RIWAYA: Sitaisahau Facebook

RIWAYA: Sitaisahau Facebook

Aise! inatia huzuni sana, poleni kwa visa vinavyo wakuta akina isabela
 
amina mabata unapenda sana hadith mpk kule kwengin nakuona jamn.
 
Umeanza, subira gani Excel?

Mie hata sijui chochote, ngoja nisubiri kujua jina halisi la isabella na wazazi wake, Au nidokeze basi kama unawafahamu

sio subira kweli?

mama yake halisi unamjua?

anaitwaaaa.... hebu ngoja!
 
Last edited by a moderator:
Umeanza, subira gani Excel?

Mie hata sijui chochote, ngoja nisubiri kujua jina halisi la isabella na wazazi wake, Au nidokeze basi kama unawafahamu

kumbe hukunielewa ram? isabella anaitwa subira kwa jina lake la asili.. trust me!

Mama yake halisi ni kichaa! huyu mwalimu nchimbi alipewa mtoto wa wizi bila yeye kujua coz mwanae alikufa wakati wa kujifungua enzi hizooo!

we ngoja uone... mi natabiri hayo kabisa!
 
kumbe hukunielewa ram? isabella anaitwa subira kwa jina lake la asili.. trust me!

Mama yake halisi ni kichaa! huyu mwalimu nchimbi alipewa mtoto wa wizi bila yeye kujua coz mwanae alikufa wakati wa kujifungua enzi hizooo!

we ngoja uone... mi natabiri hayo kabisa!

Aisee! Sasa kama mama yake ni kichaa majanga yanayomuandama subira a.k.a Isabella yataishaje sasa
 
kumbe hukunielewa ram? isabella anaitwa subira kwa jina lake la asili.. trust me!

Mama yake halisi ni kichaa! huyu mwalimu nchimbi alipewa mtoto wa wizi bila yeye kujua coz mwanae alikufa wakati wa kujifungua enzi hizooo!

we ngoja uone... mi natabiri hayo kabisa!

Hahahahah....huu utabiri kiboko...unatabiri ambayo yamekwisha kutokea....!!
 
Baada ya salamu mbili tatu. Moja kwa moja ikawa zamu ya yule nesi kumueleza mwenzake juu ya tukio la miaka zaidi ya ishirini iliyopita.
Kama ilivyokuwawakati tunamueleza na yeye alileta ujanja wa kutaka kumruka mwenzakelakini alipothibitishiwa kuwa akileta udanganyifu yupo shahidi napolisi pia. Naye akanywea!
"Tunachohitajikujua ni kitu kimoja tu!! Mama aliyeibiwa mtoto ni nani."Nilikoroma kwa hasira. Suzi na mama wakawa wakimya.
"Ni Dina….Dinayule….."
"Dina ni nani naanakaa wapi."
"Dina nikichaa…eeh! Mungu nisamehe mimi nisamehe…" alianza kulia yulemwanamke." Hakuna aliyembembeleza.
Neno lake la kuwaDina ni kichaa liliniacha njia panda, ina maana mama yangu ni kichaana anaitwa Dina? Hapana haiwezi kuwa!!! Nilipinga kimya kimya.

ENDELEA


Baada ya kutulia tena akatueleza juu ya kichaa aliyepewa mimba miaka mingi iliyopita.Mimba iliyotaka kuchukua uhai wake kwa sababu ya kukosa matunzo.Ilikuwa kama bahati diwani wa kata hiyo ambaye alikuwa mwanamkealipata kukutana na kichaa huyu. Wakati huo mimba ilikuwa na miezisaba. Huruma ilimshika kutoka na na imani yake ya kiroho.."

"Ooh!! Jesus Christ!!" Suzi alinong'ona huku akiwa kama anasali.
Akaendelea yulemama. "Basi akafika mwenyewe hospitali na kutoa amri ya mwanamke yule kusaidiwa. Hatua za haraka zikachukuliwa. Mwanamke akaanzakukamatwa kinguvu na kupelekwa kliniki. Baadaye akafungiwa kabisabila kutoka hospitali. Hatimaye miezi tisa ikatimia akajifungua bila kufanyiwa upasuaji. Mtoto wa kike!!!!
Wakati anajifungua mtoto huyu ndipo ilipatikana biashara hii ya kuiba mtoto. Hakika hali ilikuwa ngumu sana kiuchumi. Utawala wa serikali ya awamu ya kwanza ulikuwa umechachamaa sana hivyo kwa pesa tuliyotangaziwa na yule kijana ambaye simkumbuki jina mimi na mwenzangu hatukuweza kuikataa.
Pia tuliamini kuwa yule kichaa asingeweza kumlea mtoto wake. Hivyo kwa huruma tukamchukua yule mtoto na kumuuza."
Simulizi ile ilinisisimua sana!! Nilikuwa natetemeka kwa kila neno alilotamka yule mwanamama. Nilijihisi kama nusu mwanadamu nusu nimekufa!!
Kimya kikatanda.Kila mmoja akiwaza lake. Mimi nikizidi kuamini maneno ya mzee yule wa Iringa. Kuwa lile halikuwa jina langu na wala haukuwa ukoo wangu.
"Mama yangu yupowapi?" hatimaye niliuliza.
"Kwa kweli ni sikuya nne hivi sijamuona lakini huwa anapatikana stendi na majalalani."Nikasisimka tena kusikia maneno haya. Mama yangu anaishimajalalani!!!
Niliumia.


Hapakuwa na jipya tena kwa pale. Kwa kuwa huyu mama alikuwa anamtambua Dina ilimlazimu kuzunguka nasi siku nzima kumtafuta.
Siku ya kwanza hatukufanikiwa kumuona.
Siku ya pili majira ya mchana baada ya kuzunguka siku nzima bado kimya. Tukapewa taarifa za juu juu kuwa aliingia katika gari la kwenda Mbeya.
Huo ukawa mwanzo wa safari nyingine.
"Tulimshusha Uyole." Kondakta alitueleza baada ya kufanikiwa kulipata lile gari alilosadikiwa kupanda mama yangu.
Wakati huu nilikuwa mimi na mama pamoja na yule mkunga. Dada Suzi alirejea nyumbani kwaajili ya kulea mtoto ambaye sasa kilio kilikuwa kinapungua na kidogoalikuwa ananyonya.


