Fortunatus Buyobe
JF-Expert Member
- Nov 9, 2011
- 463
- 1,107
- Thread starter
- #41
4
“
ANGALAU NIMEPUNGUZA HISIA ZANGU” Koplo Tsega alijisemea
moyoni baada ya mjadala mkubwa kumalizika nafsini mwake. Matukio ya jana
usiku yalikuwa yamemuacha hoi kwa uchovu baada ya kugaragazwa na kupindwa
katika kila namna ya mkao na mwanaume shababi mfanyakazi wa hoteli ile aliyelala
naye usiku kucha.
Tangu aliposalitiwa na mpenzi wake Koplo Tsega alikuwa ameapa kutojihusisha
tena na mapenzi katika maisha yake lakini hilo lilikuwa gumu kutekelezeka. Hisia
zikakataa kabisa kukubaliana na akili yake hivyo mapenzi akayageuza na kuyafanya
kama starehe nyingine ambapo angeyatafuta na kuyafanya na mwanaume yeyote yule
ambaye angekuwa na vigezo vyake na baada ya hapo kila mtu angeshika hamsini zake.
Usiku wa jana aliporudi kwenye hoteli ile aliyofikia iliyopo nyuma ya stendi kuu ya
mabasi yaendayo kasi eneo la Ubungo Koplo Tsega aliingia kwenye eneo la mgahawa
wa hoteli na kujipatia mlo wa nguvu kisha akashushia na kinywaji baridi huku akili
yake ikitafakari matukio yaliyopita.
Akiwa kwenye mgahawa ule akajikuta akikumbuka zile kukurukakara zilizotokea
kule nyumbani kwa Guzibert Kojo huku akijaribu kuwaza ni kwa namna gani polisi
na vyombo vya habari vitakavyolichukulia tukio lile. Akiwa katikati ya tafakari ile mara
akajikuta akimkumbuka yule mtu aliyekuwa akimfuatilia usiku wa jana tangu alipotoka
kule Vampire Casino huku akijiuliza kuwa mtu yule alikuwa nani na alikuwa akihitaji
nini kutoka kwake.
Halafu mawazo yake yakatoweshwa na taswira ya kijana mzuri handsome mhudumu
wa hotelini pale. Kijana mrefu na mweusi mwenye sura nzuri,kifua kipana kiasi chenye
misuli imara na macho ya huruma huku akiwa katika sare zake za kazi akiwahudumia
wateja.
Kijana yule alipokuwa akiinama ili aondoe vyombo na kusafisha meza aliyoketi Koplo Tsega. Koplo Tsega akabahatika kukiona kifua imara cha kijana yule
kilichohifadhiwa vyema ndani ya singlet yake nyeupe. Kukiona kifua cha kijana yule
hisia za mapenzi zikaanza kuitongoza nafsi yake na kujikuta akianza kumtamani
huku manukato yenye harufu nzuri ya kijana yule yakiziteka kabisa hisia zake. Kiu ya
mapenzi ikiwa imemnasa vilivyo Koplo Tsega akaamua kuvunja ukimya.
“Pole na kazi” Koplo Tsega akamwongelesha yule kijana wakati alipokuwa
akimalizia kufuta ile meza.
“Ahsante! dada yangu” kijana yule akaitikia kwa bashasha zote za kirafiki huku
akifikiria Tip ya mteja.
“Hivi wifi yangu akikuona unafanya kazi hizi si atakasirika?” Koplo Tsega
akachombeza utani.
“Ah! wapi mwanamke gani wa nyakati hizi utakayempata kwa mshahara wa
hotelini” yule kijana akaangua kicheko hafifu huku akiendelea kufuta ile meza aliyoketi
Koplo Tsega kwenye mgahawa ule.
“Kwa hiyo hujaoa wewe?” Koplo Tsega akauliza kwa sauti ya kubembeleza.
“Hao wasichana wenyewe wa kuoa wako wapi dada yangu. Sasa hivi kila msichana
unayemgusa hapa mjini anataka maisha mazuri utasema sisi wanaume hatuyataki hayo
maisha mazuri” yule kijana akaongea huku akionekana kufurahishwa na maongezi
yale. Ukimya kidogo ukapita kisha Koplo Tsega akavunja ukimya akimuuliza yule
kijana
“Unaitwa nani?”
“Mimi?” yule kijana akauliza kwa haya huku akijua fika kuwa ni yeye ndiye
aliyekuwa akiongeleshwa halafu walipotazamana akaachia tabasamu maridhawa
lililozidi kumchanganya vibaya Koplo Tsega.
“Naitwa Sikawa”
“Mh! jina lako tamu kama asali” Koplo Tsega akaongea huku akijitahidi kuilegeza
sauti yake ya kiafande.
“Acha utani dada yangu tangu lini jina la mtu likawa tamu kama asali” Sikawa
akaongea huku akiangua kicheko chake hafifu lakini kilichopeleka ujumbe kwa Koplo
Tsega kuwa yupo tayari kwa hatua inayofuata.
“Au hupendi nikusifie kuwa wewe ni mzuri?”
“Mh! hata sijui nisemeje dada yangu” Sikawa akaongea katika mazingira ya
kuruhusu urafiki kisha kitambo kifupi cha ukimya kikapita kabla ya Koplo Tsega
kuvunja tena ukimya.
“Utatoka kazini saa ngapi?”
“Saa nne usiku baada ya mwenzangu anayenipokea zamu kufika” Sikawa akaongea
kwa utulivu.
“Unaishi wapi hapa Dar es Salaam?”
“Nimepanga chumba mtaa wa mama Ngoma eneo la Mwenge” Sikawa akaongea
kwa utulivu huku akishindwa kuelewa muelekeo wa maongezi yale.
“Unaishi na nani?” Koplo Tsega akazidi kumdadisi Sikawa.
“Naishi peke yangu” Sikawa akaongea kwa utulivu huku akiutathmini uzuri wa
Koplo Tsega mbele yake.
“Usijali siku moja utampata mwenza wako. Mimi nipo chumba namba 18
ghorofa ya pili. Utakapotoka kazini kama hutojali unaweza kuja chumbani kwangu
tukabadilishana mawazo” Koplo Tsega akaongea kwa sauti ya kubembeleza kiasi cha
kuzivuruga hisia za Sikawa na kumfanya atabasamu.
“Sawa nitajitahidi” hatimaye Sikawa akaukubali mwaliko wa Koplo Tsega huku
akimaliza kufanya usafi juu ya ile meza na kuondoa vyombo kisha akaondoka na
kuelekea dirisha la jikoni.
Koplo Tsega akamsindikiza Sikawa kwa macho hadi pale alipotoweka mbele
yake huku wazimu wa mapenzi ukizitaabisha vibaya hisia zake. Kisha akasimama na
kuanza kuzitupa hatua zake za shibe kivivuvivu kuelekea chumbani kwake ghorofa
ya pili ya hoteli ile.
Tangu tukio la kifo cha Guzbert Kojo,Koplo Tsega alikuwa ameamua kutojitokeza
mitaani kwa muda wa siku mbili au zaidi huku akisubiri mambo yatulie kwanza.
_____
SAA TATU NA NUSU USIKU ILIPOTIMIA Koplo Tsega aliamka kutoka
kitandani alipokuwa amelala kwa muda wa masaa kadhaa akiupunguza uchovu.
