mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,135
- 276
SIMULIZI.......PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY
SEHEMU YA 3
Suto Sutani, hakuwa na sura inayopendeza sana machoni mwa watu, hakuwa na mwili unaovutia sana. Lakini Suto alikuwa na upekee na ubora wake. Suto alikuwa na tabia nzuri kwa kila mtu, Suto alikuwa na nidhamu, alikuwa na heshima. Kwa ujumla Suto alikuwa na sifa zote za mwanamke anayepaswa kuitwa mke. Lakini wanaume wengi hawakulijua hilo. Wao walikuwa wanaamini mwanamke ni yule mwenye sura nzuri pekee, yule mwenye umbo zuri sana. Wanaume wengi walikuwa na fikra kama walizonazo baba na mama Bruno. Wao walikuwa wanaamini katika elimu, walikuwa wanaamini katika uzuri, walikosea sana, na wanaume wengi wanaendelea kukosea mpaka leo.
"Bruno unataka kumuoa Suto ?" Mama Bruno aliuliza kama katoka usingizini vile.
" Namaanisha mama !"
" Nipe sababu moja inayokufanya utake kumuoa Suto ?"
"Tabia"
" Sijakuelewa Bruno"
" Suto ana tabia nzuri mama"
"Hoja zako hazijitoshelezi Bruno ! " baba yake alisema kwa jazba.
Bruno alikaa kimya.
"Mimi ni nani yako ? "
"Baba "
"Mimi ni nani yako ?"
"Mama"
Sasa tunasema hivi, huwezi kumuoa Suto hata tukiwa tumekufa !"
"Nipeni sababu moja ya kunizuia kutomuuoa Suto?"
"Siyo chaguo letu" Wote walijibu kwa pamoja.
" Mnataka kunambia mke bora ni chaguo lenu tu, chagua langu Mimi siyo mke bora ?"
"Elimu yako ya sheria isikuvuruge Bruno, wewe ni wathamani, lazima upate mke wa thamani pia... "
"Kama Suto Sutani ! " Bruno alimalizia.
"Karogwaaa huyuuu nakwambia ! " Mama Bruno alipiga kelele kali.
"Ndio nimerogwa, nimerogwa na tabia nzuri ya Suto mama "
"Tabia ipi hasa ?" Mama Bruno aliuliza.
"Hana wanaume huyu, ametulia mama "
"Hahaha, wewe hujui sababu ya Suto kutokuwa na mwanaume ?"
"Najua "
" Ni nini ?"
"Msimamo wake thabiti, wa kutotaka kuchezewa na wanaume waongo ! "
" Bruno unapotea, sura ya Suto ndio sababu" Mama Bruno alisema.
Bruno alikuwa jasiri, hakuwa anampenda kabisa Suto kabla, lakini sasa alimpenda Suto ghafla. Ni kweli Suto hakuwa na mwanaume, ni kweli Suto alikuwa na heshima na nidhamu kubwa sana, lakini kwanini Bruno ameviona leo ? Tena ghafla ?
"Niliapa sitompenda mwanaume katika maisha yangu, nilijengwa hivyo na baba yangu mzazi, baba alimtesa sana mama yangu, alinitekeleza na mimi, alinikataa ningali mtoto mdogo sana. Kwa sababu nisizozielewa mpaka leo.
Labda sipendezi kweli machoni mwenu, lakini kwani mimi nimejiumba ?
Ngoja niwaambie kitu, kosa kubwa wanaolifanya Wanaume wengi, mnaenda kulifanya na ninyi. Ukitaka mwanamke angalia sura, lakini ukitaka mke angalia tabia "
Suto alijieleza kwa kirefu.
Sasa Bruno alipata nguvu mpya.
" Mama na baba, wote mna elimu kubwa sana, lakini kwa hili mnazidiwa busara na Suto ? "
"Unatutukana sasa ! " Baba Bruno alisema kwa hasira huku amekunja ndita.
" Siwatukani wazazi wangu, nawaambia ukweli, hivi inamaana hamjui kama uzuri wa mwanamke ni tabia ? "
" Hatutaki maelezo, sisi tunasema haumuoi Suto !" Walijibu kwa pamoja.
"Namuoa ! " Bruno alijibu kwa nguvu.
"Atanioa ! " Suto nae alipigilia msumari .
Sasa yalikuwa maigizo hasa. Kila mmoja jasho linamtoka. Wote wamekunja ndita.
Wazazi hawataki.
Watoto wanataka.
ITAENDELEA KESHO
Kwa maoni zaidi
0757 633010/0714526379
MWANDISHI..HALFANI SUDY
SEHEMU YA 3
Suto Sutani, hakuwa na sura inayopendeza sana machoni mwa watu, hakuwa na mwili unaovutia sana. Lakini Suto alikuwa na upekee na ubora wake. Suto alikuwa na tabia nzuri kwa kila mtu, Suto alikuwa na nidhamu, alikuwa na heshima. Kwa ujumla Suto alikuwa na sifa zote za mwanamke anayepaswa kuitwa mke. Lakini wanaume wengi hawakulijua hilo. Wao walikuwa wanaamini mwanamke ni yule mwenye sura nzuri pekee, yule mwenye umbo zuri sana. Wanaume wengi walikuwa na fikra kama walizonazo baba na mama Bruno. Wao walikuwa wanaamini katika elimu, walikuwa wanaamini katika uzuri, walikosea sana, na wanaume wengi wanaendelea kukosea mpaka leo.
"Bruno unataka kumuoa Suto ?" Mama Bruno aliuliza kama katoka usingizini vile.
" Namaanisha mama !"
" Nipe sababu moja inayokufanya utake kumuoa Suto ?"
"Tabia"
" Sijakuelewa Bruno"
" Suto ana tabia nzuri mama"
"Hoja zako hazijitoshelezi Bruno ! " baba yake alisema kwa jazba.
Bruno alikaa kimya.
"Mimi ni nani yako ? "
"Baba "
"Mimi ni nani yako ?"
"Mama"
Sasa tunasema hivi, huwezi kumuoa Suto hata tukiwa tumekufa !"
"Nipeni sababu moja ya kunizuia kutomuuoa Suto?"
"Siyo chaguo letu" Wote walijibu kwa pamoja.
" Mnataka kunambia mke bora ni chaguo lenu tu, chagua langu Mimi siyo mke bora ?"
"Elimu yako ya sheria isikuvuruge Bruno, wewe ni wathamani, lazima upate mke wa thamani pia... "
"Kama Suto Sutani ! " Bruno alimalizia.
"Karogwaaa huyuuu nakwambia ! " Mama Bruno alipiga kelele kali.
"Ndio nimerogwa, nimerogwa na tabia nzuri ya Suto mama "
"Tabia ipi hasa ?" Mama Bruno aliuliza.
"Hana wanaume huyu, ametulia mama "
"Hahaha, wewe hujui sababu ya Suto kutokuwa na mwanaume ?"
"Najua "
" Ni nini ?"
"Msimamo wake thabiti, wa kutotaka kuchezewa na wanaume waongo ! "
" Bruno unapotea, sura ya Suto ndio sababu" Mama Bruno alisema.
Bruno alikuwa jasiri, hakuwa anampenda kabisa Suto kabla, lakini sasa alimpenda Suto ghafla. Ni kweli Suto hakuwa na mwanaume, ni kweli Suto alikuwa na heshima na nidhamu kubwa sana, lakini kwanini Bruno ameviona leo ? Tena ghafla ?
"Niliapa sitompenda mwanaume katika maisha yangu, nilijengwa hivyo na baba yangu mzazi, baba alimtesa sana mama yangu, alinitekeleza na mimi, alinikataa ningali mtoto mdogo sana. Kwa sababu nisizozielewa mpaka leo.
Labda sipendezi kweli machoni mwenu, lakini kwani mimi nimejiumba ?
Ngoja niwaambie kitu, kosa kubwa wanaolifanya Wanaume wengi, mnaenda kulifanya na ninyi. Ukitaka mwanamke angalia sura, lakini ukitaka mke angalia tabia "
Suto alijieleza kwa kirefu.
Sasa Bruno alipata nguvu mpya.
" Mama na baba, wote mna elimu kubwa sana, lakini kwa hili mnazidiwa busara na Suto ? "
"Unatutukana sasa ! " Baba Bruno alisema kwa hasira huku amekunja ndita.
" Siwatukani wazazi wangu, nawaambia ukweli, hivi inamaana hamjui kama uzuri wa mwanamke ni tabia ? "
" Hatutaki maelezo, sisi tunasema haumuoi Suto !" Walijibu kwa pamoja.
"Namuoa ! " Bruno alijibu kwa nguvu.
"Atanioa ! " Suto nae alipigilia msumari .
Sasa yalikuwa maigizo hasa. Kila mmoja jasho linamtoka. Wote wamekunja ndita.
Wazazi hawataki.
Watoto wanataka.
ITAENDELEA KESHO
Kwa maoni zaidi
0757 633010/0714526379