Riwaya: Konstebo Zungu

Riwaya: Konstebo Zungu

SEHEMU YA KUMI NA TISA

Na hapo akayabwaga makaratasi kadhaa mbele ya maaskari wenzake na Kobo akayashuhudia.
Alikuwa ni mnyonge lakini haya yalimtia unyonge zaidi.
Mikataba!
Mikataba baina yake na mmiliki wa nyumba aliyokuwa akiishi hawara yake.
Koplo Zubeda!
Alitamani ardhi ifunguke atumbukie humo, alijiona waziwazi kuwa alikuwa anaelekea pabaya.
Kwanza alidanganya kuwa hana makazi mengine zaidi ya hayo, pili mikataba yote aliiandikisha kwa majina yake na si ya Zubeda.
Mkataba wa mwisho aliuandikisha miezi miwili tu iliyopita.
Anakwepa vipi rungu la sheria?
Watamuhesabu kama mnyang'anyi ambaye analo eneo la siri kwa ajiri ya kufanyia shughuli zake haramu.
Inspekta Kobo akaumia zaidi kwa sababu alikuwa anakwenda kumweka Koplo Zubeda na maaskari aliowaweka kumlinda matatani.
Wote hawa watahesabika kuwa ni chama kimoja cha kimafia na wataminywa kama alivyominywa yeye hadi kufikia hapo alipo.
Akaunganisha meno yake kwa uchungu mkubwa.
"Tunaenda moja kwa moja hadi katika nyumba hii. Ukithubutu kutudanganya utajutia uongo wako" Akachimbwa mkwara, akamtazama yule bwana kwa jicho kali, akajilaumu sana kwa sababu alikuwa na pingu, vinginevyo angefanya shambulizi kwake.
Hakupendelea masuala ya kuchimbwa mkwara!
Inspekta Kobo akawaelekeza nyumba ile inapopatikana, na hata asingewaelekeza bado kuna namba ya nyumba iliorodheshwa katika ile mikataba.
Bila kusahau kiherehere cha mmiliki wa nyumba ile kuweka nambari yake sahihi kabisa ya simu ya mkononi na ile ya ofisi.
Wakatoweka kuelekea nyumbani kwa Zubeda!
____
ZUBEDA hakuamini macho yake pindi alipomshuhudia inspekta Kobo akishushwa garini huku akiwa hajiwezi walau kutembea, nguo yake kwa mbali kabisa ilionekana kumpwaya, na ilikuwa imefubaa huku mabakamabaka yaliyoashiria kugandiana kwa damu yalionekana.
Donge la uchungu likamkaba kooni, akajikuta yungali katika mfadhaiko mkubwa sana.
Hakujua ni kwanini Kobo yu katika hali ile lakini kichwani aliitabiri kuwa haikuwa ya heri hata kidogo.
"Martin...... Inspekta Kobo..." Alimwita kutoka pale alipokuwa ameinama bafuni.
Martin akajikuta akisimama wima na hapo akawa amejitonesha mbavu zilizokuwa katika maumivu makali.
Hakujikunja tena, akanyoosha shingo akakiona kile ambacho Zubeda alikuwa anakiona.
Mpango huu ulikuwa maridhawa kabisa.
"Hatuchomoki!" Zubeda alijikuta akitokwa na kauli ile ya kukata tamaa.
Kauli ile haikuelea sana hewani kabla mlipuko mkubwa haujasikika na palepale askari wawili walio katika sare wakaanguka chini.
Mmoja aliyekuwa amemshika Kobo ili aweze kutembea alimwachia na Kobo akatua chini mzimamzima.
Akatulia!
Hapoikazuka vita mpya, Nguzu na Zubeda wakashindwa kuelewa hii vita inahusisha pande ngapi.
Wakati wanaamini kuwa ni pande mbili pekee sasa wanashangaa kuwa wao hawahusishwi na wakati huohuo vita inaendelea.
Milio ya risasi za kuviziana ikaendelea huku askari wakipokea amri kalikali kutoka kwa kiongozi wao.
Mambo yalikuwa magumu haswa!
Asakari walikuwa wamepagawa, ni kama walikuwa hawajatarajia upinzani wa aina ile kutoka katika nyumba ile aliyokuwa akiishi Zubeda.
_______
HAKUWA katika mavazi yake yaliyowatisha wengi pindi walipomuona, hakuwa katika kiti chake cha kuzunguka huku akipokea taarifa zilizopaswa kumfikia yeye na kisha kutoa maamuzi.
Hakuwa katika nafasi yake ya kuwasiliana na raisi wa jamuhuri wa muungano.
Alikuwa katika fulana yake pamoja na bukta laini, na alikuwa chumbani kwake.
Vyeo vyote aliamua kuviweka kando.
Alichoingia nacho pale chumbani ni thamani ya urafiki.
Hakuwa na roho mbaya, na hilo alilitambua vyema bali alikuwa ni mtu anayesimamia haki na usawa.
Ukimwona ana roho mbaya kwa sababu tu amekushinda kwa kuusema ukweli basi alikuwa tayari kuonekana hivyo.
Aliijua mipaka yake vyema, hakuwa shabiki wa mateso wala vifo vya hovyohovyo.
Alikuwa na weledi wa kutosha na hii haikuwashangaza wenzake baada ya kusikia jina lake likitajwa kuwa atakuwa mkuu wa majeshi ya polisi.
Hata yeye hakushangaa, maana hakupewa cheo kile kwa bahati mbaya.
Alistahili!
Sasa alikuwa hayafikirii yote haya, alikuwa akimfikiria Kobo, ambaye alitokea kuwa rafiki yake sana mpaka mtafaruku ulivyokuja kuwaweka mbali kidogo kisha madaraka yakahakikisha wapo mbali kabisa.
Kwa kufumba ama kufumbua macho IGP hakuacha kuiona sura ya Kobo ikiitaka huruma yake, akayakumbuka maneno ya Kobo juu ya mkewe ambaye yu katika kuzimia.
"Nampenda sana mke wangu, ninapaswa kumuomba msamaha. Kama haitafaa mimi kubaki huru nakusihi rafiki yangu na mkuu wangu nifanyie upendeleo nisining'inie katika kitanzi kabla mke wangu hajazinduka."
Maneno haya yalimuumiza mno, akajaribu kuelekeza macho huku na kule ili asahau kuhusu Kobo lakini akajikuta akilitazama tukio la Kobo kujitoa muhanga na kumsukuma kando ili asipatwe na risasi iliyomkusudia.
Akajikaza hisia zisimwendeshe lakini chozi likamsaliti.
Akajikuta analia!
Akayakumbuka maneno makali ya Kobo juu yake alipomwambia kuhusu pambazuko baya kupindukia.
"Jitazame yawezekana pambazuko hili likakuandama wewe pindi utakapogundua kuwa sikuwa nyuma ya maovu haya."
IGP akasimama na kujifuta machozi pamoja na jasho lililoanza kumtoka.
Akachukua simu yake na kumpigia msaidizi wake, ambaye pia alikuwa ni rafikii yake nje ya madaraka hayo.
Akajaribu kumweleza kwa kifupi, akaeleweka na hatimaye wakachukua maamuzi ya kutuma watu watatu wa ziada katika tukio hili kutazama jinsi linavyokwenda.
Walikuwa ni vijana wanaoaminika sana kiuwezo katika mapambano na pia katika umakini.
Walau IGP aliweza kulala vyema baada ya kufanya hatua za mwisho kabisa za kutambua ikiwa Kobo anastahili jela ama la?
Majira ya saa kumi jioni alishtuliwa na simu yake ya mkononi.
Ni nambari aliyompatia msaidizi wake ili lolote litakalotokea waweze kupeana taarifa.
Akaipokea upesi ile simu.
"KIjana mmoja ameuwawa na mwingine amejeruhiwa begani." Taarifa ile ilimtisha mno IGP.
Alitambua kuwa jambo hili lina uzito lakini hakukadiria uzito ule kufikia huku kwa vijana ngangari kama wale kutetemeshwa.
Akamsihi aongeze vijana na amri iwe moja tu, warejee na majibu.
"Kiongozi kuna kitu kingine cha ziada." Alisema kisha akamwacha IGP apumue kidogo.
"Ile sauti uliyoniambia imesikika tena. 'SHUSHA MBUYU KUNA NYOKA..."
"Ni sauti ya nani?" Aliuliza kwa utulivu wa hali ya juu.
"Aliyeisikia ni marehemu tayari. Lakini ni mmoja kati ya timu uliyoipa dhamana ya kwenda kuikagua nyumba ya Kobo."
"Na ni nani anayeshambulia ikiwa sio hao wapekuzi?"
"Kuna safu nyingine kutoka katika kona za nyumba waliyoenda kuipekua. Kuna vita ya pande zaidi ya mbili mkuu."
"Ongeza vijana, fanya wanane. Wahakikishe wanaleta majibu."
"Sawa. Afande..." Alijibu na kukata simu.
Hali ilikuwa mbaya tayari.
_____
INSPEKTA KOBO alianguka mwili wote lakini hakuzimika macho yake. Alitulia kama aliyekwishapoteza uhai tayari.
Aliendelea kutazama mashambulizi yalivyokuwa ya kutisha, kuna jambo alikuwa akilisoma.
Wapinzani waliokuwa wamejificha katika kuta na dari walikuwa wakifanya mashambulizi ya akili sana huku hawa waliomsindikiza kukagua nyumba walikuwa wengi lakini bure kabisa.
Walikuwa ni watu wanaotii sheria tu, wakiambiwa waachie risasi wanamimimina hovyo bila kumaanisha kudhuru!
Akiwa palepale alizungusha macho yake huku na kule, na mara akatua katika madirisha ya nyumba ile.
Akaona kama kivuli kikivuka upesi kwa kuinama chini.
Kivuli kile alikuwa amekizoea sana, kama kisingekuwa chenyewe basi kingekuwa ni pacha ya kile alichokizoea.
Zubeda! Inspekta akatokwa na jina lile huku akiwa bado amenasa pale chini, kulia kwake pakiwa na mwili wa askari aliyetokwa na uhai tayari.
Kwa umakini wa hali ya juu akajisogeza mita kadhaa taratibu hadi akawa jirani kabisa na yule askari. Muda wote macho yake yaliwatazama wale washambuliaji waliojificha.
Alishagundua tayari kuwa washambuliaji walikuwa wanaye mdunguaji wao na alijua vyema kazi ya kudungua maana alikuwa hakosi kila akishambulia.
Faida kuu kwa Kobo ni kwamba huo ulikuwa moja kati ya mchezo wake uliompandisha cheo upesi na mchezo huohuo ulikuwa umemuingiza matatani.
Shabaha!
Kobo akainyakua silaha ya askari mfu pale chini.
Akatabasamu baada ya kuitambua kuwa ni silaha aipendayo.
Akatulia tena kama mfu huku akiangalia ni wapi anapoweza kuanza kushambulia. Alitambuwa wazi kuwa hawezi kushambulia kwa muda mrefu kabla nguvu hazijamwisha na pia kuchabangwa risasi na kupoteza maisha hivyo alihitaji akifanya shambulizi liwe kubwa na lenye maana kubwa.
Akiwa bado katika kuliandaa shambulizi aliisikia simu ya upepo jirani na lile gari waliloingia nalo pale ikiunguruma maneno kadhaa ya kusihi.
Hakuwa na uhakika kama msikilizaji wa ile simu aliamua tu asiijibu ama simu ilikuwa haina msikilizaji.
"Shusha mbuyu kuna nyoka. Shusha sasa hivi ova!"
Sauti ile ilitokea nyuma ya gari ambalo lilikuwa limeharibika vibaya kutokana na milipuko ya risasi.
Mapigo ya moyo yakaongeza kasi, umakini ukatoweka akataka kukurupuka lakini alipokumbuka kuhusu 'sniper' aliyejificha mahakli fulani aliendelea kutulia.
Punde baada ya amri ile kutoka mita kadhaa hadi kuufikia ukuta mrefu kiasi ulioizunguka nyumba ile akasikia kishindo kikali, na kisha kikasikika kilio.
Kuna mwanaume alikuwa amemezeshwa risasi tayari. Alikisia
Huyu ni nani? alijiuliza kisha akajigeuza na kuilalia ile bunduki na kuendelea kubaki kana kwamba hana uhai.
Alikuwa na uhakika wote kuwa alichokisikia katika simu ni sauti ileile iliyomkosesha shabaha na utulivu mjini Shinyanga na kisha kumletea majanga.
Lakini safari hii ilisikika katika simu ya upepo. Hakufahamu fika ni nani mzungumzaji na alikuwa upande upi.
Na punde baada ya kauli ile shambulizi likafanyika.
Ni nani huyu? likabaki kuwa swali zito kwa Kobo.
Tukio la Kobo kuichukua bunduki hadi kuilalia lilikuwa likifuatiliwa vyema na mdomo wa bunduki iliyokuwa tayari kukohoa risasi.
Kobo hakujua, aliamini kuwa umakini wake ulikuwa wa kiwango cha juu zaidi.
Baada ya shambulizi lile akazisikia hatua zikisogea kwa kujiamini kuja mahali alipokuwa.
Akazivuta pumzi zake kisha akaanza kuzitoa nje taratibu kabisa.
Akakisikia kiatu kigumu kikimkanyaga mguuni.
"Huyu tayari... hamna kitu humu." bwana aliyekuwa anamkanyaga akatoa jibu lile.
"Chapa risasi kabisa kujihakikishia, hakawii kuwa hai akatuharibia." Iliamrisha sauti nyingine kwa ukali iliyotawaliwa na madaraka.
Kobo akaanza kuweweseka pale chini, alijilazimisha kuendelea kutulia kana kwamba ni mfu lakini kitendo cha kusikia kuwa anapaswa kuchapawa risasi ili kuhakikisha juu ya uzima ama kifo chake, hii ilikuwa ni sahihihi mbaya kabisa.
Kobo hakumsikia yule aliyeamriwa akijibu kitu chochote, alishindwa kuelewa nini maana ya kimya kile.
Hakutaka kucheza bahati nasibu ya 'nitakufa ama wataniacha'
Akaamua kutumia nguvu zake za mwisho na njia pekee iliyosalia katika kujitetea.
Akageuka upesi mtutu wa bunduki katika mikono yake tayari kwa kufyatua.
Lakini hakuwa na mwendokasi wake wa zamani, Kobo huyu alikuwa mgonjwa, mzito, asiyeweza kuona vyema.
Hakuwa Kobo anayetisha tena.
Inspekta Kobo alikuwa amechelewa tayari.......
Hichi unachofanya wewe mzaramo siyo sahihi,unatakiwa unapocopy hadithi ya mtu huwe unaandika na jina LA mtunzi,je hiki unafanya,George iron mosenya anakijua??? Shame on you!!
 
Hichi unachofanya wewe mzaramo siyo sahihi,unatakiwa unapocopy hadithi ya mtu huwe unaandika na jina LA mtunzi,je hiki unafanya,George iron mosenya anakijua??? Shame on you!!
Na wewe siku nyingene usicopy story nzima kwa maneno machachi hivi.
Ungesema tuu si ungesomeka
 
Hichi unachofanya wewe mzaramo siyo sahihi,unatakiwa unapocopy hadithi ya mtu huwe unaandika na jina LA mtunzi,je hiki unafanya,George iron mosenya anakijua??? Shame on you!!
duh we jamaa utakuwa una lako jambo. hufuatilii haata previous comments. anyway, lets say hukuona. shame on you na wewe kama vizuri... kwa kufanya pre judgements kabla hujafafanya research..
 
mzaramo hadithi nzuri sana. kama kawaida G. Mosenya huwa hafanyi makosa tangu nianze kufuatilia riwaya zake...
kwa wapenzi wa hii riwaya..... mi nahisi inspekta atakufa halafu IGP atabeba majukumu yake kuhakikisha mambo yanakuwa katika haki. au zubeda na nguzu watamsaidia kwa kuwatandika risasi wale jamaa kina 'mbuyu'...
 
Hichi unachofanya wewe mzaramo siyo sahihi,unatakiwa unapocopy hadithi ya mtu huwe unaandika na jina LA mtunzi,je hiki unafanya,George iron mosenya anakijua??? Shame on you!!
What if mzaramo ndiye mosenya Wa jf.?
 
Hichi unachofanya wewe mzaramo siyo sahihi,unatakiwa unapocopy hadithi ya mtu huwe unaandika na jina LA mtunzi,je hiki unafanya,George iron mosenya anakijua??? Shame on you!!
Sasa na wewe umejuaje na una uhakika na hayo usemayo?? We mzaramo unamjua vizuri?? Je! Kama yeye ndo George Iron Mosenya unajuaje? Kuna watu wana account zaidi ya3 humu uzuri ni ID fake unajua George mwenyewe Anatumia ID gani?? Au umetumwa??
 
Sasa na wewe umejuaje na una uhakika na hayo usemayo?? We mzaramo unamjua vizuri?? Je! Kama yeye ndo George Iron Mosenya unajuaje? Kuna watu wana account zaidi ya3 humu uzuri ni ID fake unajua George mwenyewe Anatumia ID gani?? Au umetumwa??
Anakurupuka tu sjui anajuaje uyu mzaramo sio iron mosenya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom