Riwaya: KITISHO

RIWAYA: KITISHO
MTUNZI: richard MWAMBE



“Haya nataka password ya hii kompyuta!” ile sauti ya kihindi ikaendelea. Alipoichukua ile kompyuta kutoka kwa kijana mmoja ndipo Chiba alipoiona kwa uvunguni na kugundua kuwa kompyuta ile si yenyewe, akamtazama Madam S, akajikohoza mara tatu kwa mtindo wa pekee, Madam akaelewa kuwa ule ni wito akamtazama Chiba, Chiba akayazungusha macho yake kwa namna ya ajabu huku akibana na kuachia kope zake, Madam S akaelewa anachoambiwa kuwa kompyuta ile ni feki.
Akawatajia password ya hiyo kompyuta, wale jamaa wakaanza kuifungua, ilipoanza kufunguka wakafurahi sana na kuondoka zao.
“Tunarudi muda si mrefu kuwaua!” mmoja wao akasema.
Wakaondoka zao.

SEHEMU YA 06

KITUO CHA POLISI KATI –saa 11 alfajiri.
KIPIGO alichokipata Ravi Kumar kutoka katika mikono ya vijana wataalam wa kazi hiyo alitapika kila alichokijua juu ya sakata hilo, ingawaje alionekana vingi hafahamu lakini alimtaja mshirika wake mkubwa aliyekuwa akimpa maagizo ya kupeleka Gerezani au kuchukua na kuleta kwake, huyu hakuwa mwingine ni Pancho Panchilio.

“Kwa hiyo Pancho ndiye alikuwa anakutuma?” kamanda akauliza.

“Ndiyo kabisa yaani, ni jeje huyo, lakini mimi sijui nini alikuwa anaadika,” akajieleza.

“Pancho anaishi wapi?” akauliza Kamanda.

“Mimi mtaniua, sijui naishi wapi najua ofisi yake tu,” Ravi akajibu huku akilia na damu zikimtoka kinywani na puani.

“Na huyu Mke wa Mahmoud umemjuaje?” kamanda akauliza.

“Huyu manamuke bana, nilikutanishwa na jeje tu,” akaeleza.

“Sasa yuko wapi?” swali linguine.

“Aliniaga anaenda Zanzibar na atarudi jumamosi hii,” akajibu.

“Zanziba sehemu gani?”

“Mimi hapana jua jamani, mambo ya familia hayo!” akaanza kulia.
Kamanda Amata akaanza kupekuwa simu moja baada ya nyingine za wale wafanyakazi, ndipo katika simu ya msichana wa kazi alipokuta ujumbe mfupi wenye maagizo Fulani kuwa mtu yeyote akiuliza aseme mama huyo kaenda Zanzibar lakini alipochunguza haraka kwa makampuni ya simu aliambiwa namba hiyo mara ya mwisho ilikuwa ikisoma eneo la Laskazoni Tanga.
Kamanda Amata akaagiza kwa Inspekta Simbeye kuwa huyo mama akamatwe mara moja, simu ikapigwa Tanga, kituo kikuucha polisi, masako wa panya wa kimya kimya ukaanza.

“Kamanda Amata,” Simbeye akaita, kisha akampa ishara ya mkono kumwita pembeni.

“Vijana wangu wawili wameuawa eneo la Klabu ya Mbowe! Masaa matatu yaliyopita,” akamnong’oneza.

“Pole sana Inspekta, walikuwa kazini, wamekufa kishujaa, na muuaji atapatikana tu!” kamanda Amata akajibu na kutoka kituoni hapo.

4
JOKI alitulia mezani kupokea taarifa zote za vikosi kazi walivyovituma kuwasaka watu hao, vikosi vinavyoongozwa na wapiganaji hodari kuanzia makabiliano ya ana kwa ana na hata yale ya silaha za kila aina. Alishangaa tu kuwa muda unakwenda lakini hapati jibu lolote juu ya kupatikana au kuonekana kwa Kamanda Amata ambaye nguvu zote walikuwa wameelekeza kwake, isitoshe ilikwisha amuriwa kuwa akipatikana wala haina haja kumleta na uhai wake bali ni kumuua kwa vyovyote vile.
Aliitazama saa yake, pambazuko lilikuwa kwenye miimo ya mlango ulio mbele yake. Wamepatwa nini hawa? Mbona muda umetutupa mkono! Alijisemea kwa sauti ndogo iliyotosha kujisikia yeye mwenyewe. Kichwa kilikuwa kikimzunguka kila mara alitamanai kuinua simu awapigie kuliza lakini alikumbuka kuwa makubaliano yao hayakuwa hivyo bai wao wakikamilisha kazi watampigia simu kama walivyofanya kwa wengine wote.
Akiwa katika kuwaza, simu yake iliita, akaiinua na kuiweka sikioni akiwa na shauku ya kujua nini kimetokea katika msakao huo.

“JoKi !” sauti iliita kisha ikakata.

“Sema, mmekamlisha kazi?” akauliza.

“Hapana JoKi, muda tulioupanga kukamilisha kazi umepita, lakini hatujafanikiwa kumpata Yule hayawani, tufanyeje?” Mkuu wa kikosi cha kwanza akajieleza.
JoKi akatulia kimya kwa fungu la sekunde, akashusha pumzi na kuitoa simu sikioni; tayari alikuwa amesahau anaongea na nani, akakumbuka, akajicheka na kurudisha simu sikioni.

“Subiri kidogo, nitakupa jibu,” JoKi akajibu. Akaitua simu chini na kuhisi kuchanganyikiwa, akabofya namba Fulani na kusikiliza. Naima alikuwa upande wa pili.

“Yes JoKi!” akaitikia.

“Niambie mmefikia wapi na harakati?” JoKi akauliza.

“Bad! Very bad! Huyu jamaa kwanza keshaua mtu mmoja, nimepambana naye lakini Polisi wameharibu muvi, kanitoroka,” akaeleza.
JoKi akapiga ngumi mezani baada ya kujua uwa keshapoteza watu wane katika harakati zake.

“Shiit!” akang’aka, “Unamwonaje?” akauliza.

“Mtepetevu, simshindwi hata kidogo, nab ado namsaka kwani amenijeruhi,” Naima akajigamba. Baada ya kuongea na Naima akapigia kikosi cha tatu nacho majibu ni yaleyale kuwa mtu huyo hajaonekana. Ni Naima peke yake aliweza kumwona na kupambana naye japo kwa sekunde chache. JoKi akatoa maagizo kuwa vikosi viwili vibaki kazini na kikosi kimoja kirudi kambini kwa ajili ya kutekeleza majukumu mengine. Kati ya vikosi viwili vilivyobaki kumsaka Amata kikosi cha Naima nacho kilikuwamo.
Tayari giza lilianza kuuachia mwanga nafasi ya utawala, kwa pande zote mbili huo haukuwa muda rafiki kufanya makeke yoyote lakini haikuwa na jinsi. Pande zote mbili zilikuwa kazini kwa umakini zaidi.
JoKi aliwapanga watu wake vyema katika jiji la Dar es salaam kuwa popote watakapomuona Kamanda Amata wasifanye lolote bali waitaarifu ofisi nayo itajua nini cha kufanya ili kumaliza kijana huyo shababi.

§§§§§
KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM-saa 1:02 asubuhi.

MITEGO MIWILI ilitegwa mahsusi kwa ajili ya Kamanda Amata, wakati huu wa jua hawakutakiwa kumuua ila walipewa amri moja tu ya kutoa taarifa kwamba kaonekana sehemu Fulani kisha kazi ya kummaliza ifanyike bila tabu.
Kikosi cha kwanza chenye watu wane kilikuwa jirani kabisa na jingo la JM Mall ambapo ndani yake, juu; ghorofa ya sita kuna ofisi ya AGI Investiment inayomilikiwa na Kamanda Amata kama Mkurugenza huku Gina akiwa kama Katibu wake, hapo ndipo hupangia mipango yote migumu na kuigeuza kuwa myepesi, nani afe na nani hasife, nani aokolewe na nani atoswe yote yalijadiliwa hapo kwa usiri mkubwa wakati leseni ya kampuni hiyo ni ya ufaulishaji mizigo bandarini.
Watu waliaanza kulijaza jiji, mishemishe za hapa na pale zilianza kuzikumba kona za jiji la Dar es salaam, jua nalo lilipanda angani taratibu likitokea pande zile za Kigamboni. Naima alikuwa ametulia katika moja ya mbao za magazeti akitazama habari nzito iliyobeba magazeti mengi ya siku hiyo.

…Mbunge wa Miroroso auawa kikatili nyumbani kwake Msasani…

Moja ya gazeti liliandika hivyo kwa wino mzito, watu walijazana kusoma habari hiyo, kila kona ya jiji liliongelewa hilo.

“Washamuua huyo! Nchi hii utaiweza!” mmoja wa madereva Tax aliropoka

“Ndiyo hivyo, hii nchi ya wenyewe hii, alikuwa anaongea sana huyu, washamtengeneza!” mwingine alidakia.

“Badala msikitike wapigania haki wanapotezwa nyie mnashabikia kwa maneno ya ajabu,” mara hii mshona viatu alimalizia.
Mazungumzo juu ya hilo yakatawala kila kona ya eneo lile, kufumba na kufumbua gazeti la Mbiu ya Mnyonge likapotea mbaoni, likaisha kabisa kwa kuwa liliandika vizuri habari hiyo.
Naima alisikiliza yote hayo, akakitazama kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume akatabasamu na kusogea pembeni ya eneo hilo, aliwatazama vijana wake wawili aliobaki nao katika kikosi chake akawapa ishara kuwa mambo yako sawa.

Kamanda Amata alikuwa akisubiriwa katika maeneo yake muhimu ya kujidai, yeye hakuwa na habari ya lolote katika kuwindwa huko. Asubuhi hiyo alirudi nyumbani kwake japo kujiweka sawa na kuanza awamu mpya ya mapambano ya mchana, muda ulimpiga kikumbo, alipenda kuibuka kidedea kabla ya jogoo kuwika lakini akajikuta akikabiliwa na mambo mengi ya kiupelelzi ili kuwajua adui zake walivyo, lakini hakujuwa bado wamejipanga vipi, kitu kilichompa ujasiri siku hiyo, ni kule kuwa peke yake katika uwanja wa mapambano, kumbe hakuhitaji kutumia akili ya pili kumlinda mwingine; lakini pia alijua wazi kuwa nalo ni hatari ubwa kwani macho ya adui yake yatakuwa na kazi moja tu ya kumtazama yeye kila anaponyanyua wayo wa mguu wake. Aliegesha pikipiki lake mahala pake na kulizima, akatulia kusikiliza lolote kama lipo, ukimya ulitawala, hakuna jipya, akavua kofia lake na kulipachika juu ya kioo cha pikipiki hilo kisha yeye kujitoma ndani huku mkono mmoja ukiwa ndani ya jaketi lake.
Alipohakikisha kila kitu ni salama, akaingia chumbani mwake na kujiweka sawa kivingine.

Alipotoka ndani; alikuwa ndani ya suti ya kijivu iliyotanguliwa na shati la buluu bahari, akalielekea jokofu na kuchukua dumu la maziwa, akamimina kwenye kikombe kikubwa, soseji tatu nene pamoja na slesi kadhaa za mkate, vikapashwa kwa microwave na toaster.
Nje ya nyumba ya Amata kulikuwa na pub ya kisasa ambayo iliendesha shughuli zake saa saa ishirini na nne, asubuhi hiyo iliyokuwa na hali ya mawingu, bado watu wachache walionekana kuwapo eneo hilo ama wakiongea hiki na kile au wakipata supu ya kongolo. Hilo halikuwa tatizo kwa Amata, aliitoa gari yake nje na kuiweka sawa tayari kwa safari, akafunga geti lake kwa kutumia rimoti maalum kwa kazi hiyo.
Huku macho yake yakifanya kazi ya ziada ya kuatzama huku na kule akili yake ilipisha uamuzi wa kuhamisha tiba za Gina na Scoba kwenda shamba ili kuepusha lolote ambalo adui yake anaweza kulifanya, kwa maana kama ni watu aliyoawategemea basi ni hao tu. Aliingia kwenye gari yake aina ya Volks Wagen, au wengi mngependa kuiita Golf, akashusha kioo taratibu na kumtazama binti aliyekuwa akipita mbele ya gari yake. “Duniani kuna viumbe mwe!” akajisemea na kisha akaingiza gia namba moja na kuondoka taratibu, alipoumaliza wigo wa ile Pub, akatupa jicho kutazama kijia kile alichoingilia Yule mwanadada, akalisanifu umbo la msichana huyo kwa nyuma, lo; akashindwa afanye nini, akaodoa gari yake na kuikamata barabara ya KInondoni kuelekea daraja la Salenda, alipoikanyaga tu barabara ile na kwenda mwendo wa mita kama 200 hivi, akatazama kioo chake cha ndani na kuona gari nyingine nyeupe ikiingia barabarani kutokea njia ileile. Hakuitilia shaka lakini alitaka kupata uhakika kama gari hiyo ana nasaba nayo au la.

Kabla hajafika kwenye makutano, akakunja kulia na kuingia ofisi za ubalozi wa Uswizz, akaweka gari katika maegesho yake, hakushuka. Akaiona ile gari ikipitiliza, hapo nay eye akatoa gari yake na kurudi barabarani, alipokunja kulia hakuiona ile gari, akajua hisia zake hazikuwa sawasawa, akaingia barabarani na kuifuata barabara ya Bagamoyo mpaka Salenda na kukunja kushoto kuingia barabara ya Ocean kisha akaegesha gari yake kwa mbele kidogo akitazama kama kunayeyote anayefuatilia nyendo hizo. Alipohakikisha hakuna jipya, akakodi Tax na kuelekea Sea View.

“Nishushe hapa!” akamwamuru dereva Tax kisha akamtupia not ya 5000 na kutokomea zake.

§§§§§
DR. KHADRAI ALIKUWA BIZE NA MGONJWA WAKE, kama Mzuka Kamanda Amata akasimama katika mlango wa chumba hicho.

“Karibu Amata,” akamkaribisha kitini.

“Asante nimekaribia, anaendeleaje huyo?” akauliza mara baada ya kuketi kitini.

“Anaendelea vyema, ameamka ila bado fahamu hazijamrudia, lakini si muda mrefu atakuwa sawa, lakini, Amata, huyu atatakiwa kupumzika kama miezi mitatu hivi asifanye shughuli za mikiki mikiki,” akaeleza.

“Ok, umeeleweka kabisa. Sasa Khadrai ipo hivi, hali ya kiusalama sio nzuri sana, na nimekuja hapa kwa jambo moja tu,” Kamanda akainuka kitini, na kuliendea dirisha kubwa la aluminium na kuchungulia nje, akaiona ile gari ikiegeshwa mahala Fulani jirani kabisa na lile jumba la Khadrai, akarudi na kusimama karibu kabisa na daktari huyo, “Sikiliza, wewe na huyu Gina nitawapeleka Safe House, leo hii, kila kitu kipo kule utatumia ofisi ya Dr. Jasmine”.

“Ni wapi huko?” Khadrai akauliza.

“We jua ni Safe House, iko wapi hilo sio swali kwa sasa, haya mwandae mgonjwa wako kwa safari, ukiwa tayari unambie, nitatumia gari yako pia,” akamwambia huku akitokea sebuleni, ukimya wa jumba hilo ulibaki hivyo hivyo, akatzama huku na huko, akachomoa bastola yake ndogo kabisa na kuiweka sawa, akavuta hatua kuuelekea mlango wa kutokea nje, akabana dirishani kutazama.
Mlinzi wa geti aliliendea kufungua baada ya kusikia mbisho, Kamanda akatulia palepale akitazama huku bastola yake ikiwa tayari kutekeleza itakaloamuriwa. Yule mlinzi akafungua geti, mtu mmoja akaingia ndani akifuatiwa na wengine wawili, alikuwa amevalia suti nyeupe kabisa na wale wenzake vivyo hivyo, hakuwa Mtanzania, wala hakuwa Mwafrika, kutoka pale dirishani Kamanda Amata akajihisi kupata ubaridi wa ghafla.

“Smart Killer!” akajisemea, kisha akarudi ndani kwa Daktari Khadrai.

“Kaeni humu, msitoke nje wala kuchungulia,” akarudi sebuleni, na kukuta wageni wake wakiujia mlango mkubwa wa nyumba ilhali mlinzi anagalagala chini pale getini.

“Haina haja ya kutukaribisha,” Yule mtu aliongea kwa Kifaransa safi huku wale wenzake wakiwa kimya na mikono yao wameifumbata ndani ya makoti yao, Yule bwana mkubwa alijishika kiuno na kuyaachia mabastola yake waziwazi yakining’inia.

“Karibuni, karibuni viti,” akawakaribisha huku yeye akikiendea kimoja ya viti hivyo.

“Hatuna haja ya kukaa! Tumeshakaa sana kwenye ndege tuliyokuja nayo!” tunataka kitu kimoja tu hapa na tunaondoka na ndege ya saa tano,” Yule bwana akajibu kijeuri huku akichomoa bastola moja na kuifunga kiwambo cha sauti.

“Kitu gani?” Amata akauliza.

“Roho, roho yako inayokutia ujeuri ndiyo tunayoitaka sisi!” Yule bwana akaeleza, huku akiwa tayari kainua bastola yake na kuielekezea katika paji la uso la Amata. Uongo wa Amata ulikuwa ukifanya kazi kwa kasi ya ajabu kuliko kawaida yake akitazama huku na kule kwa kuzungusha macho, akiwatazama wote watatu na kuuona kwa haraka haraka uhatari wa viumbe hao waliovalia sare mpaka mtindo wa viatu vyao ulikuwa wa kipiganaji kabisa. “Kazi ipo, hapa ni kufa nakupona,” Kamanda akawaza.

§§§§§

5
KANAYO O. KANAYO ALIKETI KATIKA NUSU UKUTA akiangali mechi ya mpira wa miguu kati ya afungwa mashabiki wa Yanga na Simba. Nywele zilianza kupoteza mng’ao wake, ndevu zilizokosa mnyoaji mzuri anayeijua kazi yake nazo zilikuwa hoi, uzee ulinyemelea mwili huo ambao ulikuwa wa kupendeza kwa mafuta na unyunyu wa gharama. Akiwa ametingwa katika kutazama mechi hiyo ambayo upande wa Yanga ulishinda 3-0 kama kawaida, alihisi kitu kikipenyeshwa kwenye kiganja cha mkono wake.
Ilikuwa kijikaratasi kidogo, akamtazama huyo aliyeifanya kazi hiyo, akamwona na kumbania jicho kisha akaifungua ile karatasi na kuisoma, alipomaliza, akaikunja na kuondoka zake.
Ndani ya chumba chao cha kulala chake cha kulala kilichokuwa na kitanda kimoja kidogo chenye tandiko tu bila godoro, aliketi kwa utulivu na kuingiza mkono uvunguni akachomoa bahasha ndogo na kuifungua ndani.

“…Kazi imeanza mtaani, tumekamata watatu, tumewaweka kwenye hali mbaya wawili, bado mmoja, Kamanda Amata.
Tumeleta Smart Killer kama mlivyoagiza, tukimmaliza yeye ndipo tutafanya plan B, kaa tayari kwa taarifa ya mapinduzi.
Mafisadi; kama wanavyotuita, tutaendelea kuwapo tu na tutaiburuza nchi kwa noti zetu.
Cheers!...”

Akaikunja ile karatasi na kuitia kinywani huku akitabasamu.

§§§§§
MAHMOUD ZEBAKI alitema karatasi iliyokuwa kinywani mwake na kuipachika uvunguni mwa kitanda chake, akatabasamu kwa tabasamu pana. Ijapokua ngozi yake ilikuwa kavu kwa kukosa japo Vaseline lakini bado ilionesha afya kwa mbali, jela ni jela tu. “Hawatuwezi hawa, tutaendelea kutafuna pesa tu, fisadi sio peke yangu kuna Magurubembe huko nje hawayajui, na kesi yetu tutashinda,” akajipa moyo huku akisimama na kutembea hapa na pale.
Kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na pesa za umma waliyoshitakiwa Mahmoud Zebaki, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Uswizz na Kanayo O. Kanayo aliyekuwa Waziri katia Wizara nyeti ya Serikali ilikuwa ikiunguruma katika Mahakama ya Kisutu, kila mara iliposomwa iliahirishwa na watu hao kurudisha lumande. Wananchi wengi walilalamika kwani hawakuelewa kwanini kesi hiyo inapigwa danadana kiasi hicho, wakati Wananchi wakilalama kuwa watu hao ‘wasulibiwe’, walioshika mpini wanasema ‘uchunguzi unaendelea’.

§§§§§§
Kama kuna kitu kilimuuzi Pancho Panchilio alipokuwa ofisini kwake ni kitendo cha kudanganywa juu ya ile kompyuta, alipoifungua akiwa ofisini mwake ilifunguka na kumuonesha picha moja tu ya fuvu lenye ujumbe chini yake ‘Ni zamu yako kufa’. “Kama wao ni wajanja basi mimi ni zaidi, na ile kompyuta lazima niipate leo hii,” akajiwazia huku mwili wake ukitetemeka kwa hasira. Aliinuka na kuliendea dirisha kubwa la kioo na kuitazama mandhari ya jiji la Dar es salaam, akasonya na kuichomoa bastola yake, alipogeuka alifyatua na kuisambaratisha ile kompyuta pale mezani, akairudisha bastola yake na kurudi kitini. “Fanya nililokuagiza, kumbuka sisi ndiyo tunaokulinda hapa nchini na hata nchi yako haijui kama upo hapa kutokana na makosa uliyoyafanya huko,” aliyakumbuka maneno ya Kanayo O. kanayo siku alipokwenda kumtembelea gerezani.

“Lazima ufe leo Kamanda,” akajisemea na kujibwaga kitini. Aliinamisha kichwa chake mezani huku mikono yake ikizitimua nywele zake za Kihindi kama anayetafuta kitu Fulani humo, kisha akakiinua ghafla na kutazama mlangoni. Akapiga ngumi mezani, akanyanyuka na kuibeba briefcase yake, akatoka mpaka kwenye ofisi ndogo ya katibu wake.

“Boss, mbona mapema?” Yule binti akauliza.

“Usijali, natoka, kuna kazi naenda kuifanya, nitarudi hapa kesho, aaah no hapana, naweza kuchukua hata siku mbili nje ya ofisi, nitakupigia baadaye,” alikuwa akiongea huku akibabaika hapa na pale. Akatoka ofisini na kuiendea gari yake kabla hajapotelea mjini.

KITUO CHA POLISI CHA KATI- muda huohuo
INSPEKTA SIMBEYE hakujua nini la kufanya asubuhi hiyo, wingu jeusi lilikuwa limekigubika kichwa chake, alijua la kufanya lakini alishindwa kulifanya. Hapo ndipo moyo wake uliporudisha uamuzi wa kustahafu kazi hiyo, uamuzi ambao ulikataliwa pindi ulipowafikia wakubwa, ulikataliwa kwa sababu ya utendaji kazi wa kiumbe huyo alijulikana kwa cheo kama jina, Inspekta. Aliipenda kazi yake sana, hata baadaye akafanya kazi nyingi kwa kushirikiana na Idara nyeti za Usalama wa Taifa, alikuwa mpole, mnyeyekevu, msiri, mwenye huruma, lakini makini katika kazi na hakufanya makosa. Hakupenda kukumbatia ujinga wala upumbavu. Alikuwa mkufunzi wa mafunzo ya polisi wapya pale CCP na ndipo alipokuatana na Kijana Amata alipoingia mafunzoni.

Mara kwa mara alikuwa akimtazama kijana huyo mchangamfu kwa jicho la pekee, “Anafaa,” alijisemea huku akitikisa kichwa alipokuwa akishuhudia shabaha ya aina yake iliyokuwa ikilengwa mazoezini, wepesi wa kufanya michezo ya karate na kungfu, alivutiwa. Alimjua vema, vema sana na alimwamini kuliko unavyofikiria.

Alijiinua kichwa chake na kuitazama picha kubwa ya Mwl. Nyerere iliyokuwa imening’inia ukutani, “Tutakumbatia waovu mpaka lini ilhali wanajulikana walipo?” alijikuta akiiuliza ile picha bila kujua kuwa haiwezi kumjibu, akatikisa kichwa. “Usifanye lolote juu ya mtu huyo! Mwache kama alivyo mpaka oda ya juu itakapotoka,” aliikumbuka sauti hiyo iliyomfikia kupitia simu yake ya ofisini pale alipoomba kumkamata bwanyenye huyo aliyezaliwa India na kutarajia kufia Tanganyika.
Akasonya, akaisogeza kofia yake pembeni na kuinyanyua simu yake, akabofya zile namba unazozifahamu, akaiweka sikioni, tayari moyo wake ulipitisha maamuzi, kifua chake kilikuwa kikipanda na kushuka, “Nitajua la kumfanya!” alijiambia.

§§§§§

ITAENDELEA....
 
RIWAYA: KITISHO
MTUNZI: richard MWAMBE
-Man In The Mirror-

Naima aliachia pigo moja kali la ‘pigo la kifo’ lililotua sawia katika uso wa Scoba, akageuka huku akipiga yowe la uchungu, pigo la pili likatua shingoni na kumfanya Scoba kutepeta. Yule mwenye bastola alamshindilia pigo la kisogoni kwa bastola yake Scoba akazimika.
Kila mmoja alikuwa anathema kwa shughuli hiyo ya sekunde chache.

“Amekufa?” mmoja aliuliza.

“Akaongee na babu zake, mtupeni vichakani huko,” Naima akaamuru na Scoba akashushwa na kutupwa katika chaka.

SEHEMU YA 8

§§§§§

SCOBA alimaliza kusimulia mkasa uliyompata, kila mmoja alisikitika sana na hali hiyo, minong’ono ikachukua nafasi kati yao.
Hosea akajikohoza na kurudisha ukimya kwa namna hiyo, “Ok, sasa nataka tuingie kazini ili kuwapata hao watu laeo kabla jua halijazama,” akatoa amri. Wakiwa bado katika kikao icho mara simu ya mezani katika chumba cha mikutano ikachukua uhai. Hosea akaipokea na kuiweka sikioni.

“Mkuu, katika barabara ya Ocean kuelekea Ikulu – Magogoni kuna gari zinafanya fujo,” ilikuwa sauti ya Avanti aliyekuwa katika chumba cha mawasiliano cha Teknohama. Baada tu ya taarifa hiyo jopo zaima likanyanyuka likimfuata Bwana Hosea na kuelekea kwenye chumba hicho kutazma hicho walichoambiwa.
Katika luninga kubwa kulikuwa kukionesha ramani ya jiji la Dar es salaam na kuonesha maeneo yote muhimu kwa ajili ya usalama wa Taifa. Zilionekana gari mbili zikielekea Upande wa Ikulu kutokea Hospitali ya Ocean Road.

“Zuia haraka, point namba mbili ifanye kazi tafadhali!” Hosea aling’aka na muda huo huo Avant aliinua kitu kama simu na kukiweka sikioni kisha akaboinyeza tufe Fulani na kuongea maneno machache, akatulia.
Bado macho hayo yote yalikodoa bila kufumba yakiangalia tukio hilo, hakuna aliyejua ni nini kinaendelea. Scoba alitulia akitazama kwa makini, akapenya katikati ya watu na kusogea karibu na Avant.

“Naomba nione picha inayowezekana tafadhari,” akamwambia Avant, naye akafanya manuva Fulani kwenye mashine yake wakaweza kuona vipande vya picha za magari hayo, Scoba alitazama kwa makini.

“Unaitambua hiyo gari?” Hosea akamwuliza.

“Yeah, kama sikosei hii Toyota Duet ni ya dada mmoja hivi ana uhusiano na Kamanda Amata, huyu dada ni daktari pale Agha Khan na huwa wakati mwingine tunamtumia kwa hili na lile, anaishi Upanga Sea View,” Scoba alieleza.

“Kamanda Amata,” Hosea akanong’ona, kisha akawaangalia watu wake, “Namtaka huyo anayefukuzana na Amata sasa hivi!!” akatoa amri na kuondoka mle ndani huku akiweka sawa miwani yake. Maafisa wale wakatazamana kisha mmoja akawapa ishara ya kutoka katika chumba kile.

“Ili tufike haraka eneo lile kwa foleni za Dar lazima tutumie njia ya anga, Chopa tafadhali, Scoba twende zetu,” afisa mmoja aliyeonekana kuwa na cheo cha juu kati yao alitoa amri hiyo, Scoba akakabidhiwa nafasi ya kuliongoza dude hilo, pamoja naye watu wengine wawili walikwea ndani yake wakiwa wamekamilika, bunduki ndogo na kubwa zilihusika, mashine ikanyanyuka.

§§§§§
Barabara ya Ocean ilikuwa imekumbwa na taharuki, Kamanda Amata, mwili wake ukiwa unavuja damu hapa na pale alikuwa akiendesha Toyota Duet kwa mwendo wa hatari akiifukuza gari ya mbele yake ambayo ilionekana wazi kuendeshwa na mtu anayeijua kazi yake. Ovateki zilizokuwa zikifanywa na huyo jamaa ni za hatari mpaka kila mtu alikuwa akishika kichwa kuhofia maisha ya hao walio ndani ya vyombo hivyo.
Walipokaribia njia panda ya Gymkhana na Ocean Road; Kamanda Amata akazipita gari mbili na kuingia upande wa kulia, baada ya kuisoma akili ya adui yake kuwa atapinda upande huo, hakuwa mbali na mawazo ya mtu huyo, gari zile zikakutana katikati ya njia panda na kusababisha ajali mbaya iliyohusisha gari kama nne hivi. Gari ya Kamanda Amata kutokana na udogo wake ilijifinya chini ya Land Cruiser Hard Top.

Gari aliyokuwa akiitumia Yule jamaa baada ya kukutana na ile ya Amata, alijaribu kuikwepa akajikuta akiingia katika ukuta wa Hospitali na ukuta ule kuvunjika vibaya. Mguu wake ulikuwa umenasa chini kwenye pedo, alijitahidi kuutoa na kufanikiwa. Akajivuta na kutoka nje kwa kupitia dirishani.
Kamanda Amata naye akajitoa taratibu huku mwili wake ukivuja damu. Kama kawaida ya Watanzania kama kawaida yao wakaanza kujazana, vibaka nao wakitafuta bahati yao, Kamanda Amata alijitupa nje na kudondokea barabarani.
Yule bwana alitazama huku na kule na kuona kundi la watu likija kwenye eneo la tukio, sura yote ilijaa damu, nguo alizovaa hazikutamanika. Mngurumo wa helkopta ndiyo uliomfanya aamue aliloamua, alitazama juu na kuona helkopta hiyo ikisogea eneo hilo, katika mlango wake mtu mmoja aliyevalia suti nyeusi akiwa kakamata bunduki yenye nguvu,

“Nimekwisha!” akajiwazia. Kitendo bila kuchelewa alichomoa bastola yake na kupiga tanko ya mafuta ile gari yake.
Mlipuko mkubwa ukatokea na gari kadhaa zilizokuwa eneo hilo zilishika moto, moshi ulitanda eneo lote, kelele za watu zikasikika huku na kule. Kamanda Amata akaenda pembeni kabisa na kuanza kutazama wapi adui yake alipo. Haikumchukua muda kumwona mtu huyo akiwa anatoroka kwa kujichanganya na watu.

“Shabash! Huwezi kunitoroka,” akasema kwa sauti ndogo, akavuta hatua na kuyapita magari matatu yaliyokuwa yamejibana hapo, akatokea upande wa pili na kumwona adui yake akipotelea katika kundi la watu. Kutokana na wingi wa watu ilikuwa ngumu kupenya eneo lile, akafikiri kwa haraka kuwa hapo ni kutumia plan B ili kumpata, lakini kabla hajatekeleza hilo. Gari ya polisi ilifika eneo hilo kwa mbwembwe na walipofika tu waliteremka haraka wakiwa na bunduki zao mikononi, mara moja walimwona Yule mtu aliyekuwa akijichanganya na watu.
Inspekta Simbeye akiwa na bastola yake mkononi, akatoa amri mtu huyo akamatwe mara moja, lakini mtu Yule naye hakuwa tayari kukamatwa namna hiyo, alichomoa bastola yake na kupiga risasi mbili hewani na kufanya hali ya taharuki mahala pale, baada ya kupiga hewani ile risasi, akashusha mkono na kufyatua tena, risasi ile ilimkosa mlengwa ikampata mmoja wa raia aliyekuwa eneo lile na kumjeruhi, hapo ndipo hasira za wananchi zilipopanda, walimvamia Yule bwana bila hata kujali polisi waliopo, walipiga na kupiga mpaka mtu Yule akapoteza uhai.
Ile Chopa ikateremka taratibu na kujiegesha pembezoni mwa ufukwe wa bahari, vijana watatu Smart Guys wakateremka na kuifikia ile maiti iliyopigwa vibaya na wananchi, Scoba aliteremka pia huku akiacha dude lile likiunguruma kwa hasira, Inspekta Simbeye na vijana wake wakawasili.

“Shiit!” akafoka Simbeye, “Siyo Mtanzania huyu!” akamalizia.
Akainua uso na kuangaza huku na kule wakatia huo tayari utepe wa polisi ulikuwa umezunguka eneo hilo na kuzuia Wananchi kufika hapo. Gari za zima moto tayari zilikuwa zikizima moto uliounguza gari takribani tano eneo hilo.
Kamanda Amata akatazama hali iliyokuwa hapo, akafikiria kama ajitokeze au la, lakini hiyo huwa si kawaida yake, alipigwa na bumbuwazi alipomuona Scoba, “Ni yeye au nimechanganyikiwa?” akajiuliza, kisha taratibu akaondoka eneo hilo huku akijiweka sawa uso wake. Akapotea eneo hilo.

6

CHIBA alimtambua mara moja Yule mtu pale mbele, ni mtu a;iyekuwa akitafutwa kwa muda mrefu, kutoweka kwake kulisababisha maandamano makubwa ya waandishi wa habari, alikuwa mwandishi nguli wa habari nchini. Wananchi waliongea, katuni zikachorwa ikasemekana watu wa Usalama wa Taifa wamemteka na siku yoyote angeonekana akiwa hana macho, au meno. Au kucha.

“Kwa nini? Kwa nini walimteka na kumleta huku?” akajiuliza bila majibu.

“Unamjua huyu?” JoKi akamuuliza.

“Ndiyo namjua, na kwa nini mmemfanya hivi?” akamuuliza.

“Aaaaa ha ha ha ha, hii ni serikali kaka, ina Rais, Mawaziri, Wabunge, Wanausalam kama sisi na kadhalika, na ina maadui kama wewe. Nusu saa ijayo nawe nitakufanya hivi,” alipomaliza kusema hayo, risasi moja ilikipasua kichwa cha Yule mwandishi na kutawanya damu iliyonganyika na ubongo. Chiba alitetemeka kwa hasira.

“Jiandae, nitawapanga wote hapa na kuwa fumua mmoja mmoja huku nikitengeneza filamu ya kumbukumbu kama za wadi ya kusherehekea miaka mingapi sijui ya uhuru wa nchi yako,” akaongea kwa kebehi.

“Hicho ni kitisho!” Chiba akaunguruma kwa hasira.

“Kitisho! Kitisho ee,” JoKi alipomaliza hiyo sentensi, aliinua mkono kwa minajiri ya kumchapa kofi Chiba. Chiba aliigundua hiyo dhamira yake akasubiri kitendo hicho, kiganja cha mkono wa JoKi kilipolifikia shavu Chiba aligeuka ghafla na kukidaka kidole kimoja kwa kinywa chake, akakibana barabara kwa meno yake imara.

“Aaaaaaiiiigggghhh!” JoKi alipiga kelele za maumivu, alijitahidi kuuchomoa mkono wake kinywani mwa Chiba lakini ilikuwa kazi bure, alitumia mkono mwingine kumpiga ngumi za tumboni na kwingine lakini Chiba hakukiacha. Wenzake walijaribu kumnasua lakini wapi.

“Mwache au la nakupiga risasi,” mmoja wao alimwambia Chiba. Lakini Chiba hakujali alizidi kung’ata na kung’ata, mishipa ya hasira ikiwa imedinda usoni na shingoni. Yule mlinzi alitumia kitako cha bunduki kumpiga Chiba mbavuni lakini Chiba hakuachia. Wakati JoKi akijitutumua kujinasua alimpiga kichwa kizito Chiba, Chiba akayumba na kuanguka chini kama mzigo kutokana na kamba alizofungwa.
JoKi akamtazama Chiba kinywani akona damu zikitiririka, mara chiba akatema kidole kutoka kinywani mwake, JoKi akajitazama mkono wake, hakuna kidole kimoja, hasira ikawaka huku akipiga kelele kama mtoto.

“Na bado ukiniua mimi wapo watakaokata miguu yako kwa meno!” Chiba akazungumza kwa gadhabu.

“Jeuri sana wewe, si ndiyo?” mlinzi mwingine akauliza huku akimpa bunduki mwenzake ili amwadhibu.

“Mtieni adabu Mwanaharamu huyo nakuja sasa hivi,” JoKi aliagiza kisha yeye akatoka huku damu zikimmwagika. Yule mlinzi alivuta teke kali kumpiga Chiba pale chini, Chiba akajizungusha na kumchota ngwala ya maana, Yule mlinzi alipiga mweleka na kudondoka chini akitanguliza kisogo, akatoa yowe la uchungu, Chiba akainua miguu yake iliyofungwa na kuitua kwa nguvu katika koromeo la mtu huyo.

“We mwache mwenzio! Mi nakuua!” mlinzi wa pili alimpiga Chiba kwa kitako cha bunduki aina ya Rifle na Chiba akatulia kimya, huku akimwacha Yule mlinzi akiwa hana uhai.

§§§§§§

Hali ya Gina ilibadilika baada ya jeraha lake kumwaga damu nyingi, Dkt. Khadrai alijitahidi kuona namna ya kumsaidia, hakuna na damu ya akiba nyumbani kwake kwani ni ni kinyume cha sheria. Akiwa bado hajui la kufanya, mlango ukafunguliwa, Kamanda Amata akaingia ndani, moja kwa moja akafikia katika chumba hicho cha matibabu na kumkuta Gina akiwa tena kitandani.

“Vipi dokta?” akauliza.

“Hali imebadilika, damu nyingi imetoka katika jeraha lake,” akajibu.

“Oh Come on Gina. Sasa tunafanyaje?”

“Hapa nikupata damu nyingine kumwongezea, haraka,” Khadrai akajibu huku bado akiwa hai hai kumsaidia Gina.

“Ita gari yenu ya wagonjwa!”

“Oh, nilisahau kabisa, asant kunikumbusha,” akachukua simu yake ya upepo ambayo madaktari wote wanazo kwa ajaili ya mawasiliano ya karibu kama inahitajika. Akaita gari na na kuagiza ije na damu kabisa.
Dakika kumi hazikupita gari ya wagonjwa ilifika eneo hilo, Gina na Dr. Khadrai waliingia na safari ya kuelekea Agha Khan ilianza kwa mbwembwe kama kawaida ya madereva wa gari hizo.
Gina alilazwa katika hospitali hiyo chumba maalum ambacho hakuruhusiwa mtu yeyote kuingia zaidi ya Dr. Khadrai tu na baadae alimjuza Amata kuwa Gina yuko mahala hapo.

§§§§§§

Kamanda Amata aliiacha hospitali ya Agha Khan na kuingia mtaani, akatembea mpaka barabara ya Ally Hassan Mwinyi, alipoona hali ya hewa ni ya utulivu, akachukua simu yake na kupiga namba ya Mkuu wa Usalama wa Taifa, Bwana Hosea na kumwuliza juu ya Scoba, akajibiwa kuwa Scoba yupo salama na anaendelea vyema.

“Ok, ninamwitaji sasa tuingie kazini kwa nguvu zote,” akamwambia Hosea.

“Haina tabu kwani huyu ni wa kwenu, mkutano wapi?” Hosea akauliza.

“Kanisa kuu la Mtakatifu Joseph dakika kumi baadae,” kisha simu ikakatika. Amata aliingia kwenye tax iliyoegeshwa jirani kabisa, na kuitaka impeleke mpaka JM Mall ilipo ofisi yake ya siri au tuiite ofisi binafsi.
Aliwasili katika jengo hilo mida ya kama saa sita hivi, moja kwa moja akaiendea mbao ya magazeti na kutazama nini kilichoandikwa. Habari zilikuwa zile zile za jana yake ila zilikolezwa wino tu. Akapita taratibu na kuuendea mlango mkubwa wa jengo hilo. Akasimama kidogo karibu na mashine za kutolea pesa, akatzama huku na kule, kila mtu alikuwa akiendelea na hamsini zake, akasogea pembeni na kubonya kidubwasha cha lifti, ilipofika akaingia na kuiamuru imfikishe ghorofa ya nne.

Alipofika ghorofa ya nne aliteremka na kwa kutumia ngazi alipanda kwenda ghorofa ya sita ambako ofisi yake ndipo ilipo. Akaufikia mlango na kusita kidogo, jicho lake likatua chini ya mlango, kulikuwa na ncha ya bahasha ikichungulia nje, akaivuta kwa vidole vyake na kuitazama. Ilikuwa bahasha nyeupe, ndani ilikuwa na kitu kama kadi ya kibiashara, akaitazama kwa makini sana, akataka kuichana, akasita, akafungua mlango wake na kuucha wazi, akatulia kidogo, kisha akaingia ndani na kutembea taratibu. Kila kitu kilikuwa kama alivyokiacha mara ya mwisho, hakuna kilichoguswa wala kusogezwa. Moja kwa moja akaiendea jokofu ndogo iliyokuwa hapo akafungua, akatazama chupa zake za kinywaji, akacheka kidogo kisha akafunga, ijapokuwa alikuwa na kiu lakini hakuchukua chochote baada ya kuona mpangilio wa zile chupa umegeuzwa kwani yeye na Gina walikuwa na mpangilio wao maalum.

“Kama mmeweka sumu mtakunywa wenyewe,” akawaza kisha akavuta droo yake na kupekua hapa na pale, akachukua saa yake ya mkononi na kuivaa, akachukua miwani yake yenye uwezo wa kurekodi picha mjongeo, kuona nyuma bila kugeuka, bastola yake ndogo kuliko zote inayotosha kwenye kiganja cha mkono akaipachika mahala pake.
Akalivua koti lake na kulitupia huko, akavua shati na kuvaa fulana nyeupe inayobana mwili kisha akarudishia kila kinachohitajika, akafungua kijikabati kidogo na kutoa kikoti cha Kodroy akakivaa juu yake, pesa kama shilingi za Kitanzania laki tano akazitia kibindoni. Akaiinua bastola yake na kuisukuma slide mbele nyuma, “Iko fiti,” akawaza na kuikubali, kisha akafyatua magazine na kuiweka mezani, akapanga risasi zake nane na kuirudishia mahala pake, akaislide tena na risasi moja ikatumbukia chemba, akailoki na kuitia mkandani.
Akatulia kwa sekunde kadhaa kisha akaamua kutoka kwa nguvu zote kwenda kumsaka mbaya wake ambaye mpaka nukta hiyo hakujua yuko wapi. Alitoka na kuufunga mlango nyuma yake, akaingia kwenye lifti kwa minajiri ya kuteremka chini, kabla mlango haujajifunga, kijana mwingine akawahi kuingia na kusimama jirani na Amata lakini kwa nyuma. Kamanda Amata aliichomo miwani yake na kuivaa kisha kumtasama kupita vioo vidogo vilivyo kwenye miimo ya miwani hiyo.

Yule kijana alikuwa ametulia tuli hasemi lolote lakini kwa jinsi macho yake yalivyokuwa yakipepesa, Amata akajua kuwa huyo si mtu mwema, akajiweka tayari kwa lolote kwani mwili wake kw muda huo ulikuwa ukichemka damu ukizingatia bado ndugu zake hakujua wako wapi, kitendawili.
Aiendelea kumtizama huku akiangalia tarakimu zinazobadilika kutoka kumi na tano na kuteremka chini kwenda G, akamwona mtu huyo akiingiza mikono ndani ya kijaketi chake, akajua nini kinataka kutokea, akajiweka sawa.
Lakini alikuwa anatamani kucheka kila akimtazama kijana huyo aliyeonekana kujawa na wasiwasi. Ilionekana katika kazi hizo huyu atakuwa ni mwanafunzi tu kwa jinsi asivyojiamini, Amata akanyoosha mkono na kubofya tarakimu zile kwa kuingiza namba kama sita hivi na lifti ikasimama ghafla. Yule kijana alitoa waya kwenye koti lake na kutaka kumkaba Amata.
Kamanda Amata hakupoteza muda, alimjifanya anaudaka ule waya kumbe ilikuwa ni danganya toto, alipiga kiwiko cha mbavu dogo akalegea, alimnyanyua kwa kumshika mikono yake na kupigiza upande wa pili, akambwaga chini hoi. Kisha akapiga goti moja na kuondo amiwani yake usoni.

“We ni nani?” akamuuliza.

“Mi-mi-mi ni-metu-mwa,” akajibu huku akijikinga mikono yake usoni.

“Najua umetumwa, wewe ni nani?”

“Jose,” akajibu.

“Nani aliyekutuma?” akamchapa swali linguine.
“Mdada mmoja, yuko hapo nje,”

“Kavaaje na anaitwa nani?” Yule kijana hakujibu hilo swali, akabaki akimwemwesa mwemwesa midomo, Amata akamwinua kichwa na kumpigiza chini kwa nguvu.

“Nasemaaaa!” akalia kwa uchungu.

“Haya sema!” akamlazimisha kusema, mara hii bastola ikiwa mkononi.

“Simjui jina, alinipa hiki, akaniahidi pesa,” akatoa kadi ya kibiashara na kumpatia.
Kamanda Amata akaitazama na kusoma jina na namba za simu zilizopo, lakini alishangaa kuona jina la mwenye kadi ni la kiume. “Haijalishi, ndiyo njia zao hizi,” akawaza, akamtazama Yule kijana, yuko hoi pale chini, akamwacha na kufyatua zile namba kisha akaiamuru ile lifti iende juu kabisa. Huko akatoka na kuiacha akatumia ngazi kuteremka mpaka ghorofa ya sita ilipo ofisi yake, akaichukua ile kadi, na kuandika zile tarakimu katika mashine maalumu ambayo ina uwezo wa kukupigia simu ukajua unaongea na binadamu kumbe kompyuta, unachokifanya ni kulisha maneno kisha kuyaoanisha na yale ya upande wa pili, kwamba huyu akisema hivi yenyewe iseme vile, kisha akaunganisha ile mashine na simu yake ndogo aliyoipachika kwa mkono huku kisikilizio chake kikiwa masikioni, akatoka na kuondoka zake.

ITAENDELEA
 
RIWAYA: KITISHO
MTUNZI: richard MWAMBE
-Man In The Mirror-

Wakakubaliana hilo na utaratibu wa kila kitu ukafanyika. Ijapokuwa Gina alikubali kwa shingo upande kwa kuwa yeye alipenda kuingia msambweni kuwasaka wenzi wake.
Inspekta Simbeye, aliyekuwa akilitumikia jeshi la Polisi kwa kofia mbili, moja kama Inspekta wa Polisi lakini ya pili ni ile ya Ukachero wa serikali, Usalama wa Taifa, aliwekwa pale kwa mpango maalumu wa kuchunguza maafisa wa Jeshi hilo kama kuna lolote baya wanalolifanya juu ya nchi hii.

SEHEMU YA 10

9
Kerege – bagamoyo

WAJUMBE WA KIKAO KILE CHA DHARULA walipiga makofi baada ya kupewa taarifa kuwa watu wao wote wamepatikana isipokuwa mmoja ambaye wao kama wao hawakuona kama anaweza kuwa na dhara lolote.

“Kazi imekwisha!” Pancho aliwaambia wenzi wake.

“Vijana wamefanya kazi ngumu na nzuri wanastahili pongezi,” mwingine aliongezea.

Baada ya furaha yao hiyo kukamilika na kugongeana bilauri kama ishara ya kupongezana,; Pancho Panchilio aliwataka watu wake kuteremka kuzimu ili kushuhudia kile kilichoitwa ‘Hukumu ya Mwisho’.

“Na tutawafuatilia mbali katika uso wa dunia,” Pancho aliwaambia wenzi wake. Kisha kila mmoja akavaa uso wake wa bandia akiwa sehemu yake ambayo mpaka hapo hawakuweza kuonana sawasawa. Wakavaa kisha Pancho akiwa katika guo jeusi akifuatiwa na wajumbe wake watatu wakatoka na kuteremka ngazi kuelekea bondeni walikopenda kukuita Kuzimu.

§§§§§
Scoba aliendlea kusukuti huku bado akiwa kasimama hakujua lipi lakufanya mbele ya kamera ile. Baada ya kuumiza sana kichwa akakumbuka kipande kimoja cha kisa ambacho aliwahi kusimuliwa na Kamanda Amata jinsi anavyozipita kamera kama hizo, akatabasamu kisha akajirusha kwa kutanua miguu na kunata ukutani, akiwa katanua miguu yake na kukanyaga huku na kule na mikono hivyo hivyo, akanata juu kabisa na kuanza kujivuta kwa namna ambayo wewe huwezi hata kidogo, ukimtazama unaweza kusema na mjusi au kenge.
Aliifikia ile kamera na kuushika waya wake kutoka nyuma akauchomoa, kisha akajiachia na kutua chini taratibu. Kisha akaenda kwa mwendo wa kasi mpaka katika zile ngazi, alipofika tu alikutana uso kwa uso na mtu mmoja aliyekuwa akipanda juu, Scoba akaruka na kutua juu ya ukingo wa ngazi uliotengenezwa kwa mabomba ya aluminiam akaseleleka na mguu mmoja akamtandika teke Yule mtu kisha akajiachia na kumshukia pale chini; kabla hajasema lolote akambana koo kwa goti lake.

“Wako wapi?” akamwuliza.

“Akina nani?” Yule bwana aliongea kwa taabu.

“Wako wapi watu wangu? Mmewaweka wapi?” akauliza kwa ukali lakini kwa sauti ambayo haiwezi kwenda popote.

“Hakuna watu wako huku aliyekwambia wapo ni nani?” Yule bwana akajibu kiujeuri. Scoba akamnyonga mkono na kuuvunja, Yule bwana akapiga yowe la uchungu, Scoba akaona itakuwa noma, akamkamata na kumvunja shingo kisha akaichukua bunduki yake aina ya S.M.G na kuteremka ngazi mpaka kwenye maboksi Fulani akajificha. Watu wawili wakapita eneo lile wakitangulizana, akatulia na kusubiri Yule wa pili ili amputeze lakini alighairi baada ya kusikia mazungumzo yao matamu.

“Wanauawa wote, tena sasa hivi,” mmoja akamweleza mwenzie.

“Yaani ni historia,” mwingine akamuunga mkono. Alipopita wa kwanza akamwacha wa pili akamkata na kabala moja matata sana kisha akamvuia kwenye maboksi taratibu na kumtuliza. Yule wa kwanza akajkuta kila akiongea hakuna kuungwa mkono akageuka kutazama kulikoni akakutana macho na Scoba. Bila kuchelewa Scoba alirusha kisu maridadi kabisa na kumchoma koromeo, akajibwaga chini.

§§§§§
Madam S alifunguliwa minyororo na kukokotwa kuelekea katika chumba cha mauaji, Chiba naye akachukuliwa kikondoo namna hiyo, Dr. Jasmin kwa kuwa yeye hakuteswa kama wengine alitembea mwenyewe mpaka ndani ya chumba kile cha kutisha.

“Wafunge pale huyo bibi na huyo kijana mtukutu, kisha mlete huyo rembo mbichi hapa,” JoKi alitoa amri nayo ikatekelezwa. Walipomaliza wakaambiwa wakamlete Kamanda Amata li kazi ya mauaji ianze kama ilivyopangwa. Amata akaletwa, na ye kama kawaida akatuliaa na kukokotwa mpaka ndani ya chumba kile kinachonuka damu mbichi na iliyoganda, macho yake yalikuwa yakiwatazama wote waliojipanga mle ndani wakiwa na silaha nzito nzito. Mara hiyo hiyo Pancho na watu wake waliingia ndani ya chumba kile na kusimama mahala Fulani.

“Sasa tunataka tuanze shughuli yetu, karamu ya damu, JoKi! Nataka ufanye kazi hii kama nilivyokuagiza, lakini kwanz ahuyo mrembo lazima aingiliwe nah ii ni motisha kwenu vijana wangu haya na muanze kazi sasa ya kumuingilia,” Pancho akatoa amri, vijana wawili walioshiba kimazoezi wakamvamia Jasmin, mmoja akaanza kumvua nguo kwa nguvu huku mwingine akishusha zipu yake kuuchomoa mshedede.
Yule jamaa aliyekuwa akimvua nguo Jasmine alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuchapwa makonde mawili matamu kabisa, akapepesuka pambeni na kujipanga upya, alipomwendea Jasmin ili ampe kibano alikutana na mapigo matano ya karate ya haraka haraka yaliyompeleka chini. Yule mwingine alitoa macho baada ya kujikuta dudu lake likikatika vipande viwili.

“Aaaaaaiiiggghhhh!!!” alipiga kelele huku akijiangalia, kila tu akashtuka waliposikia sauti ya kisu kikitua ardhini huku kikiwa kimekata dhakari ya Yule bwana.

“Shit! Muue huyo mwanamke haraka!” JoKi alitoa amri huku akiwakinga Pancho na wenzake.

“Nini JoKi?” Pancho akauliza.

“Tumevamiwa!” akatamka neno hilo na hapo hapo alishuhudia minyororo aliyofungwa Kamanda Amata ikikatika kwa shabaha maridhawa kutoka kwa Scoba. Amata aliruka sarakasi maridadi na risasi nne zilichimba chini, alipotua chini tayari alikuwa na shingo ya mtu, alimkamata na kumzungusha kichwa, Yule bwana akatoa macho na kuachama kinywa chake,kisha akambwaga chini. Alipogeuka huku na kule, JoKi hayupo, Pancho na watu wake hawapo.

“Scoba fungua hao, fanya juu chini wafike kwenye gari, hii kazi niachie mimi niimaize, pumbavu zao,” Kamanda Amata akampa maagizo Scoba kisha yeye akajibana mahali na S.M.G mkononi, akanyata kwa tahadari akiwa hajui wapi wale watu wamepotea ghafla namna hiyo. Mara taa zote zikazimika, giza likachukua nafasi ndani ya jingo hilo.
Scoba akaivaa miwani yake na kuendelea kuona vizuri kabisa, akawafungua Chiba na Madam S.

“Asante T.S.A 4, hakikisheni humu ndani hatoki mtu akiwa hai,” Madam S alitoa amri mara moja kama cheo chake kilivyo.
Mara sauti ikasikika kutoka katika vipaaza sauti vizivyoonekana.

“Ak! Ak!Ak! Ak! Hii ndiyo himaya ya Shetani, Taifa ndani ya nchi, hamjafanya lolote na hakika hamtatoka humu mkiwa hai, lazima muongee na bwana ngurumo,” ile sauti ikacheka tena kwa dhihaka.

“Usimsikilize huyo hanithi, Scoba ongoza mbele Jasmine linda nyuma ninyi ndio mna nguvu kwa sasa mi namaliza kazi,” Kamanda Amata akatoa maelekezo kisha kwa mwendo wa taratibu alipita kwenye ujia mrefu ulioonekana ukienda mahala Fulani.

“Nitakukamata tu, na leo itajulikana mbivu na mbichi,” akajisemea. Mara nyuma yake akasikia kama mtu aiyetua ghafla kwa miguu laini, akageuka ghafla na kujikuta akipata pigo moja kali la kung fu, akayumba na kusimama tena, akajikuta akipigwa ngwala tamu, akapaa hewani na kujibwaga chini, akajikunja na kujiinua kwa ustadi. Alikuwa ni Naima aliyemtembezea mchezo huo.

“Malaya mkubwa wewe! Sasa umeingia mikononi mwangu!” Kamanda akaunguruma.
Mara ile sauti ikasikika tena ikicheka na cheko lake likifanya mwangwi,

“Mtoto wa kike kutoka Kigoma lazima akuoneshe kazi”.
Mara taa zikawaka, Naima akajizungusha huku akipiga vijikelele kama nyau, akampelekea pigo la kwanza Kamanda akaliona, la pilia akaliona la tatu akaliona, la nne Kaliepa kwa chini na kujizungusha kwa kasi, aliupiga mguu wa Naima lakinia Naima aliruka sarakasi hiyo ile ngwala ikamkosa, Naima alitua sakafuni na kupiga teke kali huku akiruka tik tak; hilo lilimpata Amata na kumuinua juu juu na kumbwaga chini mzima mzima.

Naima alitua sakafuni na kusimama kwa madoido huku akimwonesha ishara ya mkono Amata akimwambia, “ Come to me boy, come to me boy”.
Dharau hizo Amata alizichoka, akajirusha kujiinua, Naima akataka kumwahi, akaruka teke ambalo lilikusudiwa kutua kidevuni mwa Amata lakini akaikinga mikono yake na kuudaka mguu wa Naima, akauzungusha kwa minajiri ya kuuvunja lakini Naima naye akaruka hewani na kujizungusha sambasamba na akili ya Amata na mguu wa pili akirusha teke lingine lakini Amata akaliepa na kumwachia, wote wakaanguka chini. Amata akawahi kuinuka na kujiweka sawa, Naima alipoinuka alikutana na mapigo kumi na mbili ya karate, kwa kasi aliyoitumia Kamanda Amata , Naima aliweza kuyakinga mapigo manne tu na nane yaliyofuata yalimwacha hoi.

“Come to me bitch!” Kamanda Amata akamwita kwa dharau, Naima damu zilimtoka kinywani na puani, alijifuta bila mafanikio.

“Hesabu ushakufa Naima!” Amata alimwambia.
Naima akasonya na kujitutumua kumvamia Amata, akakutana na kono lenye nguvu lilimtandika ngumi moja ya maana katika ziwa lake la kushoto. Naima alisimama ghafla akiwa katoa macho, akijitahidi kuongea lolote lakini alijikuta hawezi. Alipotaka kuanguka Amata akamwahi, akamtazama husoni, akambusu kwenye paji la uso. Mara taa zikazimika akasikia sauti ya bastola inayoondolewa usalama, akawahi kuruka na kumwacha Naima akifumuliwa vibaya na risasi hizo.

“Tulia, fuata maelekezo yangu, sasa hivi sina masihara na kiumbe yoyote Yule, nipeleke walipo mabosi wako,” akaamuru.
JoKi akiwa mikono juu, akatulia kama alivyoamuriwa, akataka kugeuka, Kamanda akamzuia.

“Sijakwambia ugeuke, nimekwambia unipeleke walipo vinyamkera wako,” akamwambia tena. JoKi akatafakari jambo,

“Sasa bila kugeuka nitakupelekaje walipo? Hivi ninyi mnachokifanya mnakijua? Mtajuta kuzaliwa ndani ya nchi hii,” JoKi akaongea.

“Funga domo lako kibaraka tu wewe, na sasa utatujua sisi ni nani, mlifikiri jaribio lenu litafika wapi? Haya nioneshe hao vinyamkera wako,” Amata akaamuru.

“Siwezi kukuonesha na huna la kunifanya,” alijibu JoKi huku akigeuka mzima mzima na kukutana na Amata aliyekuwa amefura kwa hasira.

“Ha ha ha ha, Kamanda Amata, nasikia tu unavyovuma katika visa vyako vya kubahatisha, safari hii maji yapo shingoni ee?” akaongea kwa ngebe zilizompandisha hasira Amata, akaiweka vizuri bunduki aliyoishika mkononi mwake.

“Amata, wanaume wakutanapo huweka silaha chini na kupambana kwa mikono,” akaongea kwa dharau huku mikono yake kaiweka kiunoni kana kwamba anaongea na mtu wa kawaida mbele yake.

“Najua hila zako, ichukue wewe utumie kunishambulia,” Amata akamwambia huku akimrushia ile bunduki. JoKi akainua mikono yake ili kuidaka na ndilo kosa alilolifanya. Konde moja la kilo nyingi lilitua sawia mbavuni, la pili na la tatu, JoKi akawa hoi, akajaribu kujipanga lakini Amata hakumpa nafasi kwani alimvurumishia makonde yasiyo na idadi mpaka akaenda chini na kuanza kubingirika kwenye ngazi, akafka chini akiwa hoi.

“Kelele zote mi nilijua unaweza mchezo kumbe hamna kitu, boya tu, haya simama sasa,” Amata akamwambia JoKi. Bado JoKi alikuwa pale chini, Kamanda Amata akamsogelea. Joki alifyatuka kasi na kumtia ngwala Amata, lakini hakukubali, aliruka beki na kusimama kwa miguu yake miwili, wakati huo tayari JoKi nae alikuwa wima. Kamanda Amata alirusha teke lililopanguliwa vyema na JoKi. JoKi alipeleka mashambulizi ya karate kwa Kamanda lakini mapigo yote yalikingwa kwa ufundi wa hali ya juu. Wakasimama pande ofauti wakitazamana kama majogoo hasimu, yenye uhasama wa kudhulumiana tetea.
JoKi alifyatuka na kucheza karate kadhaa kwa kumwelekezea mapigo ya hatari Amata, lakini alijikuta hapati kitu baada ya Kamanda Amata kuyacheza vizuri na kubaki imara akimtazama JoKi aliyeishiwa cha kufanya. JoKi akajikunja na kuanza upya mashambulizi, safari hii alikuja na ujanja mwingine ambao umakini kwa kamanda Amata ulihitajika. JoKi alipeleka mashambulizi makali ya mikono na wakati huo huo akibadilika na kutumia miguu yake. Kasi ya mashambulizi hayo ilimfanya kamanda Amata apate tabu kucheza na akili mtu huyo, lakini yote ya yote Kamanda Amata aliyakinga kwa ufundi. JoKi alimpiga ngwala ya nguvu na Amata .lirushwa juu, lakini akiwa hewani alijigeuza na kutumia mguu mwingine na kumzabua teke kali la shavu na kumvunja taya. JoKi akayumba na kujibamiza ukutani huku akijishika taya lake la chini lililohama mahala pake. Hakumjali, alimpa mapigo makali na kumwacha akiwa hoi sakafuni hajielewi, akamfuata na kumkamata kichwa chake akambamiza ukutani kwa nguvu kisha akamwinua mzima mzima.

“Nioneshe walipo,” akamwambia huku akiwa kamkunja vyema shati lake, damu zikimvuja.

“Wapo safe house,” akajibu huku mabonge ya damu yakimtoka kinywani.

“Safe house ndo wapi?” akamwuliza.

“Ipo chini kabisa ya jingo hili, lakini huwezi kufika kabla hujauawa,” akamjibu huku akitoa cheko la ajabu kisha akatokwa na uhai.

§§§§§
Kazi nzito ilikuwa upande wan je ambako Scoba na Jasmin walikuwa wakiwadhibiti walinzi wa jengo hilo. Watu wa kijiji hicho walikimbia mbali wakisema majambazi yamevamia jumba hilo.
Chiba alipita huu na kule na kutokea kwenye mlango mmoja ulioandikwa ‘Control Room’ akauchezea huo mlango kidogo tu na kujikuta ndani. Chumba kikubwa kilichojawa na mitambo ya mawasiliano, kompyuta na vitu vingine, kutoka pale ndipo alipoona kamera zote za usalama za eneo lile jinsi zilivyokuwa zikifanya kazi na kuangaza kila eneo, alitikisa kichwa baada ya kuona ugumu wa kazi yao ulikuwa wapi kwani walionekana kila walipokwenda, jambo la kwanza alizima tambo uliokuwa ukiwaunganisha watu wote wa jengo hilo kwa simu maalum za ndani ‘Voip’. Baada ya hapo akaelekea mahala palipokuwa na kitu kama kabati lenye switch mbalimbali, akaelewa ni switch za milango, akaibofya na kufungua milango yote ya jumba hilo kisha akaharibu mfumo mzima.
Akiwa katika shughuli hiyo akasikia mlio hafifu wa bastola inayoondolewa usalama.

“Nani alikwambia?” sauti ikatoka nyuma yake, “Haya mikono kichwani kisha geuka taratibu,” aliamuriwa. Chiba aliweka mikono kichwani na kugeuka kwa kasi na kuipiga teke ile bastola kisha akajirusha sarakasi na kuichukua mikononi mwake, Yule bwana alijikuta hana ujanja, macho yakamtoka. Kisha akamuongoza kwenye mitambo yake.

“Nioneshe mabosi wako walipo,” akamwamuru. Yule bwana hakuwa na aujanja aliwasha luninga mojawapo iliyowaonesha wale mabwanyenye kila mmoja akiwa katika harakati za kuiacha himaya hiyo, Chiba alibaki kinywa wazi, hakuamini kile anachokiona, aliwatambua watu wale kwa uwazi kabisa bila kificho akajikuta akiishiwa nguvu. Alipogeuka nyuma kumtazama Yule kijana hakumuona, katoweka. “Shiit!” akang’aka na kuiweka bastola yake vyema mkononi mwake kisha akaanza kuzunguka humo ndani kumtafuta.
Yule kijana alijificha kimya upande wa pili wa mashine zile, mkononi alikuwa na kisu akimvizia Chiba kufika upande huo ili amfanyie kweli, masikini, hakujua anacheza na kiumbe cha aina gani katika tasnia hiyo ya mchezo wa visu. Katika kupita akitafuta, Chiba alimwona Yule kijana akichungulia, akajifanya hamwoni kabisa na kuendelea kutafuta huku kampa mgongo. Yule kijana akaona hapo ndipo pa kumpata adui yake, akatoka mzima mzima na kisu mkononi kumpamia Chiba kwa nyuma. Chiba alimkwepa na kumdaka mkono, akauzungusha na kumnyanyua kisha kumbwaga chini na kumbana vyema.

“Nipe namba za milango!” akamwamuru.

“Sizijui,” akajibu huku akikunja sura kwa maumivu.
Chiba akaunyonga mkono kwa nguvu, “Taja, kabla sijakumaliza,” akamlazimisha huku akiunyonga ule mkono.

“Nataja, na-ta …” kabla hajamaliza, Chiba alishuhudia Yule kijana akitoa macho na kisu kimedinda shingoni mwake,

“Wamemuua!” akajisemea; kwa kasi ya ajabu alikichomoa kile kisu na kukirusha upande kilipotokea huku yeye mwenyewe akibiringika kuliacha eneo lile, akashuhudia risasi zikiufumua mwili wa Yule kijana ilhali mtu aliyemlenga akidondoka jirani na mlango bila uhai. Chiba akasimama chapchap na kuangaza macho huku na huko, chumba kilikuwa kimya, hakuna mtu zaidi yake na zile maiti mbili tu. Akahakikisha usalama kisha akazipekua zile maiti na kupata funguo moja ambayo hakujua hata ni ya kitu gani, akaitia mfukoni. Hakuzijali maiti akapanda juu ya kiti cha magurudumu kilichokuwa hapo na kuanza kucheza na zile kompyuta. Alishangaa kuona kuwa wale jamaa walikuwa wamejiunganisha na vitengo vyote muhimu vya serikali wakipata siri mbalimbali za vitengo hivyo.
Akaendelea kupekuwa na kukuta habari nyingi za Usalama wa Taifa zikiwa katika moja ya kompyuta hizo.

“Ni nani hawa?” akajiuliza bila kupata jibu. Akasogeza kiti chake na kuelekea kwenye luninga kubwa iliyoonesha jingo lote ndani na nje na kuanza kukagua sehemu moja baada ya nyingine, akatazama vyumba mbalimbali vya jingo hilo na kugundua kuwa bado walikuwa hawajafika hata nusu ya hifadhi ya jingo hilo.

“Shiit!” alijikuta aking’aka na kujisukuma kwa nguvu mpaka kwenye meza ndogo yenye simu na kuiyakua kisha akabofya namba fuklani na kuweka sikioni.

“…Inspekta Simbeye, Chiba anaongea hapa!” akaijibu sauti ya pili iliyoitikia simu hiyo.

“…Oh, Chiba, nafarijika kusikia sauti yako Kamanda wangu, nipe dondoo,” akamwambia.

“…Inspekta naomba haraka iweekanavyo uje na vijana wa kazi wasiopungua kumi na tano wenye silaha nzito zilizoshiba, eneo ni Kerege, Bagamoyo, plot namba KG/BY 1230p…” kisha akakata simu. Alipogeuka kwenye luninga hakuwaona wale Mabwanyenye kwenye vyumba vyao, wametoroka! Akazima swichi kubwa na umeme ukakatika kila kona ya jengo lile, akilenga kuwanasa kama walikuwa wakijaribu kutoroka na chombo chochote kitumiacho umeme, kisha akachukua silaha kutoka kwa mmoja wa maiti wale na kutaka kutoka kwenye kile chumba, akakumbuka kitu; akarudi.
Akaenda kwenye moja ya kisanduku na kutaka kufungua akashindwa, akagundua kuna funguo hutumika, akafikiri kidogo na kuchukua kale kafunguo alikochomoa ka Yule jamaa, akatumbukiza na kuzungusha kidogo tu, mlango ukafunguka. Ilikuwa na sisytem unity iliyounganisha kompyuta zote ikiwa na maana kuwa ilihifadhi data zote za wale jamaa. Kwa kutumia ile bunduki akavunja kufuli lililokuwako nyuma ya dubwasha hilo, akaondoa funiko lake na kutazama anachokitaka, akafyatua waya nene nene zilizojaa huko, akavuta dubwasha Fulani kubwa kubwa na kulichomoa kutoka kwenye system ile, akatikisa kichwa kwa ushindi, kisha akatokomea nalo.

ITAENDELEA
 
RIWAYA: KITISHO
MTUNZI: richard MWAMBE
-Man In The Mirror-
WASAP: +255 766 974865

Akaenda kwenye moja ya kisanduku na kutaka kufungua akashindwa, akagundua kuna funguo hutumika, akafikiri kidogo na kuchukua kale kafunguo alikochomoa ka Yule jamaa, akatumbukiza na kuzungusha kidogo tu, mlango ukafunguka. Ilikuwa na sisytem unity iliyounganisha kompyuta zote ikiwa na maana kuwa ilihifadhi data zote za wale jamaa. Kwa kutumia ile bunduki akavunja kufuli lililokuwako nyuma ya dubwasha hilo, akaondoa funiko lake na kutazama anachokitaka, akafyatua waya nene nene zilizojaa huko, akavuta dubwasha Fulani kubwa kubwa na kulichomoa kutoka kwenye system ile, akatikisa kichwa kwa ushindi, kisha akatokomea nalo.

SEHEMU YA 11

§§§§§

“Hapana, lazima niende!” Gina alimsisitizia Inspekta Simbeye.

“Gina nimekuleta huku ili upumzike, sasa acha tupeleke kikosi katika eneo la tukio,” Inspekta Simbeye akambembeleza Gina lakini Gina hakukubaliani na bembelezo hilo. Mwisho alikubali kwa shingo upande kubaki Hospitali ya Lugalo chini ya uangalizi wa madaktari wa kijeshi.
Inspekta Simbeye alichukua vijana wachache wanaojua kazi, kikosi maalumu cha kukomesha ujambazi kilichoundwa na Kamanda Toss kikaingia kwenye Land Cruiser za Polisi. Kutoka kituo kikuu gari hizo zilichukua uelekeo wa Makongo mpaka Mwenge waipomchukua Inspekta huyo na kuongoza kwenda Kerege. Kwenye gari hizo hakuna aliyeongea, kila mmoja alikuwa kimya kabisa akiitafakari shughuli inayomkabili, bunduki zilikuwa tayari zimejazwa risasi na magazine za akiba zikipachikwa kwenye vikoba maalum tayari kupokea zile zilizopo chemba pale itakapobidi.

KEREGE
KAMANDA AMATA BAADA YA KUHAKIKISHA JOKI AMEKATA ROHO; akaondoka upesi eneo lile, kila alipokuwa akipita kutazama tazama alikuwa safari hii milango iko wazi kabisa, hakuna tena milango ya siri, kazi ya Chiba ilisaidia. Akaiendea lifti ili aweze kushuka chini kabisa ya jengo hilo. Kwa mbali akiwa anasikia milio ya risasi za piga nikupige alijua wazi kuwa huko kazi inaendelea.
Ghafla akasimama kwenye moja ya kona za ndani ya jingo hilo baada ya kusikia michakacho ya viatu vya mtu anayekuja upande wake, akajiandaa kwa shambulizi la dharula, alipohisi mtu huyo amekaribia, alijitoa mzima mzima lakini pigo lake likakingwa kwa ustadi wa hali ya juu.

“Oh, sorry asee! Chiba vipi?” kumbe alikuwa Chiba.

“Yeah, hapa ni kujilinda muda wote, tuelekee chini, hawa jamaa wako huko,” Chiba akatoa maelekezo na kisha wote wakateremka kwa kutumia ngazi kwa maana Chiba alikuwa amezima umeme na kufanya lift zote zisifanye kazi. Haikuwachukua muda kuwasili chini kabisa ya jingo hilo kubwa na la kisasa, “Lilijengwa kwa miaka mingapi hili?” Kamanda akajiuliza, huku wakiufuata mlango mmoja baada ya mwingine, lakini vyumba vyote vilionekana tupu.

“Hawapo Chiba, laiti ningewapata!” Kamanda alimwambia Chiba huku akiiteremsha silaha yake kutoka mikononi na kuiweka mahala pake.

“Nimempa taarifa Inspekta, yuko njiani,” Chiba akatoa taarifa kwa Kamanda.

“Safi sana Chiba, kumbuka hapa sote hatuna mawasiliano na dunia ya nje,” kamanda akaitikia kisha wakaendelea kupekua chumba kimoja na kingine. Katika moja ya vyumba hivyo kulionekana kuna mlango wa siri lakini ulikuwa wazi ndani yake, akausogelea na kuchungulia ndani yake, ulikuwa ujia mrefu sana uliopotelea gizani.

“Hii ni njia ambayo kwa vyovyote wametorokea,” Kamanda akamwambia Chiba.

“Kila mmoja alikuwa na njia yake Kamanda, hapa alitumia mmoja wao,” Chiba akajibu. Kamanda Amata akageuka kumtazama kama akihoji kitu, lakini mwisho aliuliza.

“Umejuaje?” akamwuliza.

“Nimewaona katika dakika zao za mwisho kutoroka lakini mshenzi mmoja akanivamia; katika kupambana naye ndipo nilipowapoteza sikuona wametorokaje lakini walikuwa vyumba tofauti,” akaeleza.

“Umenikiwa kuona sura zao?” akauliza tena.
Chiba akatulia kwa nukta chache kwa maana aliwaona mara hii wakiwa hawana vinyago na aliwatambua kuwa ni vigogo wakubwa serikalini, “Je kama walitumia sura za bandia kutughilibu?” akawaza, kisha akamtazama Amata.

“Hapana, walificha sura zao kama kawaida,” akajibu.

“Ok, tutawajua tu, usiguse kitu watu wa Foresinc Bureau waje kufanya kazi yao ya kunasa alama za vidole na nyinginezo,” kamanda akamwambia Chiba huku wakitoka na kuelekea chumba kingine, nako wakakuta mambo hayo hayo, wakatoka na kupita vyumba vingine kama vitatu vilivyoonekana viko katika mtindo huohuo. Wakaviacha na kuendelea na uchunguzi wao zaidi na zaidi. Katika ghorofa ya chini wakagundua jambo ambalo liliwatia hofu, mioyo yao ikashtuka, kama wangekuwa na mioyo myepesi wangeziamia au hata kufa kabisa.

“Hawa ni mashetani!” Chiba akasema.

“Nin hiki?” Kamanda akauliza huku akivuta hatua ndani ya chumba hicho kikubwa, “Hawa jamaa hawastahili kuishi kabisa, ningewatia mkononi wangejuta kuzaliwa,” akaongeza.

“Kamanda, hapa msaada wa haraka unahitajika, nafikiri vijana watakuwa tayari nje,” akasema Chiba.

§§§§§
LAND CRUISER ZA POLISI ziliingia kwa fujo eneo lile na vijana wa kazi wakaruka tayari kuanza kudhibiti eneo hilo. Ilikuwa kama sinema ya kizungu vile. Inspekta Simbeye akawapanga vijana kuzunguka jingo hilo na wengine kuingia ndani kupitia lango kuu, haikuchukua dakika kumi tayari walizingira na risasi kadhaa zilirindima ndani ya wigo huo, kisha kundi la watu waliokuwa katikanulinzi wa jingo ilo waliwekwa chini ya ulinzi.

“Hivi hili jumba lina milikiwa na nani?” Simbeye akajiuliza bila kupata jibu. Vijana wake bado wakiwa katika sakasaka hiyo upande wa pili wa jingo walipomweka chini ya ulinzi Madam S na Jasmine. Kutii sheria bila shuruti, Madam S akiwa kachafuka damu zilizoganda, alisalimisha silaha yake na Jasmine akafanya hivyo kisha wakatiwa pingu. Inspekta Simbeye aliwaona wakiletwa kwake wakiwa na pingu mikononi, wakaamuriwa kukaa chini pembeni kidogo kwa wenzao.
Scoba alitokea pale ambapo gari ya Gina iliegeshwa baada ya kutekwa na kuletwa huku, moja kwa moja akaliendea lango na kulifungua na kuchungulia nje kwa minajiri ya kuwashambulia waliopo huko na apate jinsi ya kutoa gari hi;lo na kuwaokoa wengine kama walivyopanga, alishangaa alipoona vijana wenye silaha wakiwa wamewalaza chini vijana wengine kama kumi hivi tena kifudifudi, kwa jinsi alivyowaona tu akajua ni Polisi, akajitokeza mzima mzima na bunduki yake mkononi.

“Jisalimishe kama ulivyo, weka silaha chini,” amri ikatoka upande wa nyuma yake, Scoba akafanya hivyo na kuamuriwa asogee mbele, akafungwa pingu na kulazwa chini kama wenzake.

§§§§§

“Inspekta!” Kamanda Amata aliita wakati alipokutana na Simbeye katika uwanja wa himaya hiyo, huku akishangaa huku na kule kuwaona wenzake wote wamepigwa pingu isipokuwa yeye na Chiba ambaye bado alimwacha ndani.

“Kamanda Amata! Pole kwa kazi na janga hili,” akampa pole huku akimpa mkono.

“Asante Inspekta, tunafuga mashetani nchi hii Inspekta, naomba vijana kama watano hivi na wewe mwenyewe, pamoja na mama yangu muache huru hakuna baya hapa tupo kazini, tuingie ndani ya jengo hili, tupite na muone wenyewe mchezo wa kuwapa watu viwanja bila kujua nia na malengo yao,” Kamanda alilalama. Madam S na Jasmine wakafunguliwa pingu zao, Scoba naye alkadhalika.

“Usishangae hawa ni watu kama wewe!” Inspekta alimwambia mmoja wa polisi ambaye alishangaa amri anayopewa ya kuwaweka huru watu hao.
Muda si mrefu, vijana watatu wakaingia ndani ya himaya hiyo wakiwa na suti nadhifu, mach yao yakiwa yamezibwa na miwani nyeusi, hakika walikuwa watanashati na nyuma yao aliwafuata mzee wa makamo mwenye mvi kadhaa kichwani mwake.

“Karibu sana Bwana Hosea, nafurahi umefika,” Inspekta alimkaribisha wakapeana mikono kisha wote wakaongozana kuingia katika jingo hilo.
Hakuna aliyekuwa akiongea, kila mmoja alikuwa makini kutazama kila kilichopo ndani humo, hakuruhusiwa mtu yeyote kugusa chochote kwa mikono uchi.
Chiba aliliongoza jopo hilo baada ya kukutana nao humo ndani, akawaingiza chumba cha mawasiliano, jopo hilo likabaki hoi.

“Tazama huu mtambo, unanasa habari kutoka ofisi zote za serikali, simu zote za kiofisi kuanzia za Rais na watu wake zote zinanaswa hapa, ona hii kompyuta ni kubwa sana inafanya mambo mengi sana, inanasa picha kule Uwanja wa Ndege, nah ii kama unavyoona inaonehsa mazingira yote ya Ikulu,” Chiba alikuwa akieleza.
Hosea akabaki kajishika kiuno, taratibu jasho lilikuwa likimtiririka.

“Nani mmiliki wa jumba hili, na alikuwa na lengo gani na Taifa hili?” akauliza, lakini wote walikuwa hawana jibu.

“Hatujamaliza, twendeni huku chini, naomba muwe na roho kavu kwa unyama uliopo huku,” Chiba akawaambia kisha akawafikisha ‘Kuzimu’, “Hapa ndipo wanapotumia kuua wabaya wao, mnauona ule mwili, mnaweza kuutambua, Mkuu?” akauliza. Hosea na vijana wake wakauendea na kuuangalia vyema, wakaugeuza huku na huko.

“Hapana simfahamu huyu,” Hosea akajibu.

“Ni mwandishi anayetafutwa na jeshi la Polisi kwa miezi mingi sasa, ameuawa mbele ya macho yangu,” Chiba akawaeleza.

“Chilese Zuberi,” Inspekta Simbeye akataja jina la Mwamndishi huyo, akachuchumaa kumwangalia vizuri na jeraha baya la risasi likiwa limeharibu kabisa sehemu ya nyuma ya kichwa chake.
Walipotoka hapo wakaelekea kwenye chumba kingine, na kukuta miili ya watu watano iliyofungwa kwa kuning’inizwa.

“Unyama gani huu?” akajiuliza Hosea. Wakatazama mwili mmoja baada ya mwingine na kuitambua miili ile kuwa ni ya watu ambao walipotea katika mazingira ya kutatanisha na hawakuonekana tena, mmoja wao akiwa Mwanasiasa machachari kabisa.

“Nimegundua kitu,” Simbeye akasema huku akiwageukia wenzake.

“Nini Inspekta,” Hosea akauliza.

“Kutokana na watu tuliowakuta humu wakiwa marehemu, na mikasa yao ambayo jeshi la polisi lilichukua kama vyanzo vya upotevu wao, kuna mtandao unaofanya kazi hii,” Simbeye akasema.

“Yeah, upo sahihi, siku zote wanalaumiwa Usalama wa Taifa pindi miili hii ikiokotwa haina kuchwa au meno, lakini hii nyumba ya nani? Lazima ukweli ujulikane,” Hosea akaongeza. Walipomaliza kukagua kila kona mle ndani wakatoka nje na kukuta tayari jeshi la Polisi limefika zaidi na waandishi wa habari kama kawaida yao walikuwa wametanda nje wakijaribu kupata habari hii na ile.
Madam S, Chiba, na Jasmine wakaingia kwenye gari maalum iliyokuja hapo, iliyofunikwa kwa vioo vyeusi, bila kupoteza muda ikaondoka eneo lile. Kamanda Amata na Scoba walibaki pamoja na vijana wa Polisi kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Akiwa kafuatana na vijana wawili wenye silaha waliingia vyumba vya chini na kupita ile milango iliyoonekana kama njia waliyotorokea wale mabwana, walitembea katika njia tofauti, moja ya njia hizo alipia Kamanda Amata na kijana mmoja wa Polisi mwenye silaha, njia nyingine aliingia Scoba na kijana mwingine nay a tatu aliingia Inspekta Simbeye na kijana wake. Cha kushangaza njia hizo tatu hazikukutana, kila moja ilikwenda kutokea mahala pake, na zilitokea kwenye nyumba tatu tofauti, utata. Mara tu baada ya hilo, uchunguzi mkali juu ya nyumba hizo, umiliki wake na uhalali wa kuwa hapo uliendelea; Mjumbe wa shina na Mwenyekiti wake walikuwa katika hali ngumu ya kuhojiwa hili na lile. Walipopata majibu ambayo kwayo yaliridhisha wakawaacha na kuondoka zao.

SHAMBA – baada ya siku 3
MADAM S, CHIBA, JASMINE, SCOBA, GINA NA KAMANDA AMATA wote walikuwa wameketi katika meza kubwa ya duara, kila mmoja mbele yake alikuwa na kabrasha lililojaa makaratasi. Walikuwa na majeraha ya hapa na pale, Gina bado alikuwa akiendelea kuuguza jeraha lake lakini sasa akiwa chini ya uangalizi wa Dkt. Jasmine.
Ukimya ulichukua nafasi kwa kila mmoja, walikutana tena katika meza hiyo ambayo daima wakikaa hapo basi ujue kuna maamuzi magumu ya kufanya. Gina alijigeuza na kujiweka vizuri kitini kwake huku mikono yake ikiwa juu ya meza na sura akiwa ameikunja kidogo.

“Pole sana Gina,” Madam S alimpa pole mwanadada huyo, akajikohoza, “Niliwaita siku tano zilizopita tuonane kwa kikao cha dharula lakini baadae nikagundua kosa nililolifanya, anyway, haina haja ya kuljadili bali tuangalie lile ambalo sasa ndio nimewaitia kabla ya kutazama lile nililotaka niwaeleze siku tano zilizopita ambalo litamhusu Kamanda zaidi,” akaongeza, alionekana wazi hata uongeaji wake haukuwa ule wa kawaida kwani bado alihisi maumivu ya hapa na pale na alihitaji mapumziko. Kipindi hicho cha siku tatu, T.S.A wote walikuwa pamoja Shamba, huko Gezaulole, wakipumzika na kuweka mikakati mipya, hakuna aliyejua walipo isipokuwa wao wenyewe.

“Kurasa ya kwanza kabisa kuna majibu kutoka kitengo cha utambuzi wa alama za mikono na vidole,” madam Sakawaambia na kila mtu akapekua jalada lake na macho kuyatumbulia hapo.

“Is it?” Gina alikuwa wa kwanza kupayuka.

“Yes It is,” Chiba akadakia. Wote wakamtazama kwa jicho kali.

“Una maana gani?” Madam akamuuliza.

“Nilikuwa nasubiri tu haya majibu kama yataoana na yangu, nilipozifanyia crossmatch hizi alama za vidole ambazo nilizipata kwenye vitasa vya milango ya mwisho ya vile vyumba vya chini, licha ya hivyo tu niliwahi kupata baadhi ya picha zao sekunde chache kabla hawajatoroka lakini sikuwa nauhakika nao kwani siku hizi teknolojia imekuwa; mtu anaweza kutengeneza sura ya Rais na kuivaa, hivyo sikuliweka wazi hili, lakini niliwaona na kila mmoja alikuwa mahala pake, bila kinyago cha usoni,” akawaeleza kisha akanyanyuka na kuiendea droo ndogo akatoa flash na kuipachika kwenye kompyuta mpakato, kisha akawasha chombo cha kutolea picha ukutani na dakika moja baadae picha zilianza kuonekana.

Pancho Panchilio, mfanyabiashara mkubwa nchini, mshawishi wa mambo mengi ya kisiasa, mwenye asili ya Kihindi, watu wengi walimjua kama si kwa jina basi kwa sura. Mhindi huyu alilindwa kwa jinsi zote, hagusiki. Alikuwa tajiri sana mwenye malori makubwa ya kusafirisha, aliwekeza kwenye sekta ya usafiri hasa sekta ya anga. Kwa ujumla alikuwa mwema mbele ya Watanzania, alitoa misaada mingi hapa na pale, alijenga mahospitali, mashule na kusaidia watoto yatima sehemu mbalimbali za nchi.
Picha ya pili nayo ilitia shaka kwa wote angu waliposoma katika lile jalada na sasa wakiona ushahdi ule wa Chiba kwa njia ya picha. Kigogo mkubwa serikalini, aliyepewa dhamana na Wasakatonge kisha anawazunguka na kuwafanyia mambo yasiyoelezeka kwa maandishi. Maisha yanakuwa magumu kila uchwao ilhali wengine wakitunisha matumbo yao kwa njia mbadala za unyonyaji na ukandamizaji.

Picha ya tatu nayo ilikuwa yaleyale, Kigogo mwingine kwenye wizara Fulani naye alikuwamo ndani ya jopo hilo la udhalimu.
Haikuishi hapo, Chiba kutoka katika Hard Disk aliyoichomoa katika ile kompyuta yao, alifumua majina mengine ya watu mbalimbali ambao kila mwezi huchukua mgawo wa pesa lukuki kwa mambo yao binafsi, wapo viongozi wa juu, wa kati na wa chini; si wanasiasa tu hata wafanyabiashara nao walikuwapo tena wengi.

“Inatosha!” Madam akamwambia Chiba, naye akazima ule mtambo wake.

“Sasa nataka operesheni ianze mara moja, taarifa tayari zipo panapohusika, lakini Pancho Panchilio akamatwe mara moja, pamoja na hawa vigogo wawili. Leo hii wanatakiwa kuwa pale kituo cha kati kwa mahojiano zaidi.
 
RIWAYA: KITISHO
MTUNZI: richard MWAMBE
-Man In The Mirror-

“Inatosha!” Madam akamwambia Chiba, naye akazima ule mtambo wake.
“Sasa nataka operesheni ianze mara moja, taarifa tayari zipo panapohusika, lakini Pancho Panchilio akamatwe mara moja, pamoja na hawa vigogo wawili. Leo hii wanatakiwa kuwa pale kituo cha kati kwa mahojiano zaidi.

SEHEMU YA 13

KATIKA JENGO NYETI LA SERIKALI
“Boss kuna mgeni anataka kukuona,” sauti nyororo ya Katibu Muhtas ilipenye kwenye sikio la Mheshimiwa Sikotu Sambwene, mmoja wa watu wazito na ‘vingunge’ katika Serikali.

“NIlikwambia sitaki kuonana na wageni au hukunielewa?” Sikotu akauliza kwa ukali, “Mwambie sina muda wa kuonana na watu sasa; aje mwezi ujao,” akaongeza kuongea kwa ukali uleule. Akiwa bado katika kumfokea huyo Katibu wake; mlango ulifunguliwa na Madam S akajitoma ndani mzima mzima na kusimama kando.

“Mgeni wako ni mimi,” akamwambia Mh. Sikotu. Mheshimiwa Yule alijkuta katika wakati mgumu, alijitupa kitini na kumtazama mwana mama huyo aliyeingia kibabe katika ofisi hiyo.

“We; nenda,” akamwambia Yule Katibu wa Mheshimiwa.

“Unafuata nini hapa?” Skotu akauliza.

“Sina jibu la kukwambia ninachokifuata, maana bila shaka unajua ninachokifuata kwako, nina swali moja tu ambalo ukinijibu shida yangu itakuwa imeisha,” Madam S aimwambia Sikotu huku akiwa kasimama mbali kwa tahadhari.
Mhesimiwa Sikotu akajifuta jasho ilhali mashine ya kupoza hewa iikuwa bize ikifanya kazi hiyo, akaweka kitambaa chake ndani ya koti lake na kumtazama mwanamama huyo aliyesimama mbele yake.

“Unasemaje?” akauliza.

“Unafahamu nini au kipi juu ya jumba kubwa la kifahari lililoko Kerege kitalu namba KG/BY 1230p?” akauliza Madam S. Sikotu akabaki kaduwaa, hakuwa na jibu. Madam S hata kabla hajapewa jibu hilo akatupa swali lingine.

“Unajua nini juu ya mwandishi wa habari mashuhuri aliyepotea miezi miwili nyuma?”

“Hivi we mwanamke una kichaa!” Sikotu akang’aka huku akiwa wima macho yamemtoka.

“Na ukichaa wangu ndio umenifikisha hapa leo, ulifikiri ukijiziba sura mbele yangu sintokujua? Kwa taarifa yako kutokana na kazi yangu, sauti zenu wote nyie nimezikariri, hukuweza kujificha mbele yangu ulipokuwa ukiongea, Sikotu, kiongozi mwenye dhamana, unajishusha hadhi kwa tamaa yako ya pesa mzee, utastahafu kwa fedheha baba, hebu jiangalie hapa,” Madam S akamtupia picha kumi na tano zinazomwonesha ndani ya jengo lile ambazo zilinaswa kwa kamera za usalama. Sikotu alizitupia jicho na machozi yakaanza kumtoka.

“Mwisho wa ubaya ni aibu, na mshahara wa dhambi mauti,” Madam S akainua akakusanya picha zake na kuzirudisha mkobani.

“Tutaonana mahakamani,” akageuka na kuondoka, akaufunga mlango nyuma yake na nukta hiyo hiyo vijana wawili waliovalia sare za jeshi la polisi waliingia ndani ya ofisi ile, pingu ikawekwa mezani.

“Siwezi kwenda popote, kwanza ni ninyi ni nani? Nani kawatuma? Ninyi mna kibali cha kunikamata mimi? Mnaitaka kazi yenu au?” Sikotu alikuwa kama akiweweseka, akavua koti na kulitupaa kando, mwili wote ulikuwa umelowa kwa jasho kana kwamba kamwagiwa maji.
Mmoja wa wale askari akatoa waraka ulioidhinishwa kukamatwa kwake, akamwonesha kwa mbali huku akimkatalia kuushika kwa mikono yake. Sikotu hakuwa na la kufanya aliahangaika, Yule askari kijana akamsogezea pigu ikiwa wazi ajipachike mikono yeye mwenyewe. Sikotu akavuta saraka katika meza yake akaitoa bastola iliyokuwamo ndani yake, wale askari wakaweka silaha zao tayari wakimwamuru kuweka chini bastola yake. Akaitumbukiza kinywani kwa minajiri ya kujilipua.

“Weweeee aaacchhhaaaaa!!!” mmoja wa askari akapiga kelele na wakati huo huo mlio wa risasi ulisikika na Mheshimiwa Sikotu akabwaga chini huku damu zikicafua vibaya shati lake, bastola yake ikitupwa mbali.

“Ha ha ha ha haujafa kiongozi lazima ufike mahakamani,” Sauti ya Chiba ilisikika nyuma ya wale askari, wakageuka na kumwona kijana huyo aliyekuwa ndani ya suti nadhifu akiiteremsha bastola yake. Chiba alipiga mkono wa Sikotu kwa risasi yake na kuumiza vibaya kiganja chake kabla hajajilipua.

WAKATI HUO HUO – ofisi nyingine ya serikali
“Una la kujitetea hapo?” Scoba na Gina walisimama mbele ya meza kubwa wakimtupia swali hilo mtu mkubwa mwenye tumbo la maana akilikuna kwa mbali. Alionekana wazi kuchanganyikiwa kwa hilo, hakuwa na la kujitetea.

“Gina, mtie pingu!” Scoba alitoa amri na Gina akaitekeleza. Gavana wa benki kuu ya Tanzania, Dkt. Shekibindu akavikwa pingu na kutolewa ofisini mpaka nje kwenye gari ya polisi, na moja kwa moja akapelekwa kituo cha kati kwa mahojiano zaidi.

WAKATI HAYO YOTE YAKITUKIA…
Kamanda Amata alisimama mikono yake akiwa kaikutanisha nyuma ikining’iniza bastola yake ndogo ya Kiitaliano ijulikanayo kama Beretta, huku usoni kajivika miwani safi nyeusi, suti yake ilimkaa vyema mwilini, kiatu chake kilichong’azwa kwa kiwi hakikuongopa kuonesha taswira ya kila kilichokaribu.

“Hajaonekana kabisa ofisini,” Msichana aliyeonekana kama Katibu wa Pancho Panchilio alimjibu Amata kwa swali aliloulizwa sekunde chache zilizopita.

“Tangu lini?” akauliza tena.

“Ana siku nne sasa, mara ya mwisho aliondoka hapa majuzi akiwa kama aliyechanganyikiwa, sikujua anakwenda wapi na wala hakusema, tangu hapo hakurudi tena,” Yule msichana akaendelea kueleza.

“Unapajua nyumbani kwake?”

“Hapana, mimi ni mfanyakazi tu huwa tunaonana hapa ofisini bas,” akajibu.

“Ok, naomba niingie ofisini kwake,” Kamanda akaomba.

“Pamefungwa, na funguo ni moja tu anayo mwenyewe,”

“We niruhusu au nikataze,” Kamanda akasisitiza.

“Sawa ingia, mi nakwambia hayupo,” Yule mwanadada
akaendelea kujibu.

“Usihofu, mimi ni afisa wa polisi,” akamwonesha kitambulisho bandia cha upolisi. Akauendea mlango na kuufungua kwa jinsi zake zilezile. Ilikuwa ofisi pana yenye kila kitu ndani yake, hakukuwa na mtu, akaiendea simu na kuitazma kisha akabonyeza kitufe cha kuiruhusu itoe ujumbe wowote uliopo.

“…Mheshimiwa booking yako imekamilika na tiketi yako tutakutumia soon katika email yako… enjoy your flight…”

Akili ya Kamanda ilisimama ghafla, “Katoroka!” akajikuta anajiuliza bila kupata jibu, akaiendea kompyuta ya mezani na kuipekua hapa na pale mpka alipopata email ya Panchilio ambayo ilikuwa wazi bila kufungwa akapekua e mail zilizoingia saa sabini na mbili zilizopita. Ilikuwa ni hiyo email ya tiketi ya ndege iliyoondoka saa arobaini zilizopita na ndege moja ya shirika la huko Uarabuni, safari yake ilionekana kuishia Bangalore, India.

“Hayawani huyu kaniwahi,” akawaza huku akitoka na nakala ya ile ytiketi aliyoitoa kwenye mashine kule ndani.

“Unaitwa nani?” akmwuliza Yule binti alipokuwa akitoka.

“Naitwa Ruth,”

“Mwenyeji wa wapi?” akamwuliza.

“Wa Arusha,” akajibu.

Kamanda Amata akamtupia jicho la wizi huku akiiondoa miwani yake usoni na kutuza muono wake juu ya kifua cha binti huyo kilichojaa vyema, matiti yaliyowekwa ndani ya sidiria yakitamanisha kila lijari. Kamanda akameza mate, akajikohoza, akaingiza mkono mfukoni na kutoa kadi ndogo ya kibiashara akampatia.

“Tuonane jioni ya leo, Hotel ya Land Mark, saa mbili kamili usiku,”

Ruth akamtupia jicho kijana huyo aliyekuwa akiipachika tena miwani usoni mwake, akaibetua midomo yake na kuuma chanda chake kwa meno ya mbele.

“Ok!” akaitikia. Kamanda Amata akauona mshtuko wa wazi mbele yake kutoka usoni mwa Yule dada, akageuka nyuma na ndipo alipogundua kuwa hawako peke yao, watu wawili walisimama nyuma yake, waliojazia kimazoezi. Akageuka na kupita katikati yao akaondoka na kuwaacha. Alipolifikia gari lake akasimama na kugeuka nyuma, akawaona wale vijana wamesimama mlangoni wakimwangalia. Akasimamisha tax na kuondoka huku akiliacha gari lake palepale.

HATIMA

“Pancho Panchilio ametoroka,” kamanda alimwambia Madam S walipokutana katika mgahawa wa Steers.

“Atapatikana tu, na lazima tumpate iwe kwa mvua iwe kwa jua,” Madam akajibu.

GEREZA LA UKONGA saa tatu baadae
“Mmefurahi sasa sio? Maana rafiki zenu wamekuja kuungana nanyi, msijali tunamleta na Yule Gabacholi, tunamfuata hukohuko India,” Madam S akamwambia Kanayo na Mahmoud Zebaki waliokuwa wakitumikia kifungo chao.

“Tunakata rufaa!” Kanayo akajibu.

“Kateni tu kwani nimewafunga kamba, hiyo ni haki yenu kimsingi na kikatiba,” Madam S aliwajibu huku akinyanyuka na kuondoka.
Kanayo akasonya kwa gadhabu, “Our day will come!”(Siku yetu inakuja) akamwambia Madam S. akageuka kumtazama Kanayo O Kanayo, “Yes, will come soon, we shall face each other in the battle field,” (ndiyo inakuja punde tu, tutaonana kwenye uwanja wa mapambano)

§§§§§
Aiwa chumbani kwake, alimtazama Gina aliyekuwa mbele yake na vazi jepesi la usiku, Amata alijikuta akipata shida maeneo ya kati kwajinsi mwili wa mrembo huyo ulivyokuwa ukiita. Gina akageuka na kumtazama.

“Vipi? Arts of War ni ipi kwa mi na wewe sasa?” alimuuliza huku akijilaza ktandani na kuruhusu sehemu kubwa ya mwili wake kujiachia wazi.

“…mwili huo uliookotwa kando kando ya pwani ya Coco ni wa msichana wa kati ya miaka 25 na 30. Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es salaam Ndugu Sekuru, amethibitisha kutokea tukio hilo na uchunguzi unaendelea kuwabaini waliofanya mauaji hayo…”
Sauti ya Mtangazaji wa TV ilimtoa Kamanda Amata katika kifua cha Gina na kutupia macho katika kioo hicho.

“Shittt!” akang’aka, “Wamemuua Ruth!” akaongeza huku akisimama.

“Ndio tatizo lako, ukisikia mwanamke kauawa unahuzunika lakini mwanume unapotezea, mwanaume Malaya wewe!” Gina akalalamika huku akikaa kitandani.

“Gina, huyu ni sekretari wa Pancho Panchilio,” akamweleza.

“What? Usinambie,” Gina naye akahamanika.

“Kwa nini wamemuua msichana mzuri kama Yule, masikini Ruth!”

MWISHO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom