Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

Hapo ndo wanapopapenda Asee!!
Yaani wanapata wasaa wa kushikana shikana au kunyonyana kiukweli then wakishapashana kinachofuata baada ya shooting..... Ai mamaa nakufa
Heheee wanapelekana juu motoooo konki fireee ai mama nakufaa mwisho wa siku wote wanakua kama amba rutty
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA HAMSINI NA SITA.

ENDELEA..................

Sarah aliendelea kutembea mwendo wa wastani mpaka akapotea machoni kwa Vin.

Baada ya dakika mbili za Sarah kupotea, Trigger alitokea na kumkuta Vin akiwa ameganda na bastola yake ikiwa mkononi, na pembeni yake alikuwepo Harry akiwa amekufa,

"umemaliza kazi tayari" Trigger aliongea huku akiumulika mwili wa Harry,

"Alafu alishaanza kuwa teja, huoni bomba la sindano hilo" Trigger aliendelea kuongea baada ya kuona bomba la sindano ambalo Sarah alitumia kujitoa damu. Muda wote ambao Trigger alikuwa akiongea Vin alikuwa kimya tu.

"huyu Harry ambaye alikuwa hapendi hata harufu ya sigara leo hii anajidunga Unga?" Trigger aliongea huku akinyanyua mguu wake kwa minajili ya kutaka kukanyaga lile bomba la sindano, ila kabla mguu wake haujafikia lile bomba, Vin alimsukuma Trigger na kumfanya apepesuke huku akirudi nyuma,

"hilo bomba amelileta Sarah, lina damu yake" Vin aliongea huku akiinama kuliokota lile bomba la sindano,

"ina maana Sarah alikuwepo hapa?" Trigger aliuliza kwa mshangao,

"na yeye ndiye aliyemuua Harry" Vin alijibu,

"sasa hiyo damu ya nini?" Trigger aliuliza,

"Sarah anadai yeye ni ndugu yangu, ameniachia hiyo damu ili nikaipime nihakikishe kuwa yeye ni dada yangu" Vin aliongea na kumfanya Trigger apate wasiwasi,

"usimsikilize, anakuchezea tu akili" Trigger aliongea kwa kujiamini,

"inawezekana, ebu tuondoke eneo hili" Vin aliongea huku akianza kupiga hatua,

"Mkuu si ulitupe tu hilo bomba la sindano, sasa unaenda nalo wapi?" Trigger alimwambia Vin,

"hakuna sababu ya kulitupa, ni muhimu pia kusikiliza malalamiko ya adui yako, unaweza kuyatumia kumuangamiza" Vin alijibu huku akiliweka lile bomba la sindano kwenye mfuko wa koti lake la suti,

"huyu Sarah anataka kuleta vita nyingine hapa" Trigger aliongea kwa sauti ndogo ambayo haikumfikia Vin,

"Sasa Vin akijua Sarah ni ndugu yake, wabaya si tutakuwa mimi na Taita?" Trigger alijiuliza huku nae akipiga hatua kuelekea upande alipoelekea Vin.

***************

Tukio la kufa kwa Harry wakati linatokea Aisha alikuwa jirani kabisa, alikuwa umbali wa mita mia mbili huku heaefone zikiwa masikioni mwake, alikuwa anasikia kila kitu kilichokuwa kinaongelewa kati ya Vin, Sarah na Harry.

Aisha kutokana na kumfuatilia Harry kwa muda kidogo ndio akafanikiwa kujua eneo analolala Harry na akatega vinasa sauti hivyo ili ajue Harry anakaa na nani?

Na siku hiyo Aisha ndio alipanga siku ya kwenda kummaliza Harry, ila wakati amefika na kutazama mazingira ndipo alipomuona Sarah akielekea eneo hilo, ikambidi asubiri aone Sarah anakwenda kwa lengo gani, ndipo pia baadae akamuona Vin pia akielekea usawa huo, hapo ndipo alipoamua atulie na kusikiliza ni kipi kitafuata.

