Riwaya: Penzi chungu

Riwaya: Penzi chungu

mapengo junior

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2011
Posts
1,135
Reaction score
276
SIMULIZI.......PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY

SEHEMU YA 3

Suto Sutani, hakuwa na sura inayopendeza sana machoni mwa watu, hakuwa na mwili unaovutia sana. Lakini Suto alikuwa na upekee na ubora wake. Suto alikuwa na tabia nzuri kwa kila mtu, Suto alikuwa na nidhamu, alikuwa na heshima. Kwa ujumla Suto alikuwa na sifa zote za mwanamke anayepaswa kuitwa mke. Lakini wanaume wengi hawakulijua hilo. Wao walikuwa wanaamini mwanamke ni yule mwenye sura nzuri pekee, yule mwenye umbo zuri sana. Wanaume wengi walikuwa na fikra kama walizonazo baba na mama Bruno. Wao walikuwa wanaamini katika elimu, walikuwa wanaamini katika uzuri, walikosea sana, na wanaume wengi wanaendelea kukosea mpaka leo.

"Bruno unataka kumuoa Suto ?" Mama Bruno aliuliza kama katoka usingizini vile.
" Namaanisha mama !"
" Nipe sababu moja inayokufanya utake kumuoa Suto ?"
"Tabia"
" Sijakuelewa Bruno"
" Suto ana tabia nzuri mama"
"Hoja zako hazijitoshelezi Bruno ! " baba yake alisema kwa jazba.
Bruno alikaa kimya.
"Mimi ni nani yako ? "
"Baba "
"Mimi ni nani yako ?"
"Mama"
Sasa tunasema hivi, huwezi kumuoa Suto hata tukiwa tumekufa !"
"Nipeni sababu moja ya kunizuia kutomuuoa Suto?"
"Siyo chaguo letu" Wote walijibu kwa pamoja.
" Mnataka kunambia mke bora ni chaguo lenu tu, chagua langu Mimi siyo mke bora ?"
"Elimu yako ya sheria isikuvuruge Bruno, wewe ni wathamani, lazima upate mke wa thamani pia... "
"Kama Suto Sutani ! " Bruno alimalizia.
"Karogwaaa huyuuu nakwambia ! " Mama Bruno alipiga kelele kali.
"Ndio nimerogwa, nimerogwa na tabia nzuri ya Suto mama "
"Tabia ipi hasa ?" Mama Bruno aliuliza.
"Hana wanaume huyu, ametulia mama "
"Hahaha, wewe hujui sababu ya Suto kutokuwa na mwanaume ?"
"Najua "
" Ni nini ?"
"Msimamo wake thabiti, wa kutotaka kuchezewa na wanaume waongo ! "
" Bruno unapotea, sura ya Suto ndio sababu" Mama Bruno alisema.

Bruno alikuwa jasiri, hakuwa anampenda kabisa Suto kabla, lakini sasa alimpenda Suto ghafla. Ni kweli Suto hakuwa na mwanaume, ni kweli Suto alikuwa na heshima na nidhamu kubwa sana, lakini kwanini Bruno ameviona leo ? Tena ghafla ?

"Niliapa sitompenda mwanaume katika maisha yangu, nilijengwa hivyo na baba yangu mzazi, baba alimtesa sana mama yangu, alinitekeleza na mimi, alinikataa ningali mtoto mdogo sana. Kwa sababu nisizozielewa mpaka leo.
Labda sipendezi kweli machoni mwenu, lakini kwani mimi nimejiumba ?
Ngoja niwaambie kitu, kosa kubwa wanaolifanya Wanaume wengi, mnaenda kulifanya na ninyi. Ukitaka mwanamke angalia sura, lakini ukitaka mke angalia tabia "
Suto alijieleza kwa kirefu.

Sasa Bruno alipata nguvu mpya.
" Mama na baba, wote mna elimu kubwa sana, lakini kwa hili mnazidiwa busara na Suto ? "
"Unatutukana sasa ! " Baba Bruno alisema kwa hasira huku amekunja ndita.
" Siwatukani wazazi wangu, nawaambia ukweli, hivi inamaana hamjui kama uzuri wa mwanamke ni tabia ? "
" Hatutaki maelezo, sisi tunasema haumuoi Suto !" Walijibu kwa pamoja.
"Namuoa ! " Bruno alijibu kwa nguvu.
"Atanioa ! " Suto nae alipigilia msumari .

Sasa yalikuwa maigizo hasa. Kila mmoja jasho linamtoka. Wote wamekunja ndita.
Wazazi hawataki.
Watoto wanataka.

ITAENDELEA KESHO
Kwa maoni zaidi
0757 633010/0714526379
 
SIMULIZI.... PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY

SEHEMU YA 4

Wazazi hawataki .
Watoto wanataka.

"Nakupenda Suto "
"Nakupenda sana Bruno"
Baba na mama Bruno walisonya msonyo mrefu. Kwa ghadhabu, wote waliingia ndani.
Pale sebuleni walibaki wawili pekee.
"Sikuwahi kufikiria kama nitakupenda siku moja, sikufikiria kwa kuwa sikuwahi kuwa karibu na wewe, ukaribu wangu huu wa leo, umefanya uniingie moyoni Suto, sitojari dunia inasema nini , nitajari tu moyo wangu unasema nini, nitakupenda Suto, nitakupenda hata kama dunia mzima itanidharau Suto , kuanzia leo nakukabidhi moyo wangu, usiutese, usiunyanyase, naomba unipende Suto ." Bruno alisema kwa sauti ya upole na yenye hisia kali.
Suto hakujibu, majimaji mepesi yalikuwa yanachuruzika katika kifua chake .
Alikuwa analia.

Huo ndio ulikuwa mwanzo wa penzi hili lililokuja kuwa chungu. Penzi lililoanza kama utani, na kukomaa ghafla, penzi lililokuwa mfano, kati ya kijana mtanashati Bruno na msichana mwenye sura ya kawaida Suto.

Ndani ya nyumba sasa ilikuwa vita, vita kali kati ya Bruno na wazazi wake. Baba na mama yake walichukia sana mahusiano yake na Suto. Taratibu walijikuta hawaelewani na mtoto wao wa pekee Bruno. Ndani ya nyumba moja lakini wakawa hawasemeshani kabisa!

Mtaani ilikuwa ni hatari. Watu walimcheka na kumdharau Bruno. Kijana mtanashati kuzama katika dimbwi la mapenzi kwa Suto. Wengi walihisi karogwa. Penzi hili likazaa chuki nyingine kali kwa Suto. Watu walizidi kumchukia pale mtaani, wakiamini Suto mchawi, karoga ili apendwe na Bruno.

************

Manka Edward, alikuwa ni binti mrembo sana pale mtaani. Alikuwa msichana mrefu wastani, alikuwa mweupe mwenye umbo lililojazia kikike, chini alikuwa na mguu hasa. Mguu unaotoa ruhusa kuvaliwa kwa kimini chochote na binti huyo. Manka alikuwa anajua kuvaa. Tabata nzima hakuna msichana aliyekuwa anamfikia Manka kwa kuvaa nguo nzuri. Alikuwa mwanamke wa kisasa, mwenye kwenda na usasa.

Baada ya matatizo yale, mama Bruno alikuwa anafikiria namna ya kusitisha penzi la Suto na Bruno. Aliamua kutafuta binti pale mtaani ili awe na mwanawe. Ilimradi tu kuvunja penzi lile changa.
Alikaa sana sebuleni, akiwa kashika tama na kutafakari, kichwani mwake lilipita jina moja tu, jina la Manka. Aliamini uzuri wa Manka unaweza kuvunja penzi kati ya Bruno na Suto. Ikapitishwa ndani ya kichwa chake, Manka akawa suluhisho ndani ya kichwa chake.Aliamua kumtumia Manka kuwatenganisha Suto na Bruno. Muda uleule alinyanyuka sofani na kwenda nyumbani kwa Manka kumpa kazi ya kutenganisha penzi la mwanawe na Suto .

***********

Wakati mama Bruno akiwaza hayo na kufikia maamuzi hayo ya kumtumia Manka. Manka Edward alikuwa mbele ya kioo kikubwa chumbani kwake. Alikuwa anautazama mwili wake mzuri, anajitathmini na kujipa maksi mwenyewe.
Mara simu yake iliyokuwa kaitupa tu kitandani iliita.
Aliacha kujiangalia kwenye kioo, kwa mwendo wa madaha alielekea kitandani. Alikaa na kuichukua simu.
Akaipokea.
"Nambie janeth"
"Eeeh nipe huo umbea shoga "
"Unasema "
"Anatoka na Suto Sutani "
"Haiwezekani"
"Itakuwa karogwa, yaani kanikataa mimi mtoto mzuri kamchukua Suto ? Si bure nakwambia "
"Hawezi kumuoa, na sisi twende kwa mtaalamu "
"Sawa kesho"
Simu ikakatwa.

Manka alikuwa anaongea kwa mbwembwe na shoga yake. Lakini baada ya simu kukatwa aliingiwa na majonzi. Ukweli alikuwa anampenda sana Bruno, alitumia mbinu zake zote kumnasa bila mafanikio. Bruno alikuwa na msimamo imara. Siyo kwa Manka tu, hakuwa na msichana mtaani. Hakuwahi kuwa na msichana kabisa hapa duniani.
Manka alinyanyuka, alisogea pale mbele ya kioo chake kikubwa.
Alijiangalia.
Akaivua ile tshirt yake ya pinki.
Akavua ile suruali yake jeans ya bluu.
Juu alibaki na bra tu, nyeupe, chini alibaki na ........ nyeupe. Alianza kuitafuta kasoro katika mwili wake, hakuiona.
Aligeuka nyuma alijiangalia kwa kutumia kile kioo, hakuiona kasoro yoyote katika mwili ule mzuri.
Alikuwa mzuri.
Alikuwa kaumbika.
Alikitazama tena kioo, alijishangaa, alikuwa anatoa machozi....