Safari ya kwenda Mbeya ikafuata. Tukaweka kituo Uyole. Kama vile chokoraa tulianza kuzurura huku na huko bila mafanikio. Yule mkunga ndiye aliyekuwa anaulizia mara kwa mara maana ni yeye alikuwa anaujua muonekano wahuyo Dina.
Siku mbili Uyolebila mafanikio. Mama alikuwa amechoka dhahiri lakini asingewezakusema, nadhani kwa kuwa aliamini nipo katika matatizo pia ni kamamwanaye wa kumzaa, maana hata titi lake nilikuwa nimenyonya.
Siku ya nne inakujahabari nyingine kuwa Dina alionekana sokoni. Asubuhi na mapema tukafunga safari kuelekea Uyole sokoni.
Tulisubiri kwa masaakadhaa.
Kelele za akina mama zilitushtua, walikuwa wanahangaika huku na huko kutaka kushuhudiajambo huku wengine wakiwa wanakimbia.
"Yule pale Dina!!"mkunga alipiga kelele huku akituelekeza kwa kidole.
Mwanamke mnene,akiwa na malapulapu mwilini alikuwa akiwaponda watoto na mawe. Hukuakiwa na fimbo mkononi. Alikuwa anajongea eneo la soko. Jambo hiloliliwapagawisha akina mama na sasa walikuwa wanapiga kelele.
Nilimtazama mwanamkehuyu anayesadikiwa kuwa ni mama yangu. Mara ghafla nikajikuta nipowima, nikakimbia mbio mbio. Umati ulikuwa unashangaa na hata mwalimuNchimbi alibaki kunitazama tu asijue la kufanya.
Macho yetuyalipogongana nikaona kitu!!
Ni kama kioo mbeleyangu na nilikuwa najitazama.
Damu nzito kulikomaji!!!
Sikuogopa mawealiyoshikilia wala mavazi yake machafu!!
Nikamsogelea na kumkumbatia.
Maajabu!! Na yeyeakanikumbatia huku akizungumza kikabila nisichoelewa. Kimya kikuukikatawala!!
Hakunaaliyetusogelea.
"Mama!!"nilinyanyua kinywa changu na kumuita!!
"Su…Subira….."aliniita kwa mshangao.
Alipotaja jina hilonikajikuta kama nasukumwa chini. Nikaanguka kama mzigo.
Nikajikuta katika filamu ya ajabu huku mimi nikiwa wa ajabu zaidi.
Nilikuwa napambanana mamia ya watu. Na sasa nilikuwa ana kwa ana na Dokta Davis.Alikuwa ananiogopa sana, nami sikuwa na huruma. Nikiwa na panga kubwamkononi. Nilimkaribia na kumfyeka.
Nikatazama maaduiwengine wanaonikabili na wao nikawatenda nilichomtenda Davis.
Likafuata pambanokuu la kupambana na joka la maajabu.
Lilinisumbua lakinikila liliponijeruhi na mimi niliondoka na kipande kimoja cha mwiliwake.
Pambano lilikuwakali hadi walipotokea viumbe weupe sana wakaniweka kando kishawakalimaliza joka.
Kisha wakakiteketezakijiji kile cha maajabu. Lakini cha kushangaza mimi sikuungua kabisa.
Moto ulipokwishanikajikuta nimesimama peke yangu. Uchi wa mnyama. Nilikuwa nimechokana nilikuwa natokwa jasho.
Ule ujasiriniliokuwanao ukayoyoma na sasa nikawa naogopa.
Maraghafla…"Mamaaaaaa!!" nikapiga kelele kubwa na kutaka kukimbia.
Nilipojaribu kufanyahivyo nikakabiliana na kamba ngumu zikiwa zimeifunga mikono yangu namiguu. Nilikuwa natokwa jasho sana.
Niliangaza huku nakule bila kupata majibu.
Mara kundi la watulikafika pale chumbani.
Wote walikuwawakinishangaa. Nikamuona mwalimu Nchimbi.
"Mama ni ninihiki…mbona nimefungwa hivi?" Niliuliza huku nikiwa nashangaa.
Mwanaume mmojanisiyemtambua akaanza kunielezea juu ya vurugu nilizokuwa nafanyalicha ya kupigwa sindano ya usingizi.
"Ni ugonjwa wakushangaza sana."
Alinielezea tukiozima la kuanguka baada ya kukumbatiana na kichaa ambaye alitoweka piabaada ya mimi kuanguka.
"Mama yangu!!"niliwaza!! Kisha nikatabasamu na akili ikiwa imerejea sawia.
Nilipofunguliwakamba niliwaelezea juu ya yote yaliyokuwa yananikabili katika maonoyangu ya ajabu.
"Nimeikamilishakazi!!!" hatimaye nilitamka hayo.
Tulikuwa hospitaliya mkoa wa Mbeya. Baada ya siku nne niliruhusiwa kuondoka.Niliambatana na mwalimu Nchimbi.
"Naitwa Subira!!"nilimweleza mama.
"Najua!!"aliniambia, nikashangaa.
"Umejuaje."
"Ulisisitiza sana wakati ukiwa umepoteza fahamu zako."
Nilitabasamu nayeakatabasamu.


*******


Mtoto wa dada Suzi alikuwa halii tena japo mkono wake ulibaki kuwa vile umejikunja.
Amani ikautawalamoyo wangu!!!
Taarifa pekeeiliyoniumiza ni juu ya kifo cha mama yule kichaa aliyekufa baada yakugongwa na gari.
Japo nilipata nafasiya kusikia neno moja tu kutoka kwake lakini alikuwa amenisaidia mengimno.
Familia yanguilimzika kwa heshima zote kama ndugu.