Mawazo yake yalipotulia akamkumbuka Sikawa na hapo akageuka kuitazama saa
iliyokuwa imetundikwa ukutani mle chumbani. Muda mfupi baadaye alitarajia kuusikia
mlango wa chumba chake ukigongwa na Sikawa kuingia mle ndani. Hivyo akaamka
na kutandika kitanda chake vizuri kisha akawasha runinga iliyokuwa mle chumbani
juu ya meza fupi iliyokuwa kwenye kona na kuweka stesheni yenye muziki laini wa
kubembeleza.
Alipomaliza akapiga simu eneo la mapokezi na kuagizia mzinga mmoja wa
kinywaji kikali ambao wangeutumia kwa pamoja kusindikiza maongezi yao. Mzinga
huo wa pombe kali ulipoletwa na mmoja wa wahudumu wa hoteli ile Koplo Tsega
akaupokea na kuuweka juu ya meza fupi ya kioo iliyokuwa pembeni ya kochi moja la
sofa lililokuwa mle ndani pamoja na bilauri mbili kisha akaelekea bafuni kuoga.
Sikawa alikuwa ni kijana aliyekuwa akipapatikiwa sana na wanawake kutokana na
sura nzuri aliyokuwa nayo,umbo lake refu lenye kifua kipana kiasi,utanashati na tabia
yake ya ucheshi. Kwa vigezo hivyo wasichana warembo walimpenda na ama kwa
hakika alijua kucheza vizuri na hisia zao. Hivyo kwa haraka sana alikuwa ameitambua
shida ya Koplo Tsega na kwa kweli hakutaka bahati ile impite hivi hivi.
Uzuri wa Koplo Tsega ulikuwa umezikoroga vibaya hisia zake za mapenzi kiasi
kwamba kila wakati alijihisi ni kama alikuwa akimuona Koplo Tsega mbele yake. Kwa
tathmini yake ni kuwa wasichana wazuri na warembo wa sampuli ya Koplo Tsega
walikuwa wachache sana jijini Dar es Salaam na wengi wao walikuwa wakiwapenda
wanaume wenye pesa. Hivyo Sikawa akajiona ni kijana mwenye bahati sana kwa
kualikwa chumbani kwa Koplo Tsega. Akaendelea kufanya kazi zake kwa furaha huku mara kwa mara akipiga mruzi mwepesi mdomoni bila wafanyakazi wenzake
kufahamu kitu kilichokuwa kikiendelea wakati huo akiomba masaa yasogee mbele.
Ilipofika saa nne usiku Sikawa alikuwa nje ya mlango wa chumba namba 18 cha
hoteli ile ghorofa ya pili akigonga mlango.
“Karibu” sauti myepesi ya Koplo Tsega kutoka ndani ya chumba kile ikamfanya
Sikawa ajitengeneze vizuri. Wakati huu alikuwa amevaa nguo zake za uraiani;fulana
nyeupe,suruali nyeusi ya jeans na raba nyepesi miguuni.
Mlango wa chumba ulipofunguliwa Sikawa akajikuta akitazamana na macho laini
ya Koplo Tsega akiwa amejifunga kanga laini kifuani iliyolishika vema umbo lake
katika baadhi ya maeneo kutokana na ubichi wa mwili wake kwani ndiyo alikuwa
anatoka kuoga.
“Karibu ndani Sikawa,utanisamehe kidogo kwani ndiyo nilikuwa natoka kuoga”
Koplo Tsega akaongea kwa sauti laini ya kubembeleza huku tabasamu lake maridhawa
likielea usoni mwake.
“Oh! samahani kwa usumbufu bila shaka nimewahi sana” Sikawa akajibaraguza
huku akiingia mle ndani na wakati akifanya hivyo harufu nzuri ya sabuni ya kuogea ya
Koplo Tsega ikapenya puani mwake na kuamsha hisia mpya za mapenzi.
“Wala usijali kwani ungechelewa zaidi ya hapa ningekulaumu Sikawa” Koplo
Tsega akaongea huku akiangua kicheko hafifu na kuufunga ule mlango wa chumba.
“Ndiyo maana sikutaka kuchelewa” Sikawa akaangua kicheko chepesi cha
kistaarabu huku akielekea kuketi kwenye kochi moja la sofa lililokuwa mle ndani.
Koplo Tsega akiwa unaufahamu vizuri udhaifu wa wanaume mara baada ya kuufunga
mlango wa kile chumba akatembea taratibu kukizunguka kitanda cha mle ndani na
hatimaye kuketi kihasara kwenye pembe ya kile kitanda huku akiwa na hakika kuwa
macho ya Sikawa yalikuwa yakimsindikiza nyuma yake. Kisha akageuka ghafla na
kukutana na macho ya Sikawa yakimtazama. Sikawa kuona vile akashikwa na haya
huku akiyakwepesha macho yake haraka kutazama muziki uliokuwa ukirushwa
kwenye ile runinga ya mle chumbani ujasiri ukiwa umeanza kupungua.
Koplo Tsega alikuwa fundi mzuri wa kuanzisha maongezi hivyo akajikuta
akianzisha mada moja na kurukia nyingine huku macho yake mara kwa mara yakitua
juu ya kifua cha Sikawa. Sikawa naye hakuwa nyuma alimpatiliza vizuri Koplo Tsega
na pale alipohisi kuwa alikuwa mbioni kuishiwa hoja akazuga kwa kuinyanyua bilauri
ya kinywaji na kugida mafunda kadhaa huku macho yake mara kwa mara yakiutazama
mlima wa matiti ya wastani yaliyokuwa kifuani mwa Koplo Tsega.
Maongezi yao hayakuwa na hoja za maana lakini yaliendelea na kila mara Sikawa
alipojaribu kumdadisi Koplo Tsega kiundani zaidi alijikuta akiambulia patupu kama
siyo kudanganywa. Maongezi yalipoonekana kufifia muziki uliokuwa ukirushwa na
runinga ya mle chumbani ukarudisha uhai wa mandhari yale.
Hatimaye mshale wa saa ya ukutani mle chumbani ukasoma saa nane na robo usiku
na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha nje ikatengeneza kizingiti kingine kwa Sikawa
huku Koplo Tsega akionekana kufurahishwa na hali ile. Kile kilevi walichokuwa wakikitumia kikaanza taratibu kuwaondoa nishai kadiri muda ulivyokuwa ukisogea
mbele.
Hatimaye uvumilivu ukaondoka na kuwapelekea washindwe kuzidhibiti vyema
hisia zao. Sikawa akahamia pale kitandani huku akijidai anataka kuugemeza mgongo
wake baada ya kuchoka kukaa muda mrefu kwenye lile kochi la sofa mle chumbani.
Koplo Tsega naye akajifungua kanga yake kwa hila na kugeukia upande wa pili wa
kitanda huku akimpa mgongo Sikawa.
Nadharia ya somo la fizikia ya unlike charges attract each other hatimaye ikachukua
nafasi yake huku kila mmoja akiacha kuigiza. Muda mfupi uliyofuata shughuli ikaanza
pale kitandani kila mmoja akijitahidi kuonesha ufundi wa mapenzi kwa mwenzake.
