile elfu kumi.
Wahenga walisema, pesa maua, pesa sabuni ya roho, mwanamke yule aliishia kujiumauma huku akinyoosha mkono na kuipokea ile pesa na kuliacha jarida la Ngano Zetu likiwa mali halali ya Bi. Jane Mgale.
“Ahsante sana, ubarikiwe kwa msaada huu ulionipa. Kuipata nakala hii kwangu ni zaidi ya pesa niliyokupa.” Jane aliongea wakati akiagana na yule mwanamke, akageuza na kukamata barabara kuelekea stendi ya daladala ili kurejea nyumbani kwake maeneo ya Msalato.