SIMULIZI........ PENZI CHUNGU - SIMULIZI........ PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY
SEHEMU YA 16
Banda alikuwa anamsogelea Suto taratibu pale chini.
Tayari kwa kubaka.
Tayari kwa kuuwa.
Banda alimkaribia Suto kabisa. Kwa kutumia mkono wake wa kulia alimziba Suto mdomo na pua kwa nguvu, na mkono wake wa kushoto aliishika sketi aliyoivaa Suto.
Suto alipata mstuko mkubwa sana, mstuko uliomuamsha toka usingizini. Sasa alikuwa anafurukuta kwa kukosa pumzi, bila kutoa sauti yoyote. Banda alikuwa mlevi mahiri, lakini alikuwa na mabaki ya nguvu katika mwili wake.
Alimbana Suto kisawasawa!
Suto alijaribu kuutoa mkono wa banda bila mafanikio. Sasa aliamua kufanya kitu. Na yeye aliamua kumkaba Banda ili ajiokoe katika kisanga kile. Alimshika banda shingoni kwa mikono yote miwili, Ilikuwa patashika ya kimya kimya ndani ya selo, sketi ya Suto Sutani ikiwa imeshuka nusu, hadi magotini.
Mizizi ya chuki moyoni kwa Suto ilikuwa imeshaanza kutamalaki, chuki na ulimwengu, chuki na walimwengu, chuki ambayo ilizidisha hasira zake, chuki ambayo ilimpa nguvu Suto ambazo hakuwa nazo kabla, Suto alipata nguvu za ghafla, kwa kutumia dole gumba lake alianza kulibinya koromea refu la Banda.
Ilikuwa ni picha mbaya sana kuangalia.
Macho ya Banda yalikuwa yametoka nje, mithili ya kijusi kabanwa na mlango.
Suto alimbinya Banda kwa nguvu zake zote zilizobakia.
Kule getini wale maaskari wawili, wenye roho mbaya walikuwa wanasubiri taarifa ya furaha kwao, taarifa ya kifo cha Suto Sutani.
Walikaa robo saa, ilikuwa kimya, Banda alikuwa hajarudi , ndipo Beji alikwenda kule selo, akitegemea Banda itakuwa kashatekeleza kazi waliyomtuma.
Alijidanganya.
Suto sasa alibadirishwa na mazingira , Suto alianza kuwa katili taratibu, mazingira yakiwa ndio mwalimu wa ukatili wa Suto Sutani, na sasa alikuwa amefuzu.
Beji alifungua geti la selo aliyowekwa Suto. Alimulka kwa tochi yake ndogo, iliyotoa mwanga hafifu, alichokikuta ndani ya selo, kilimuacha mdomo wazi.
Alikuta mwili wa Banda ukiwa umelala chini, huku Suto akiwa amesimama wima, jasho linamtoka !
"Umefanya nini Suto?" Beji aliuliza kwa sauti ndogo.
"Nimemuuwa jamaa yenu" Suto alisema bila wasiwasi wowote.
"Suto!" Beji alisema akiwa na uwoga mkubwa sana.
Beji aliingiwa na wasiwasi, maana endapo Banda itakuwa amefia ndani ya gereza, wao walikuwa na chakujibu kuwa ameingia vipi ndani ya gereza, na wao ndio walikuwa zamu usiku ule ?
Alisogea pale ulipo mwili wa Banda na kumwangalia mapigo yake ya moyo.
*************
Huko nje, maisha yaliwaendea vizuri sana baba Bruno, mama Bruno, Manka na Bruno. Walikuwa wanaishi kwa furaha sana, huku wote wakiwa wamesahau kabisa habari kuhusu Suto.
Baada ya kutoka gerezani siku ile mama Suto alienda kwa kina Bruno, ila alijibiwa majibu ya kejeri, dharau na kebehi, toka kwa Bruno na mama yake. Mama Suto aliondoka kichwa chini. Aliumia sana moyoni, lakini angefanya nini?
Beji aligusa kifuani kwa Banda, alisikia mapigo ya moyo kwa mbali. Ishara kwa Banda alikuwa hajafariki bado. Beji alishusha pumzi ndefu..
Beji alirudi mbio mpaka getini. Akamuekeza Zura kila kitu kilichotokea, kwa kushirikiana na Zura walimtoa Banda kwa usiri mkubwa sana.
Banda hakufanikiwa kubaka wala kuuwa.
Banda alifanikiwa kukabwa na Suto Sutani mpaka kuzimia.
Suto Sutani, alielewa kwamba zile zilikuwa ni njama za Beji na Zura, sasa alikuwa makini zaidi. Alielewa kwamba askari wale walikuwa na nia mbaya sana na yeye.
Upelelezi wa kesi ya mauaji ikiyomkabiri Suto uliendelea. Inspekta wa kike, Jasmine, ndiye alipewa jukumu la kuipeleleza kesi ile.
Inspekta Jasmine alikuwa askari hodari sana katika jeshi la Polisi, jasiri na mtu anayetumia akili nyingi sana katika kuvumbua sababu za vifo vya kutatanisha. Taifa lilikuwa linamtegemea sana,hasa katika kipindi kama hiki ambacho mpelelezi namba moja Tanzania, Daniel Mwaseba, alikuwa mapumzikoni nchini Ujerumani. Baada ya kufanya kazi kubwa sana ya kuwakamata maadui wa nchi yetu waliokuwa na Mpango wa Siri. Inspekta Jasmine sasa aliingia kazini mzima mzima, akidhani hii ni kesi rahisi sana, laiti angejua atakayokutana nayo......
ITAENDELEA