mpasta
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 917
- 1,997
SURA YA KWANZA
Sakarati mauti ya Kapteni Wandawanda Jijini London, Uingereza
Marafiki, ndugu na jamaa wa karibu wa Kapteni mstaafu Wandawanda wakiwa wamegubikwa na nyuso za huzuni, walionekana wamejikusanya sehemu moja, ndani ya hospitali ya "St Thomas' Hospital" iliyopo nchini Uingereza, ndani ya Jiji la London katika barabara ya Westminster Bridge SE1 7EH.
Kwa Watanzania walio wengi, wenye umri wa kuanzia miaka 30 na fauka ya hapo, jina la hospitali hiyo sio geni kwenye masikio yao. Ndani ya jengo la hospitali hiyo, Baba wa Taifa la Tanzania, Rais wa awamu ya kwanza, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliaga dunia tarehe 14/10/1999.
Ndugu na jamaa hao ambao wengi ni Watanzania waishio nchini Uingereza, walijikusanya hospitalini hapo sio kuadhimisha kifo cha mpendwa wao Hayati Nyerere, bali walikuja kufuatilia kwa ukaribu hali ya afya ya kipenzi chao, Kapteni Wandawanda, aliyelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi ndani ya hospitali hiyo.
Kila mmoja wao alishikwa na daka la roho, wanajitahidi kadri wawezavyo kufarijiana wao kwa wao. Walishindwa kabisa kuyazuia machozi kutoka kwenye mboni za macho yao yasichuruzike kutokana na uchungu wa nafsi zao. Walishajiandaa kisaikolojia kupokea taarifa yoyote mbaya juu ya mgonjwa wao.
Kapteni huyo mstaafu wa Jeshi la Wananchi, JWTZ, Bwana Wandawanda alikuwa anapitishwa na Mola wake kwenye sakarati mauti. Katika hali hiyo, mtu anakuwa baina ya uhai na kifo, hivyo huanza kutapatapa katika kupigania roho yake. Kuna wakati alikuwa anapata nafuu na kuleta matumaini ya kupona, kisha hali yake inabadilika ghafla na kumfanya apumue kwa misaada wa mipira ya gesi.
Ghafla bin vuu katika viunga vya hospitali hiyo, likaonekana gari la kifahari la Kijapani, aina ya "Honda Accord" lenye rangi ya kahawia linaingia ndani ya uzio wa hospitali. Likaegeshwa gari hilo kwenye eneo maalumu lililotengwa kwa ajili ya maegesho ya magari.
Wakashuka watu wawili, na kumuacha dereva pekee kubakia ndani ya gari hilo. Watu hao mmoja wapo alikuwa ni mwanamama mweusi wa rangi yake, mrefu kiasi, shaibu wa umri hapungui miaka 70. Mwenzake aliyeambatana nae alikuwa ni kijana wa makamo chotara wa kizungu mkononi amefumbata mkoba mdogo wenye rangi nyeusi.
Huyo mwanamke ni mke wa Kapteni Wandawanda aliambatana na mwanasheria wao, anayesimamia masuala ya urathi katika familia hiyo. Walikuja hospitalini hapo mintarafu kuitikia wito maalumu wa kushtukiza toka kwa Kapteni Wandawanda.
Walipoingia tu ndani ya jengo la hospitali na kukatiza eneo lililotengwa watu kupumzikia, watu wawili miongoni mwa wale ndugu na marafiki waliokuja mapema hospitalini hapo wakanyanyuka vitini na kwenda kuwalaki kwa nyuso za bashasha.
Baada ya habari sijambo na kusogoa kwa dakika mbili tatu, msafara wa watu wanne ukaongozana sako kwa bako kuelekea kwenye lifti kwa ajili ya kuisubiria iwapeleke roshani za juu alipolazwa Kapteni Wandawanda.
"Najiona sina uhai mrefu, saa na wakati wowote kuanzia sasa Malaika mtoa roho nahisi atanitembelea kwenye kitanda changu hicho cha mauti kwa jinsi ninavyougua" alifungua maongezi yake Kapteni Wandawanda kwa watu wake waliomzunguka kitandani.
Walikuwa wamejifungia ndani ya chumba cha mgonjwa hiyo wakisikiliza wosia wake. Baada ya kumeza mate kwa sekunde kadhaa, akaendelea na hotuba yake iliyowatia kiwewe na kuibua taharuki kubwa nafsini mwao.
"Hivyo nimewaita mke wangu na mwanasheria wangu ili muwakabidhi nyaraka zangu za siri nilizozitunza kwa ajili ya vijana wangu hawa wawili" alisema kwa tabu Kapteni Wandawanda huku sasa macho yao wote ndani ya chumba kile yakiwaelekea vijana wale wawili walioambatana nao toka chini ya jengo la hospitali.
Walikuwa ni vijana rika la makamo wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Oxford kilichopo nchini Uingereza, moja ya chuo chenye hadhi ya juu sana nchini humo. Wote walikuwa wanasomea shahada zao za Uzamivu, wakiwa ni waajiriwa katika taasisi tofauti ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Vijana hao walikuwa hawakauki nyumbani kwa Kapteni Wandawanda anayeishi katika mtaa wa Cannon Street, Jijini London. Mmoja wao kati yao, alilelewa na kusomeshwa tokea akiwa kinda na Kapteni Wandawanda, huku mwingine waliunganishwa nae na kabila. Wote watatu walikuwa wana asili ya kabila la Nyasa, linalozunguka Ziwa Nyasa.
Enzi za afya yake, walikuwa wawili hao walikuwa ni wabaraza kwenye majilisi, nyumbani kwa Kapteni Wandawanda mpaka manane ya usiku wanasogoa. Walikuwa wanapanga na kupangua mipango yao ya siri, ambayo hata mwandani wa Kapteni haifahamu vizuri kwa undani wake.
"Naomba mwanasheria wangu Mr.Harrison Ferguson uwakabidhi rasmi kimaandishi mkoba wangu mweusi uliokuja nao wenye nyaraka zangu mbalimbali nilizozitunza tokea harakati za ukombozi wa nchi ya Tanganyika toka kwenye makucha ya Mkoloni. Mkazisome kwa umakini na kuzifanyia kazi, mkifanikisha kuyatekeleza yaliyomo humo, mifupa yangu itarukaruka kwa furaha nikiwa jongomeo, mwili wangu umeoza. Mtatimiza ndoto yetu, wazee wenu wa Nyasa tuliyoshindwa kuitimiza kwa miongo kadhaa. Aluta kontinua kila la heri, Dola ya Nyasa itasimama kwa jasho na damu".
Alimalizia maongezi yake mafupi Kapteni Wandawanda huku sasa machozi ya uchungu yanambubujika akiwa yupo juu ya kitanda chake cha mauti.
Baada ya kitambo cha muda wa nusu saa tu, shughuli zote za makabidhiano hayo ya nyaraka hizo zikamalizika. Wote kwa pamoja kama walivyokuja, wakaondoka vichwa chini kama kuku wenye mdondo.
Wakawaacha madaktari na manesi wakifanya kazi yao waliyosomea ya utabibu, kujaribu kuokoa uhai wa mpendwa wao Kapteni Wandawanda.
MKOBA MWEUSI UNA SIRI GANI?? FUATILIA RIWAYA HII
KUPATA KITABU WASILIANA NA KIJOGOO PUBLISHERS AND BOOKSHOP
0678683278
Sakarati mauti ya Kapteni Wandawanda Jijini London, Uingereza
Marafiki, ndugu na jamaa wa karibu wa Kapteni mstaafu Wandawanda wakiwa wamegubikwa na nyuso za huzuni, walionekana wamejikusanya sehemu moja, ndani ya hospitali ya "St Thomas' Hospital" iliyopo nchini Uingereza, ndani ya Jiji la London katika barabara ya Westminster Bridge SE1 7EH.
Kwa Watanzania walio wengi, wenye umri wa kuanzia miaka 30 na fauka ya hapo, jina la hospitali hiyo sio geni kwenye masikio yao. Ndani ya jengo la hospitali hiyo, Baba wa Taifa la Tanzania, Rais wa awamu ya kwanza, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliaga dunia tarehe 14/10/1999.
Ndugu na jamaa hao ambao wengi ni Watanzania waishio nchini Uingereza, walijikusanya hospitalini hapo sio kuadhimisha kifo cha mpendwa wao Hayati Nyerere, bali walikuja kufuatilia kwa ukaribu hali ya afya ya kipenzi chao, Kapteni Wandawanda, aliyelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi ndani ya hospitali hiyo.
Kila mmoja wao alishikwa na daka la roho, wanajitahidi kadri wawezavyo kufarijiana wao kwa wao. Walishindwa kabisa kuyazuia machozi kutoka kwenye mboni za macho yao yasichuruzike kutokana na uchungu wa nafsi zao. Walishajiandaa kisaikolojia kupokea taarifa yoyote mbaya juu ya mgonjwa wao.
Kapteni huyo mstaafu wa Jeshi la Wananchi, JWTZ, Bwana Wandawanda alikuwa anapitishwa na Mola wake kwenye sakarati mauti. Katika hali hiyo, mtu anakuwa baina ya uhai na kifo, hivyo huanza kutapatapa katika kupigania roho yake. Kuna wakati alikuwa anapata nafuu na kuleta matumaini ya kupona, kisha hali yake inabadilika ghafla na kumfanya apumue kwa misaada wa mipira ya gesi.
Ghafla bin vuu katika viunga vya hospitali hiyo, likaonekana gari la kifahari la Kijapani, aina ya "Honda Accord" lenye rangi ya kahawia linaingia ndani ya uzio wa hospitali. Likaegeshwa gari hilo kwenye eneo maalumu lililotengwa kwa ajili ya maegesho ya magari.
Wakashuka watu wawili, na kumuacha dereva pekee kubakia ndani ya gari hilo. Watu hao mmoja wapo alikuwa ni mwanamama mweusi wa rangi yake, mrefu kiasi, shaibu wa umri hapungui miaka 70. Mwenzake aliyeambatana nae alikuwa ni kijana wa makamo chotara wa kizungu mkononi amefumbata mkoba mdogo wenye rangi nyeusi.
Huyo mwanamke ni mke wa Kapteni Wandawanda aliambatana na mwanasheria wao, anayesimamia masuala ya urathi katika familia hiyo. Walikuja hospitalini hapo mintarafu kuitikia wito maalumu wa kushtukiza toka kwa Kapteni Wandawanda.
Walipoingia tu ndani ya jengo la hospitali na kukatiza eneo lililotengwa watu kupumzikia, watu wawili miongoni mwa wale ndugu na marafiki waliokuja mapema hospitalini hapo wakanyanyuka vitini na kwenda kuwalaki kwa nyuso za bashasha.
Baada ya habari sijambo na kusogoa kwa dakika mbili tatu, msafara wa watu wanne ukaongozana sako kwa bako kuelekea kwenye lifti kwa ajili ya kuisubiria iwapeleke roshani za juu alipolazwa Kapteni Wandawanda.
"Najiona sina uhai mrefu, saa na wakati wowote kuanzia sasa Malaika mtoa roho nahisi atanitembelea kwenye kitanda changu hicho cha mauti kwa jinsi ninavyougua" alifungua maongezi yake Kapteni Wandawanda kwa watu wake waliomzunguka kitandani.
Walikuwa wamejifungia ndani ya chumba cha mgonjwa hiyo wakisikiliza wosia wake. Baada ya kumeza mate kwa sekunde kadhaa, akaendelea na hotuba yake iliyowatia kiwewe na kuibua taharuki kubwa nafsini mwao.
"Hivyo nimewaita mke wangu na mwanasheria wangu ili muwakabidhi nyaraka zangu za siri nilizozitunza kwa ajili ya vijana wangu hawa wawili" alisema kwa tabu Kapteni Wandawanda huku sasa macho yao wote ndani ya chumba kile yakiwaelekea vijana wale wawili walioambatana nao toka chini ya jengo la hospitali.
Walikuwa ni vijana rika la makamo wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Oxford kilichopo nchini Uingereza, moja ya chuo chenye hadhi ya juu sana nchini humo. Wote walikuwa wanasomea shahada zao za Uzamivu, wakiwa ni waajiriwa katika taasisi tofauti ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Vijana hao walikuwa hawakauki nyumbani kwa Kapteni Wandawanda anayeishi katika mtaa wa Cannon Street, Jijini London. Mmoja wao kati yao, alilelewa na kusomeshwa tokea akiwa kinda na Kapteni Wandawanda, huku mwingine waliunganishwa nae na kabila. Wote watatu walikuwa wana asili ya kabila la Nyasa, linalozunguka Ziwa Nyasa.
Enzi za afya yake, walikuwa wawili hao walikuwa ni wabaraza kwenye majilisi, nyumbani kwa Kapteni Wandawanda mpaka manane ya usiku wanasogoa. Walikuwa wanapanga na kupangua mipango yao ya siri, ambayo hata mwandani wa Kapteni haifahamu vizuri kwa undani wake.
"Naomba mwanasheria wangu Mr.Harrison Ferguson uwakabidhi rasmi kimaandishi mkoba wangu mweusi uliokuja nao wenye nyaraka zangu mbalimbali nilizozitunza tokea harakati za ukombozi wa nchi ya Tanganyika toka kwenye makucha ya Mkoloni. Mkazisome kwa umakini na kuzifanyia kazi, mkifanikisha kuyatekeleza yaliyomo humo, mifupa yangu itarukaruka kwa furaha nikiwa jongomeo, mwili wangu umeoza. Mtatimiza ndoto yetu, wazee wenu wa Nyasa tuliyoshindwa kuitimiza kwa miongo kadhaa. Aluta kontinua kila la heri, Dola ya Nyasa itasimama kwa jasho na damu".
Alimalizia maongezi yake mafupi Kapteni Wandawanda huku sasa machozi ya uchungu yanambubujika akiwa yupo juu ya kitanda chake cha mauti.
Baada ya kitambo cha muda wa nusu saa tu, shughuli zote za makabidhiano hayo ya nyaraka hizo zikamalizika. Wote kwa pamoja kama walivyokuja, wakaondoka vichwa chini kama kuku wenye mdondo.
Wakawaacha madaktari na manesi wakifanya kazi yao waliyosomea ya utabibu, kujaribu kuokoa uhai wa mpendwa wao Kapteni Wandawanda.
MKOBA MWEUSI UNA SIRI GANI?? FUATILIA RIWAYA HII
KUPATA KITABU WASILIANA NA KIJOGOO PUBLISHERS AND BOOKSHOP
0678683278