bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,095
RIWAYA: HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA
MTUNZI: Richard MWAMBE
MAHALI: BAGAMOYO
SIMU: 0766974865
Riwaya ya kufikirika, itakayokupa taharuki, tafadhalisoma kwa makini ikiwezekana rudia mara kadhaa iliupate uhusiano wa mtukio yaliyoitengeneza riwayahii kali, tamu, haijawahi tokea katika kare hii
CHAPISHO LA 1
Seidon alipita kwa kasi na farasi wake mweupe,mwendo aliokuwa akienda ulikuwa si wa kawaidahata kidogo, kwa kuwa farasi huyo alimjua vyemabwana wake, alitii kila amrisho apewalo.
Kila alipogeuka nyuma, Seidon alishuhudia vumbilikitimka katika jangwa lile umbali mfupi kutokayeye alipo, aliongeza mwendo, na farasi wake alitii.Njia ilikuwa na mchanga mwingi, jua kali la utosililimfanya Seidon alowe kwa jasho, akiwa mkonommoja kashika lijamu ya farasi wake, mkonomwingine ulikuwa umeshika mfuko mweusi,hakukubali kuachia hata kimoja wapo kati ya vyote.Alimaliza kijangwa kile kwa tabu na kuuanza msitumdogo lakini wenye miti mingi na mirefu, vichakavilivyofungamana, aliangalia nyuma kwa maranyingine, bado aliona vumbi lile na sasa halikuwambali sana na hapo, moyo ulimdunda kwa kasi, kiuilimshika koo na kuipoza kwa jasho lililokuwalikitiririka usoni mwake.
Mara ghafla alijikuta akipaajuu na kujibwaga chini kama mzigo, mfuko mweusiulimtoka mikononi na kuangukia pembeni, farasiwake alikuwa akijaribu kuinuka kutoka palealipoanguka.“Ha ha ha ha aaaaaa, mbio za sakafuni huishiaukingoni!” sauti ilisikika kutoka katika kichaka chajirani. Seidon alishtuka na kujaribu kunyanyuka lakinialishindwa, kumbe alipoanguka aliteguka mgongo,alibaki kugugumia tu.Mwanaume mrefu aliibuka kutoka kichakani akiwaamevaa nguo nyeusi na kichwani kajifungakitambaa cheusi, kiunoni mwake alikuwa na jisukubwa, aliuokota mfuko ule na kuuchungulia ndani,kisha akatikisa kichwa kuashiria kuwa kilichomohumo ndani ndicho hasa akitakacho.
Akapiga mbinja kali, na mara katika vichaka vile waliibukawatu takribani kumi na tano wenye mavazi yakufanana na wote wameweka majisu makubwaviunoni mwao, wakakaribia eneo lile ambalo Seidonameangukia, wakamzunguka. Yule mkubwa waoakasogea jirani na Seidon, akamwinamia kamaanataka kumwambia kitu. Akamtazama, Seidonalikuwa nusu mfu.Yule kiongozi wao akatwaa upanga wake nakumchoma kidogo shingoni, Seidon aliinua kichwakumtazama.“Hata nikikukata kichwa nitapoteza nguvu zangu tu.Hao wanaokuja ndiyo watakaokuua.”
Yule kiongozi alirudisha upanga wake alani na kuwatazama vijanawake “Ale!” alito amri na mara farasi kwa idadi yaowalitoka porini na kufika eneo lile, wakapanda nakutokomea zao porini.∞∞∞“Shit!!!” aling’aka kwa hasira Bw. Kalban. Alimwangalia Seidon pale chini akiwa hajitambui.Alijishika nywele zake ndefu na kuzitimuatimua hukuakizungukazunguka bila mpangilio, aliona wazi kuwawamewahiwa kwa kila hali.“Kichwa kiko wapi?” alimuuliza Seidon kwa hasirahuku akimnyooshea upanga wake mkali.Seidon kwa shida aliinua mkono kumuonesha jamaawalipoelekea.
Bw. Kalban aliwageukia wafuasi wakeambao bado walikuwa juu ya farasi zao,“Wahamsud, wametuwahi!” aliwaambia vijana wake,ambao wote walionekana kugadhibika kwa hilo,wakifikiri jinsi walivyo mkimbiza kutoka mbali sanana wasipate wanachotaka.“Hatuwezi kukata tamaa, lazima tukipate kilekichwa, twendeni tuwafuate” Bw Kalban na wafuasiwake walipotelea porini kuwafuata waamsud nakumuacha Seidon palepale akiwa hajiwezi kwalolote.“Ha ha ha ha ha !!!” Bw. Hamsud alicheka akiwakashika fuvu la kichwa mikononi mwakeakiligeuzageuza “Mmmmh! Hapa ndiyo kila kitu,neema zote za ‘Klakos’ ziwe juu yetu” alipomalizakusema hayo wale wafuasi wake wakapiga magotina kuinamisha vichwa vyao, kwa pamoja wakaitikia“Amin, viwe kwetu sote”Kisha kwa pamoja walielekea kwenye jingo la kale,hamamu la Kipersia lililojengwa miaka zaidi ya miatano nyuma na kuingia, ndani humo kulijawa na gizanene lakini walipoingia tu lile fuvu likang’aa nakufanya mwanga ndani ya lile hamamu, mwangawake ulikuwa ni zaidi ya wa mchana unaoujuawewe.
Wakiwa ndani ya mavazi meusi, walizivutakofia zao zilizounganishwa na maguo yao meusiambazo daima huning’inia kwa mgongoni,wakajifunika na kukaa kwa kutumi amagoti katikamtindo maalumu.Bw. Hamsud akiwa na fuvu lile alitembea taratibuhuku akisemasema maneno Fulani kwa sauti yachinichini, mara akafika sehemu ya mbele kabisa,ambapo palikuwa na kitu kama sanamu ya mtulakini hakikuwa na kichwa, akainua lile fuvu nakukipachika kile kichwa juu yake. Radi kali ilipigana kulikata anga lote, vishindo vya kutishavikaendelea kusikika, wafuasi Wahamsud ndani yalile hamamu walilala kifudifudi wakisema manenoFulani Fulani.Wingu zito lilifunika anga lote na mvua yenye upepoikaanza kunyesha kwa fujo.“Shusha mema yako ee Klakos,” walirudiarudiamaneno yale wakiwa bado katika hamamu lile.Wahamsud, walikuwa ni jamii ya watu iliyoishi hukopembezoni mwa mto Ganges, jamii ya wakulimailiyokuwa na roho mbaya ya ubinafsi, kijiji chaokilikuwa ni kijiji chenye kila uhai, ardhi yenye rutuba,mazao na uoto wenye afya.
Lakini daima walipendakunyenyekewa na majirani zao, walipendakuonekana wao ni Miungu watoto , walizuia majiyam to Ganges yasiende kwa wengine, daimaalipora mali za majirani zao na kujilimbikizia wao,walikuwa hata wakipita maeneo mengine, wakionawanawake wazuri huwateka na kuwapeleka kijinikwao.Mara hii walipata habari juu ya fuvu la Klakos,Mungu wa zamani wa Wahabesiani, kihistoriailiaminika Mungu huyo aliishi miaka zaidi yamamilioni yaliyopita huko Hamunaptra, India.Ilisemekana kuwa Klakos aliweza kukupa kilautakacho, mvua, jua, mali, mazao, kuishi mudamrefu, kushinda vita na kila utakacho.
Tamaailimjaa Bw Hamsud, kiongozi wa jamii hiyo, aliwaitavijana wake wakakamavu na kuwapa habari hiyo, nakuamua kufunga safari kwenda Hamunaptra kutafutafuvu hilo kwa hali yoyote ile, wakafanya hivyo. Safariyao haikuwa rahisi kama walivyofikiria, ilikuwangumu sana ukizingatia wao hawakuwahi kuishijangwani, ilibidi wakatishe jangwa kubwa ili kufikahuko. Kama walitegemea wafike na kulichukua fuvuhilo na kuondoka basi haiakuwa hivyo, walikutajamii nyingi za watu wakitafuta kitu hicho hicho,achana na wale ambao wamekuja huko kujifunza‘study tour’ kutoka nchi mbalimbali za ulimwengu.Kulikuwa na mchanganyiko wa watu wengi eneohilo.∞∞∞Warelvesh, walikuwa wakiishi kwa shida sana katikajangwa kubwa la Persia, wao walikuwa niwafanyabiashara lakini mara nyingi walikuwawakiporwa biashara zao na Wahamsud kilawaendapo kupeleka bidhaa zao sehemu mbalimbaliza ulimwengu.
Wakawa masikini, mji wao haukuwa na rutuba sanaya ardhi, walitegemea vitu vingi kutoka nje ya mjiwao kwa kununua au kubadilishana. Walikuwawema, wakarimu, hata wasafiri wakipita hapoilikuwa lazima wasimame na kupata japo chakulaau kinywaji.Walisikia habari fuvu lile wakiwa katika misafara yabiashara katika nchi za bara Hindi.Miaka 1200 iliyopitaSiku moja wakiwa katikati ya mji wa Jamunah, mtummoja aliyeonekana kama kichaa alikuwaakipayuka huku na huko habari juu ya fuvu hilo.Watu walimsikiliza na kumpuuzia.
Vernadalisimamisha farasi wake mweusi mwenye manyoyamengi ya kuvutia mbele ya kichaa huyo, alimtazamakwa tuo, juu mpaka chini, watu walikuwawakimfukuza kila apitapo na kelele zake. Vernadalimsikiliza kwa makini sana mtu huyo mwenyenywele ndefu na nguo chafu. Alipoona watuwatamshtukia kwa jinsi alivyomwangalia kichaa yulealimuamuru farasi wake kusonga mbele, baada yaumbali mfupi alisimama na kushuka kwenyemgahawa mmoja ili kupata kahawa.“Huyu mtu mbona ana kelele sana?” alimuulizammoja wa wahudumu wa mgahawa huo hukutaratibu akinywa kahawa yake na kashatazilizotengenezwa kwa karanga.“Ah huyo ni kichaa tu hana lolote, kila siku yeye nikelele hizo hizo, amechanganyikiwa” alijibiwa.“Mh!” Vernad aliguna na kumkazia macho mhudumuyule, kisha akaendelea “Fuvu! Fuvu ganianazungumzia?”“Aaah habari za zamani hizo kaka!”“Za zamani?! Kivipi?”“Huyu jamaa wanasema ni mchunguzi wa mamboya kale, sasa amechanganyikiwa na mambo mengiya ajabu aliyokuwa akiyaona wakati huo.
Hakunaanayejua kuhusu hilo fuvu, yeye anakazania ‘ukilipatalinakupa kila kitu’”Vernad alipotelea katika mawazo mazito, moyonimwake hakuona chembe ya uongo hata kidogokatika kelele zile za kichaa.Alitafakari kwa kina na akaona hakuna la kufanyalazima juu chini ampate kichaa yule ili apate ukweliwa habari hiyo na ikibidi ahakikishe fuvu hiloanalitia mkononi. Aliinua kichwa chake nakumtazama yule mhudumu, hakumuona, moyoulienda mbio au alikuwa anaongea na Jini?Hakupata jibu. Aliuvuta mkoba wake na kutoa dinarikadhaa na kuziweka mezani pale, moyoni aliazimiawazi kuwa lazima alale katika mji huo wa Hampustana kuhakikisha usiku huo ampate kichaa yule.Alitoka nje ya mgahawa ule na kushangaa kukutanana giza lililotanda nje, watu wakikimbia kimbia hukuna huko, alitazama vizuri angani na kuona ni kundikubwa la nzige likipita na kuzuia mwanga wa juakuifikia dunia.
Alipiga hatua chache na kuchukuafarasi wake kisha kurejea kule alikomuona kichaayule.Alikodi chumba kwenye nyumba ya kulala wagenikatikati ya mji ule. Baada ya kujipumzisha jioni ilealitoka na kutembeatembea mitaani, hakuchukuamuda mrefu sana mbele yake alikuta jumba kubwala kifahari lenye kila nakshi za kisultani,liliyapendeza macho yake hata kumfanya asimamekuliangalia.
Akiwa katika kulishangaa jumba hilondipo alipohisi kama kuna mtu nyuma yake,akageuka taratibu huku mkono wake ukiwaumeshika mpini wa jambia lake tayari kwashambulizi la aina yoyote ile.“Ha ha ha ha ha!!!!” kicheko cha kutisha kilizifanyanywele zake kusimama, hakuelewa aliyetazamanana ye ni binadamu au ni nani. Katika mtu huyo maraaliona sura ya yule kichaa mara kwa mchanganyikoiligeuka na kuwa ya nyoka, mara ya kobe. Vernadalirudi nyuma hatua kadhaa sasa jmabia lake likiwamkononi.“Unanitafuta! Umenipata, haya sema shida yako”Vernad alisikia sauti kama kumi na tano zikitokakatika kinywa cha mtu yule. Alishindwa afanyeje,aliendelea kurudi nyuma lakini bado alimuona mtuyule bado akiwa umbali ule ule kutoka kwake,aliamua kutimua mbio.
Kelele nyingi zilimfuatianyuma yake kana kwamba kuna watu walikuwawakimfukuza. Aliongeza mwendo kukimbia, hamad!Alijikwaa na kuanguka chini, alipojigeuza kutazamajuu kwa mtindo wa ‘chali’,radi kali ilimpiga usonihata kuhisi kuwa amepoteza nuru ya kuona.
USIKOSE SEHEMU YA 2
MTUNZI: Richard MWAMBE
MAHALI: BAGAMOYO
SIMU: 0766974865
Riwaya ya kufikirika, itakayokupa taharuki, tafadhalisoma kwa makini ikiwezekana rudia mara kadhaa iliupate uhusiano wa mtukio yaliyoitengeneza riwayahii kali, tamu, haijawahi tokea katika kare hii
CHAPISHO LA 1
Seidon alipita kwa kasi na farasi wake mweupe,mwendo aliokuwa akienda ulikuwa si wa kawaidahata kidogo, kwa kuwa farasi huyo alimjua vyemabwana wake, alitii kila amrisho apewalo.
Kila alipogeuka nyuma, Seidon alishuhudia vumbilikitimka katika jangwa lile umbali mfupi kutokayeye alipo, aliongeza mwendo, na farasi wake alitii.Njia ilikuwa na mchanga mwingi, jua kali la utosililimfanya Seidon alowe kwa jasho, akiwa mkonommoja kashika lijamu ya farasi wake, mkonomwingine ulikuwa umeshika mfuko mweusi,hakukubali kuachia hata kimoja wapo kati ya vyote.Alimaliza kijangwa kile kwa tabu na kuuanza msitumdogo lakini wenye miti mingi na mirefu, vichakavilivyofungamana, aliangalia nyuma kwa maranyingine, bado aliona vumbi lile na sasa halikuwambali sana na hapo, moyo ulimdunda kwa kasi, kiuilimshika koo na kuipoza kwa jasho lililokuwalikitiririka usoni mwake.
Mara ghafla alijikuta akipaajuu na kujibwaga chini kama mzigo, mfuko mweusiulimtoka mikononi na kuangukia pembeni, farasiwake alikuwa akijaribu kuinuka kutoka palealipoanguka.“Ha ha ha ha aaaaaa, mbio za sakafuni huishiaukingoni!” sauti ilisikika kutoka katika kichaka chajirani. Seidon alishtuka na kujaribu kunyanyuka lakinialishindwa, kumbe alipoanguka aliteguka mgongo,alibaki kugugumia tu.Mwanaume mrefu aliibuka kutoka kichakani akiwaamevaa nguo nyeusi na kichwani kajifungakitambaa cheusi, kiunoni mwake alikuwa na jisukubwa, aliuokota mfuko ule na kuuchungulia ndani,kisha akatikisa kichwa kuashiria kuwa kilichomohumo ndani ndicho hasa akitakacho.
Akapiga mbinja kali, na mara katika vichaka vile waliibukawatu takribani kumi na tano wenye mavazi yakufanana na wote wameweka majisu makubwaviunoni mwao, wakakaribia eneo lile ambalo Seidonameangukia, wakamzunguka. Yule mkubwa waoakasogea jirani na Seidon, akamwinamia kamaanataka kumwambia kitu. Akamtazama, Seidonalikuwa nusu mfu.Yule kiongozi wao akatwaa upanga wake nakumchoma kidogo shingoni, Seidon aliinua kichwakumtazama.“Hata nikikukata kichwa nitapoteza nguvu zangu tu.Hao wanaokuja ndiyo watakaokuua.”
Yule kiongozi alirudisha upanga wake alani na kuwatazama vijanawake “Ale!” alito amri na mara farasi kwa idadi yaowalitoka porini na kufika eneo lile, wakapanda nakutokomea zao porini.∞∞∞“Shit!!!” aling’aka kwa hasira Bw. Kalban. Alimwangalia Seidon pale chini akiwa hajitambui.Alijishika nywele zake ndefu na kuzitimuatimua hukuakizungukazunguka bila mpangilio, aliona wazi kuwawamewahiwa kwa kila hali.“Kichwa kiko wapi?” alimuuliza Seidon kwa hasirahuku akimnyooshea upanga wake mkali.Seidon kwa shida aliinua mkono kumuonesha jamaawalipoelekea.
Bw. Kalban aliwageukia wafuasi wakeambao bado walikuwa juu ya farasi zao,“Wahamsud, wametuwahi!” aliwaambia vijana wake,ambao wote walionekana kugadhibika kwa hilo,wakifikiri jinsi walivyo mkimbiza kutoka mbali sanana wasipate wanachotaka.“Hatuwezi kukata tamaa, lazima tukipate kilekichwa, twendeni tuwafuate” Bw Kalban na wafuasiwake walipotelea porini kuwafuata waamsud nakumuacha Seidon palepale akiwa hajiwezi kwalolote.“Ha ha ha ha ha !!!” Bw. Hamsud alicheka akiwakashika fuvu la kichwa mikononi mwakeakiligeuzageuza “Mmmmh! Hapa ndiyo kila kitu,neema zote za ‘Klakos’ ziwe juu yetu” alipomalizakusema hayo wale wafuasi wake wakapiga magotina kuinamisha vichwa vyao, kwa pamoja wakaitikia“Amin, viwe kwetu sote”Kisha kwa pamoja walielekea kwenye jingo la kale,hamamu la Kipersia lililojengwa miaka zaidi ya miatano nyuma na kuingia, ndani humo kulijawa na gizanene lakini walipoingia tu lile fuvu likang’aa nakufanya mwanga ndani ya lile hamamu, mwangawake ulikuwa ni zaidi ya wa mchana unaoujuawewe.
Wakiwa ndani ya mavazi meusi, walizivutakofia zao zilizounganishwa na maguo yao meusiambazo daima huning’inia kwa mgongoni,wakajifunika na kukaa kwa kutumi amagoti katikamtindo maalumu.Bw. Hamsud akiwa na fuvu lile alitembea taratibuhuku akisemasema maneno Fulani kwa sauti yachinichini, mara akafika sehemu ya mbele kabisa,ambapo palikuwa na kitu kama sanamu ya mtulakini hakikuwa na kichwa, akainua lile fuvu nakukipachika kile kichwa juu yake. Radi kali ilipigana kulikata anga lote, vishindo vya kutishavikaendelea kusikika, wafuasi Wahamsud ndani yalile hamamu walilala kifudifudi wakisema manenoFulani Fulani.Wingu zito lilifunika anga lote na mvua yenye upepoikaanza kunyesha kwa fujo.“Shusha mema yako ee Klakos,” walirudiarudiamaneno yale wakiwa bado katika hamamu lile.Wahamsud, walikuwa ni jamii ya watu iliyoishi hukopembezoni mwa mto Ganges, jamii ya wakulimailiyokuwa na roho mbaya ya ubinafsi, kijiji chaokilikuwa ni kijiji chenye kila uhai, ardhi yenye rutuba,mazao na uoto wenye afya.
Lakini daima walipendakunyenyekewa na majirani zao, walipendakuonekana wao ni Miungu watoto , walizuia majiyam to Ganges yasiende kwa wengine, daimaalipora mali za majirani zao na kujilimbikizia wao,walikuwa hata wakipita maeneo mengine, wakionawanawake wazuri huwateka na kuwapeleka kijinikwao.Mara hii walipata habari juu ya fuvu la Klakos,Mungu wa zamani wa Wahabesiani, kihistoriailiaminika Mungu huyo aliishi miaka zaidi yamamilioni yaliyopita huko Hamunaptra, India.Ilisemekana kuwa Klakos aliweza kukupa kilautakacho, mvua, jua, mali, mazao, kuishi mudamrefu, kushinda vita na kila utakacho.
Tamaailimjaa Bw Hamsud, kiongozi wa jamii hiyo, aliwaitavijana wake wakakamavu na kuwapa habari hiyo, nakuamua kufunga safari kwenda Hamunaptra kutafutafuvu hilo kwa hali yoyote ile, wakafanya hivyo. Safariyao haikuwa rahisi kama walivyofikiria, ilikuwangumu sana ukizingatia wao hawakuwahi kuishijangwani, ilibidi wakatishe jangwa kubwa ili kufikahuko. Kama walitegemea wafike na kulichukua fuvuhilo na kuondoka basi haiakuwa hivyo, walikutajamii nyingi za watu wakitafuta kitu hicho hicho,achana na wale ambao wamekuja huko kujifunza‘study tour’ kutoka nchi mbalimbali za ulimwengu.Kulikuwa na mchanganyiko wa watu wengi eneohilo.∞∞∞Warelvesh, walikuwa wakiishi kwa shida sana katikajangwa kubwa la Persia, wao walikuwa niwafanyabiashara lakini mara nyingi walikuwawakiporwa biashara zao na Wahamsud kilawaendapo kupeleka bidhaa zao sehemu mbalimbaliza ulimwengu.
Wakawa masikini, mji wao haukuwa na rutuba sanaya ardhi, walitegemea vitu vingi kutoka nje ya mjiwao kwa kununua au kubadilishana. Walikuwawema, wakarimu, hata wasafiri wakipita hapoilikuwa lazima wasimame na kupata japo chakulaau kinywaji.Walisikia habari fuvu lile wakiwa katika misafara yabiashara katika nchi za bara Hindi.Miaka 1200 iliyopitaSiku moja wakiwa katikati ya mji wa Jamunah, mtummoja aliyeonekana kama kichaa alikuwaakipayuka huku na huko habari juu ya fuvu hilo.Watu walimsikiliza na kumpuuzia.
Vernadalisimamisha farasi wake mweusi mwenye manyoyamengi ya kuvutia mbele ya kichaa huyo, alimtazamakwa tuo, juu mpaka chini, watu walikuwawakimfukuza kila apitapo na kelele zake. Vernadalimsikiliza kwa makini sana mtu huyo mwenyenywele ndefu na nguo chafu. Alipoona watuwatamshtukia kwa jinsi alivyomwangalia kichaa yulealimuamuru farasi wake kusonga mbele, baada yaumbali mfupi alisimama na kushuka kwenyemgahawa mmoja ili kupata kahawa.“Huyu mtu mbona ana kelele sana?” alimuulizammoja wa wahudumu wa mgahawa huo hukutaratibu akinywa kahawa yake na kashatazilizotengenezwa kwa karanga.“Ah huyo ni kichaa tu hana lolote, kila siku yeye nikelele hizo hizo, amechanganyikiwa” alijibiwa.“Mh!” Vernad aliguna na kumkazia macho mhudumuyule, kisha akaendelea “Fuvu! Fuvu ganianazungumzia?”“Aaah habari za zamani hizo kaka!”“Za zamani?! Kivipi?”“Huyu jamaa wanasema ni mchunguzi wa mamboya kale, sasa amechanganyikiwa na mambo mengiya ajabu aliyokuwa akiyaona wakati huo.
Hakunaanayejua kuhusu hilo fuvu, yeye anakazania ‘ukilipatalinakupa kila kitu’”Vernad alipotelea katika mawazo mazito, moyonimwake hakuona chembe ya uongo hata kidogokatika kelele zile za kichaa.Alitafakari kwa kina na akaona hakuna la kufanyalazima juu chini ampate kichaa yule ili apate ukweliwa habari hiyo na ikibidi ahakikishe fuvu hiloanalitia mkononi. Aliinua kichwa chake nakumtazama yule mhudumu, hakumuona, moyoulienda mbio au alikuwa anaongea na Jini?Hakupata jibu. Aliuvuta mkoba wake na kutoa dinarikadhaa na kuziweka mezani pale, moyoni aliazimiawazi kuwa lazima alale katika mji huo wa Hampustana kuhakikisha usiku huo ampate kichaa yule.Alitoka nje ya mgahawa ule na kushangaa kukutanana giza lililotanda nje, watu wakikimbia kimbia hukuna huko, alitazama vizuri angani na kuona ni kundikubwa la nzige likipita na kuzuia mwanga wa juakuifikia dunia.
Alipiga hatua chache na kuchukuafarasi wake kisha kurejea kule alikomuona kichaayule.Alikodi chumba kwenye nyumba ya kulala wagenikatikati ya mji ule. Baada ya kujipumzisha jioni ilealitoka na kutembeatembea mitaani, hakuchukuamuda mrefu sana mbele yake alikuta jumba kubwala kifahari lenye kila nakshi za kisultani,liliyapendeza macho yake hata kumfanya asimamekuliangalia.
Akiwa katika kulishangaa jumba hilondipo alipohisi kama kuna mtu nyuma yake,akageuka taratibu huku mkono wake ukiwaumeshika mpini wa jambia lake tayari kwashambulizi la aina yoyote ile.“Ha ha ha ha ha!!!!” kicheko cha kutisha kilizifanyanywele zake kusimama, hakuelewa aliyetazamanana ye ni binadamu au ni nani. Katika mtu huyo maraaliona sura ya yule kichaa mara kwa mchanganyikoiligeuka na kuwa ya nyoka, mara ya kobe. Vernadalirudi nyuma hatua kadhaa sasa jmabia lake likiwamkononi.“Unanitafuta! Umenipata, haya sema shida yako”Vernad alisikia sauti kama kumi na tano zikitokakatika kinywa cha mtu yule. Alishindwa afanyeje,aliendelea kurudi nyuma lakini bado alimuona mtuyule bado akiwa umbali ule ule kutoka kwake,aliamua kutimua mbio.
Kelele nyingi zilimfuatianyuma yake kana kwamba kuna watu walikuwawakimfukuza. Aliongeza mwendo kukimbia, hamad!Alijikwaa na kuanguka chini, alipojigeuza kutazamajuu kwa mtindo wa ‘chali’,radi kali ilimpiga usonihata kuhisi kuwa amepoteza nuru ya kuona.
USIKOSE SEHEMU YA 2