Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,821
- 6,122
GOBA DRC:
Hali ya hewa ilikuwa metulia,si ndege wa usiku au wadudu waliokuwa wakisikika,haijulikani kwanini kulikuwa na hali Kama hiyo usiku mnene namna ile ambao ni lazima kuzisikia sauti zao hasa kwenye msitu mkubwa kama ule,.
Utulivu ule uliondoshwa muda mfupi baadae pale ambapo ilitokea helkopita ya kijeshi na kuganda juu ya anga la eneo hili la Monigi pembeni kidogo ya mji wa Goba,.
Helkopita ile ilikuwa imebeba wanajeshi wapatao watano,huku mmoja miongoni mwao alieonekana kuwa kiongozi aliwasihi vijana wake washuke kwa kutumia kamba.
Alianza wa kwanza,wa pili...walipendeza katika ushukaji wao,ilionesha ni wazoefu katika fani hiyo,na haikuwa na Shaka wote walikuwa ni makomando katika kikosi flani cha jeshi,
Wapili alivyofika chini tayari watatu na wanne nao walikuwa wapo kwenye kamba wanateremka huku silaha zao za kivita zikiwa tayari mikononi mwao,kwa lolote huku wale waliotangulia kushuka wakihakikisha usalama wa wenzao washukao,.Walitua chini kwa kishindo kidogo kisha mmoja akatikisa kamba kuashiria tayari wametua salama,.
Kapten Shayo aliona mtikisiko ule wa kamba alijua ni nini maana yake nae akaamuru rubani wa helkopta ile ya kijeshi iuache salama msitu wa Monig,wakati rubani akiigeuza helkpita ile,kepten Shayo yeye alikuwa anatafuta mawasiliano na upande mwingine anaojua kisha bila kusikiwa na rubani yule alisema maneno machache tu kwa upande wa pili "Wameshuka salama" kisha bila kungoja akaweka pembeni kifaa kile na kutulia kimya.
Msitu ule uliwalaki kwa utulivu wa hali ya juu,hakuna walichosikia zaidi ya hatua zao wenyew,huku kwa mbali wakisikia sauti za vibuyu vyao vya maji walivyufunga viunoni mwao,.hawakutaka kuhadaika na ukimya ule wa msitu,walitembea kiuangalifu huku wakiwekeana ulinzi wao kwa wao,
Mmoja akiwa mbele alitoa ishara kwa wenzie kwa kukunja ngumi kisha kunyoosha mkono juu,wenzie walipoona hivyo wakajiweka tayari maana hiyo ilikuwa ni ishara ya kuwataarifu kuwa kuna jambo mbele yao na wanapaswa kutulia kimya nao wakatii na kusimama,.
Kama ungeliwaona katikati ya kiza kile ungelidhani ni kichaka kidogo kilichokatikati ya miti mirefu iliotosha kutengeneza msitu ule mkubwa,
Wakiwa katika utulivu wao walihisi kama mvumo wa kitu mita kadhaa mbele yao,na hapo tena yule aliekuwa mbele akatoa ishara ya kusambaza vidole vyake viwili mara tatu kisha bila kusubiri na kwa wepesi wa karatasi akaruka upande wa pili kuliko kuwa na majani marefu,wakati yeye akifanya hivyo wenzie nao wakachumpa na kuangukia upande tofauti kila mmoja huku wakiiacha njia ikiwa nyeupe kama vile hakukua na watu waliokuwa wakiipita dakika kadhaa nyuma.
Wakiwa wapo makini kufuatilia mvumo ule wa sauti nao ukakaribia zaidi punde ikatokea gari aina ya jeep yenye kubeba watu wawili ndani na dereva,iliwapita wanajeshi wale wakiwa wametulia kwenye maficho yao,.
Wakiwa bado wametulia ili kuthibitisha usalama kabla ya kuendelea na safari,wakasikia tena sauti zikijia njia hiyo hiyo ilikotokea ile jeep, Mara hii haikuwa gari ila ilikuwa ni watu waliokuwa wakipita pale kwa miguu,miongoni mwa watu wale ambao kwa idadi walikuwa saba wawili walikuwa wamefungwa kamba miguuni na mikononi huku waliosalia walikuwa wamebeba bunduki mikononi mwao na walionesha wako makini kwa kila hatua waliopiga mateka wao,haikueleweka watu wale walitekwa kwanini na kwanini walikuwa wakisafirishwa usiku ule na walikuwa wakipelekwa wapi nao ni kinanini? Ni maswali ambayo walijiuliza wanajeshi wale bila majibu.
Baada ya dakika zipatazo kama kumi hivi masikio ya makomando wale yalipata uhai na hii ni kulingana na vifaa vya mawasiliano vilivyofungwa masikioni mwao ili waweze kuwasiliana bila kutoa sauti ilianza kwa mmoja kusikia akiitwa,
Code 01" mwenye utambulisho wa namba hiyo akaitika "clear"
"Z4"
"clear"
G2"
"clear"
Basi alipokwisha kuwaita wenzie akatoa kauli moja kwa wote "let's go" nao pale walipokuwa wakanyanyuka na kurudi njiani huku usimamji wao ukiwa ni wa tahadhari zaidi kila mmoja akijaribi kutazama ndani ya kiza kile,kuhakikisha usalama wake na wawenzie.
Walipokwisha kuungana wote wakaanza tena Safari yao huku wakiwa kimya kila mmoja,mitutu ya bunduki ikitizama mbele na mitutu mingine ikitizama nyuma,kisha yule kiongozi wao akanyoosha mkono juu wote wakasimama napo akawaelekeza kwa ishara ya kidole kimoja kuelekea mbele na hapo wakaihama njia na kuanza kutembea msituni.Ilikuwa ni mwendo wa nusu saa hadi kufika kwenye eneo la Rukoko mji ambao wakazi wake walishahama,hapo makomando wale wanne wakapokewa na utulivu wa kutisha,hawakujali na hapo wakajadili jambo kidogo kisha alieitika kwa codename Z4 akatoa ramani na kwa kusaidiwa penlight akawaonesha wenzie ni wapi walipo na hapo ikasikika sauti kutoka kwa G2 sauti ilioongea kiswahili safi kabisa akawashauri wenzie "badala ya kwenda na njia hii itakayo tufikisha Kibati,sisi tupite upande huu wa magharibi ili tutokee kwenye eneo husika,kisha tukifanikiwa hapo tutatokea huku na kwenda kutokea buhimba."
Hakukua na maelezo zaidi ya kutekeleza wazo na hapo wakaamua kuanza safari ya kukatiza katikati ya msitu wa Rukoko ili wawahi kufika nyiragongo sehemu watakayoenda kukamilisha mpango wao,
Iliwachukua dakika araobaino na tano kuikaribia ngome hiyo ya waasi wa AGFT(Against Government we make Future Tommorow),walizidi kuikaribia ngome ile inayolindwa na waasi wenye mafunzo ya hali ya juu,makomando wale walisimama baada ya kufika karibu kabisa na eneo hilo la kambi ya Nyiragongo,Z4 na G2 wakachukua jukumu la kubaki nyuma ya wenzao wawili ambao wao waliamua kuingia kambini humo kwa kupitia nyuma ambako kwa uelewa wao huko ndiko hakukua na ulinzi mkali,
01 na yule kiongozi ambae namba yake ya utambulisho ni K3 walisonga kwenda kulifuata lango la nyuma ya kambi ile,iliwabidi watambae ili kukwepa taa za ulinzi zisiwamulike,Z4 na G2 wao walikuwa wakifuata kila hatu ya 01 na K3 kwa kutumia lens za sniper rifle walizokuwa wamebeba mikononi mwao ili kuhakikisha mpango wao unakamilika kabla ya saa kumi usiku....
DAR ES LAAM saa nane na nusu usiku.
Kikao kiliendelea huku kila aliehudhuria kikao kile akiwa amekwisha kuchangia hoja yake,huku sasa ikiwa imebaki hitimisho la kiongozi wa kikao kile macho ya wanakikao kile yakiwa kwake alitingishika kidogo kisha akajikohoza na hatua kwa hatua aliwatupia jicho wajumbe wake na hapo sauti ikamtoka
"hakuna namna kepten shayo lazima afe na rubani wake leutanant Koba,maana hawa hawajui chochote kinachoendelea,ila inaweza kuja kuleta shida wakibaki hai na wakajua walitumika kinyume cha kazi yao" hapo akanyamaza kisha kama mwanzo aliendelea kuwatizama wajumbe wake,aliporidhika na utulivu wao akaendelea
"vijana hao walioenda Goba na imani watakamilisha huo mpango ila kabla ya kesho jioni nao wawe wamekwisha kuondolewa duniani na atakae waondoa taarifa anayo tayari"
Wajumbe wengine wakasimama na na kupiga salute kwa kiongozi huyo kisha wakaanza kutoka chumbani humo na kila mmoja alkielekea anakokujua..
Helkopita iliombeba kepten Shayo na Lieutenant Koba iliendelea kuyakata mawimbi na sasa ilikuwa inaikaribia kambi yao kijeshi ilioko mkoani humo na kwa maelezo ya wakuu wao ilipaswa helkopita hiyo kutua hapo,Kisha wao watapewa usafiri wa gari ili kuwarudisha morogoro ilipo kambi yao ya kuripoti kazini,
Walitua salama na bila kuchelewa wakapikiwa ndani ya gari Safari ya kutoka Kigoma kwenda morogoro ikaanza,ndani ya gari hakuna aliemsemesha mwenzie huku kichwa cha Kepten Shayo kikiwa na mawazo lukuki kuhusu mpango huo asioulewa na vijana wake kawaacha huko Goba,
Kukiwa kunakaribia kukuchwa tayari wao walikuwa wamekwisha iacha tabora wameikanyaga singida,na walikuwa katikati ya pori la Chaya kilometa chache kabla hujaifikia Manyoni na hapo si dereva au leutanant,aliegundua kitu isipokuwa kepten Shayo alieona mtu alievalia kijeshi huku akiwa na kiona mbali,akiwatizama wakati bado akifikiria hilo dereva wa gari lao akapiga ukulele mdogo na kisha kuulalia usukani huku gari likikosa mwelekeo na likiongeza kasi,
Si leutanant Koba au Kepten Shayo aliefanikiwa kutoka ndani yake gari likapaa juu na kushuka chini kwa kasi kisha kujipigiza chini huku moto ukiwaka juu yake na injini ya gari lile aina ya Ashok ikizimika,akiwa anaona kwa mbali kepten Shayo aliona wanajeshi wawili wakiwa na silaha wakilifuata gari lao na hapo hakushuhudia tena zaidi ya kusikia milio ya risasi ikiliendea gari lao linaloteketea kwa moto huku Leutaenant Koba akiwa mbali na dunia hii...
Hali ya hewa ilikuwa metulia,si ndege wa usiku au wadudu waliokuwa wakisikika,haijulikani kwanini kulikuwa na hali Kama hiyo usiku mnene namna ile ambao ni lazima kuzisikia sauti zao hasa kwenye msitu mkubwa kama ule,.
Utulivu ule uliondoshwa muda mfupi baadae pale ambapo ilitokea helkopita ya kijeshi na kuganda juu ya anga la eneo hili la Monigi pembeni kidogo ya mji wa Goba,.
Helkopita ile ilikuwa imebeba wanajeshi wapatao watano,huku mmoja miongoni mwao alieonekana kuwa kiongozi aliwasihi vijana wake washuke kwa kutumia kamba.
Alianza wa kwanza,wa pili...walipendeza katika ushukaji wao,ilionesha ni wazoefu katika fani hiyo,na haikuwa na Shaka wote walikuwa ni makomando katika kikosi flani cha jeshi,
Wapili alivyofika chini tayari watatu na wanne nao walikuwa wapo kwenye kamba wanateremka huku silaha zao za kivita zikiwa tayari mikononi mwao,kwa lolote huku wale waliotangulia kushuka wakihakikisha usalama wa wenzao washukao,.Walitua chini kwa kishindo kidogo kisha mmoja akatikisa kamba kuashiria tayari wametua salama,.
Kapten Shayo aliona mtikisiko ule wa kamba alijua ni nini maana yake nae akaamuru rubani wa helkopta ile ya kijeshi iuache salama msitu wa Monig,wakati rubani akiigeuza helkpita ile,kepten Shayo yeye alikuwa anatafuta mawasiliano na upande mwingine anaojua kisha bila kusikiwa na rubani yule alisema maneno machache tu kwa upande wa pili "Wameshuka salama" kisha bila kungoja akaweka pembeni kifaa kile na kutulia kimya.
Msitu ule uliwalaki kwa utulivu wa hali ya juu,hakuna walichosikia zaidi ya hatua zao wenyew,huku kwa mbali wakisikia sauti za vibuyu vyao vya maji walivyufunga viunoni mwao,.hawakutaka kuhadaika na ukimya ule wa msitu,walitembea kiuangalifu huku wakiwekeana ulinzi wao kwa wao,
Mmoja akiwa mbele alitoa ishara kwa wenzie kwa kukunja ngumi kisha kunyoosha mkono juu,wenzie walipoona hivyo wakajiweka tayari maana hiyo ilikuwa ni ishara ya kuwataarifu kuwa kuna jambo mbele yao na wanapaswa kutulia kimya nao wakatii na kusimama,.
Kama ungeliwaona katikati ya kiza kile ungelidhani ni kichaka kidogo kilichokatikati ya miti mirefu iliotosha kutengeneza msitu ule mkubwa,
Wakiwa katika utulivu wao walihisi kama mvumo wa kitu mita kadhaa mbele yao,na hapo tena yule aliekuwa mbele akatoa ishara ya kusambaza vidole vyake viwili mara tatu kisha bila kusubiri na kwa wepesi wa karatasi akaruka upande wa pili kuliko kuwa na majani marefu,wakati yeye akifanya hivyo wenzie nao wakachumpa na kuangukia upande tofauti kila mmoja huku wakiiacha njia ikiwa nyeupe kama vile hakukua na watu waliokuwa wakiipita dakika kadhaa nyuma.
Wakiwa wapo makini kufuatilia mvumo ule wa sauti nao ukakaribia zaidi punde ikatokea gari aina ya jeep yenye kubeba watu wawili ndani na dereva,iliwapita wanajeshi wale wakiwa wametulia kwenye maficho yao,.
Wakiwa bado wametulia ili kuthibitisha usalama kabla ya kuendelea na safari,wakasikia tena sauti zikijia njia hiyo hiyo ilikotokea ile jeep, Mara hii haikuwa gari ila ilikuwa ni watu waliokuwa wakipita pale kwa miguu,miongoni mwa watu wale ambao kwa idadi walikuwa saba wawili walikuwa wamefungwa kamba miguuni na mikononi huku waliosalia walikuwa wamebeba bunduki mikononi mwao na walionesha wako makini kwa kila hatua waliopiga mateka wao,haikueleweka watu wale walitekwa kwanini na kwanini walikuwa wakisafirishwa usiku ule na walikuwa wakipelekwa wapi nao ni kinanini? Ni maswali ambayo walijiuliza wanajeshi wale bila majibu.
Baada ya dakika zipatazo kama kumi hivi masikio ya makomando wale yalipata uhai na hii ni kulingana na vifaa vya mawasiliano vilivyofungwa masikioni mwao ili waweze kuwasiliana bila kutoa sauti ilianza kwa mmoja kusikia akiitwa,
Code 01" mwenye utambulisho wa namba hiyo akaitika "clear"
"Z4"
"clear"
G2"
"clear"
Basi alipokwisha kuwaita wenzie akatoa kauli moja kwa wote "let's go" nao pale walipokuwa wakanyanyuka na kurudi njiani huku usimamji wao ukiwa ni wa tahadhari zaidi kila mmoja akijaribi kutazama ndani ya kiza kile,kuhakikisha usalama wake na wawenzie.
Walipokwisha kuungana wote wakaanza tena Safari yao huku wakiwa kimya kila mmoja,mitutu ya bunduki ikitizama mbele na mitutu mingine ikitizama nyuma,kisha yule kiongozi wao akanyoosha mkono juu wote wakasimama napo akawaelekeza kwa ishara ya kidole kimoja kuelekea mbele na hapo wakaihama njia na kuanza kutembea msituni.Ilikuwa ni mwendo wa nusu saa hadi kufika kwenye eneo la Rukoko mji ambao wakazi wake walishahama,hapo makomando wale wanne wakapokewa na utulivu wa kutisha,hawakujali na hapo wakajadili jambo kidogo kisha alieitika kwa codename Z4 akatoa ramani na kwa kusaidiwa penlight akawaonesha wenzie ni wapi walipo na hapo ikasikika sauti kutoka kwa G2 sauti ilioongea kiswahili safi kabisa akawashauri wenzie "badala ya kwenda na njia hii itakayo tufikisha Kibati,sisi tupite upande huu wa magharibi ili tutokee kwenye eneo husika,kisha tukifanikiwa hapo tutatokea huku na kwenda kutokea buhimba."
Hakukua na maelezo zaidi ya kutekeleza wazo na hapo wakaamua kuanza safari ya kukatiza katikati ya msitu wa Rukoko ili wawahi kufika nyiragongo sehemu watakayoenda kukamilisha mpango wao,
Iliwachukua dakika araobaino na tano kuikaribia ngome hiyo ya waasi wa AGFT(Against Government we make Future Tommorow),walizidi kuikaribia ngome ile inayolindwa na waasi wenye mafunzo ya hali ya juu,makomando wale walisimama baada ya kufika karibu kabisa na eneo hilo la kambi ya Nyiragongo,Z4 na G2 wakachukua jukumu la kubaki nyuma ya wenzao wawili ambao wao waliamua kuingia kambini humo kwa kupitia nyuma ambako kwa uelewa wao huko ndiko hakukua na ulinzi mkali,
01 na yule kiongozi ambae namba yake ya utambulisho ni K3 walisonga kwenda kulifuata lango la nyuma ya kambi ile,iliwabidi watambae ili kukwepa taa za ulinzi zisiwamulike,Z4 na G2 wao walikuwa wakifuata kila hatu ya 01 na K3 kwa kutumia lens za sniper rifle walizokuwa wamebeba mikononi mwao ili kuhakikisha mpango wao unakamilika kabla ya saa kumi usiku....
DAR ES LAAM saa nane na nusu usiku.
Kikao kiliendelea huku kila aliehudhuria kikao kile akiwa amekwisha kuchangia hoja yake,huku sasa ikiwa imebaki hitimisho la kiongozi wa kikao kile macho ya wanakikao kile yakiwa kwake alitingishika kidogo kisha akajikohoza na hatua kwa hatua aliwatupia jicho wajumbe wake na hapo sauti ikamtoka
"hakuna namna kepten shayo lazima afe na rubani wake leutanant Koba,maana hawa hawajui chochote kinachoendelea,ila inaweza kuja kuleta shida wakibaki hai na wakajua walitumika kinyume cha kazi yao" hapo akanyamaza kisha kama mwanzo aliendelea kuwatizama wajumbe wake,aliporidhika na utulivu wao akaendelea
"vijana hao walioenda Goba na imani watakamilisha huo mpango ila kabla ya kesho jioni nao wawe wamekwisha kuondolewa duniani na atakae waondoa taarifa anayo tayari"
Wajumbe wengine wakasimama na na kupiga salute kwa kiongozi huyo kisha wakaanza kutoka chumbani humo na kila mmoja alkielekea anakokujua..
Helkopita iliombeba kepten Shayo na Lieutenant Koba iliendelea kuyakata mawimbi na sasa ilikuwa inaikaribia kambi yao kijeshi ilioko mkoani humo na kwa maelezo ya wakuu wao ilipaswa helkopita hiyo kutua hapo,Kisha wao watapewa usafiri wa gari ili kuwarudisha morogoro ilipo kambi yao ya kuripoti kazini,
Walitua salama na bila kuchelewa wakapikiwa ndani ya gari Safari ya kutoka Kigoma kwenda morogoro ikaanza,ndani ya gari hakuna aliemsemesha mwenzie huku kichwa cha Kepten Shayo kikiwa na mawazo lukuki kuhusu mpango huo asioulewa na vijana wake kawaacha huko Goba,
Kukiwa kunakaribia kukuchwa tayari wao walikuwa wamekwisha iacha tabora wameikanyaga singida,na walikuwa katikati ya pori la Chaya kilometa chache kabla hujaifikia Manyoni na hapo si dereva au leutanant,aliegundua kitu isipokuwa kepten Shayo alieona mtu alievalia kijeshi huku akiwa na kiona mbali,akiwatizama wakati bado akifikiria hilo dereva wa gari lao akapiga ukulele mdogo na kisha kuulalia usukani huku gari likikosa mwelekeo na likiongeza kasi,
Si leutanant Koba au Kepten Shayo aliefanikiwa kutoka ndani yake gari likapaa juu na kushuka chini kwa kasi kisha kujipigiza chini huku moto ukiwaka juu yake na injini ya gari lile aina ya Ashok ikizimika,akiwa anaona kwa mbali kepten Shayo aliona wanajeshi wawili wakiwa na silaha wakilifuata gari lao na hapo hakushuhudia tena zaidi ya kusikia milio ya risasi ikiliendea gari lao linaloteketea kwa moto huku Leutaenant Koba akiwa mbali na dunia hii...