Sikawa alikuwa fundi mzuri wa mapenzi aliyejua vizuri kumridhisha mwanamke
mwenye kiu ya mapenzi. Alimgeuza Koplo Tsega upande ule kisha akamkunja upande
huu halafu akamuinua hapa na kumkandamiza pale huku ndimi zao zikitekenyana
mdomoni na kutengeneza kiwango cha mwisho cha hisia za mapenzi kwenye miili
yao.
Mara ya kwanza,mara ya pili,mara ya tatu na walipofika mara ya nne walikuwa hoi
taaban hawajitambui kwa uchovu. Usingizi ukaja na kuwachukua huku kila mmoja
akiwa amelala kwa namna yake. Mvua kubwa ilikuwa ikiendelea kunyesha jijini Dar
es Salaam.
_____
Koplo Tsega ALIKUWA wa kwanza kuamka kutoka usingizini. Kitendo
cha kuuona mkono wa kiume juu ya titi lake kifuani kukamfanya amkumbuke
Sikawa,mhudumu wa hoteli ile aliyelala naye jana usiku.
Sikawa alikuwa hajitambui kwa uchovu na alikuwa akiachia sauti ya mkoromo
hafifu kinywani mwake huku miguu na mikono yake ameisambaza ovyo pale
kitandani.
Koplo Tsega akageuka na kumtazama Sikawa kwa makini pale kitandani huku
nafsi yake ikimsuta kwa kitendo cha kujirahisisha na hatimaye kugawa penzi lake
kwa kijana yule mhudumu wa hoteli. Hata hivyo kwa upande mwingine hakutaka
kujilaumu sana. Penzi zito la Sikawa lilikuwa limefanikiwa kukata kiu yake ya mapenzi
ya muda mrefu tangu alipoachana na mpenzi wake mara ya mwisho.
Koplo Tsega aliendelea kumtazama Sikawa pale kitandani huku uso wake
ukiumba tabasamu laini la shukrani. Mikiki mikiki ya usiku pale kitandani ilikuwa
imemuacha na uchovu wa aina yake. Kila kiungo cha mwilini alipojaribu kukisogeza
kilikuwa kikilalamika. Sikawa alikuwa ameitosheleza vizuri haja yake katika kila eneo
la mapenzi. Hata hivyo hisia mpya zilipomjia juu ya sababu iliyomrudisha jijini Dar
es Salaam zikamfanya aanze kuyapuuza matukio yote waliyoyafanya usiku yeye na
Sikawa.
Koplo Tsega akatupa shuka pembeni na kushuka kitandani. Kioo kikubwa
cha kabati lililokuwa mle ndani ukutani kikamfanya asimame kidogo na kuanzakujitathmini.
Macho yake makubwa bado yalikuwa legevu kwa uchovu,matiti yake madogo ya
wastani yalisimama wima kifuani pamoja na misukosuko ya Sikawa iliyoyapitia wakati
wa usiku. Kiuno chake chembamba kilichofuatiwa na mzigo wa wastani wa makalio
yake imara yaliyoshikiliwa na mihimili thabiti ya misuli ya mapaja yake yaliyonona
vikamfanya ajizungushe mbele ya kioo cha lile kabati huku akijitazama.
Matokeo ya tathmini yake kupitia taswira iliyojengeka kwenye kioo kile cha kabati
yakampelekea Koplo Tsega ajiridhishe kuwa bado alikuwa kwenye soko la uzuri kama
walivyokuwa wasichana wengine wa mijini.
Hatimaye Koplo Tsega akavinyoosha viungo vyake mwilini kwa mazoezi mepesi
kisha akaelekea maliwatoni huko ambako alimaliza haja zake zote pamoja na kuoga.
Koplo Tsega aliporudi kutoka maliwatoni akavaa bukta yake nyepesi na blauzi
yake mchinjo kisha akaelekea pale kitandani na kumwamsha Sikawa.
Sikawa alishtuka kutoka usingizini huku akiwa mwingi wa uchovu. Haraka
akayapeleka macho yake kuitazama saa ya ukutani iliyokuwa mle chumbani. Ilikuwa
ikielekea kutimia saa mbili asubuhi lakini alipokumbuka kuwa alikuwa na zamu
ya usiku ya kuingia kazini hakujipa haraka na badala yake akageuka pembeni yake
na kumtazama Koplo Tsega kwa macho yenye haya kidogo lakini yasiyojali kitu
chochote huku akitabasamu. Sikawa alitamani sana kuwa wangeendelea kulala mle
chumbani na kuendeleza starehe hata hivyo macho ya Koplo Tsega yalimuonya kuwa
hilo lisingewezekana tena kwa wakati ule.
“Umeamka saa ngapi?” Sikawa akavunja ukimya huku akitabasamu.
“Muda siyo mrefu”
“Mh! usingizi wa leo ulikuwa mzito kama wa Pono!” Sikawa akaongea huku
akivinyoosha viungo vyake mwilini na kuzipa uhai fikra zake pale kitandani.
“Mimi ndiyo hata sikumbuki kuwa ni wakati gani nilipitiwa na usingizi mpenzi”
Koplo Tsega akaongea kwa sauti nyepesi kisha walipotazamana usoni kila mmoja
akatabasamu kabla ya Koplo Tsega kuvunja ukimya.
“Amka ukaoge kumeshapambazuka”
“Asubuhi yote hii kwani tunakimbilia wapi?” Sikawa akauliza kichovuchovu.
“Huingii kazini leo?” Koplo Tsega akamuuliza Sikawa akiutazama mchoro wa
umbo la Sikawa ndani ya lile shuka la kitandani.
“Leo nina zamu ya usiku” Sikawa akajitetea.
“Hata hivyo kumeshapambazuka”
“Lakini mimi sina haraka!”
“Mimi nina haraka” Koplo Tsega akaongea kwa msisitizo huku hisia za mapenzi
zikiwa mbali naye.
“Sasa nani kakuzuia?’’ Sikawa akaongea kwa jazba akichukia kushurutishwa.
“Umeshasahau kuwa hapa siyo kwako!” Koplo Tsega akafoka.
“Lakini si ni wewe mwenyewe ndiye uliyeniita humu ndani?” Sikawa akauliza kwa
mshangao.
“Ndiyo! lakini ilikuwa jana siyo leo”
“Kwa hiyo haja yako ilikuwa ni ngono tu?”
“Pigia mstari” Koplo Tsega akaongea kwa jazba huku akihisi kuanza kukereka.
“Sasa kwanini hukuniambia mapema ili nijue?”
“Hata kama ungejua kwani ungekataa?”
“Sikiliza wewe dada…” Sikawa akaanza kujitetea hata hivyo alikatishwa.
“Nashukuru sana kwa penzi lako lakini muda wa starehe umeisha. Inuka
ukajiandae uondoke” Koplo Tsega akaongea huku haraka akiliondoa shuka mwilini
kwa Sikawa na hapo Sikawa akabaki akimshangaa kwa hasira.
“Sasa kama hutaki wanaume ilikuwaje ukajitongozesha kwangu?” Sikawa
akaongea kwa jazba.
“Nilikujua kuwa wewe ni malaya mwenzangu” Koplo Tsega akaongea kwa
msisitizo.
“Malaya ni wewe au mimi?” Sikawa akauliza kwa mshangao
“Simama ujiandae uende mpenzi malumbano hayatakusaidia kitu” Koplo
Tsega akaongea katika namna ya kupuuza hoja za Sikawa kwani alikuwa ameanza
kuwachukia tena wanaume baada ya kumkumbuka Kiango. Kiango alikuwa mpenzi
wake wa muda mrefu na mwanaume aliyemkabidhi moyo wake wote lakini siku moja
akaambulia kumfumania bila kificho akiivuruga amri ya sita na rafiki yake wa karibu.
“Hivi wewe malaya una wazimu?” Sikawa akauliza kwa hasira lakini kabla
hajamalizia kuongea ngumi mbili za korodani pale kitandani zikamfanya atulie kwa
sekunde kadhaa huku ameachama mdomo wake kama anayeimba wimbo wa taifa.
“Tafadhali! usiniite malaya wewe mpuuzi” Koplo Tsega akamuonya Sikawa huku
Sikawa akiendelea kugugumia kwa maumivu makali pale kitandani. Sikawa alipotaka
kufurukuta akatulizwa pale kitandani kama mtoto mdogo huku akishindwa kuamini
ubabe na nguvu za ajabu za msichana yule mbele yake. Hatimaye Sikawa akaacha
upinzani hivyo akaamka pale kitandani na kuelekea maliwatoni ambapo alimaliza haja
zake na kuoga ndani ya muda mfupi.
Aliporudi mle chumbani akamkuta Koplo Tsega akiwa amerejewa na utulivu
na bashasha zote za kirafiki huku akishindwa kumuelewa vizuri mwenyeji wake.
Walipotazamana tena wote wakajikuta wakitabasamu.
“Nisamehe mpenzi wangu” Koplo Tsega akaongea kwa sauti ya kubembeleza na
yenye urafiki ndani yake.
“Usijali lakini umeniumiza sana!” Sikawa akaongea kivivuvivu huku donge la
hasira limemnasa kooni.
“Pole mpenzi lakini nilitaka uamke mapema” Koplo Tsega akajitetea huku
akizunguka na kumkumbatia Sikawa kwa nyuma na hapo wote wakaondoa tofauti
zao huku wakitabasamu.
“Unajisikiaje kwa sasa?” Koplo Tsega akamuuliza Sikawa huku akiupeleka mkono
kuzishika korodani zake. Sikawa akiwa ameshtukia hali ile akajitoa mikononi mwa
Koplo Tsega haraka huku akiangua kicheko cha kimahaba.
KEVIN e. MPONDA
“Please don’t touch them,they are still very hot” Sikawa akaongea kwa ujivuni huku
akianza kuvaa nguo zake na hapo wote wakacheka.
“Mwenge unakaa sehemu gani?” Koplo Tsega akavunja ukimya.
“Mtaa wa mama Ngoma nyumba namba 11” Sikawa akaongea huku akiendelea
kuvaa nguo zake.
“Nikija kukutembelea kuna shida yoyote?” Koplo Tsega akauliza huku akiumba
tabasamu usoni.
“Shaka ondoa mpenzi” Sikawa akaongea kwa furaha.
“Naomba namba yako ya simu”
Sikawa hakusita badala yake akaanza kuitaja namba yake ya simu taratibu katika
namna ya kuhakikisha kuwa Koplo Tsega anazinakili namba zile bila usumbufu.
“Mchana utakuwa na ratiba gani?” Sikawa akauliza
“Bado sijafahamu ila huwenda nikawa na mizunguko ya hapa na pale” Koplo
Tsega akaongea kwa utulivu huku akifikiria jambo.
“Basi tutawasiliana mpenzi” Sikawa akaongea baada ya kumaliza kujiandaa.
“Ondoa shaka ila usije humu ndani hadi tuwasiliane kwanza”
“Kama jana?”
Sikawa akachombeza utani huku akielekea sehemu ulipokuwa mlango wa
kile chumba. Alipofika akaufungua ule mlango na kabla hajatoka nje akageuka na
kumkonyeza Koplo Tsega kimahaba kisha akatoka nje ya kile chumba na kutokomea
zake.
_____
MUDA MFUPI BAADA YA SIKAWA kuondoka mle chumbani Koplo Tsega
akaichukua ile kamera yake kutoka kwenye begi lake lililokuwa chini ya uvungu wa
kile kitanda na kuanza kufanya mapitio makini ya zile picha alizopiga usiku wa jana
nje ya Vampire Casino.
Ile kamera aina ya Toymaster ilikuwa imenasa picha nne safi na zenye ubora
wa kuaminika. Katika zile picha nne zilizokuwa kwenye ile kamera picha mbili
zilimuonesha msichana mmoja aliyevaa gauni fupi akishuka kutoka kwenye gari refu
na jeusi aina ya Texas Longhorn Tailgate Van huku akiwa ameongozana na wapambe
wawili waliovaa suti nadhifu kuificha miili yao imara iliyojengeka vema.
Picha nyingine mbili zilizosalia zilimuonesha msichana yule akisalimiana na
mwanaume mwingine aliyevaa suti nadhifu huku wale wapambe wakiwa wamesimama
kando yake.
Koplo Tsega akaendelea kuzitazama zile picha moja baada ya nyingine kwa utulivu
huku akijaribu kurudisha kumbukumbu zake. Muda mfupi uliyofuata baridi nyepesi
ikaanza kuusimanga mtima wake pale alipogundua kuwa msichana yule kwenye zile
picha ndiye yule aliyemuona kwenye habari picha za magazeti fulani huko siku za
nyuma.
Koplo Tsega akaendelea kukumbuka namna picha zile za magazetini zilivyokuwa zikimuonesha msichana yule wakati akiwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu
J.K.Nyerere huku akiwa ameongozana na kiongozi mmoja wa ngazi ya juu wa serikali
kuelekea nchi fulani ya ughaibuni katika safari ya kikazi ya kiongozi huyo.
Koplo Tsega akaendelea kukumbuka tena namna ambavyo habari za msichana
yule zilivyovuma huko siku za nyuma baada ya picha zake za ngono na mfanyabiashara
mmoja maarufu wa jijini Dar es Salaam kusambazwa mitandaoni kama rasimu ya
katiba mpya.
Koplo Tsega akajikuta akimkumbuka mwandishi wa habari aliyefahamika kwa
jina la Mtenzi Binagwa ambaye baadaye alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya
kusemekana kuwa ndiye yeye aliyehusika katika kuzipiga picha hizo na kuzieneza
mitandaoni.
Koplo Tsega akajikuta akizikumbuka picha hizo za utupu namna zilivyolitikisa jiji
la Dar es Salaam kwa muda wa wiki kadhaa na kupamba vichwa vya habari magazetini.
Kabla ya kwenda nchini D.R Congo Koplo Tsega akakumbuka kuwa yeye na
Sajenti Chacha Marwa walikuwa katika hatua za mwisho kabisa za kuonana na meneja
wa Vampire Casino baada ya kuhisi kuwa katika casino ile kulikuwa na mambo fulani
ya chinichini yaliyokuwa yakiendelea. Lakini walijikuta wakipigwa chenga na uongozi
wa casino ile mara kwa mara na walipokuwa wakijiandaa kutumia njia mbadala ndiyo
wakapokea wito wa kujumuishwa kwao kwenye mpango wa amani ya kudumu nchini
D.R Congo.
Akili yake ikiwa imezama kwenye tafakuri nzito Koplo Tsega akajikuta akipiga
mwayo mwepesi wa uchovu huku akiendelea kuzitumbulia macho zile picha za
kwenye ile kamera.
“
ANGALAU NIMEPUNGUZA HISIA ZANGU” Koplo Tsega alijisemea
moyoni baada ya mjadala mkubwa kumalizika nafsini mwake. Matukio ya jana
usiku yalikuwa yamemuacha hoi kwa uchovu baada ya kugaragazwa na kupindwa
katika kila namna ya mkao na mwanaume shababi mfanyakazi wa hoteli ile aliyelala
naye usiku kucha.
Tangu aliposalitiwa na mpenzi wake Koplo Tsega alikuwa ameapa kutojihusisha
tena na mapenzi katika maisha yake lakini hilo lilikuwa gumu kutekelezeka. Hisia
zikakataa kabisa kukubaliana na akili yake hivyo mapenzi akayageuza na kuyafanya
kama starehe nyingine ambapo angeyatafuta na kuyafanya na mwanaume yeyote yule
ambaye angekuwa na vigezo vyake na baada ya hapo kila mtu angeshika hamsini zake.
Usiku wa jana aliporudi kwenye hoteli ile aliyofikia iliyopo nyuma ya stendi kuu ya
mabasi yaendayo kasi eneo la Ubungo Koplo Tsega aliingia kwenye eneo la mgahawa
wa hoteli na kujipatia mlo wa nguvu kisha akashushia na kinywaji baridi huku akili
yake ikitafakari matukio yaliyopita.
Akiwa kwenye mgahawa ule akajikuta akikumbuka zile kukurukakara zilizotokea
kule nyumbani kwa Guzibert Kojo huku akijaribu kuwaza ni kwa namna gani polisi
na vyombo vya habari vitakavyolichukulia tukio lile. Akiwa katikati ya tafakari ile mara
akajikuta akimkumbuka yule mtu aliyekuwa akimfuatilia usiku wa jana tangu alipotoka
kule Vampire Casino huku akijiuliza kuwa mtu yule alikuwa nani na alikuwa akihitaji
nini kutoka kwake.
Halafu mawazo yake yakatoweshwa na taswira ya kijana mzuri handsome mhudumu
wa hotelini pale. Kijana mrefu na mweusi mwenye sura nzuri,kifua kipana kiasi chenye
misuli imara na macho ya huruma huku akiwa katika sare zake za kazi akiwahudumia
wateja.
Kijana yule alipokuwa akiinama ili aondoe vyombo na kusafisha meza aliyoketi Koplo Tsega. Koplo Tsega akabahatika kukiona kifua imara cha kijana yule
kilichohifadhiwa vyema ndani ya singlet yake nyeupe. Kukiona kifua cha kijana yule
hisia za mapenzi zikaanza kuitongoza nafsi yake na kujikuta akianza kumtamani
huku manukato yenye harufu nzuri ya kijana yule yakiziteka kabisa hisia zake. Kiu ya
mapenzi ikiwa imemnasa vilivyo Koplo Tsega akaamua kuvunja ukimya.
“Pole na kazi” Koplo Tsega akamwongelesha yule kijana wakati alipokuwa
akimalizia kufuta ile meza.
“Ahsante! dada yangu” kijana yule akaitikia kwa bashasha zote za kirafiki huku
akifikiria Tip ya mteja.
“Hivi wifi yangu akikuona unafanya kazi hizi si atakasirika?” Koplo Tsega
akachombeza utani.
“Ah! wapi mwanamke gani wa nyakati hizi utakayempata kwa mshahara wa
hotelini” yule kijana akaangua kicheko hafifu huku akiendelea kufuta ile meza aliyoketi
Koplo Tsega kwenye mgahawa ule.
“Kwa hiyo hujaoa wewe?” Koplo Tsega akauliza kwa sauti ya kubembeleza.
“Hao wasichana wenyewe wa kuoa wako wapi dada yangu. Sasa hivi kila msichana
unayemgusa hapa mjini anataka maisha mazuri utasema sisi wanaume hatuyataki hayo
maisha mazuri” yule kijana akaongea huku akionekana kufurahishwa na maongezi
yale. Ukimya kidogo ukapita kisha Koplo Tsega akavunja ukimya akimuuliza yule
kijana
“Unaitwa nani?”
“Mimi?” yule kijana akauliza kwa haya huku akijua fika kuwa ni yeye ndiye
aliyekuwa akiongeleshwa halafu walipotazamana akaachia tabasamu maridhawa
lililozidi kumchanganya vibaya Koplo Tsega.
“Naitwa Sikawa”
“Mh! jina lako tamu kama asali” Koplo Tsega akaongea huku akijitahidi kuilegeza
sauti yake ya kiafande.
“Acha utani dada yangu tangu lini jina la mtu likawa tamu kama asali” Sikawa
akaongea huku akiangua kicheko chake hafifu lakini kilichopeleka ujumbe kwa Koplo
Tsega kuwa yupo tayari kwa hatua inayofuata.
“Au hupendi nikusifie kuwa wewe ni mzuri?”
“Mh! hata sijui nisemeje dada yangu” Sikawa akaongea katika mazingira ya
kuruhusu urafiki kisha kitambo kifupi cha ukimya kikapita kabla ya Koplo Tsega
kuvunja tena ukimya.
“Utatoka kazini saa ngapi?”
“Saa nne usiku baada ya mwenzangu anayenipokea zamu kufika” Sikawa akaongea
kwa utulivu.
“Unaishi wapi hapa Dar es Salaam?”
“Nimepanga chumba mtaa wa mama Ngoma eneo la Mwenge” Sikawa akaongea
kwa utulivu huku akishindwa kuelewa muelekeo wa maongezi yale.
“Unaishi na nani?” Koplo Tsega akazidi kumdadisi Sikawa.
“Naishi peke yangu” Sikawa akaongea kwa utulivu huku akiutathmini uzuri wa
Koplo Tsega mbele yake.
“Usijali siku moja utampata mwenza wako. Mimi nipo chumba namba 18
ghorofa ya pili. Utakapotoka kazini kama hutojali unaweza kuja chumbani kwangu
tukabadilishana mawazo” Koplo Tsega akaongea kwa sauti ya kubembeleza kiasi cha
kuzivuruga hisia za Sikawa na kumfanya atabasamu.
“Sawa nitajitahidi” hatimaye Sikawa akaukubali mwaliko wa Koplo Tsega huku
akimaliza kufanya usafi juu ya ile meza na kuondoa vyombo kisha akaondoka na
kuelekea dirisha la jikoni.
Koplo Tsega akamsindikiza Sikawa kwa macho hadi pale alipotoweka mbele
yake huku wazimu wa mapenzi ukizitaabisha vibaya hisia zake. Kisha akasimama na
kuanza kuzitupa hatua zake za shibe kivivuvivu kuelekea chumbani kwake ghorofa
ya pili ya hoteli ile.
Tangu tukio la kifo cha Guzbert Kojo,Koplo Tsega alikuwa ameamua kutojitokeza
mitaani kwa muda wa siku mbili au zaidi huku akisubiri mambo yatulie kwanza.
_____
SAA TATU NA NUSU USIKU ILIPOTIMIA Koplo Tsega aliamka kutoka
kitandani alipokuwa amelala kwa muda wa masaa kadhaa akiupunguza uchovu.
Mawazo yake yalipotulia akamkumbuka Sikawa na hapo akageuka kuitazama saa
iliyokuwa imetundikwa ukutani mle chumbani. Muda mfupi baadaye alitarajia kuusikia
mlango wa chumba chake ukigongwa na Sikawa kuingia mle ndani. Hivyo akaamka
na kutandika kitanda chake vizuri kisha akawasha runinga iliyokuwa mle chumbani
juu ya meza fupi iliyokuwa kwenye kona na kuweka stesheni yenye muziki laini wa
kubembeleza.
Alipomaliza akapiga simu eneo la mapokezi na kuagizia mzinga mmoja wa
kinywaji kikali ambao wangeutumia kwa pamoja kusindikiza maongezi yao. Mzinga
huo wa pombe kali ulipoletwa na mmoja wa wahudumu wa hoteli ile Koplo Tsega
akaupokea na kuuweka juu ya meza fupi ya kioo iliyokuwa pembeni ya kochi moja la
sofa lililokuwa mle ndani pamoja na bilauri mbili kisha akaelekea bafuni kuoga.
Sikawa alikuwa ni kijana aliyekuwa akipapatikiwa sana na wanawake kutokana na
sura nzuri aliyokuwa nayo,umbo lake refu lenye kifua kipana kiasi,utanashati na tabia
yake ya ucheshi. Kwa vigezo hivyo wasichana warembo walimpenda na ama kwa
hakika alijua kucheza vizuri na hisia zao. Hivyo kwa haraka sana alikuwa ameitambua
shida ya Koplo Tsega na kwa kweli hakutaka bahati ile impite hivi hivi.
Uzuri wa Koplo Tsega ulikuwa umezikoroga vibaya hisia zake za mapenzi kiasi
kwamba kila wakati alijihisi ni kama alikuwa akimuona Koplo Tsega mbele yake. Kwa
tathmini yake ni kuwa wasichana wazuri na warembo wa sampuli ya Koplo Tsega
walikuwa wachache sana jijini Dar es Salaam na wengi wao walikuwa wakiwapenda
wanaume wenye pesa. Hivyo Sikawa akajiona ni kijana mwenye bahati sana kwa
kualikwa chumbani kwa Koplo Tsega. Akaendelea kufanya kazi zake kwa furaha huku mara kwa mara akipiga mruzi mwepesi mdomoni bila wafanyakazi wenzake
kufahamu kitu kilichokuwa kikiendelea wakati huo akiomba masaa yasogee mbele.
Ilipofika saa nne usiku Sikawa alikuwa nje ya mlango wa chumba namba 18 cha
hoteli ile ghorofa ya pili akigonga mlango.
“Karibu” sauti myepesi ya Koplo Tsega kutoka ndani ya chumba kile ikamfanya
Sikawa ajitengeneze vizuri. Wakati huu alikuwa amevaa nguo zake za uraiani;fulana
nyeupe,suruali nyeusi ya jeans na raba nyepesi miguuni.
Mlango wa chumba ulipofunguliwa Sikawa akajikuta akitazamana na macho laini
ya Koplo Tsega akiwa amejifunga kanga laini kifuani iliyolishika vema umbo lake
katika baadhi ya maeneo kutokana na ubichi wa mwili wake kwani ndiyo alikuwa
anatoka kuoga.
“Karibu ndani Sikawa,utanisamehe kidogo kwani ndiyo nilikuwa natoka kuoga”
Koplo Tsega akaongea kwa sauti laini ya kubembeleza huku tabasamu lake maridhawa
likielea usoni mwake.
“Oh! samahani kwa usumbufu bila shaka nimewahi sana” Sikawa akajibaraguza
huku akiingia mle ndani na wakati akifanya hivyo harufu nzuri ya sabuni ya kuogea ya
Koplo Tsega ikapenya puani mwake na kuamsha hisia mpya za mapenzi.
“Wala usijali kwani ungechelewa zaidi ya hapa ningekulaumu Sikawa” Koplo
Tsega akaongea huku akiangua kicheko hafifu na kuufunga ule mlango wa chumba.
“Ndiyo maana sikutaka kuchelewa” Sikawa akaangua kicheko chepesi cha
kistaarabu huku akielekea kuketi kwenye kochi moja la sofa lililokuwa mle ndani.
Koplo Tsega akiwa unaufahamu vizuri udhaifu wa wanaume mara baada ya kuufunga
mlango wa kile chumba akatembea taratibu kukizunguka kitanda cha mle ndani na
hatimaye kuketi kihasara kwenye pembe ya kile kitanda huku akiwa na hakika kuwa
macho ya Sikawa yalikuwa yakimsindikiza nyuma yake. Kisha akageuka ghafla na
kukutana na macho ya Sikawa yakimtazama. Sikawa kuona vile akashikwa na haya
huku akiyakwepesha macho yake haraka kutazama muziki uliokuwa ukirushwa
kwenye ile runinga ya mle chumbani ujasiri ukiwa umeanza kupungua.
Koplo Tsega alikuwa fundi mzuri wa kuanzisha maongezi hivyo akajikuta
akianzisha mada moja na kurukia nyingine huku macho yake mara kwa mara yakitua
juu ya kifua cha Sikawa. Sikawa naye hakuwa nyuma alimpatiliza vizuri Koplo Tsega
na pale alipohisi kuwa alikuwa mbioni kuishiwa hoja akazuga kwa kuinyanyua bilauri
ya kinywaji na kugida mafunda kadhaa huku macho yake mara kwa mara yakiutazama
mlima wa matiti ya wastani yaliyokuwa kifuani mwa Koplo Tsega.
Maongezi yao hayakuwa na hoja za maana lakini yaliendelea na kila mara Sikawa
alipojaribu kumdadisi Koplo Tsega kiundani zaidi alijikuta akiambulia patupu kama
siyo kudanganywa. Maongezi yalipoonekana kufifia muziki uliokuwa ukirushwa na
runinga ya mle chumbani ukarudisha uhai wa mandhari yale.
Hatimaye mshale wa saa ya ukutani mle chumbani ukasoma saa nane na robo usiku
na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha nje ikatengeneza kizingiti kingine kwa Sikawa
huku Koplo Tsega akionekana kufurahishwa na hali ile. Kile kilevi walichokuwa wakikitumia kikaanza taratibu kuwaondoa nishai kadiri muda ulivyokuwa ukisogea
mbele.
Hatimaye uvumilivu ukaondoka na kuwapelekea washindwe kuzidhibiti vyema
hisia zao. Sikawa akahamia pale kitandani huku akijidai anataka kuugemeza mgongo
wake baada ya kuchoka kukaa muda mrefu kwenye lile kochi la sofa mle chumbani.
Koplo Tsega naye akajifungua kanga yake kwa hila na kugeukia upande wa pili wa
kitanda huku akimpa mgongo Sikawa.
Nadharia ya somo la fizikia ya unlike charges attract each other hatimaye ikachukua
nafasi yake huku kila mmoja akiacha kuigiza. Muda mfupi uliyofuata shughuli ikaanza
pale kitandani kila mmoja akijitahidi kuonesha ufundi wa mapenzi kwa mwenzake.
Sikawa alikuwa fundi mzuri wa mapenzi aliyejua vizuri kumridhisha mwanamke
mwenye kiu ya mapenzi. Alimgeuza Koplo Tsega upande ule kisha akamkunja upande
huu halafu akamuinua hapa na kumkandamiza pale huku ndimi zao zikitekenyana
mdomoni na kutengeneza kiwango cha mwisho cha hisia za mapenzi kwenye miili
yao.
Mara ya kwanza,mara ya pili,mara ya tatu na walipofika mara ya nne walikuwa hoi
taaban hawajitambui kwa uchovu. Usingizi ukaja na kuwachukua huku kila mmoja
akiwa amelala kwa namna yake. Mvua kubwa ilikuwa ikiendelea kunyesha jijini Dar
es Salaam.
_____
Koplo Tsega ALIKUWA wa kwanza kuamka kutoka usingizini. Kitendo
cha kuuona mkono wa kiume juu ya titi lake kifuani kukamfanya amkumbuke
Sikawa,mhudumu wa hoteli ile aliyelala naye jana usiku.
Sikawa alikuwa hajitambui kwa uchovu na alikuwa akiachia sauti ya mkoromo
hafifu kinywani mwake huku miguu na mikono yake ameisambaza ovyo pale
kitandani.
Koplo Tsega akageuka na kumtazama Sikawa kwa makini pale kitandani huku
nafsi yake ikimsuta kwa kitendo cha kujirahisisha na hatimaye kugawa penzi lake
kwa kijana yule mhudumu wa hoteli. Hata hivyo kwa upande mwingine hakutaka
kujilaumu sana. Penzi zito la Sikawa lilikuwa limefanikiwa kukata kiu yake ya mapenzi
ya muda mrefu tangu alipoachana na mpenzi wake mara ya mwisho.
Koplo Tsega aliendelea kumtazama Sikawa pale kitandani huku uso wake
ukiumba tabasamu laini la shukrani. Mikiki mikiki ya usiku pale kitandani ilikuwa
imemuacha na uchovu wa aina yake. Kila kiungo cha mwilini alipojaribu kukisogeza
kilikuwa kikilalamika. Sikawa alikuwa ameitosheleza vizuri haja yake katika kila eneo
la mapenzi. Hata hivyo hisia mpya zilipomjia juu ya sababu iliyomrudisha jijini Dar
es Salaam zikamfanya aanze kuyapuuza matukio yote waliyoyafanya usiku yeye na
Sikawa.
Koplo Tsega akatupa shuka pembeni na kushuka kitandani. Kioo kikubwa
cha kabati lililokuwa mle ndani ukutani kikamfanya asimame kidogo na kuanzakujitathmini.
Macho yake makubwa bado yalikuwa legevu kwa uchovu,matiti yake madogo ya
wastani yalisimama wima kifuani pamoja na misukosuko ya Sikawa iliyoyapitia wakati
wa usiku. Kiuno chake chembamba kilichofuatiwa na mzigo wa wastani wa makalio
yake imara yaliyoshikiliwa na mihimili thabiti ya misuli ya mapaja yake yaliyonona
vikamfanya ajizungushe mbele ya kioo cha lile kabati huku akijitazama.
Matokeo ya tathmini yake kupitia taswira iliyojengeka kwenye kioo kile cha kabati
yakampelekea Koplo Tsega ajiridhishe kuwa bado alikuwa kwenye soko la uzuri kama
walivyokuwa wasichana wengine wa mijini.
Hatimaye Koplo Tsega akavinyoosha viungo vyake mwilini kwa mazoezi mepesi
kisha akaelekea maliwatoni huko ambako alimaliza haja zake zote pamoja na kuoga.
Koplo Tsega aliporudi kutoka maliwatoni akavaa bukta yake nyepesi na blauzi
yake mchinjo kisha akaelekea pale kitandani na kumwamsha Sikawa.
Sikawa alishtuka kutoka usingizini huku akiwa mwingi wa uchovu. Haraka
akayapeleka macho yake kuitazama saa ya ukutani iliyokuwa mle chumbani. Ilikuwa
ikielekea kutimia saa mbili asubuhi lakini alipokumbuka kuwa alikuwa na zamu
ya usiku ya kuingia kazini hakujipa haraka na badala yake akageuka pembeni yake
na kumtazama Koplo Tsega kwa macho yenye haya kidogo lakini yasiyojali kitu
chochote huku akitabasamu. Sikawa alitamani sana kuwa wangeendelea kulala mle
chumbani na kuendeleza starehe hata hivyo macho ya Koplo Tsega yalimuonya kuwa
hilo lisingewezekana tena kwa wakati ule.
“Umeamka saa ngapi?” Sikawa akavunja ukimya huku akitabasamu.
“Muda siyo mrefu”
“Mh! usingizi wa leo ulikuwa mzito kama wa Pono!” Sikawa akaongea huku
akivinyoosha viungo vyake mwilini na kuzipa uhai fikra zake pale kitandani.
“Mimi ndiyo hata sikumbuki kuwa ni wakati gani nilipitiwa na usingizi mpenzi”
Koplo Tsega akaongea kwa sauti nyepesi kisha walipotazamana usoni kila mmoja
akatabasamu kabla ya Koplo Tsega kuvunja ukimya.
“Amka ukaoge kumeshapambazuka”
“Asubuhi yote hii kwani tunakimbilia wapi?” Sikawa akauliza kichovuchovu.
“Huingii kazini leo?” Koplo Tsega akamuuliza Sikawa akiutazama mchoro wa
umbo la Sikawa ndani ya lile shuka la kitandani.
“Leo nina zamu ya usiku” Sikawa akajitetea.
“Hata hivyo kumeshapambazuka”
“Lakini mimi sina haraka!”
“Mimi nina haraka” Koplo Tsega akaongea kwa msisitizo huku hisia za mapenzi
zikiwa mbali naye.
“Sasa nani kakuzuia?’’ Sikawa akaongea kwa jazba akichukia kushurutishwa.
“Umeshasahau kuwa hapa siyo kwako!” Koplo Tsega akafoka.
“Lakini si ni wewe mwenyewe ndiye uliyeniita humu ndani?” Sikawa akauliza kwa
mshangao.
“Ndiyo! lakini ilikuwa jana siyo leo”
“Kwa hiyo haja yako ilikuwa ni ngono tu?”
“Pigia mstari” Koplo Tsega akaongea kwa jazba huku akihisi kuanza kukereka.
“Sasa kwanini hukuniambia mapema ili nijue?”
“Hata kama ungejua kwani ungekataa?”
“Sikiliza wewe dada…” Sikawa akaanza kujitetea hata hivyo alikatishwa.
“Nashukuru sana kwa penzi lako lakini muda wa starehe umeisha. Inuka
ukajiandae uondoke” Koplo Tsega akaongea huku haraka akiliondoa shuka mwilini
kwa Sikawa na hapo Sikawa akabaki akimshangaa kwa hasira.
“Sasa kama hutaki wanaume ilikuwaje ukajitongozesha kwangu?” Sikawa
akaongea kwa jazba.
“Nilikujua kuwa wewe ni malaya mwenzangu” Koplo Tsega akaongea kwa
msisitizo.
“Malaya ni wewe au mimi?” Sikawa akauliza kwa mshangao
“Simama ujiandae uende mpenzi malumbano hayatakusaidia kitu” Koplo
Tsega akaongea katika namna ya kupuuza hoja za Sikawa kwani alikuwa ameanza
kuwachukia tena wanaume baada ya kumkumbuka Kiango. Kiango alikuwa mpenzi
wake wa muda mrefu na mwanaume aliyemkabidhi moyo wake wote lakini siku moja
akaambulia kumfumania bila kificho akiivuruga amri ya sita na rafiki yake wa karibu.
“Hivi wewe malaya una wazimu?” Sikawa akauliza kwa hasira lakini kabla
hajamalizia kuongea ngumi mbili za korodani pale kitandani zikamfanya atulie kwa
sekunde kadhaa huku ameachama mdomo wake kama anayeimba wimbo wa taifa.
“Tafadhali! usiniite malaya wewe mpuuzi” Koplo Tsega akamuonya Sikawa huku
Sikawa akiendelea kugugumia kwa maumivu makali pale kitandani. Sikawa alipotaka
kufurukuta akatulizwa pale kitandani kama mtoto mdogo huku akishindwa kuamini
ubabe na nguvu za ajabu za msichana yule mbele yake. Hatimaye Sikawa akaacha
upinzani hivyo akaamka pale kitandani na kuelekea maliwatoni ambapo alimaliza haja
zake na kuoga ndani ya muda mfupi.
Aliporudi mle chumbani akamkuta Koplo Tsega akiwa amerejewa na utulivu
na bashasha zote za kirafiki huku akishindwa kumuelewa vizuri mwenyeji wake.
Walipotazamana tena wote wakajikuta wakitabasamu.
“Nisamehe mpenzi wangu” Koplo Tsega akaongea kwa sauti ya kubembeleza na
yenye urafiki ndani yake.
“Usijali lakini umeniumiza sana!” Sikawa akaongea kivivuvivu huku donge la
hasira limemnasa kooni.
“Pole mpenzi lakini nilitaka uamke mapema” Koplo Tsega akajitetea huku
akizunguka na kumkumbatia Sikawa kwa nyuma na hapo wote wakaondoa tofauti
zao huku wakitabasamu.
“Unajisikiaje kwa sasa?” Koplo Tsega akamuuliza Sikawa huku akiupeleka mkono
kuzishika korodani zake. Sikawa akiwa ameshtukia hali ile akajitoa mikononi mwa
Koplo Tsega haraka huku akiangua kicheko cha kimahaba.
KEVIN e. MPONDA
“Please don’t touch them,they are still very hot” Sikawa akaongea kwa ujivuni huku
akianza kuvaa nguo zake na hapo wote wakacheka.
“Mwenge unakaa sehemu gani?” Koplo Tsega akavunja ukimya.
“Mtaa wa mama Ngoma nyumba namba 11” Sikawa akaongea huku akiendelea
kuvaa nguo zake.
“Nikija kukutembelea kuna shida yoyote?” Koplo Tsega akauliza huku akiumba
tabasamu usoni.
“Shaka ondoa mpenzi” Sikawa akaongea kwa furaha.
“Naomba namba yako ya simu”
Sikawa hakusita badala yake akaanza kuitaja namba yake ya simu taratibu katika
namna ya kuhakikisha kuwa Koplo Tsega anazinakili namba zile bila usumbufu.
“Mchana utakuwa na ratiba gani?” Sikawa akauliza
“Bado sijafahamu ila huwenda nikawa na mizunguko ya hapa na pale” Koplo
Tsega akaongea kwa utulivu huku akifikiria jambo.
“Basi tutawasiliana mpenzi” Sikawa akaongea baada ya kumaliza kujiandaa.
“Ondoa shaka ila usije humu ndani hadi tuwasiliane kwanza”
“Kama jana?”
Sikawa akachombeza utani huku akielekea sehemu ulipokuwa mlango wa
kile chumba. Alipofika akaufungua ule mlango na kabla hajatoka nje akageuka na
kumkonyeza Koplo Tsega kimahaba kisha akatoka nje ya kile chumba na kutokomea
zake.
_____
MUDA MFUPI BAADA YA SIKAWA kuondoka mle chumbani Koplo Tsega
akaichukua ile kamera yake kutoka kwenye begi lake lililokuwa chini ya uvungu wa
kile kitanda na kuanza kufanya mapitio makini ya zile picha alizopiga usiku wa jana
nje ya Vampire Casino.
Ile kamera aina ya Toymaster ilikuwa imenasa picha nne safi na zenye ubora
wa kuaminika. Katika zile picha nne zilizokuwa kwenye ile kamera picha mbili
zilimuonesha msichana mmoja aliyevaa gauni fupi akishuka kutoka kwenye gari refu
na jeusi aina ya Texas Longhorn Tailgate Van huku akiwa ameongozana na wapambe
wawili waliovaa suti nadhifu kuificha miili yao imara iliyojengeka vema.
Picha nyingine mbili zilizosalia zilimuonesha msichana yule akisalimiana na
mwanaume mwingine aliyevaa suti nadhifu huku wale wapambe wakiwa wamesimama
kando yake.
Koplo Tsega akaendelea kuzitazama zile picha moja baada ya nyingine kwa utulivu
huku akijaribu kurudisha kumbukumbu zake. Muda mfupi uliyofuata baridi nyepesi
ikaanza kuusimanga mtima wake pale alipogundua kuwa msichana yule kwenye zile
picha ndiye yule aliyemuona kwenye habari picha za magazeti fulani huko siku za
nyuma.
Koplo Tsega akaendelea kukumbuka namna picha zile za magazetini zilivyokuwa zikimuonesha msichana yule wakati akiwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu
J.K.Nyerere huku akiwa ameongozana na kiongozi mmoja wa ngazi ya juu wa serikali
kuelekea nchi fulani ya ughaibuni katika safari ya kikazi ya kiongozi huyo.
Koplo Tsega akaendelea kukumbuka tena namna ambavyo habari za msichana
yule zilivyovuma huko siku za nyuma baada ya picha zake za ngono na mfanyabiashara
mmoja maarufu wa jijini Dar es Salaam kusambazwa mitandaoni kama rasimu ya
katiba mpya.
Koplo Tsega akajikuta akimkumbuka mwandishi wa habari aliyefahamika kwa
jina la Mtenzi Binagwa ambaye baadaye alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya
kusemekana kuwa ndiye yeye aliyehusika katika kuzipiga picha hizo na kuzieneza
mitandaoni.
Koplo Tsega akajikuta akizikumbuka picha hizo za utupu namna zilivyolitikisa jiji
la Dar es Salaam kwa muda wa wiki kadhaa na kupamba vichwa vya habari magazetini.
Kabla ya kwenda nchini D.R Congo Koplo Tsega akakumbuka kuwa yeye na
Sajenti Chacha Marwa walikuwa katika hatua za mwisho kabisa za kuonana na meneja
wa Vampire Casino baada ya kuhisi kuwa katika casino ile kulikuwa na mambo fulani
ya chinichini yaliyokuwa yakiendelea. Lakini walijikuta wakipigwa chenga na uongozi
wa casino ile mara kwa mara na walipokuwa wakijiandaa kutumia njia mbadala ndiyo
wakapokea wito wa kujumuishwa kwao kwenye mpango wa amani ya kudumu nchini
D.R Congo.
Akili yake ikiwa imezama kwenye tafakuri nzito Koplo Tsega akajikuta akipiga
mwayo mwepesi wa uchovu huku akiendelea kuzitumbulia macho zile picha za
kwenye ile kamera.