Alisikia yote mpaka tukio la Harry kupigwa risasi na Sarah. Na mwisho akamuona Sarah akitoka na kuelekea kwenye gari yake, Aisha akatoka mafichoni na kwenda kwenye kugonga kwenye kioo cha gari ya Sarah, Sarah akashtuka na kushusha kioo,

"fungua mlango bibie, acha uoga" Aisha aliongea huku akitabasamu,

"kwanini nikuogope?" Sarah aliuliza huku akimfungulia mlango wa gari Aisha, Aisha akaingia na kukaa,

"ondoa gari" Aisha aliongea,

"unaelekea wapi?" Sarah aliuliza huku akiwa bado hajaondoa gari,

"twende popote tu, utaniacha mbele hapo" Aisha aliongea na kisha Sarah akawasha gari na kuliondoa,

"ulikuwa unanifuatilia?" Sarah aliuliza,

"hapana, nilikuwa namfuatilia Harry, ila nashukuru kwa kazi uliyoifanya to kumuua" Aisha aliongea na kutabasamu,

"kwanini ushukuru?" Sarah aliuliza,

"kwa maana hata mimi nilikuwa na mipango huo wa kumuua leo, ila wewe umeifanya hiyo kazi" Aisha aliongea,

"sawa, si unaweza kushukia hapa, maana ninapoenda sitopenda upajue" Sarah aliongea huku akiwa anaegesha gari ili Aisha ashuke,

"nina ombi moja" Aisha aliongea,

"sema" Sarah aliongea,

"nilikuwa nasikiliza maongezi yenu kupitia vinasa sauti, nimegundua kuwa ulifanyiwa unyama mkubwa sana na Taita, pia nikafikiria kuwa kwa namna moja au nyingine wewe peke yako huwezi kupambana na huyo Taita" Aisha aliongea na kumeza mate,

"kwa hiyo wamekutuma kunitisha?" Sarah aliuliza kwa jeuri,

"hapana, ninachotaka ni kukusaidia kumaliza machungu yako" Aisha aliongea,

"sihitaji msaada, nilianza mwenyewe na nitamaliza mwenyewe" Sarah alijibu,

"kumaliza huwezi, kwenye utata ni kwa huyo mdogo wako aitwae Vin, yule ameshamezeshwa chuki dhidi yako na Taita anajua kabisa huwezi kumuua Vin, ila Vin ndiye atakayekuua wewe" Aisha aliongea na kufanya Sarah amtazame,

"siwezi kumuua eee? Sawa ngoja muone, nimemuacha mara mbili, kama wamekutuma waambie waendelee kuhesabu" Sarah aliongea na kutabasamu,

"hawajanituma na wala sina uhusiano nao, ni ubinadamu tu ndio umenisukuma kukusaidia" Aisha aliongea,

"ubinadamu? Kwa hiyo ubinadamu unafanya unisaidie kuua binadamu wenzako?" Sarah aliuliza,

"kwani wewe unaeua sio binadamu?" Aisha aliuliza,

"Sarah sio mtu, Sarah ni mnyama au malaika, sihishi kwa malengo, naishi kwa maarifa ya kulipa kisasi, nikishaimaliza kulipa kisasi, naweza kufa kwa amani kwa maana sitokuwa na deni" Sarah alijibu,

"sawa, endelea na mambo yako" Aisha aliongea na kufungua mlango,

"sawa, na wewe endelea na ya kwako" Sarah alijibu na wakati huo Aisha alikuwa anatelemka kwenye gari, kisha akafunga mlango na Sarah akaiondoa gari yake.

"watu wengine wendawazimu kweli, baada ya kugeukana ndio aje kutaka kunisaidia?" Sarah aliongea huku akikanyaga mafuta ya gari na kufanya gari iongeze mwendo.

***************

Vin na Trigger walipotoka eneo ambalo alifia Harry, wakaelekea moja kwa moja kwenye gari, Trigger ndio alikuwa dereva, akawasha gari na kuiondoa. Kipindi chote hicho Vin alikuwa na mawazo,

"nikurudushe hotelini au unaenda hospitali kumuona mzee?" Trigger aliuliza,

"nipeleke hospitali" Vin aliongea,

"vipi, unaumwa?" Trigger aliuliza,

"fanya kama nilivyokuagiza" Vin aliongea na kumfanya Trigger akae kimya.

Trigger aliendesha gari mpaka nje ya hospitali moja ya kisasa, kisha akasimamisha gari na vin akashuka, Trigger nae akaamua ashuke.

Vin alielekea moja kwa moja mpaka eneo la mapokezi na akaomba aonane na Daktari, akaelekezwa mahala ofisi ya daktari ilipo, akaingia na kumuacha Trigger eneo la mapokezi akimsubiri.

Harry akaingia katika chumba cha Dokta na kumkuta mwanaume wa makamo akiwa amevaa koti jeupe na mbele yake kulikuwa na kibao kilichomtambulisha kama daktari.

Vin akakaa kwenye kiti na kumsalimia Dokta.

"nahitaji kupima DNA" Vin aliongea,

"kwa ajili ya kutaka kujua nini?" Dokta aliuliza kwa utulivu,

"kuna mtu anadai mimi ni ndugu yake, kwa hiyo nataka kuthibitisha Kama ni kweli" Vin aliongea,

"hapo itabidi tuwapime damu, huyo mtu yupo wapi?" Dokta aliuliza,

"sijaja naye" Vin alijibu,

"basi itakubidi kesho uje naye ili tuwatoe damu kwa pamoja" Dokta aliongea,

"ila damu yake ninayo hapa, aliitoa mbele ya macho yangu" Vin aliongea huku akiingiza mkono kwenye mfuko wa koti lake la suti na kutoa bomba la sindano lenye damu ya Sarah na kumpa daktari,

"kama hivyo ni sawa, je wewe upo tayari kutolewa damu yako muda huu?" Daktari aliuliza,

"Mimi nipo tayari" Vin alijibu, kisha daktari akavuta karatasi iliyokuwepo juu ya meza na kuandika maelezo kadhaa likiwemo jina la Vin.

"chukua hii karatasi uende maabara" Daktari aliongea huku akimpa Vin karatasi,

"maabara ipo kwa wapi?" Vin aliuliza,

"ukifika mapokezi utauliza" Daktari aliongea na kisha Vin akachukua bomba la sindano lenye damu ya Sarah na kutoka nalo mpaka eneo la mapokezi,

"maabara ipo upande upi?" Vin alimuuliza dada aliyekuwepo hapo,

"nyoosha na hii korido mpaka mwisho mlango wa kushoto" Dada wa mapokezi alijibu na kisha Vin akaelekea maabara, alipofika uko aliwapa ile karatasi aliyopewa na Daktari na kisha wakamtoa damu.

"urudi kesho saa kumi jioni" mtu wa maabara alimwambia Vin,

"nikija nije huku moja kwa moja?" Vin aliuliza,

"hapana, utaenda kwa daktari uliyempa maelezo" Mtu wa maabara aliongea na kisha Vin akatoka zake mpaka eneo la maabara na kumtaka Trigger waondoke.

Wakatoka mpaka nje na kuingia kwenye gari,

"nipeleke hotelini" Vin aliongea,

"ila mzee anaweza kuruhusiwa leo, kwa nini tusiende wote hospitali?" Trigger aliuliza,

"nipeleke hotelini" Vin aliongea kwa msisitizo na Trigger hakutaka kuongea tena, aliamua kufuata maelezo ya Vin.

Njia nzima ukimya ulitawala, hakuna aliyemuongelesha mwenzake, wakati Vin aliwaza utata wa undugu baina yake na Sarah, na kipindi hicho hicho Trigger alihisi Vin ameanza kugundua kitu kuhusu undugu Sarah.

Trigger alifika Vin hotel na kuegesha gari kwa nje na kisha Vin akafungua mlango na kutelemka,

"mzee akikuulizia nimwambiaje?" Trigger alimuuliza Vin,

"mwambie sijisikii vizuri, nimepumzika" Vin alijibu,

"sawa" Trigger alijibu huku akijiandaa kuondoa gari, Vin akageuka haraka,

"usimwambie kama tumekutana na Sarah" Vin akamwambia Trigger,

"kwanini?" Trigger akauliza,

"nitamwambia mwenyewe kesho" Vin alijibu,

"na kuhusu kifo cha Harry?" Trigger aliuliza,

"unaweza kumwambia, ila epuka kumtaja Sarah" Vin aliongea na kuondoka zake.

****************

Sarah alivyomshusha Aisha aliendelea kuendesha gari lake kwa mwendo wa kasi, alikuwa akielekea kwenye makazi yake mapya ambayo hayakuwa mbali sana na mjini, aliamua kununua nyumba nyingine na kuhamia uko kwa ajili ya kuwakwepa watu wanaopafahamu kwake hasa polisi. Alikuwa hataki usumbufu wa aina yoyote. Na uko kwenye makazi mapya alikuwa akihishi na dokta Pendo na babu yake.

Sarah alifika mpaka kwenye hiyo nyumba yake mpya na kufungua geti, akaingiza gari, kisha akashuka na kwenda kufunga geti.

Akazunguka nyumba yake kwa lengo la kukagua, hakuona kitu chochote cha hatari, alipomaliza kukagua akaamua aingie ndani, akafungua mlango wa sebuleni na kuingia ndani, alipotupa macho kwenye makochi akashuhudia Dokta Pendo na babu yake wakiwa wamefungwa kamba mikononi na miguuni na mdomoni waliwekwa plasta ya kuzuia kupiga kelele. Sarah akiwa akajiuliza ni nani aliyefanya hivyo, akahisi kitu cha baridi kikigusa shingo yake, kwa kuwa ni mtaalam akagundua hiyo ni bastola na pia akajiuliza huyo mtu ni nani?

"hutakiwi kugeuka nyuma" Sauti nzito ya kiume iliongea na kufanya Sarah kutoitambua sauti hiyo, kwa maana hakuwahi kuisikia hata mara moja,

"wewe nani?" Sarah aliuliza kwa ujeuri ili kumuadaa na ikiwezekana amuotee kwa pigo, ila mtu badala ya kujibu, alimpiga Sarah kofi zito la shingoni,

"na ukiendelea kuuliza bila ruhusa, utaumia zaidi" Mtu yule aliongea na kumfanya Sarah agundue huyo mtu hakuwa akifanya utani..............

**********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA HAMSINI NA SABA.

ENDELEA..................

"kakae pale kwenye kochi uungane na wenzako" Sauti ile iliongea kwa mamlaka na kumfanya Sarah akakae na hapo akaweza kuiona vizuri sura ya yule mtu aliyemteka, alikuwa ni Strategic,

"kumbe Sarah mwenyewe ndio wewe, mbona hufanani na unyama unaoufanya?" Strategic aliuliza lakini Sarah hakujibu, strategic akatoa simu na kubonyeza namba anayoijua yeye, kisha akaiweka simu sikioni na kuisikiliza wakati ikiita,

"hoya Vin, nimefanikiwa kumteka Sarah, vipi nimmalize?" Strategic aliuliza,

"ooh, hapana, muache" Vin alitoa kauli iliyomshangaza Strategic,

"kwanini nimuache mkuu?" Strategic aliuliza kwa mshangao?

"nitakuja kukueleza, wewe muache tu, na usimdhuru" Vin aliongea,

"sawa mkuu" Strategic alijibu na kukata simu, kisha akamtupia jicho Sarah na kumuangalia kwa dakika kadhaa,

"bahati yako, tutakutana siku nyingine" Strategic aliongea na kisha akaelekea kwenye mlango na kuufungua kisha akaondoka.

Baada ya Strategic kuondoka, Sarah alivuta bastola yake na kutoka mbio mpaka nje, hakukuta mtu,

"mpuuzi huyu" Sarah aliongea kwa hasira huku akirudi ndani. Alipofika ndani aliwafungua kamba Dokta Pendo na babu yake,

"muda gani aliingia hapa?" Sarah aliuliza wakati akimaliza kumfungua kamba Dokta Pendo,

"kama nusu saa hivi iliyopita" Babu yake alijibu,

"amepajuaje hapa?" Sarah aliuliza lakini hakuna aliyejibu kwa maana hakuna aliyejua.

"hii ni hatari Sarah, yaani wamepajua mpaka hapa?" Babu yake Sarah aliuliza huku akisikitika,

"itabidi tuhame na hapa, tuhamie hotelini sasa" Sarah aliongea huku akikaa kwenye kochi,

"hakuna sababu ya kuhama, sasa tutahama hama mpaka lini?" Dokta Pendo aliuliza,

"tunahitaji kuwa sehemu salama, kwa kuwa hawa manyang'au wameshajua tunapoishi, wanaweza kuja kutushambulia" Sarah aliongea,

"kama angekua na lengo la kutuua angetumaliza mapema tu, ila mbona amekuachia?" Dokta Pendo aliuliza,

"Vin itakuwa ameanza kuelewa kitu kati yangu na yeye, ila isiwe sababu ya kujiamini kiasi cha kuwa huru muda wote, itabidi tukiwa ndani mlango yote ya geti ifungwe" Sarah aliongea kwa utulivu,

"mama nadhani ungeachana nao tu, watakumaliza hawa" Babu yake Sarah aliongea,

"hilo haliwezekani, hata nikiachana nao bado wao hawatoachana na mimi, watataka tu kuniua au kuwaua watu wote mlio upande wangu" Sarah alijibu,

"shoga pambana, maji umeshayavulia nguo" Dokta Pendo aliongea kwa ya upole,

"usimshauri mwenzako ujinga, je akifa utajisikiaje?" Babu yake Sarah aliuliza kwa ukali,

"je wakati wewe unamchongea kwa polisi ulikuwa unajisikiaje?" Dokta Pendo aliuliza huku akinyanyuka na kuanza kutembea kwa mwendo wa taratibu kuelekea chumbani na kumuacha Sarah akitabasamu,

"usimsikilize maneno yake huyo mwenzako, hana nia nzuri na wewe" Babu yake Sarah alimwambia Sarah,

"Mimi namsikiliza shoga yangu, nampenda kwa maana amenisaidia mambo mengi" Sarah aliongea kwa utani huku akielekea chumbani akicheka,

"mabaradhuli nyie, ukifa shauri yako" Babu aliongea kwa hasira huku akimtazama Sarah anavyoondoka.

**********************

Sajenti Minja alihisi kuchanganyikiwa, na kilichomchanganya Sajenti Minja ni kupotea kwa ghafla kwa Sarah huku akiwa na Dokta Pendo. Sajenti Minja akili yake ikamtuma aende uwanja wa ndege kwenda kukagua watu waliokwenda nje ya nchi ndani ya wiki hii, aliamini huenda Sarah ametoroka nchini baada ya kufanya mauaji ya familia ya Harry.

Sajenti Minja alichukua gari na kwenda moja kwa moja mpaka uwanja wa ndege, alipofika haikuwa rahisi kukubaliwa kufanya kazi yake, ilimbidi ampigie simu waziri wa wizara husika na kumueleza lengo lake, kisha waziri akapiga simu uwanja wa ndege na kuwaamuru wamuache Sajenti Minja afanye kazi yake.

"nenda kwenye chumba namba saba, uko ndipo kuna orodha yote" Mfanyakazi Mmoja alimuelekeza Sajenti Minja huku akimpatia kibali ambacho kilimtambulisha Sajenti Minja kama mtu maalum na aachwe afanye kazi yake.

Sajenti Minja alielekea moja kwa moja mpaka chumba kilichokuwa na mlango uliochorwa namba saba na kisha akabonyeza kengele iliyokuwepo hapo mlangoni, na mlango ukafunguliwa na msichana, Sajenti Minja akamsalimu na kisha akamuonesha kile kibali, akaruhusiwa kuingia ndani na kukuta watu kama watano wakiwa bize na computer, kila mtu alikuwa na computer yake.

Sajenti Minja akawasalimia, kuna waliotikia na wengine walikuwa bize kubonyeza computer zao.

"samahani jamani, mimi ni askari, nimekuja kuangalia orodha ya watu waliotoka nje ya nchi ndani ya wiki hii" Sajenti Minja aliongea kwa sauti tulivu na kufanya watu wote wamuangalie,

"ni wengi sana bro, au labda ueleze shida yako ni ipi hasa?" Kijana mmoja mtanashati alimuuliza Sajenti Minja,

"kuna mtu anatafutwa na serikali, sasa nataka kujua kama yupo ndani ya nchi au ametoroka?" Sajenti Minja aliuliza,

"una kibali cha kuruhusiwa kufanya ukaguzi ndani ya ofisi hii?" Yule kijana akamtupia swali jingine Sajenti Minja,

"anacho, waoneshe" Dada aliyemfungulia mlango Sajenti Minja alijibu huku akimtazama Sajenti Minja na kufanya Sajenti Minja awaoneshe kile kibali alichopewa,

"tupe jina lake tafadhali" Yule kijana aliongea,

"Sarah Isack" Sajenti Minja aliongea huku akiandika jina la Sarah kwenye karatasi na kisha yule kijana akaliingiza lile jina kwenye computer yake na kubonyeza sehemu iliyoandikwa "search", baada ya muda jina la Sarah likatokea kwenye computer ya yule kijana,

"bro, huyo mtu jina lake limeaonekana kwa mara ya mwisho mwaka mmoja uliopita, tena imeonesha alikuwa akiingia kama mtalii kutoka nchini uingereza" Yule kijana alimpa maelezo Sajenti Minja,

"hakuna sehemu iliyoonesha akitoka?" Sajenti Minja aliuliza,

"ipo, ila imeonesha alitokaga miaka ishirini iliyopita na amerudi mwaka uliopita" Kijana alijibu,

"na sehemu ya kutoka imeonesha ametoka kwenda wapi, na ametoka kwenda wapi na kufanya nini?" Sajenti Minja aliuliza,

"imeonesha alitoka kwenda uingereza, na alienda kwa ajili ya masomo" Kijana alijibu,

"dah, hii report yenu hapa ni ya abiria wa uwanja huu tu au ni report ya viwanja vyote?" Sajenti Minja aliuliza,

.

.
"ni ya viwanja vyote vya Tanzania" Yule kijana alijibu,

"sawa, asante kwa ushirikiano wako" Sajenti Minja aliongea huku akianza kuondoka,

"au bro kwa kukushauri, ni bora ukaangalie na vituo vya mabasi, huenda ametumia njia ya mabasi kusafiri mpaka Kenya, alafu akifika Kenya ndio achukue ndege" Kijana aliongea huku akimtazama Sajenti Minja,

"nashukuru, ngoja nikafanye hivyo" Sajenti Minja alijibu, ila kiukweli aliona hiyo njia ni ngumu sana kuitumia kwa kuwa stand ya mabasi haina utaratibu maalum wa kukata tickets na kuifadhi kumbukumbu.

Sajenti Minja alirudi mpaka sehemu alipochukulia kibali, akakirudisha na kisha akashukuru. Akatoka zake mpaka nje ya eneo la uwanja wa ndege na kisha akaingia kwenye gari lake.

Wakati akiwa anajiandaa kuwasha gari yake, simu yake iliita na kupokea,

"Minja anaongea" Sajenti Minja aliongea,

"tumeokota mwili ukiwa na majeraha ya risasi" Mtu wa upande wa pili aliongea,

"mmemtambua?" Sajenti Minja aliuliza,

"tumemtambua kupitia kitambulisho chake" Mtu wa upande wa pili alijibu,

"sawa, mpelekeni hospitali na mruhusu uchunguzi ufanyike, mimi nakuja" Sajenti Minja aliongea na kukata simu, kisha akaondoa gari.

***************

Trigger alifika hospitali na kumkuta Taita akiwa amekaa kitandani,

"Vin yupo wapi?" Taita aliuliza,

"anadai hajisikii vizuri, amerudi hotelini kupumzika" Trigger alijibu,

"na mmefanikisha kumuona Harry?" Taita aliuliza,

"tutaongea baadae, je kuna habari mpya?" Trigger aliuliza,

"mpya sina, ila cha muhimu ni kwamba nimeruhusiwa" Taita aliongea,

"kwa hiyo tunaondoka?" Trigger aliuliza,

"ndio, ebu nisaidie kusimama" Taita aliongea huku akisimama na Trigger aksmsaidia kwa kumshika mkono na kisha wakaelekea mpaka nje, wakaingia kwenye gari na kisha Trigger akawasha gari na kuondoka.

Walifika nyumbani kwa Taita na kisha Taita akafikia kukaa kwenye kochi,

"mzee, Harry ameuawa" Trigger aliongea baada ya Taita kukaa,

"ameuawa au mmemuua?" Taita aliuliza,

"Sarah ndio amemuua" Trigger alijibu,

"umejuaje kama Sarah amemuua?" Taita aliuliza,

"wakati Sarah akimuua Harry, Vin alikuwepo na yeye ndiye aliyemuona" Trigger alijibu,

"sasa kwanini Vin hakumuua Sarah?" Taita aliuliza,

"kuna kitu cha ajabu sana kimetokea, Sarah anamuaminisha Vin kuwa yeye ni dada yake, na leo ametoa damu na kumpa Vin akaipime ili ahakikisha" Trigger aliongea na kumfanya Taita ashtuke,

"na vin ameamini?" Taita aliuliza,

"itakuwa, maana alipitia hospitali na kwenda kuacha damu ya Sarah" Trigger aliongea,

"hii hatari, itabidi uende hiyo hospitali ukasimamishe huo mpango" Taita aliongea,

"kwa njia gani?" Trigger aliuliza,

"kaongee na Dokta akupe hayo majibu" Taita aliongea,

"na akikataa?" Trigger aliuliza,

"ua" Taita alijibu,

"sawa mkuu, hiyo kazi itafanyika kesho" Trigger alijibu.

***************

Siku iliyofuata Vin alipata wazo jipya, aliona ni bora amtume Strategic aende maeneo ya hospitali kuimalisha ulinzi mpaka mida ya saa kumi ambao ni muda Vin alitakiwa kufika kuchukua majibu.

Vin alifanya hivyo kwa maana alihisi huenda Sarah anaweza kufika eneo la hospital na kumteka Dokta na kumshurutisha aandike majibu ya uongo ya DNA, bado Vin hakuwa na imani na Sarah.

Strategic alifika eneo la hospital kuimarisha ulinzi, hakuwa akimjua Dokta muhusika, ila alichoenda kufanya ni kumuwinda Sarah endapo atakuja eneo hilo.

Muda ulizidi kwenda tu, ilipofika saa kumi, strategic alimshuhudia Trigger akifika eneo lile, strategic akataka kushuka ila akaamua auchune tu ndani ya gari, akatoa simu na kumpigia Vin,

"nimemuona Trigger eneo hili" Strategic aliongea,

"amekuja kufanya nini?" Vin aliuliza,

"sijui kwa kweli" Strategic alijibu,

"amekuona?" Vin aliuliza,

"hapana" Strategic alijibu,

"endelea kukaa hapo na ufuatilie amefuata nini?" Vin aliongea baada ya kuhisi huenda Trigger ameenda kwa ajili ya kuchunguza ni kipi Vin alikifuata siku iliyopita,

"sawa mkuu" Strategic alijibu.

Huko ndani Trigger alipitiliza mpaka ndani kwa Dokta na kumkuta akiwa anajiandaa kuondoka, akamsalimu,

"Dokta nimetumwa nifuate majibu ya damu" Trigger aliongea,

"na nani?" Dokta aliuliza,

"mdogo wangu alikuja jana hapa na bomba la sindano lililokuwa na damu" Trigger aliongea na kumfanya Dokta amkumbuke Vin,

"sasa kijana, hapa haturuhusiwi kumpa mtu majibu ya mwingine, ni vyema angekuja mwenyewe" Dokta aliongea huku akipekua pekua karatasi juu ya meza yake,

"kwa hiyo haiwezekani?" Trigger aliuliza,

"hiyo haiwezekani" Dokta alijibu na kisha Trigger akaondoka kwa hasira.

Baada ya Trigger kuondoka, Dokta alipekua zile karatasi mezani na kuchukua karatasi moja ambayo ilikuwa na majibu ya DNA ya Vin, akaitia kwenye bahasha ya njano.

Trigger alitoka na kusimama mlangoni, akili yake ikamtuma arudi ndani ya ofisi ya daktari. Trigger akageuka na kusukuma mlango, akaingia,

"nipe majibu niliyotumwa, vinginevyo amani itapotea" Trigger aliongea huku akiichomoa bastola yake na kumuelekezea Dokta, Dokta akapata mshtuko na kujikuta akiichomoa bahasha moja ya njano na kumpatia Trigger, Trigger akafungua na kusoma maelezo ya juu katika karatasi, alikuta kumeandikwa " DNA TEST" na chini ya hayo maneno kulikuwa na jina la Vin na Sarah.

Trigger akaitudishia ile karatasi ndani ya bahasha na kisha akamtupia jicho Dokta,

"Trigger akikuoneshea bastola uwa haishushi chini mpaka itoe risasi" Trigger aliongea huku akitabasamu na kumfanya Dokta macho yamtoke,

"unamaanisha nini?" Dokta aliuliza kwa hofu, ila Trigger hakujibu, badala yake alimfyatulia Dokta risasi mbili na kisha Dokta akaanguka chini. Trigger akafungua mlango na kutoka zake kimya kimya na bahasha mkononi utasema hajatoka kufanya tukio la kinyama........

**********ITAENDELEA************

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom