josephdeo
Member
- Nov 23, 2015
- 95
- 196
JICHO LA SANAAA
MATAA HEIST
Based on true event
"Wakati adui anahitaji nafasi moja katika kutekeleza mipango yake ya kidhalimu, vyombo vya usalama na ulinzi vinahitaji kila nafasi, kila fursa, kila sekunde, kila dakika, kila saa, kila siku na kila wiki ili kuhakikisha wanamzuia adui huyo kutekeleza azima yake".
Ilikuwa ni Alhamisi ya tarehe 20 April 2020, katika jiji la Mwanza. Siku ilianza vizuri kwani hakukuwa na dalili yoyote ya mvua. Katika miezi hii ambayo iliitwa miezi ya masika. Mvua ni kikwazo kikubwa hasa hasa kwa wakazi wa mijini kwani huwa inakwamisha shughuli nyingi za kuingiza kipato. Kwa siku hii katika jiji hili hali hiyo haikuwepo. Kama mamlaka za hali ya hewa zilivyotoa maelekezo yake siku moja kabla ya alhamisi hii kuwa kutakuwa na jua na mawingu kiasi ndivyo ilivyokuwa.
Jua kama kawaida yake lilianza kuchomoza saa kumi na mbili na dakika arobaini kwa madaha na mwendo wa taratibu. Shughuli za kusukuma gurudumu la maendeleo ya nchi yetu zilikuwa tayari zimekwisha kuanza.
Kila kona na sekta watu walikuwa wakikimbizana na hali ya uchumi wa kati ambao taifa letu liliingia siku chache nyuma.
Asbuhi hiyo katika benki ya NMB linayopatikana katika barabara ya Kenyata huku pia ikiwa makao ya makuu ya benki hiyo kanda ya ziwa. Kulikuwa na shughuli za kila siku zikiendelea lakini siku hii kulikuwa na shughuli ya ziada, shughuli hiyo ilikuwa ni kuhamisha kiasi cha billioni nne Tanzania shilingi kuzipeleka katika tawi la NMB Igoma.
Usafirishwaji huo ulikuwa ni ushafirishaji wa kwanza kufanywa na matawi yanayopatikana jijini hapa. Msafara wa fedha mara zote ulifanywa na benki kuu ya Tanzania. Lakini ilikuwa tofauti na siku hii ambapo tawi lilipewa ruhusa kufanya usafirishaji wa fedha.
Majira ya saa mbili kamili msafara wa gari mbili aina ya Landcruser zilizokuwa na usajili wa SU35490 iliyokuwa ikiendeshwa na Joshua Samweli na SU37200 iliyokuwa ikiendeshwa na Malima Mwenda zilianza kutoka pale. Ndani ya kila gari kulikuwa na askari wawili pia kulikuwa na wafanyakazi wa NMB Kenyata road.
Msafara huo Ulianza kutoka katika benki hiyo na kushika barabara ya Kenyata na kisha kuingia katika mzunguko wa Makongoro Avenue. Walipoumaliza mzunguko ule wakachukua uelekeo wa barabara ya Nyerere. Zilipofika makutano ya mataa ambapo makutano hayo yanaziunganisha barabara za Nyerere, station na Nkuruma zilikutana na kizuizi cha taa za barabarani. Iliwabidi kusimama kama sheria za barabarani zilivyotaka. Hilo likawa kosa kubwa sana kwa gari zile kwani majambazi wakiwa na siraha za kivita SMG, LMG, AK 47 na SHOTGUN yalivamia msafara wa magari hayo yaliyokuwa yakisindikiza pesa Kutoka NMB Kenyata road kupeleka NMB IGOMA BRANCH.
******
Kabla ya tukio gari moja aina ya Corolla ilipaki kituo cha mafuta cha TOTAL kilichopo mtaa wa Kemondo huku kikitazamana na jengo la benki kuu la zamani, kisha ikafata pickup na kupaki nyuma yake. Hakuna ambaye angeweza kubashiri kama magari yale yangeleta hatari kubwa sana masaa machache mbele. Kila mmoja alifuata kilichomleta mjini na kuacha kuchukua tahadhali yoyote juu ya gari zile kwani kulikuwa na gari nyingi ambazo ziliegesha maeneo mbalimbali bila kuwa na sababu yoyote ile.
Barabara ya Station nayo pia kulikuwa na pikipiki kubwa iliyoegesha huku dereva wake akiwa kakaa mita chache kutoka kwenye pikipiki hiyo. Alikuwa kajidhatiti kiasi cha kutia shaka lakini hakuna aliyemjali kwani kila mmoja alikuwa akishughulika na kilichomleta mjini. Wakati wote dereva huyo wa pikipiki alikuwa akifanya mawasiliano huku hakiwa na hali ya mashaka lakini kwa sababu watu walikuwa bize hakuna aliyelijali hilo.
Msafara wa gari zile zilizobeba fedha ulipofika kwenye mzunguko wa Makongoro Avenue ndipo gari ile aina ya Corola ilianza kutangulia mbele na zilipopita gari za benki ndipo pickup ile nayo ilizifuata kwa nyuma. Huku dereva wa piki piki akiiwasha pikipiki yake na kuiacha ikiunguruma huku yeye akiwa juu yake.
Wale jamaa waliokuwa kwenye gari la mbele la corola walipofika kwenye makutano ya mataa na taa za barabarani zilipozuia magari yanayotokea barabara ya Nyerere kutokea kwenye mzunguko wa Makongoro Avenue. Ndipo walipoanza kuinyeshea risari gari ya mbele SU35490 hadi likakosa uelekeao na kwenda kuigonga kwa nyuma gari ya BENZ T560 DCU. Gari ya nyuma kwenye msafara SU 37200 baada ya kuona hayo ikataka kuchepuka uelekeo wa barabara ya stesheni. Hii ikawa kosa kubwa sana kwani yule aliyekuwa juu ya pikipiki aliipiga risasi nyingi sana kuliko hata ile ya kwanza hali iliyomfanya dereva kukosa uhimili wa gari na kwenda kujikita kwenye taa za barabarani.
Kila gari ilikuwa imebeba pesa kiasi cha Bilioni 2 Tanzania shilingi.
Majambazi waliokuwa kwenye pickup walishuka kwa kasi huku wakirusha risasi hewani na kusababisha wananchi kuhamaki na kushikwa na bumbuwazi wasijue kipi cha kufanya wakalisogelea na kuanza kupakua makasha ya fedha kwenye gari ya nyuma na wale wa kwenye corola nao walianza kupakua kwenye gari ya mbele na kumuacha yule wa kwenye pikipiki hakihakikisha usalama.
Wakati upakuaji unaendelea jambazi aliyekuwa akilinda usalama alionekana ana usongo sana alikuwa anazidi kupiga risasi hali iliyowafanya watu wayaache magari na kuanza kutafuta maeneo ya kujificha. Kila mmoja alikuwa akikumbushia ni kwa kiasi gani miguu yake bado ina uimara wa kuhimili mbio zisizokuwa na mshindani. Askari waongoza magari waliokuwa zamu asbuhi hiyo walibaki na mshangao kwani tukio lile lilikuwa la kushitukiza na watekelezaji walikuwa wameliratibu vyema. Hata wao pia waliwaza wanawezaje kutoka eneo hilo ambalo liligeuka kiwanja cha kivita ndani ya mda mfupi.
Katika Maaskari walikuwepo eneo la tukio, kuna mmoja aliitwa Sajenti Adam Mashimbi. Naye alikuwa kwenye mshangao sana juu ya hali ile ya ghafla katika nchi iliyojaa amani. Kwa weledi na alivyoipenda kazi yake hakuridhika kuaibishwa namna ile. Askari huyu alikimbia kwenye kituo kidogo cha polisi pale PAMBA akatoa taarifa juu ya tukio kisha akachukua SMG na kurudi tukioni akawakuta majambazi wanamalizia kushusha pesa na wanaondoka.
Afande Adam akaanza naye kuwarushia risasi majambazi huku kila mara akijikinga ndani ya mtaro wa maji machafu na kufanya nguo zake nyeupe zisitamanike kwa uchafu. Alifanikiwa kuwapotezea muda majambazi wale lakini walifanikiwa kuondoka.
Hadi majambazi wanaondoka eneo la tukio tayari yalikuwa wamemuua askari mmoja D3866 PC Mwita Jonas kutoka kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) cha jijini Mwanza na mfanyakazi wa NMB NSSF plaza Agnes Solomoni. Wote hawa walikuwa kwenye ile gari ya nyuma iliyotaka kuchepuka kuingia barabara ya stesheni. Askari wengine watatu walijeruhiwa.
Umakini, umahiri katika kurusha risasi na pia jinsi walivyoondoka eneo la tukio ndio sababu kubwa ya mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio kuamini kuwa wale hawakuwa majambazi wa kawaida bali ni askari au watu wenye mafunzo makubwa na pia lazima walifanya majaribio kadhaa kabla ya tukio wakiwa na mipango yote A na B mpaka C ikiwa ingehitajika.
Mara baada ya kuzipata pesa majambazi wale walijigawa pale pale. Yule wa kwenye pikipiki alitoka eneo la tukio na kwenda mpaka Isamilo. Wengine waliondoka na magari yao kwa kutumia barabara ya Nyerere na kwenda kizitelekeza Kisesa mitaa ya Kanyama. Baada ya hapo walijigawa ili kuipoteza helicopter ya polisi iliyokuwa ikiwafuatilia huku wakiyateketeza magari waliyokuwa nayo kuondoa ushahidi.
Wawili kati yao walipitia njia ya Nyamongoro na kuishika Buswelu na baada ya hapo walipitia Kiseke na kuja kuishika Sabasaba na baadae kwenda Airport. Wawili wengine walipitia Nyamongoro ya chini ambapo kuna viwanja vya nanenane na kisha kuishika kishiri na baadae mahina na hapo wakaja mpaka bendera tatu na kuitafuta Bugarika na kisha Bugando wakaishia hapo.
Tukio lile lilikuwa limetekelezwa na watu walikuwa mahili sana kwani mita chache kutoka pale kulikuwa na ofisi za usalama wa taifa kanda ya Nyamagana. Pia mita chache kulikuwa na kituo cha kati cha polisi pia mita chache kulikuwa na kituo kidogo cha polisi Pamba. Achana na utitiri wa benki ambazo zote zilikuwa zikilindwa na askari wenye silaha za moto. Lakini bado wavamizi wale walifanikiwa kuondoka tena wakiwa sio peke yao bali na lundo la fedha.
*******
Wakati haya yote yanatokea aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Deusi Kalumuna alikuwa njiani safarini kwenda Shinyanga na taarifa hizi zilipomfikia aligeuza gari haraka sana kurudi eneo la tukio ambapo alipofika hakuamini kama mkoa wake unaweza kuwa na majambazi wa aina hiyo. Mshango ulikuwa dhahiri katika sura yake hakuamini kuwa tukio la namna hiyo linaweza kutokea katikati ya mji tena sehemu ambayo ina kituo kikubwa cha polisi mkoa na watekelezaji wakaondoka pasipo kufahamika walipitia wapi?.
Mara moja kamada Deusi aliamuru vikosi vyote vilivyo chini ya jeshi la polisi viingie kazini ili kuwatafuta majambazi hao kwani waliamini bado wapo jijini hapo. Pia waliimarisha ulinzi njia zote ambazo zilikuwa zinatoka nje ya jiji hili kwa maji, anga na barabara. Bahati mbaya hawakuwa na pa kuanzia zaidi ya kuwa na majeruhi wasioweza kujitambua baada ya kushambuliwa kwa risasi.
INAENDELEA
Muandishi:- Joseph .D. Migini
Call/txt:- +255766604683
Josephdeo70@gmail.com
Kwa maoni na ushauri nifuate kwenye mitandao ya kijamii kama:-
Fb:- josephdeo
Insta:- falsafa70
Twitter:- falsafa70
MATAA HEIST
Based on true event
"Wakati adui anahitaji nafasi moja katika kutekeleza mipango yake ya kidhalimu, vyombo vya usalama na ulinzi vinahitaji kila nafasi, kila fursa, kila sekunde, kila dakika, kila saa, kila siku na kila wiki ili kuhakikisha wanamzuia adui huyo kutekeleza azima yake".
Ilikuwa ni Alhamisi ya tarehe 20 April 2020, katika jiji la Mwanza. Siku ilianza vizuri kwani hakukuwa na dalili yoyote ya mvua. Katika miezi hii ambayo iliitwa miezi ya masika. Mvua ni kikwazo kikubwa hasa hasa kwa wakazi wa mijini kwani huwa inakwamisha shughuli nyingi za kuingiza kipato. Kwa siku hii katika jiji hili hali hiyo haikuwepo. Kama mamlaka za hali ya hewa zilivyotoa maelekezo yake siku moja kabla ya alhamisi hii kuwa kutakuwa na jua na mawingu kiasi ndivyo ilivyokuwa.
Jua kama kawaida yake lilianza kuchomoza saa kumi na mbili na dakika arobaini kwa madaha na mwendo wa taratibu. Shughuli za kusukuma gurudumu la maendeleo ya nchi yetu zilikuwa tayari zimekwisha kuanza.
Kila kona na sekta watu walikuwa wakikimbizana na hali ya uchumi wa kati ambao taifa letu liliingia siku chache nyuma.
Asbuhi hiyo katika benki ya NMB linayopatikana katika barabara ya Kenyata huku pia ikiwa makao ya makuu ya benki hiyo kanda ya ziwa. Kulikuwa na shughuli za kila siku zikiendelea lakini siku hii kulikuwa na shughuli ya ziada, shughuli hiyo ilikuwa ni kuhamisha kiasi cha billioni nne Tanzania shilingi kuzipeleka katika tawi la NMB Igoma.
Usafirishwaji huo ulikuwa ni ushafirishaji wa kwanza kufanywa na matawi yanayopatikana jijini hapa. Msafara wa fedha mara zote ulifanywa na benki kuu ya Tanzania. Lakini ilikuwa tofauti na siku hii ambapo tawi lilipewa ruhusa kufanya usafirishaji wa fedha.
Majira ya saa mbili kamili msafara wa gari mbili aina ya Landcruser zilizokuwa na usajili wa SU35490 iliyokuwa ikiendeshwa na Joshua Samweli na SU37200 iliyokuwa ikiendeshwa na Malima Mwenda zilianza kutoka pale. Ndani ya kila gari kulikuwa na askari wawili pia kulikuwa na wafanyakazi wa NMB Kenyata road.
Msafara huo Ulianza kutoka katika benki hiyo na kushika barabara ya Kenyata na kisha kuingia katika mzunguko wa Makongoro Avenue. Walipoumaliza mzunguko ule wakachukua uelekeo wa barabara ya Nyerere. Zilipofika makutano ya mataa ambapo makutano hayo yanaziunganisha barabara za Nyerere, station na Nkuruma zilikutana na kizuizi cha taa za barabarani. Iliwabidi kusimama kama sheria za barabarani zilivyotaka. Hilo likawa kosa kubwa sana kwa gari zile kwani majambazi wakiwa na siraha za kivita SMG, LMG, AK 47 na SHOTGUN yalivamia msafara wa magari hayo yaliyokuwa yakisindikiza pesa Kutoka NMB Kenyata road kupeleka NMB IGOMA BRANCH.
******
Kabla ya tukio gari moja aina ya Corolla ilipaki kituo cha mafuta cha TOTAL kilichopo mtaa wa Kemondo huku kikitazamana na jengo la benki kuu la zamani, kisha ikafata pickup na kupaki nyuma yake. Hakuna ambaye angeweza kubashiri kama magari yale yangeleta hatari kubwa sana masaa machache mbele. Kila mmoja alifuata kilichomleta mjini na kuacha kuchukua tahadhali yoyote juu ya gari zile kwani kulikuwa na gari nyingi ambazo ziliegesha maeneo mbalimbali bila kuwa na sababu yoyote ile.
Barabara ya Station nayo pia kulikuwa na pikipiki kubwa iliyoegesha huku dereva wake akiwa kakaa mita chache kutoka kwenye pikipiki hiyo. Alikuwa kajidhatiti kiasi cha kutia shaka lakini hakuna aliyemjali kwani kila mmoja alikuwa akishughulika na kilichomleta mjini. Wakati wote dereva huyo wa pikipiki alikuwa akifanya mawasiliano huku hakiwa na hali ya mashaka lakini kwa sababu watu walikuwa bize hakuna aliyelijali hilo.
Msafara wa gari zile zilizobeba fedha ulipofika kwenye mzunguko wa Makongoro Avenue ndipo gari ile aina ya Corola ilianza kutangulia mbele na zilipopita gari za benki ndipo pickup ile nayo ilizifuata kwa nyuma. Huku dereva wa piki piki akiiwasha pikipiki yake na kuiacha ikiunguruma huku yeye akiwa juu yake.
Wale jamaa waliokuwa kwenye gari la mbele la corola walipofika kwenye makutano ya mataa na taa za barabarani zilipozuia magari yanayotokea barabara ya Nyerere kutokea kwenye mzunguko wa Makongoro Avenue. Ndipo walipoanza kuinyeshea risari gari ya mbele SU35490 hadi likakosa uelekeao na kwenda kuigonga kwa nyuma gari ya BENZ T560 DCU. Gari ya nyuma kwenye msafara SU 37200 baada ya kuona hayo ikataka kuchepuka uelekeo wa barabara ya stesheni. Hii ikawa kosa kubwa sana kwani yule aliyekuwa juu ya pikipiki aliipiga risasi nyingi sana kuliko hata ile ya kwanza hali iliyomfanya dereva kukosa uhimili wa gari na kwenda kujikita kwenye taa za barabarani.
Kila gari ilikuwa imebeba pesa kiasi cha Bilioni 2 Tanzania shilingi.
Majambazi waliokuwa kwenye pickup walishuka kwa kasi huku wakirusha risasi hewani na kusababisha wananchi kuhamaki na kushikwa na bumbuwazi wasijue kipi cha kufanya wakalisogelea na kuanza kupakua makasha ya fedha kwenye gari ya nyuma na wale wa kwenye corola nao walianza kupakua kwenye gari ya mbele na kumuacha yule wa kwenye pikipiki hakihakikisha usalama.
Wakati upakuaji unaendelea jambazi aliyekuwa akilinda usalama alionekana ana usongo sana alikuwa anazidi kupiga risasi hali iliyowafanya watu wayaache magari na kuanza kutafuta maeneo ya kujificha. Kila mmoja alikuwa akikumbushia ni kwa kiasi gani miguu yake bado ina uimara wa kuhimili mbio zisizokuwa na mshindani. Askari waongoza magari waliokuwa zamu asbuhi hiyo walibaki na mshangao kwani tukio lile lilikuwa la kushitukiza na watekelezaji walikuwa wameliratibu vyema. Hata wao pia waliwaza wanawezaje kutoka eneo hilo ambalo liligeuka kiwanja cha kivita ndani ya mda mfupi.
Katika Maaskari walikuwepo eneo la tukio, kuna mmoja aliitwa Sajenti Adam Mashimbi. Naye alikuwa kwenye mshangao sana juu ya hali ile ya ghafla katika nchi iliyojaa amani. Kwa weledi na alivyoipenda kazi yake hakuridhika kuaibishwa namna ile. Askari huyu alikimbia kwenye kituo kidogo cha polisi pale PAMBA akatoa taarifa juu ya tukio kisha akachukua SMG na kurudi tukioni akawakuta majambazi wanamalizia kushusha pesa na wanaondoka.
Afande Adam akaanza naye kuwarushia risasi majambazi huku kila mara akijikinga ndani ya mtaro wa maji machafu na kufanya nguo zake nyeupe zisitamanike kwa uchafu. Alifanikiwa kuwapotezea muda majambazi wale lakini walifanikiwa kuondoka.
Hadi majambazi wanaondoka eneo la tukio tayari yalikuwa wamemuua askari mmoja D3866 PC Mwita Jonas kutoka kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) cha jijini Mwanza na mfanyakazi wa NMB NSSF plaza Agnes Solomoni. Wote hawa walikuwa kwenye ile gari ya nyuma iliyotaka kuchepuka kuingia barabara ya stesheni. Askari wengine watatu walijeruhiwa.
Umakini, umahiri katika kurusha risasi na pia jinsi walivyoondoka eneo la tukio ndio sababu kubwa ya mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio kuamini kuwa wale hawakuwa majambazi wa kawaida bali ni askari au watu wenye mafunzo makubwa na pia lazima walifanya majaribio kadhaa kabla ya tukio wakiwa na mipango yote A na B mpaka C ikiwa ingehitajika.
Mara baada ya kuzipata pesa majambazi wale walijigawa pale pale. Yule wa kwenye pikipiki alitoka eneo la tukio na kwenda mpaka Isamilo. Wengine waliondoka na magari yao kwa kutumia barabara ya Nyerere na kwenda kizitelekeza Kisesa mitaa ya Kanyama. Baada ya hapo walijigawa ili kuipoteza helicopter ya polisi iliyokuwa ikiwafuatilia huku wakiyateketeza magari waliyokuwa nayo kuondoa ushahidi.
Wawili kati yao walipitia njia ya Nyamongoro na kuishika Buswelu na baada ya hapo walipitia Kiseke na kuja kuishika Sabasaba na baadae kwenda Airport. Wawili wengine walipitia Nyamongoro ya chini ambapo kuna viwanja vya nanenane na kisha kuishika kishiri na baadae mahina na hapo wakaja mpaka bendera tatu na kuitafuta Bugarika na kisha Bugando wakaishia hapo.
Tukio lile lilikuwa limetekelezwa na watu walikuwa mahili sana kwani mita chache kutoka pale kulikuwa na ofisi za usalama wa taifa kanda ya Nyamagana. Pia mita chache kulikuwa na kituo cha kati cha polisi pia mita chache kulikuwa na kituo kidogo cha polisi Pamba. Achana na utitiri wa benki ambazo zote zilikuwa zikilindwa na askari wenye silaha za moto. Lakini bado wavamizi wale walifanikiwa kuondoka tena wakiwa sio peke yao bali na lundo la fedha.
*******
Wakati haya yote yanatokea aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Deusi Kalumuna alikuwa njiani safarini kwenda Shinyanga na taarifa hizi zilipomfikia aligeuza gari haraka sana kurudi eneo la tukio ambapo alipofika hakuamini kama mkoa wake unaweza kuwa na majambazi wa aina hiyo. Mshango ulikuwa dhahiri katika sura yake hakuamini kuwa tukio la namna hiyo linaweza kutokea katikati ya mji tena sehemu ambayo ina kituo kikubwa cha polisi mkoa na watekelezaji wakaondoka pasipo kufahamika walipitia wapi?.
Mara moja kamada Deusi aliamuru vikosi vyote vilivyo chini ya jeshi la polisi viingie kazini ili kuwatafuta majambazi hao kwani waliamini bado wapo jijini hapo. Pia waliimarisha ulinzi njia zote ambazo zilikuwa zinatoka nje ya jiji hili kwa maji, anga na barabara. Bahati mbaya hawakuwa na pa kuanzia zaidi ya kuwa na majeruhi wasioweza kujitambua baada ya kushambuliwa kwa risasi.
INAENDELEA
Muandishi:- Joseph .D. Migini
Call/txt:- +255766604683
Josephdeo70@gmail.com
Kwa maoni na ushauri nifuate kwenye mitandao ya kijamii kama:-
Fb:- josephdeo
Insta:- falsafa70
Twitter:- falsafa70