ITAENDELEA....
 
SIMULIZI...PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY.

SEHEMU YA 5

Chozi lile lilitengeneza chuki mbaya sana, toka kwa Manka kwenda kwa Suto Sutani.

Manka alirudi kitandani, alikaa taratibu. Mawazo mengi yalipita katika kichwa chake. Ila moja lilipitishwa na kichwa chake.
Aliamua kuuwa !
Ndio, aliamua kumuua Suto Sutani.

Alisimama. Aliziangalia nguo zake pale chini. Alizikanyaga kwa miguu yake yote miwili. Alikunja ngumi kwa mkono wake wa kulia. Aliubana mdomo wake kwa meno, kwa hasira. Akawa anapiga ile ngumi kwa nguvu katika kiganja chake cha mkono wa kushoto.
Alipiga ngumi mara tano.
"Lazima nikuuwe Suto Shetani!" Alimpa Suto jina baya ili kuhalalisha dhamira yake mbaya.

Ghafla, mlango wa chumba chake uligongwa.
"Karibu " Alisema kwa sauti yenye mikwaruzo, bila shaka kutokana na hasira.
Mgeni aliingia, alikuwa ni mama Bruno.
Mama Bruno alivyomwangalia Manka alipigwa na butwaa. Manka naye alijiangalia. Akagundua kilichomshangaza mama Bruno, badala ya nguo kuzivaa, yeye alikuwa amezikanyaga.
lakini hakujari kabisa.

"Karibu mama "
"Mbona hivyo Manka ?"
"Suto "
"Suto kafanyaje tena ?"
"Shetani ! "
"Tena jini kabisa " mama Bruno alimalizia kwa hasira.

Baada ya Manka kutulia kidogo. Mama Bruno alimwambia lililompeka. Waligundua wote wana adui mmoja, Suto Sutani.

"We unataka tumfanyaje Suto ?"
" Mimi nataka aachane na mwanangu kabisa"
"Halafu ?"
"Bruno akuowe wewe"
"Ni ngumu sana"
"Kwanini Manka ?"
"Bruno hanitaki !"
"Yule mtoto karogwa haki ya Mungu !"
"La kufanya ni moja tu hapa"
"Lipi Manka ?"
"Kuuwa !"
"Unasema "
"Suto kwenda kuzimu ndio suluhisho pekee!"
"Siyo haki Manka "
"Kila kitu ni haki kwenye mapenzi na vita "
"Hivi unasema kweli Manka"
"Namaanisha "

Mama Bruno alichanganyikiwa. Pamoja na kumchukia sana Suto lakini hakutaka Suto auwawe.
Alikuwa muoga sana kuuwa.

"Nitamuua Suto kwa mkono huu!" Manka alimuonesha mama Bruno ule mkono alioukunja ngumi.
"Nakuomba usimuue Suto !"
"Toka nje mama "
"Manka unanifukuza"
"Kwanini hunielewi Dina" Manka alimwita mama Bruno kwa jina lake halisi.
"Sawa nakubaliana na wewe tumuue Suto '
" Karibu kwenye kochi Mama" Manka alibadirika ghafla.
Sasa walielewana.

**********
Wakati Manka na Mama Bruno wanapanga kumuua, Suto Sutani alikuwa anaosha vyombo nyumbani kwao. Alikuwa anaosha vyombo huku anaimba mashairi ya wimbo wa Rachel, kizunguzungu.
Mara mama yake alirejea kutoka sokoni. Alisikia sauti ya Suto ikiimba tangu yuko nje. Aliingia kimya kimya. Alimkuta Suto ameacha vyombo kabisa, akicheza mziki. Mwimbaji alikuwa yeye.
Mchezaji alikuwa yeye.
Kiuno cha Suto kilikuwa kazini tena.
Ama kweli mapenzi kizunguzungu.....

*****
Maoni kwenye namba ya mwandishi, Usicomment hapa please !
ITAENDELEA.....
 
SIMULIZI..... PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY

SEHEMU YA 6

"Naona una furaha sana mwanangu "
"Kawaida tu Mama "
"Siyo kawaida yako Suto, siku zote umekuwa mtu wa huzuni sana "
"Nimeamua kujikubari Mama, naamini furaha yangu ipo ndani yangu, nikisubiri watu wa nje waniletee furaha, nitakuwa mtu wa kulia siku zote "
"Naona umekuwa sasa Suto, umenifurahisha sana leo"
"Hahaha, mimi nimekuwa zamani sana Mama "

*********

Baba Bruno nae hakuupenda kabisa uhusiano wa Bruno na Suto. Aliona ni dharau kuwa na mkwe kama Suto.
Dharau kwa marafiki zake, dharau kwa wafanyakazi wenzake, dharau kwa ndugu zake.
Alikuwa amekaa ofisini kwake, akiwaza mbinu za kutenganisha penzi lile changa.
Bado alikuwa hajapata suluhisho. Nini afanye kuvunja uhusiano ule.

Mama Suto aliingia ndani akiwa na furaha sana.
Kabla hajatokea Bruno katika maisha yake, Suto alikuwa anapendwa na mtu mmoja tu Duniani, mama yake mzazi. Mama Suto hakumwacha Suto peke yake siku zote. Pamoja na watu wengi kutompenda Suto, lakini mama yake alimpenda sana.
Mara nyingi walikuwa wanalia pamoja Suto anaponyanyaswa. na kucheka pamoja Suto anapofurahi, kama hii leo.

Bruno alikuwa chuoni, alikuwa anasomea sheria katika Chuo kikuu cha Dar es salaam. Tangu asubuhi alivyoenda Chuo mpaka sasa alikuwa anawaza mustakabari wa mahusiano yake na wazazi wake. Aliona sio busara kugombana na wazazi. Akaamua baada ya vipindi awapigie simu wazazi wake, kuwaomba radhi. Lakini pamoja na kuomba radhi alipanga kupinga ushauri wowote utakaohusu kuachana na Suto.

Muda wa vipindi uliisha, Bruno alitoka nje ya darasa. Kabla hajawapigia wazazi wake, simu yake iliita.
Alikuwa Manka.

"Haloo Bruno "
"Nambie Manka"
"Uko wapi ?"
"Sema shida yako Manka"
"Naomba tuonane leo jioni"
" Samahani, sina muda"
"Hivi kwanini unanichukia Bruno kiasi hicho ?"Bruno hakujibu swali lile, nae aliuliza swali.
"Kwa nini umeweka 'loud speaker'....?"
Ghafla simu ikakatwa.

Simu ile alipiga Manka akiwa chumbani kwake na mama yake Bruno, Manka aliweka simu 'loud speaker' ili mama Bruno asikie majibu ya mwanae. Bila kutegemea Bruno aligundua kama simu ile imewekwa loud speaker.
Sasa wanawake wale wawili walikuwa wamehemewa. Wakishangaa Bruno kajuaje kama waliweka 'loud speaker'.

Bruno nae alibaki na maswali mengi.
" Kwanini Manka aweke 'loud speaker ?, na baada ya kumuuliza kwanini akate simu ghafla ? Kwa vyovyote vile, wakati Manka anapiga simu ile alikuwa na mtu, je mtu huyo ni nani ?"
Bruno alibaki na maswali bila ya majibu. Aliamua kumpigia simu Manka ili apate majibu ya maswali yake.
Bruno alipiga simu, mara ya kwanza simu iliita mpaka ikakatika, alipiga tena simu.

Kule chumbani kwa Manka, kulikuwa na mabishano, kati ya mama Bruno na Manka.
"Pokea sasa simu hiyo"
"Nitamwambia nini mama"
"We mwambie sikuweka 'loud speaker' tu "
Walibishana sana, hadi simu ikakatika. Baada ya muda mfupi, simu iliita tena
"Ngoja niwashe redio halafu nimwambie nipo kwenye kelele" Manka alitoa wazo.Hakusubiri kujibiwa.
Aliisogelea redio.
Akaiwasha.
Wimbo wa Ommy Dimpoz, Baadae, ulikuwa unarindima kwenye spika za redio ya Manka.

"Hallo" Bruno aliita.
"Nipo kwenye kelele nitakupigia baadae "
"Sawa "
Simu ikakatwa.

Bruno alitembea kama hatua kumi. Sasa alikumbuka wazo lake la kuwapigia simu wazazi wake, ili awaombe radhi. Alianza kumpigia mama yake.
Simu ikapokelewa.
"Hallo Mama "
"Nipo kwenye kelele nitakupigia baadae"
Simu ikakatwa .

Bruno kengele ya hatari iligonga kichwani kwake.
Aliyasikia maneno yaleyale.
Wimbo uleule.
Toka kwa watu wawili tofauti, alioongea nao muda mfupi sana.
Alivyompigia Manka alisikia vizuri wimbo ule.
"Baadae"
Na sasa kampigia Mama yake. Anausikia tena wimbo uleule.
Mbaya zaidi wote wameongea maneno yaleyale .
Kuna kitu.

ITAENDELEA....
 
SIMULIZI....PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY

SEHEMU YA 9

Kwa mwendo wake wa taratibu Suto alikuwa anaelekea mlangoni, kuufungua ule mlango.

Kule nje, Killer alikuwa nyuma ya Dungu kwa ukaribu wa kama hatua moja. Killer alinyanyua juu ule mkono wenye kisu kirefu kinachomeremeta gizani. Kwa kasi na nguvu kubwa akawa anaushusha shingoni kwa Dungu ule mkono wenye kisu!
Dungu alikuwa anaona kila kitu kwa jicho la pembeni. Kwa kasi naye aliinama, mkono wenye kisu wa Killer ulikosa kwa kupiga, ulipita hewani bila kumpata aliyemlenga.

Kule ndani, Suto alikuwa anaingiza funguo katika kitasa cha mlango. Aliona kuna ugumu kidogo.
Akalazimisha.
Kumbe kule nje Dungu aliacha funguo zake zikining'inia pale kitasani, ghafla zikadondika!
Mlango ukafunguka.

Baada ya kukwepa kile kisu, Dungu aligeuka nyuma, akiacha funguo zikining'inia pale kwenye kitasa.
Sasa Dungu na Killer walikuwa wanatazamana. Killer kashika kisu kwa mkono wake wa kulia, Huku Dungu kashika panga kwa mkono wake wa kushoto!

Suto alikuwa amesimama katikati ya mlango, akiwashuhudia wale majabali wawili wakitazamana. Suto alipigwa na butwaa, hakuweza kutoa sauti yoyote. Na wala hakutoa ishara yoyote.
Alitulia tuli.

Killer alirusha ngumi ya nguvu kwa mkono wake wa kushoto. Ngumi iliyompata Dungu shavuni. Dungu alinesa kidogo, akiwa kwenye ule mneso alirudi kwa nguvu na lile panga, panga lilitua shingoni kwa Killer barabara. Nusu ya panga liliingia pale shingoni, Dungu aliacha lile panga likining'inia shingoni kwa Killer.
Alikimbia mbio!

Suto Sutani, alikuwa kama kapigwa na ganzi pale mlangoni. Kwa mara ya kwanza katika maisha yake alishuhudia tukio la hatari. Suto alishuhudia binadamu akiwa anakufa huku akimwaga damu mithili ya bomba bovu la maji.
Ghafla, alipata kauli. Alipiga kelele kubwa sana.
Huku akilia kwa woga!
Huku akilia kwa hofu!

Ndani ya dakika tano, watu walikuwa wamejaa. Wenye silaha mbali mbali.
Walifika kwenye ile nyumba akiyokaa Suto Sutani.
Walipofika pale watu wote walipigwa na butwaa. Walikuta picha mbaya sana. Maiti ya mtu ikiwa imedondoka chini, na panga shingoni.

Suto alikuwa analia sana, kila anachoulizwa yeye analia. Mjumbe alipiga simu, kituo cha Polisi Tabata.
Baada ya robo saa polisi waliwasiri.
Polisi waliikagua nyumba yote kuangalia mazingira ya mauaji yale. Ndipo waliikuta miili mengine miwili.
Waliichukua.
Walimchukua na Suto Sutani. Yeye ndiye alikuwa mshtumiwa namba moja katika kesi ya mauaji yale!

Dungu alikimbia sana usiku ule. Alikuwa kama amechanganyikiwa.
Hakuelewa kabisa kimetokea nini?
Hakujua yule mtu ni nani?
Hakuelewa wenzake wake wapi?
Alipofika mbali na nyumba ya kina Suto alisimama, huku anahema, alitoa simu yake mfukoni. Alilitafuta jina la Manka na kumpigia.

"Halloo Bosi"
"Nambie Dungu, mmefanikiwa?"
"Hapana Bosi"
"Kwa nini"
'Mimi sielewi Bosi"
"Dungu! Mbona unanichanganya!"
"Misheni imefeli Manka"
"Kwanini?"
"Suto Sutani analindwa kumbe!"
"Analindwa ??!!"
"Ndio, sijui kama kina Zinja wako salama kweli"
"We uko wapi, nije tuongee maana hata sikuelewi"

Dungu alimuelekeza Manka alipo. Usiku wa manane Manka aliamka na kumfuata Dungu. Ajue kilichowasibu.
Mambo sasa yaliwaendea kombo. Tofauti na wakivyotarajia kabisa

ITAENDELEA KESHO
 
SIMULIZI....PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY

SEHEMU YA 9

Kwa mwendo wake wa taratibu Suto alikuwa anaelekea mlangoni, kuufungua ule mlango.

Kule nje, Killer alikuwa nyuma ya Dungu kwa ukaribu wa kama hatua moja. Killer alinyanyua juu ule mkono wenye kisu kirefu kinachomeremeta gizani. Kwa kasi na nguvu kubwa akawa anaushusha shingoni kwa Dungu ule mkono wenye kisu!
Dungu alikuwa anaona kila kitu kwa jicho la pembeni. Kwa kasi naye aliinama, mkono wenye kisu wa Killer ulikosa kwa kupiga, ulipita hewani bila kumpata aliyemlenga.

Kule ndani, Suto alikuwa anaingiza funguo katika kitasa cha mlango. Aliona kuna ugumu kidogo.
Akalazimisha.
Kumbe kule nje Dungu aliacha funguo zake zikining'inia pale kitasani, ghafla zikadondika!
Mlango ukafunguka.

Baada ya kukwepa kile kisu, Dungu aligeuka nyuma, akiacha funguo zikining'inia pale kwenye kitasa.
Sasa Dungu na Killer walikuwa wanatazamana. Killer kashika kisu kwa mkono wake wa kulia, Huku Dungu kashika panga kwa mkono wake wa kushoto!

Suto alikuwa amesimama katikati ya mlango, akiwashuhudia wale majabali wawili wakitazamana. Suto alipigwa na butwaa, hakuweza kutoa sauti yoyote. Na wala hakutoa ishara yoyote.
Alitulia tuli.

Killer alirusha ngumi ya nguvu kwa mkono wake wa kushoto. Ngumi iliyompata Dungu shavuni. Dungu alinesa kidogo, akiwa kwenye ule mneso alirudi kwa nguvu na lile panga, panga lilitua shingoni kwa Killer barabara. Nusu ya panga liliingia pale shingoni, Dungu aliacha lile panga likining'inia shingoni kwa Killer.
Alikimbia mbio!

Suto Sutani, alikuwa kama kapigwa na ganzi pale mlangoni. Kwa mara ya kwanza katika maisha yake alishuhudia tukio la hatari. Suto alishuhudia binadamu akiwa anakufa huku akimwaga damu mithili ya bomba bovu la maji.
Ghafla, alipata kauli. Alipiga kelele kubwa sana.
Huku akilia kwa woga!
Huku akilia kwa hofu!

Ndani ya dakika tano, watu walikuwa wamejaa. Wenye silaha mbali mbali.
Walifika kwenye ile nyumba akiyokaa Suto Sutani.
Walipofika pale watu wote walipigwa na butwaa. Walikuta picha mbaya sana. Maiti ya mtu ikiwa imedondoka chini, na panga shingoni.

Suto alikuwa analia sana, kila anachoulizwa yeye analia. Mjumbe alipiga simu, kituo cha Polisi Tabata.
Baada ya robo saa polisi waliwasiri.
Polisi waliikagua nyumba yote kuangalia mazingira ya mauaji yale. Ndipo waliikuta miili mengine miwili.
Waliichukua.
Walimchukua na Suto Sutani. Yeye ndiye alikuwa mshtumiwa namba moja katika kesi ya mauaji yale!

Dungu alikimbia sana usiku ule. Alikuwa kama amechanganyikiwa.
Hakuelewa kabisa kimetokea nini?
Hakujua yule mtu ni nani?
Hakuelewa wenzake wake wapi?
Alipofika mbali na nyumba ya kina Suto alisimama, huku anahema, alitoa simu yake mfukoni. Alilitafuta jina la Manka na kumpigia.

"Halloo Bosi"
"Nambie Dungu, mmefanikiwa?"
"Hapana Bosi"
"Kwa nini"
'Mimi sielewi Bosi"
"Dungu! Mbona unanichanganya!"
"Misheni imefeli Manka"
"Kwanini?"
"Suto Sutani analindwa kumbe!"
"Analindwa ??!!"
"Ndio, sijui kama kina Zinja wako salama kweli"
"We uko wapi, nije tuongee maana hata sikuelewi"

Dungu alimuelekeza Manka alipo. Usiku wa manane Manka aliamka na kumfuata Dungu. Ajue kilichowasibu.
Mambo sasa yaliwaendea kombo. Tofauti na wakivyotarajia kabisa

ITAENDELEA KESHO

naisubir
 
RIWAYA......... PENZI CHUNGU - RIWAYA......... PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY

SEHEMU YA 7

"Kuna kitu "
Bruno alihisi kuna kitu, alihisi Manka na mama yake wapo sehemu moja.
"Inawezekana vipi watu waliopo sehemu mbili tofauti, waongee maneno yanayofanana , na usikike wimbo unaofanana
Katika muda unaofanana ". Bruno alikuwa anajiuliza mwenyewe kimoyomoyo.
"Coincidence" Alijijibu mwenyewe pia.
"Coincidence gani hii?"
Hakupata jibu.
'Coincidence ni hali ya vitu viwili au zaidi vinavyofanana kutokea katika muda unaofanana lakini bila kupangwa'
Bruno sasa aliamua kumpigia simu baba yake, ili amuombe msamaha. Baba yake hakuwa anapatikana kwenye simu.

Manka na mama Bruno walipanga vizuri mipango yao. Mipango Ikatekelezwa na wao wenyewe. Sasa Manka alikuwa na jukumu la kwenda kuwatafuta vijana wa kumuua Suto kesho yake usiku.
**************

Katika jiji la Dar es salaam, mtaa wa Tandale ni mtaa uliokuwa maarufu sana kwa watu wa hali ya chini. Kutokana na ukosefu wa ajira vijana wengi wa Tandale walijishughulisha na matumizi yaliyokithiri ya bangi na matumizi ya madawa ya kulevya.

Ili kufanikisha azma yao, Manka alienda Tandale ili kutafuta vijana watakaoenda kumuua Suto , mtu waliyetokea kumchukia zaidi Duniani bila sababu za msingi.
Pesa haishindwi kitu !
Manka alifanikiwa kuwapata vijana watatu mahiri katika mauaji.
Vijana ambao hawakuwa na huruma.
Vijana ambao hawakuwahi kuwa na huruma tangu wazaliwe.
Wawe vipi na huruma wakati Dunia haijawahi kuwaonea huruma.

Manka na wale vijana wauaji walipanga usiku wa kesho yake ndio waende kumuua Suto. Kumuua mwanamke yule asiyekuwa na hatia kabisa.

Siku ile waliitumia kufahamu mazingira ya nyumba anayokaa Suto huko Tabata. Vijana wale walirudi Tandale kujipanga ili wajue kwa jinsi gani wataenda kuivamia nyumba aishiyo Suto, na kumuua!

Kinje, Zinja na Dungu ndio vijana waliokodiwa na kina Manka, walikuwa vijana hatari na makatili sana.
Historia ya maisha yao iliwatengeneza wawe hivyo. Walikuwa na historia mbaya katika maisha yao iliyowapelekea kumchukia kila aina ya binadamu duniani. Walikuwa wanatamani kuua hata dunia nzima kwa sababu wakiozijua wao. Leo wamepewa pesa ili wakatekeleze mchezo waupendao, walifurahi sana !

****************

Bruno alirudi nyumbani, alimkuta mama yake amekaa sebuleni. Tofauti na jana, leo mama yake alimchangamkia sana.
Bruno alishangaa.

Muda wa jioni baba yake alirudi. Nae alikuwa na furaha pia. Walikaa sebuleni na kuongea na kucheka kama zamani. Familia hii ilirudi tena kwenye furaha ghafla, bila kujua Kila mmoja alikuwa na siri nzito kichwani mwake.

Wakati mama Bruno akiwa na furaha akijua kesho usiku atapokea taarifa za kifo cha Suto Sutani !
Baba Bruno nae alikuwa na furaha akijua kesho usiku atapokea taarifa ya kifo cha Suto Satani !
Baba Bruno nae aliongea na mtu ili akamuue Suto!
Alikuwa anaitwa Killer, alikuwa jambazi maarufu sana mitaa ya Sinza. Sinza nzima walikuwa wanamjua Killer.
Killer aliupenda sana mchezo wa kuua !
Mchezo wa kuua nao ulitokea kumpenda pia Killer.
Hakika walipendana sana.

ITAENDELEA
 
SIMULIZI.......PENZI CHUNGU - SIMULIZI.......PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY

SEHEMU YA 8

Hatimaye ilifika siku ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu na Manka, pamoja na mama na baba Bruno.

Ilikuwa siku jumatano, iliyoambatana na mvua mchana kutwa katika Jiji la Dar es salaam. Mvua ambayo Suto ilimfanya ashinde ndani muda mwingi. Akiwa anachati na mpenz wake Bruno.

Usiku wa siku ile ukaingia. Kutokana na mvua , usiku ule yakatengenezwa mawingu mazito angani. Hakukuwa na mbalamwezi hata kidogo.
Kulikuwa na giza totoro!

Saa saba ya usiku, watu watu walikuwa wanaizunguka nyumba moja mitaa ya Tabata. Walikuwa watu watatu hatari, walikuwa makini na kila hatua waliyokuwa wanapiga.

Kinje alisimama katika kona moja, upande wa magharibi wa nyumba ile, Zinja yeye alisimama katika kona nyingine, upande wa mashariki, huku Dungu yeye alikuwa katika mlango wa kuingia nyumba kubwa ya kina Suto Sutani.

Dungu alikuwa na rundo la funguo bandia. Sasa alikuwa anajaribu funguo wa nne kufungua mlango ule.
Funguo tatu za awali zilikuwa zimekataa.

Nyuma ya nyumba ile, kulikuwa na kivuli kimoja kirefu. Kivuli kile kilikuja muda mrefu pale. Kivuli kiliwashuhudia watu watatu tangu walivyokuja mpaka wakivyoinyatia nyumba ile. Kivuli kile kilikuwa kimeshika kisu kirefu!
Pamoja na kuwa na giza totoro, lakini kisu kile kilikuwa kinameremeta.
Tayari kwa kumchoma mtu yeyote kitakapoamrishwa kufanya hivyo!

Kivuli sasa kilisogea taratibu. Bila kutoa sauti yoyote.
Kilikuwa kinamsogelea yule mtu aliyopo upande wa magharibi wa nyumba ya kina Suto.

Kinje alijibana vizuri pale konani, ingawa hakuwa makini sana. Akili yake yote ilikuwa ipo pale mlangoni, akimwangalia Ngudu akijaribu kufungua ule mlango.

Sasa kile kivuli kilikuwa hatua kama tatu nyuma ya Kinje.
HISIA, Kinje alihisi kuna kitu cha hatari nyuma yake. Aligeuka kwa haraka akiwa kashika panga lake kubwa mkononi.
Alichelewa!
Kwa mkono wake wa kulia kile kivuli kilizamisha kile kisu kwa nguvu katika kifua cha Kinje.
Kisu kilizama kifuani !
Kinje alitaka kupiga kelele, lakini kivuli kilimuwahi. Kinje alizibwa mdomo na kile kivuli. Kivuli kilikuwa kimevaa gloves mkononi.
Kivuli kile, kilikuwa kivuli cha Killer !

Killer aliulaza chini taratibu mwili wa marehemu Kinje. Sasa Killer aliizunguka tena ile nyumba kwa nyuma ili aende upande wa mashariki aliokuwa Zinja.
Killer alilipwa kuuwa mtu mmoja, lakini hakuwa na jinsi. Ilikuwa lazima aue watu watatu hawa, na wengine endapo ikilazimu ili aipate shabaha yake, Suto Sutani !

Killer sasa alikuwa hatua chache sana nyuma ya Zinja. Zinja hakuwa na hisia zozote kama kuna mtu nyuma yake. Alijibana pale mkononi huku akiomba dua mlango akioufungua Dungu ufunguke.
Ghafla! Alizibwa mdomo kwa mkono mpana wa Killer. Kisu kilekile kilichomuuwa Kinje, sasa kilizama tumboni kwa Zinja mara tatu na kutoka. Kilitengeneza jeraha baya sana!

Killer aliulaza pia mwili wa Zinja pale chini. Sasa kwa mwendo wa kunyata alikuwa anamfata Dungu pale mlangoni.

Kule ndani, Suto Sutani aliamka ghafla kutoka usingizini. Alikaa kitandani akikumbuka ni kitu gani kichomuamsha.
Alikumbuka.
Suto alikuwa amebanwa na haja ndogo. Haja ndogo iliyomtoa usingizini na kumleta duniani.
Choo cha nyumba ile kilikuwa cha nje. Ilimlazimu Suto atoke nje usiku ule wa manane, wenye giza la kutisha, ili akajisaidie.
Alinyanyuka pale kitandani na kuelekea nje.
Nje ambako kulikuwa na Dungu, nje ambako kulikuwa na Killer, pia kulikuwa na maiti mbili zenye majeraha mabaya ya kisu !

Suto alitoka taratibu kitandani, huku akiwa na maluweluwe ya usingizi. Alitokea kwenye sebule pana ya nyumba ile. Alichukua funguo Kwenye msumari mrefu uliokuwepo pale sebuleni.
Sasa alielekea kufungua mlango.

Kule nje Killer alikuwa amemkaribia kabisa Dungu. Dungu alikuwa tofauti sana na kina Zinja. Dungu alikuwa mtu hatari sana, aliuhisi ujio wa mtu nyuma yake zamani sana, alijifanya kama hajui kama kuna mtu nyuma yake.
Dungu alijiandaa tayari kwa kwa ujio wa mtu huyo.

Killer alikuwa anavizia, wakati mviziwaji alikuwa ashajua kama anaviziwa!

ITAENDELEA .....
 
Sorry kwa yeyote anae fatilia nilikuwa porini kidogo...but nimerudi mujini
 
SIMULIZI....PENZI CHUNGU - SIMULIZI....PENZI CHUNGU
MWANDISHI..HALFANI SUDY

SEHEMU YA 9

Kwa mwendo wake wa taratibu Suto alikuwa anaelekea mlangoni, kuufungua ule mlango.

Kule nje, Killer alikuwa nyuma ya Dungu kwa ukaribu wa kama hatua moja. Killer alinyanyua juu ule mkono wenye kisu kirefu kinachomeremeta gizani. Kwa kasi na nguvu kubwa akawa anaushusha shingoni kwa Dungu ule mkono wenye kisu!
Dungu alikuwa anaona kila kitu kwa jicho la pembeni. Kwa kasi naye aliinama, mkono wenye kisu wa Killer ulikosa kwa kupiga, ulipita hewani bila kumpata aliyemlenga.

Kule ndani, Suto alikuwa anaingiza funguo katika kitasa cha mlango. Aliona kuna ugumu kidogo.
Akalazimisha.
Kumbe kule nje Dungu aliacha funguo zake zikining'inia pale kitasani, ghafla zikadondika!
Mlango ukafunguka.

Baada ya kukwepa kile kisu, Dungu aligeuka nyuma, akiacha funguo zikining'inia pale kwenye kitasa.
Sasa Dungu na Killer walikuwa wanatazamana. Killer kashika kisu kwa mkono wake wa kulia, Huku Dungu kashika panga kwa mkono wake wa kushoto!

Suto alikuwa amesimama katikati ya mlango, akiwashuhudia wale majabali wawili wakitazamana. Suto alipigwa na butwaa, hakuweza kutoa sauti yoyote. Na wala hakutoa ishara yoyote.
Alitulia tuli.

Killer alirusha ngumi ya nguvu kwa mkono wake wa kushoto. Ngumi iliyompata Dungu shavuni. Dungu alinesa kidogo, akiwa kwenye ule mneso alirudi kwa nguvu na lile panga, panga lilitua shingoni kwa Killer barabara. Nusu ya panga liliingia pale shingoni, Dungu aliacha lile panga likining'inia shingoni kwa Killer.
Alikimbia mbio!

Suto Sutani, alikuwa kama kapigwa na ganzi pale mlangoni. Kwa mara ya kwanza katika maisha yake alishuhudia tukio la hatari. Suto alishuhudia binadamu akiwa anakufa huku akimwaga damu mithili ya bomba bovu la maji.
Ghafla, alipata kauli. Alipiga kelele kubwa sana.
Huku akilia kwa woga!
Huku akilia kwa hofu!

Ndani ya dakika tano, watu walikuwa wamejaa. Wenye silaha mbali mbali.
Walifika kwenye ile nyumba akiyokaa Suto Sutani.
Walipofika pale watu wote walipigwa na butwaa. Walikuta picha mbaya sana. Maiti ya mtu ikiwa imedondoka chini, na panga shingoni.

Suto alikuwa analia sana, kila anachoulizwa yeye analia. Mjumbe alipiga simu, kituo cha Polisi Tabata.
Baada ya robo saa polisi waliwasiri.
Polisi waliikagua nyumba yote kuangalia mazingira ya mauaji yale. Ndipo waliikuta miili mengine miwili.
Waliichukua.
Walimchukua na Suto Sutani. Yeye ndiye alikuwa mshtumiwa namba moja katika kesi ya mauaji yale!

Dungu alikimbia sana usiku ule. Alikuwa kama amechanganyikiwa.
Hakuelewa kabisa kimetokea nini?
Hakujua yule mtu ni nani?
Hakuelewa wenzake wake wapi?
Alipofika mbali na nyumba ya kina Suto alisimama, huku anahema, alitoa simu yake mfukoni. Alilitafuta jina la Manka na kumpigia.

"Halloo Bosi"
"Nambie Dungu, mmefanikiwa?"
"Hapana Bosi"
"Kwa nini"
'Mimi sielewi Bosi"
"Dungu! Mbona unanichanganya!"
"Misheni imefeli Manka"
"Kwanini?"
"Suto Sutani analindwa kumbe!"
"Analindwa ??!!"
"Ndio, sijui kama kina Zinja wako salama kweli"
"We uko wapi, nije tuongee maana hata sikuelewi"

Dungu alimuelekeza Manka alipo. Usiku wa manane Manka aliamka na kumfuata Dungu. Ajue kilichowasibu.
Mambo sasa yaliwaendea kombo. Tofauti na wakivyotarajia kabisa

ITAENDELEA badae sehemu ya kami..
 
SIMULIZI.....PENZI CHUNGU - SIMULIZI.....PENZI CHUNGU
MWANDISHI...HALFANI SUDY

SEHEMU YA 10

Suto Sutani alifikishwa kituo cha Polisi Tabata usiku, hakuhojiwa.
Aliwekwa selo.
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Suto kupelekwa Polisi, Ilikuwa ni mara ya kwanza pia kwa Suto kuingizwa selo. Ulikuwa ni usiku mbaya sana kwake. Ndani ya selo kulikuwa na mazingira magumu sana kwa mtu kuishi. Kilikuwa ni chumba kidogo sana, chenye dirisha moja juu. Chumba chenye hewa nzito iliyoambatana na harufu ya damu iliyokauka.
Pamoja na Jiji la Dar es salaam, kuwa na hali ya mvua, ambayo ilipooza hali ya joto na kuigeuza kuwa ya baridi, lakini mbu hawakukoma katika selo ile. Kulikuwa na mbu waumao na wenye kuleta kelele mbaya masikioni.

Suto aliwakuta watuhumiwa watatu ndani ya ile selo. Walikuwa wamekonda na majeraha kwenye miili yao. Suto alihisi walikuwa mateja au wanywaji wa pombe za kienyeji, waliodhulumiana na kuamua kupigana. Wote walikuwa wamelala usingizi nzito.

Suto nae alichagua kona moja ya selo ile. Akaiegemea, akawa anajikokota chini taratibu kwa kutumia mgongo.
Suto alijiburuza mpaka akajipweteka chini, alikunja miguu na kuiweka sura yake juu ya magoti yake.
Alikuwa analia..

Kule Tabata, Manka na Dungu walikutana. Dungu alimueleza kila kitu kilichotokea usiku ule. Manka hakuamini kabisa, alijua ni hila tu za Dungu ili asiitekeleze kazi yake. Mwishowe waliagana wakiwa wamekubaliana watakutana kesho yake saa nne. Kulijadiri vizuri jambo lile.

Nyumbani kwa kina Suto kulikuwa hakueleweki. Kulikuwa na kelele za kilio toka kwa mama Suto. Mama Suto alimlilia sana mwanae, huku akimlaani mtu aliyeua na kumsababishia balaa lile mwanae.

Usiku uleule Manka alienda nyumbani kwa kina suto. Aliyoyakuta, yalimshangaza sana. Alikuta kuna umati mkubwa wa watu, alimvuta mwanamke mmoja pembeni na kumuuliza kilichotokea pale.
"Kuna watu watatu wameuliwa na dada mmoja anakaa ndani humu"
"Ziko wapi maiti zao?"
"Zishapelekwa hospitali"
"Huyo dada yuko wapi sasa?"
"Dada amechukuliwa na polisi, amewauwa kinyama kweli, sijui hata walimkosea nini....?"
Yule dada aliendelea kuongea, lakini Manka hakuendelea kumsikiliza. Alihisi kelele kichwani kwake kama kuna watu wanagonga vyuma.
Kwa kifupi alichanganyikiwa !
Muda uleule, alichukua simu yake, na kumpigia mama Jfloux.

Mama Bruno na baba Bruno walikuwa wamelala kitandani. Walilala huku wakitarajia kupigiwa simu. Wakati mama Bruno akiitarajia simu kutoka kwa Manka, baba Bruno alikuwa akiitarajia simu kutoka kwa Killer. Simu zenye ujumbe sawa. Toka kwa watu wawili tofauti.
Ujumbe, wa kifo cha Suto Sutani !

Simu ya mama Bruno ndio ilianza kuita...

ITAENDELEA Kesho
 
SIMULIZI... PENZI CHUNGU
MWANDISHI...HALFANI SUDY

SEHEMU YA 11

( Upumzike salama Shangazi)

**************

Mama Bruno akiwa na sura yenye furaha sana alienda bafuni kuipokea ile simu aliyotarajia ina habari za kufurahisha toka kwa Manka.
Alienda kwa furaha, lakini alirudi na huzuni kuu.

Bruno alikuwa amelala chumbani kwake akiwa hana habari yoyote iliyotokea duniani. Alikuwa njozini, akiota jinsi penzi lake jipya na Suto jinsi likivyochanua. Penzi lao lilikuwa linazidi kukomaa, likichagizwa na meseji wakizotumiana mara kwa mara.
Hakujua kabisa, wakati yeye akiota ndoto nzuri, Suto Sutani alikuwa katika selo moja chafu sana, katika kituo cha Polisi Tabata.

Mama Bruno alirudi toka bafuni, alifika kitandani, alikaa kitako pembeni kabisa mwa kitanda. Alishika tama na kuanza kuichambua habari ile mbaya aliyopewa na Manka kwa njia ya simu.

Baba Bruno alikuwa amejifanya amelala, lakini alikuwa hajalala kabisa. Alikuwa macho Akisubiri simu toka kwa Killer. Baba Bruno, alikuwa anazishuhudia pilikapilika zote za mkewe usiku ule. Lakini hakuelewa nini kimemsibu mke wake. Na wala hakumuuliza.
Mtu na mkewe walikesha macho siku ile.

Asubuhi na mapema bila kujua hili wala lile, Bruno alijiandaa kuelekea chuoni.
Akiwa njiani, alimuona kijana mmoja akiuza magazeti. Bruno alimuita kijana muuza magazeti kwa lengo la kununua gazeti. Vichwa vya habari vya magazeti yale yalimstua sana Bruno.
Alilichagua gazeti litokalo kila siku, gazeti pendwa la Dumizo lililokuwa na kichwa cha habari...

'Muuaji katili wa kike aibuka Tabata !'

Bruno akiwa ndani ya daladala alianza kuisoma habari ile. Kila alivyoendelea kuisoma habari ile mwili wake ulimuingia baridi.
Jinsi mwandishi wa kike, Veronica Baro, alivyoisimulia habari ile ilikuwa inasisimua sana, alieleza jinsi walivyoukuta mwili wa marehemu ukiwa na panga shingoni.
Mwishoni akiishauri serikali impe adhabu kali muuaji, huku akimtaja kwa jina muuaji kuwa ni Suto Sutani!

Veronica Baro, kwa kutumia kalamu yake, aliiaminisha jamii kwamba, muuaji wa watu wale ni Suto Sutani.

Wakati anamaliza kusoma Jfloux machozi yalikuwa yanamdondoka. Aliamua kugairisha safari ili aende Tabata, kwa Suto. Kuthibitisha habari zile. Hakuamini kabisa kama Suto anaweza kuuwa kikatili namna ile.
Suto alikuwa mwoga, hakuweza hata kuua panya !

Kule selo, Suto aliendelea kuteseka hadi asubuhi. Hakulala kabisa. Mbu na harufu vilimtesa sana.

Lilikuja gari la gereza la Segerea, Suto aliingizwa kwenye karandinga na kupelekwa kwenda kuanza maisha mapya gerezani.

Alitolewa pale Polisi bila ya kuhojiwa chochote, haukuwa utaratibu kabisa, lakini Suto alifanyiwa hivyo. Huku akipandishwa KEEN YEAR karandinga kwa mateke na mangumi toka kwa askari Polisi mmoja. Suto alimuangalia kwa jicho kali sana yule askari, alirushwa kwa nguvu na kujipweteka kwa nguvu nyuma ya lile gari. Akiwa kalala chini, Suto alimwangalia tena askari yule.
Utajuta !
Macho ya Suto yalieleza hivyo.

Kule kwa baba Bruno, Mzee Boe na mama Bruno waliamka wakiwa hoi, wote walikuwa hawajalala, wote walificha siri nzito vifuani mwao. Hakuna aliyemshirikisha mwenzie.

Baba Bruno alikuwa anapiga simu kila mara, simu Ilikuwa haipatikani.
Killer alikuwa hana tabia ya kufanya kazi hatari kama zile akiwa na simu. Huwa anazima na kuiacha nyumbani. Anajua madhara ya kwenda kufanya mauaji akiwa na simu.
Sasa Killer ameuwawa, na simu yake ikiwa haipatikani.
Baba Bruno jasho lilimtoka.

ITAENDELEA BAADAE
 
SIMULIZI.. PENZI CHUNGU - SIMULIZI.. PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY

SEHEMU YA 12

'Ulale salama Shangazi'

Upande wa mama Bruno nae aliamka akiwa anawasiliana na Manka kwa njia ya meseji.
"Lazima tuhakikishe Suto anafia jela" mama Bruno aliandika.
"Kweli maana hatujui kama kina Zinja walitutaja au vipi?"
"Tutamuuaje sasa ?"
"Tutajua tukikutana"
"Sawa"

Wanawake hawa hawakuwa na huruma kabisa. Walipania kumuua Suto Sutani, kwa hali yoyote ile, kwa namna yoyote ile .

******************

Habari nzuri husambaa taratibu, lakini habari mbaya husambaa haraka sana !
Habari za mauaji ya kikatili ya watu watatu Tabata, yalisambaa haraka sana Tanzania nzima.
Yaliishangaza nchi hasa baada ya kugundulika kuwa muuaji wa watu hao alikuwa ni mwanamke. Kama habari ilivyoandikwa kwa uhakika mkubwa na mwandishi wa habari wa gazeti la Dumizi, Veronica Baro.
Veronica Baro hakuandika tu habari, alihukumu pia, tena bila uhakika.
Bila kufanya uchunguzi wa kina.

Tanzania nzima sasa ikawa inamlaani Suto Sutani !
Bila kujua undani wa sakata hili. Bila kujua chanzo halisi cha mauaji yale.
Mwandishi ni mtu anayeaminiwa sana kwa kila anachokiandika, Watanzania wengi walimwamini Veronica Baro. Kalamu ya Veronica Baro ikamsulubu vilivyo Suto Sutani.
Tanzania nzima wakawa wanaimba, anyongwe.... anyongwe, Suto muuaji !

**********

Bruno alienda nyumbani kwa Suto Asubuhi ile. Hakumkuta Suto, wala mama yake Suto. Aliwakuta majirani wachache, baada ya kuulizia aliambiwa Suto na mama yake, wameenda kituo cha Polisi Tabata.
Bruno nae alienda kituo cha Polisi akiwa na mawazo tele. Huku habari iliyoandikwa na Veronica Baro ikijirudiarudia kichwani mwake.

Alifika Polisi, majibu ya askari Polisi yalimchosha kabisa, walimwambia Suto amepelekwa mahabusu, Segerea.
Bruno alikaa huku kashika tama kwenye benchi la pale kituo cha Polisi.
Alichoka kabisa.

Segerea, Suto alikaribishwa vibaya sana. Askari magereza, Wafungwa na mahabusu wenzake walimchukia sana Suto. Walikuwa wanamuona ni mwanamke muuaji.
Hawakumpenda, walimtenga na kumnyanyasa sana. Wakisahau kabisa kama nao walipelekwa pale kwa makosa mbali mbali. Wakisahau kama kama Suto alikuwa Mtuhumiwa tu, mahakama ilikuwa haijamtia hatiani bado.

Saa nne kamili asubuhi, Manka na Dungu walikutana, ilikuwa katika mgahawa mdogo uliopo Magomeni. Hawakutaka kukutania Tabata.
Sasa walipanga vizuri mpango wao, walitaka kuhakikisha Suto Sutani anaozea jela, au anafia jela. Waliamua kutumia Pesa. Kumhonga yeyote yule ili Kuhakikisha adhma yao inakamilika!
Walipanga mipango, mipango ikapangika!

Bruno alitoka pale kituo cha Polisi kichwa chini, mikono nyuma, alirudi nyumbani kwao kwa mwendo wa taratibu.
Alipofika nyumbani, aliwakuta wazazi wake wakiwa kimya sebuleni. Naye alichagua kochi moja, akakaa.
Bruno aliuvunja ukimya !

"Wazazi wangu, Suto amepatwa na matatizo makubwa..!"
"Matatizo gani?" Baba Bruno aliuliza kwa fadhaa.
"Suto, amekamatwa na Polisi"
"Unasemaaa!" Baba Bruno hakutarajia taarifa hiyo. Yeye alikuwa anatarajia kupokea taarifa ya kuuwawa kwa Suto.
"Suto amekamatwa babaa" kwa mara ya kwanza tangu sakata hili litokee, Bruno alidondosha chozi.

Mama Bruno alibaki midomo inamtetemeka. Ilikuwa habari anayoijua lakini hakupenda kabisa kuisikia...


ITAENDELEA KESHO.
 
SIMULIZI.... PENZI CHUNGU SIMULIZI.... PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY

SEHEMU YA 13

'Upumzike salama Shangazi'
**********

Ilikuwa taharuki ndani ya nyumba ile. Mipango hasi ya Baba na mama Bruno sasa ilileta taharuki kuu katika familia ile. Wote watatu walikaa pale sebuleni wamechoka mwili, wamechoka na akili.

***********

Kule gerezani, Suto sasa alibatizwa jina kwa baba mpya, badala ya Sutani, jina la baba yake mzazi, sasa alipewa jina la baba anayeitwa muuaji.
Sasa aliitwa Suto muuaji !

Gerezani pia Suto aliendelea kuwa na damu ya kunguni. Suto hakupendwa na watu wote mle gerezani, lakini kuna watu wawili walimchukia zaidi Suto, watu hao walikuwa ni askari magereza wa kike, Beji na Zura.

Beji na Zura, walikuwa ni askari makatili sana katika Gereza la Segerea. Beji na Zura walihakikisha wanapeleka mateso makali sana kwa Suto.
Sababu ya kumtesa Suto waliijua wao, labda ni chuki tu ndizo zilisababisha mateso hayo kwa Suto.

Beji na Zura walimpa Suto kila aina ya mateso waliyoyafikiria, walikuwa wanamyima Suto chakula, wanampiga na kumgomea.
Suto maisha yake siku zote yakawa ya kulia mle gerezani.

************

Siku ya jumapili, Bruno alitoka nyumbani kwao na kwenda katika Gereza la Segerea, ili kumuona mpenzi wake Suto.
Siku hiyo mlangoni ilikuwa zamu ya kulinda ya Beji. Ingawa ilikuwa siku ya kuwaangalia mahabusu na wafungwa, lakini Beji alimkatalia katakata Bruno kuingia gerezani kumuona Suto. Bruno alipambana sana bila mafanikio, mwishoni aliamua kurudi nyumbani. Bruno alirudi nyumbani akiwa na mawazo tele, aliyakumbuka sana maneno ya askari yule kuwa eti hawezi kumuona Suto kwa kuwa alikuwa muuaji. Wakihofia usalama wa Bruno.

Bruno alifika nyumbani kwao. Alikaribishwa na maneno makali toka kwa mama yake mzazi.

"Ndio ulienda kwa huyo muuaji wako, utajitia hatiani mwanangu, Suto siyo mtu wa kukaa nae karibu kwa sasa !"

Sasa maneno ya yule askari, Beji, kule gerezani yaliunganika na maandishi ya mwandishi mahiri wa gazeti la Dumizi, Veronica Baro, yakipewa nguvu nzito na mama yake mzazi, kidogo kidogo Bruno mbegu ya chuki ilianza kujengeka kifuani kwake.
Alianza kumchukia Suto!

Baadae jumapili ileile, mama yake Suto alienda kumwangalia Suto gerezani. Mtu wa kwanza Suto kumuulizia ni Bruno, hata mama Suto ilimshangaza sana taarifa ya kuwa Bruno hakuwahi kufika gerezani kumuangalia Suto. Mama Suto aliahidi, ataenda kumtafuta Bruno.

***********

Baba Bruno alipata taarifa ya kifo cha Killer, kijiweni Sinza. Ilikuwa taarifa ya kushangaza sana masikioni mwa baba Bruno.
Hakuamini .
Hakutegemea.
Taarifa ya Killer kuuwawa na mtoto wa kike ilikuwa taarifa ya kushangaza sana. Haikuingia kichwani kwa mtu yeyote pale Sinza.
Wote walikuwa wanamjua Killer, Killer hakuwa mtu lelemama kabisa..I

ITAENDELEA badae
 
SIMULIZI.... PENZI CHUNGU - SIMULIZI.... PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY

SEHEMU YA 14

killer hakuwa mtu lelemama kabisa, alikuwa mbabe kweli. Hadi umauti ule mbaya unamkuta, Killer alishauwa watu wengi sana pale Sinza. Ni Polisi gani Sinza ambaye alikuwa hamjui na kumuogopa Killer ?. Killer alikuwa mtemi, alikuwa jasiri, alikuwa mbabe.
Nani atakubali kwa anayemjua Killer umwambie ameuliwa na mtoto wa kike, eti Suto Sutani!
Suto Sutani sasa akaingia katika orodha ya watu hatari sana nchini Tanzania.

Kifo cha killer sasa kilimtia kiwewe baba Bruno. Alianza kumfikiria Suto kwa fikra zingine.
Alianza kumuogopa Suto !
Mtu wa kuweza kupambana na wanaume watatu, tena wauaji na kuweza kuwauwa kinyama vile. Lazima umwangalia katika jicho la tatu.

************

Hatimaye siku ikiyosubiriwa kwa hamu, siku ya kesi ya Suto Sutani ilifika.
Ilikuwa jumatatu tulivu ndani ya Jiji la Dar es salaam. Kama kawaida ya Jiji, kulikuwa na joto kali sana lililotokana na jua kali lichomalo.

Karandinga la Gereza la Segerea, lilikuwa njiani kuelekea Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu. Ndani ya gari hilo, katika kiti cha mwisho kilikaliwa na Suto Sutani. Mwili wa Suto ulikuwa umedhoofika sana, kwa kukosa chakula bora na malezi mazuri huko gerezani.

Waliwasiri viwanja vya Mahakama ya Kisutu saa mbili kamili asubuhi. Mahakama ilikuwa na umati mkubwa wa watu. Umati uliotokana na umaarufu wa kesi ya Suto.

Hatimaye, Suto alishuka katika gari lile kubwa la kijani la Magereza ya Segerea.
Mguu wake ulivyogusa ardhi tu, Suto alivamiwa.
Waandishi wa habari walimvamia huku wakisukumana wao wenyewe. Angalau tu wapate nafasi ya kumpiga picha Suto, Suto muuaji!
Kukosa picha za Suto ilimaanisha kutouza magazeti yao kesho yake asubuhi.
Suto alikuwa maarufu sana.

Alivyoingia Mahakamani, Suto hakumuona mtu yeyote anayemfahamu zaidi ya mama yake mzazi. Hata Bruno mwanaume aliyetokea kumpenda sana hakumwona Mahakamani. Muda wa kupandishwa kizimbani Suto ulifika, huku chozi la uchungu lilimtirika pale Kizimbani. Alisomewa mashtaka yake, na Hakimu alimwambia Suto asijibu chochote. Uchunguzi wa kesi ile ulikuwa bado unaendelea.

Suto alirudishwa kwenye gari, huku akifatwa nyuma na rundo la waandishi wa habari. Suto aliwashangaa waandishi wale. Kwanini walikuwa wanamfata yeye tu.
Miongoni mwa waandishi wale, alikuwepo mwandishi mahiri wa Gazeti la Dumizi, Veronica Baro.
Veronica alimfata dirishani Suto na kumuuliza kwa sauti kubwa.
"Kwanini uliua wewe binti ?"
Suto alimwangalia mwandishi yule kwa jicho kali sana....

ITAENDELEA KESHO
 
SIMULIZI.... PENZI CHUNGU - SIMULIZI.... PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY

SEHEMU YA 15

Lakini Suto hakumjibu, alikaa kimya. Baada ya kesi za mahabusu wengine, Suto na mahabusu wenzake walirudishwa gerezani, Segerea.

Jumanne asubuhi magazeti yote yaliandika habari kuhusu kesi ya Suto Sutani. Magazeti mengi yaliandika habari hiyo katika kurasa zake za mbele kabisa, zikiambatanishwa na picha za Suto Sutani akiwa anashuka katika karandinga la Segerea.

Veronica Baro wa gazeti la Dumizi nae hakuwa nyuma, kama kawaida yake alipata cha kuandika kuhusu Suto. Kichwa cha habari katika gazeti la Dumizi kilisomeka hivi.

"Suto Sutani ni Muuaji Kiburi na jeuri ! "

Kwa kiasi kikubwa katika habari ile Veronica Baro alikuwa anazungumzia kutojibiwa swali lake na Suto Sutani pale kwenye dirisha la gari la Segerea.
Suto sasa alipachikwa sifa nyingine mpya, sifa ya kiburi na sifa ya jeuri. Huku ile sifa ya uuaji ikiendelea kumng'ang'ania.

*************

Upande wa kina Bruno walisahau kabisa habari kuhusu Suto. Sasa Bruno alizama katika dimbwi la mapenzi na Manka. Aliendelea na Chuo kama kawaida. Huku akiamini suto aliua kweli, na kusubiri kwa hamu kusikia adhabu kali atakayopewa Suto.

Kwa upande wa baba na mama Bruno, maisha yaliendelea vizuri, kwa kuwa adui yao alikuwa jela. Upendo ulirudi kama zamani, huku wakifurahi sana kuwa na mkwe mzuri kama Manka.

*************

Kule gerezani, maisha ya Suto yaliendelea kuwa magumu.
Sababu kuu ikiwa Beji na Zura, Askari hao sasa walikuja na mpango mpya, walikuwa wanataka Suto Sutani abakwe na kuuwawa mlemle gerezani !

Ulikuwa usiku wa giza totoro. Ndani ya Gereza la Segerea, kulikuwa kimya, wafungwa wote wamelala, askari wachache walikuwa doria. Wakizunguka ndani na nje ya Gereza.

Katika lango kuu kulikuwa na askari wawili, Beji na Zura. Walikuwa wameweka sawa mipango yao, ya kumpitisha mtu kwa siri ili akambake Suto, ili akamuue Suto Sutani.

Banda, alikuwa mlevi maarufu katika vilabu vya Tandale. Yeye ndiye alikuwa amepewa kazi maalumu, kazi ya kwenda kumbaka na kumuua Suto, ilipangwa itekelezwe na Banda chini ya usimamizi wa
Beji na Zura, Beji na Zura walikuwa ndio wasimamizi wa jambo hilo.

Kule ndani ya selo, Suto alikuwa amejikunyata katika kona moja ya selo ile.
Suto akiwa amelala usingizi nzito.
Kwa kushirikiana na kina Beji, Banda aliingia kwa siri ndani ya selo ya Suto. Beji alimfungulia mlango wa selo na kumfungia kwa nje ili Banda atekeleze kilichopangwa. Kule kwenye geti kuu alibakia Zura, akiwa makini kulinda usalama.

Sasa ndani ya selo ile, kulikuwa na watu wawili, Suto Sutani akiwa amelala, na Banda Mlevi akiwa anamnyatia Suto....

ITAENDELEA
 
SIMULIZI........ PENZI CHUNGU - SIMULIZI........ PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY

SEHEMU YA 16

Banda alikuwa anamsogelea Suto taratibu pale chini.
Tayari kwa kubaka.
Tayari kwa kuuwa.
Banda alimkaribia Suto kabisa. Kwa kutumia mkono wake wa kulia alimziba Suto mdomo na pua kwa nguvu, na mkono wake wa kushoto aliishika sketi aliyoivaa Suto.

Suto alipata mstuko mkubwa sana, mstuko uliomuamsha toka usingizini. Sasa alikuwa anafurukuta kwa kukosa pumzi, bila kutoa sauti yoyote. Banda alikuwa mlevi mahiri, lakini alikuwa na mabaki ya nguvu katika mwili wake.
Alimbana Suto kisawasawa!
Suto alijaribu kuutoa mkono wa banda bila mafanikio. Sasa aliamua kufanya kitu. Na yeye aliamua kumkaba Banda ili ajiokoe katika kisanga kile. Alimshika banda shingoni kwa mikono yote miwili, Ilikuwa patashika ya kimya kimya ndani ya selo, sketi ya Suto Sutani ikiwa imeshuka nusu, hadi magotini.
Mizizi ya chuki moyoni kwa Suto ilikuwa imeshaanza kutamalaki, chuki na ulimwengu, chuki na walimwengu, chuki ambayo ilizidisha hasira zake, chuki ambayo ilimpa nguvu Suto ambazo hakuwa nazo kabla, Suto alipata nguvu za ghafla, kwa kutumia dole gumba lake alianza kulibinya koromea refu la Banda.
Ilikuwa ni picha mbaya sana kuangalia.
Macho ya Banda yalikuwa yametoka nje, mithili ya kijusi kabanwa na mlango.
Suto alimbinya Banda kwa nguvu zake zote zilizobakia.

Kule getini wale maaskari wawili, wenye roho mbaya walikuwa wanasubiri taarifa ya furaha kwao, taarifa ya kifo cha Suto Sutani.
Walikaa robo saa, ilikuwa kimya, Banda alikuwa hajarudi , ndipo Beji alikwenda kule selo, akitegemea Banda itakuwa kashatekeleza kazi waliyomtuma.
Alijidanganya.
Suto sasa alibadirishwa na mazingira , Suto alianza kuwa katili taratibu, mazingira yakiwa ndio mwalimu wa ukatili wa Suto Sutani, na sasa alikuwa amefuzu.

Beji alifungua geti la selo aliyowekwa Suto. Alimulka kwa tochi yake ndogo, iliyotoa mwanga hafifu, alichokikuta ndani ya selo, kilimuacha mdomo wazi.
Alikuta mwili wa Banda ukiwa umelala chini, huku Suto akiwa amesimama wima, jasho linamtoka !

"Umefanya nini Suto?" Beji aliuliza kwa sauti ndogo.
"Nimemuuwa jamaa yenu" Suto alisema bila wasiwasi wowote.
"Suto!" Beji alisema akiwa na uwoga mkubwa sana.
Beji aliingiwa na wasiwasi, maana endapo Banda itakuwa amefia ndani ya gereza, wao walikuwa na chakujibu kuwa ameingia vipi ndani ya gereza, na wao ndio walikuwa zamu usiku ule ?
Alisogea pale ulipo mwili wa Banda na kumwangalia mapigo yake ya moyo.

*************

Huko nje, maisha yaliwaendea vizuri sana baba Bruno, mama Bruno, Manka na Bruno. Walikuwa wanaishi kwa furaha sana, huku wote wakiwa wamesahau kabisa habari kuhusu Suto.

Baada ya kutoka gerezani siku ile mama Suto alienda kwa kina Bruno, ila alijibiwa majibu ya kejeri, dharau na kebehi, toka kwa Bruno na mama yake. Mama Suto aliondoka kichwa chini. Aliumia sana moyoni, lakini angefanya nini?

Beji aligusa kifuani kwa Banda, alisikia mapigo ya moyo kwa mbali. Ishara kwa Banda alikuwa hajafariki bado. Beji alishusha pumzi ndefu..

Beji alirudi mbio mpaka getini. Akamuekeza Zura kila kitu kilichotokea, kwa kushirikiana na Zura walimtoa Banda kwa usiri mkubwa sana.
Banda hakufanikiwa kubaka wala kuuwa.
Banda alifanikiwa kukabwa na Suto Sutani mpaka kuzimia.

Suto Sutani, alielewa kwamba zile zilikuwa ni njama za Beji na Zura, sasa alikuwa makini zaidi. Alielewa kwamba askari wale walikuwa na nia mbaya sana na yeye.

Upelelezi wa kesi ya mauaji ikiyomkabiri Suto uliendelea. Inspekta wa kike, Jasmine, ndiye alipewa jukumu la kuipeleleza kesi ile.
Inspekta Jasmine alikuwa askari hodari sana katika jeshi la Polisi, jasiri na mtu anayetumia akili nyingi sana katika kuvumbua sababu za vifo vya kutatanisha. Taifa lilikuwa linamtegemea sana,hasa katika kipindi kama hiki ambacho mpelelezi namba moja Tanzania, Daniel Mwaseba, alikuwa mapumzikoni nchini Ujerumani. Baada ya kufanya kazi kubwa sana ya kuwakamata maadui wa nchi yetu waliokuwa na Mpango wa Siri. Inspekta Jasmine sasa aliingia kazini mzima mzima, akidhani hii ni kesi rahisi sana, laiti angejua atakayokutana nayo......

ITAENDELEA
 
SIMULIZI........ PENZI CHUNGU - SIMULIZI........ PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY

SEHEMU YA 16

Banda alikuwa anamsogelea Suto taratibu pale chini.
Tayari kwa kubaka.
Tayari kwa kuuwa.
Banda alimkaribia Suto kabisa. Kwa kutumia mkono wake wa kulia alimziba Suto mdomo na pua kwa nguvu, na mkono wake wa kushoto aliishika sketi aliyoivaa Suto.

Suto alipata mstuko mkubwa sana, mstuko uliomuamsha toka usingizini. Sasa alikuwa anafurukuta kwa kukosa pumzi, bila kutoa sauti yoyote. Banda alikuwa mlevi mahiri, lakini alikuwa na mabaki ya nguvu katika mwili wake.
Alimbana Suto kisawasawa!
Suto alijaribu kuutoa mkono wa banda bila mafanikio. Sasa aliamua kufanya kitu. Na yeye aliamua kumkaba Banda ili ajiokoe katika kisanga kile. Alimshika banda shingoni kwa mikono yote miwili, Ilikuwa patashika ya kimya kimya ndani ya selo, sketi ya Suto Sutani ikiwa imeshuka nusu, hadi magotini.
Mizizi ya chuki moyoni kwa Suto ilikuwa imeshaanza kutamalaki, chuki na ulimwengu, chuki na walimwengu, chuki ambayo ilizidisha hasira zake, chuki ambayo ilimpa nguvu Suto ambazo hakuwa nazo kabla, Suto alipata nguvu za ghafla, kwa kutumia dole gumba lake alianza kulibinya koromea refu la Banda.
Ilikuwa ni picha mbaya sana kuangalia.
Macho ya Banda yalikuwa yametoka nje, mithili ya kijusi kabanwa na mlango.
Suto alimbinya Banda kwa nguvu zake zote zilizobakia.

Kule getini wale maaskari wawili, wenye roho mbaya walikuwa wanasubiri taarifa ya furaha kwao, taarifa ya kifo cha Suto Sutani.
Walikaa robo saa, ilikuwa kimya, Banda alikuwa hajarudi , ndipo Beji alikwenda kule selo, akitegemea Banda itakuwa kashatekeleza kazi waliyomtuma.
Alijidanganya.
Suto sasa alibadirishwa na mazingira , Suto alianza kuwa katili taratibu, mazingira yakiwa ndio mwalimu wa ukatili wa Suto Sutani, na sasa alikuwa amefuzu.

Beji alifungua geti la selo aliyowekwa Suto. Alimulka kwa tochi yake ndogo, iliyotoa mwanga hafifu, alichokikuta ndani ya selo, kilimuacha mdomo wazi.
Alikuta mwili wa Banda ukiwa umelala chini, huku Suto akiwa amesimama wima, jasho linamtoka !

"Umefanya nini Suto?" Beji aliuliza kwa sauti ndogo.
"Nimemuuwa jamaa yenu" Suto alisema bila wasiwasi wowote.
"Suto!" Beji alisema akiwa na uwoga mkubwa sana.
Beji aliingiwa na wasiwasi, maana endapo Banda itakuwa amefia ndani ya gereza, wao walikuwa na chakujibu kuwa ameingia vipi ndani ya gereza, na wao ndio walikuwa zamu usiku ule ?
Alisogea pale ulipo mwili wa Banda na kumwangalia mapigo yake ya moyo.

*************

Huko nje, maisha yaliwaendea vizuri sana baba Bruno, mama Bruno, Manka na Bruno. Walikuwa wanaishi kwa furaha sana, huku wote wakiwa wamesahau kabisa habari kuhusu Suto.

Baada ya kutoka gerezani siku ile mama Suto alienda kwa kina Bruno, ila alijibiwa majibu ya kejeri, dharau na kebehi, toka kwa Bruno na mama yake. Mama Suto aliondoka kichwa chini. Aliumia sana moyoni, lakini angefanya nini?

Beji aligusa kifuani kwa Banda, alisikia mapigo ya moyo kwa mbali. Ishara kwa Banda alikuwa hajafariki bado. Beji alishusha pumzi ndefu..

Beji alirudi mbio mpaka getini. Akamuekeza Zura kila kitu kilichotokea, kwa kushirikiana na Zura walimtoa Banda kwa usiri mkubwa sana.
Banda hakufanikiwa kubaka wala kuuwa.
Banda alifanikiwa kukabwa na Suto Sutani mpaka kuzimia.

Suto Sutani, alielewa kwamba zile zilikuwa ni njama za Beji na Zura, sasa alikuwa makini zaidi. Alielewa kwamba askari wale walikuwa na nia mbaya sana na yeye.

Upelelezi wa kesi ya mauaji ikiyomkabiri Suto uliendelea. Inspekta wa kike, Jasmine, ndiye alipewa jukumu la kuipeleleza kesi ile.
Inspekta Jasmine alikuwa askari hodari sana katika jeshi la Polisi, jasiri na mtu anayetumia akili nyingi sana katika kuvumbua sababu za vifo vya kutatanisha. Taifa lilikuwa linamtegemea sana,hasa katika kipindi kama hiki ambacho mpelelezi namba moja Tanzania, Daniel Mwaseba, alikuwa mapumzikoni nchini Ujerumani. Baada ya kufanya kazi kubwa sana ya kuwakamata maadui wa nchi yetu waliokuwa na Mpango wa Siri. Inspekta Jasmine sasa aliingia kazini mzima mzima, akidhani hii ni kesi rahisi sana, laiti angejua atakayokutana nayo......

ITAENDELEA

Mkuu big up sana
 
Back
Top Bottom