Baada ya kuyawekahaya yote pembeni niliirejesha akili yangu jijini Mwanza.
Mama alikopa pesa nikasafiri kurejea chuoni.
Safari ilikuwa njemasana.
Maria akawa mwenyeji wangu jijini Mwanza. Akanielezea juu ya yote yaliyotokea. Hapakuwa na lolote baya, zaidi ya maajabu ya kanisa fulani kudai limemtoa Johnmsukule kutoka gamboshi.
Nilitabasamu na kukiri kuwa dini imegeuka biashara. Lakini sikumwelezea Maria juu yayote tuliyoyapitia.
"Jesca na Jenipherje?" nilimuulizia na kutegemea jibu la maajabu tena.
"Kumbe mwenzangu na wao hawakufa..eti vilizikwa vinu badala ya watu!! Dunia ina mambo." Alijibu.
"Kwa hiyo badowapo chuo."
"Hapana hawapo kwasasa. Lakini Jesca yupo mtaani.'
"Ama kweli duniaina mambo…" nilimuunga mkono.
Maria hakujua lolote lile kuhusu yaliyonisibu mimi. Na alikuwa kama anayenifahamisha juu ya yaliyotokea huku akiamini kuwa ile ruhusa niliyoomba ndioiliyonifanya nitoweke ghafla.
"mwenzangu na mimisiku moja sijui nikaota madudu gani. Wacha nipagawe.." Maria alinisimulia alichokiota na kilikuwa sawa na kilke kichotutokeamsituni.
Maria hakujua kamani kweli alikuja kule msituni!!!
"Nilipiga kelelewewe nikamuita Mungu, mama na mizimu yote!!" aliendelea kusimulia.
Baada ya mazungumzohayo marefu. Niliingia kuoga.
Baada ya kuoganikiwa katika kutafuta nguo ya kubadilisha nikakutana na kadi yabenki. Nikaitazama huku nikiweka mbali kabisa tamaa.
Nilipokuwa nimebadilisha nguo, nikaanzisha moto mdogo nyuma ya nyumba na kuviteketeza baadhi ya vitu ambavyo nilihisi vitakuwa vinanikumbusha juu ya Dokta Davis. Nilitaka kuiteketeza kadi ya benki pia lakininikakumbuka kuwa ilikuwa pia kwa ajili ya matumizi ya chuoni.Nikaghairi zoezi hilo.
******
Baada ya wiki mojanikapata fursa ya kukutana na John!! Nilikutana naye akiwa anaelekeakanisani.
"Bwana asifiwe dada..Bela." alinisalimia huku akionekana kutokumbuka lolote.
Nikamjibu,tukabadilishana naye mawili matatu. Akaenda zake huku akinisihi kuwa akitoka kanisani atanitafuta.


Niliondoka pale nikiwa natabasamu na kujipongeza kwa vita ile kuu ambayo nimeibukakuwa mshindi. Vita ambayo nimepoteza kipande kidogo tu cha nyama yangu lakini kwa ukombozi wa mamia ya watu..kutoka katika milki ya Shetani na chapa yake ya 666.
Japo sikutaka tenakurejea katika mtandao huo lakini nilikiri kwa kila neno la lugha ninayoifahamu kuwa kamwe SITAISAHAU facebook.





HADITHI NYINGINE ZAEMMY J.



HARUFU YA KIFO
YATIMA
MWALIMU NCHIMBI


M W I S H O


148



culbby mlyn Analyse princetx slim5 MUSSOLIN ram Angelicious showtie Ngoami amina mabata Moderator binti kiziwi Nicas Mtei korinoSukula aniceth mzahula Khantwe kelcie Meljons
 
Waaawo jaman asante casuist! Hakika nmeenjoy na hadithi hii nzur! Hongera sana
 
kumbe hukunielewa ram? isabella anaitwa subira kwa jina lake la asili.. trust me!

Mama yake halisi ni kichaa! huyu mwalimu nchimbi alipewa mtoto wa wizi bila yeye kujua coz mwanae alikufa wakati wa kujifungua enzi hizooo!

we ngoja uone... mi natabiri hayo kabisa!

Hongera..
 
Back
Top Bottom