saul19
Member
- Aug 11, 2015
- 35
- 9
THE WORLD IN THE NEW WORLD
(Dunia ndani ya dunia mpya).
SEHEMU YA…………………………01.
Mtunzi: Saul David
Tel: +255756862047
Email: Saulstewarty@gmail.com ******
Tarehe 29-09-2008. Dar es Salaam - Tanzania.
Hali ya sintofahamu iliendelea kutanda ndani ya jiji la Dar es salaam, ni baada ya mfuatano wa matukio mengi ya kustaajabisha yaliyomfanya kila mmoja kutoka sehemu mbalimbali nje na ndani ya Tanzania kuwa makini kufuatilia mambo yaliyokuwa yakiendelea ndani ya jiji hilo.
Ulikuwa ni mwezi mmoja sasa umepita tangu kupotea kwa binti mmoja mrembo kupindukia aliyejipatia umaarufu mkubwa baada ya kulitwaa taji la Miss Tanzania 2008, aliitwa CATHERINE PETER, binti mwenye umri yapata miaka 23.
Ikiwa ni siku mbili tu baada ya Catherine kutwaa taji hilo la miss Tanzania, alipotea ghafula na hakuna mtu aliyejua mahali alipokwenda, ilibidi wazazi wake watoe taarifa kituo cha polisi na hapo msako mkali wa kumtafuta Catherin ulianza mara moja.
Waandishi wa habari pamoja na watu wengine wengi bado walitamani kujua mawili matatu kumuhusu mlimbwende huyo ambaye ama kwa hakika alikuwa na sifa zote za kulitwaa taji hilo la Miss Tanzania 2008, lakini Catherine hakuwepo tena.
Taarifa za kupotea kwa binti huyo mrembo Catherine zilikuwa za ghafula na kushtusha mno, hali hii iliwafanya wapambe na mashabiki wake kuisisitiza serikali kuhakikisha wanampata Catherine mapema akiwa salama salmini.
****
KELVIN JOHNSON kijana mwenye umri wa miaka 25, alikuwa ni mmoja kati ya askari makini wa kitengo cha upelelezi waliopewa jukumu la kuifuatilia kesi ya kupotea kwa Catherine.
Kelvin akiwa ndio kwanza ana miaka miwili tu tangu aanze kazi hii ya upelelezi tayari alikuwa amejipatia sifa na umaarufu mkubwa kutokana na namna alivyokuwa akifanya kazi kwa kujituma na kwa usahihi,
pamoja na umri wake kuwa mdogo lakini Kelvin alikuwa akifanya kazi vizuri mno kuwazidi hata askari wengine waliokuwa na uzoefu.
hali hii ilimfanya Kelvin kuaminika zaidi na wakubwa wake na ndio sababu alikuwa miongoni mwa askari watano waliokabidhiwa jukumu la kuipeleleza kesi hii ya Miss Catherine.
Mara tu baada ya Kelvin kukabidhiwa kesi hii alianza upelelezi mara moja akishirikiana na askari wenzake wanne, lakini Kelvin alikuwa akitumia mda mwingi sana kuifuatilia kesi hii wakati mwingine alilazimika kufanya kazi hadi nyakati za usiku jambo lililomshangaza sana kiongozi wa timu yake waliyependa kumuita Chief Mark.
Ni kweli Chief Mark alielewa kuwa Kelvin ni askari bora anaefanya kazi kwa kujituma sana lakini katika kesi hii ya Catherine, Kelvin alionekana kuvuka mipaka.
alikuwa akiifanya kazi kwa nguvu kubwa sana wakati mwingine alisahau hata kula hali iliyomfanya Chief Mark amtilie shaka.
Waliendelea kufanya kazi kama kawaida lakini safari hii Chief mark alikuwa akifuatilia kila jambo aliloifanya Kelvin kwa siri.
Siku chache baadae Chief Mark alimuita Kelvin ofisini kwake.
“Kelvin unaweza kuniambia wewe na Catherine mnajuana kwa mda gani mpaka sasa hivi?” Aliuliza Chief Mark.
Swali hili lilimfanya Kelvin ashituke kidogo lakini akajitahidi kuficha mshtuko wake.
“Ca..catherine?, catherine yupi?” Kelvin alijibu kwa swali.
“Catherine peter, miss Tanzania 2008 aliyepotea mwezi mmoja uliopita, umejuana nae wapi na ni kwa mda gani mpaka sasa?” Chief Mark aliuliza tena kwa msisitizo zaidi.
Kelvin alitoa macho kwa mshangao, hakutegemea kabisa kama kiongozi wake wa kazi angemuliza swali hilo.
Ni kweli Kelvin anafahamiana vizuri sana Catherine lakini alifanya jambo hilio kuwa siri, hakutamani mtu yoyote wakiwemo polisi wenzake wajue.
Kelvin alibaki ametulia kimya huku akijaribu kumtafakari Chief mark akiwa haelewi ni vipi ameweza kugundua kama yeye na Catherine wanafahamiana.
“Kelvin mbona haunijibu swali langu, okay basi haina shida nakuuliza swali lingine,
Ni kwanini unatumia nguvu kubwa sana ukijaribu kumsaidia Catherine mwanamke ambaye alikuacha na kukutamkia wazi kuwa hakupendi?”
“Heee!! Chief umejuaje haya yote?”.
“Kumbuka mimi ni mpelelezi wa mda mrefu zaidi yako Kelvin na istoshe ni mkubwa wako wa kazi, huna haja ya kuendelea kunificha”.
Yalikuwa ni maneno yaliyomfanya Kelvin akabiki kimya kwa sekunde kadhaa,
“Ni kweli mimi na Catherine tunafahamiana, tulikuwa na mahusiano yaani eeeh! Mmh, tulikuwa tuna…” Kelvin alisita kidogo kueleza
“Kwa nini mlitengana?”
“Aaah! Ni hostoria ndefu sana chief, ila bado nampenda sana Cathe, naamini na yeye pia ananipenda japo ndio ni kweli kwa mara ya mwisho aliniambia kuwa hanipendi lakini……. ” Kelvin aliongea kwa masikitiko mwisho Chief Mark alinyoosha mkono akimtaka asiongee zaidi.
“Okay inatosha, hayo ni mambo yako mwenyewe sitaki kufahamu zaidi kuhusu mahusiano yenu, ila pata muda wa kupumzika na usipende kufanya kazi peke yako, hii kazi ni ya timu nzima haijalishi tunamfahamu au hatumfahamu Catherine.” Alisema Chief Mark kisha akaondoka na kumuacha Kelvin ndani ya ofisi yake hali akiwa na mawazo mengi a akitafakari mambo kadhaa yalyotokea kipindi cha nyuma pindi alipokuwa pamoja na Catherine.
“Am so sorry Catherine, I miss you much”(Samahani sana Catherine, nimekukumbuka mno) Alisema Kelvin huku akisimama kwa unyonge na kuondoka.
*********
Upelelezi uliendelea huku safari hii Kelvin akijitahidi kushirikiana na timu yake kama alivyoelekezwa na Chief mark,
Baada ya upelelezi wa kina hatimae walifanikiwa kumbaini dereva taksi mmoja ambaye ndiye aliyembeba Miss Catherine kwa mara ya mwisho kabla ya kupotea.
Dereva huyu alijulikana kwa jina la Thomas Maziku, picha zake zilisambazwa katika maeneo mbalimbali huku Thomas akihusushwa moja kwa moja na tukio la kumteka Catherine.
Kwa msaada wa raia hatimae polisi walifankiwa kupajua eneo aliloishi Thomas nje kidogo na jiji la Dar es salaam, haraka walifika eneo hilo lakini haikuwa kazi rahisi kumkamata kwani Thomas alikuwa akiishi kama gaidi, alimiliki siraha nyingi za moto.
Baada ya purukushani nzito na ya aina yake hatimae askari walifanikiwa kumkamata bwana Thomas wakafika nae kituo cha polisi kwa ajili ya hamojiano zaidi ikiwa ni pamoja na kusema mahali alipompeleka Catherine.
********
Baada ya Kelvin kuhakikisha mtuhumiwa ameingizwa ndani ya kituo cha polisi aliondoka taratibu hali alionekana kuchoka sana baada ya purukushani nzito wakati wa kumkamata Bwana Thomas.
Alipiga hatua taratibu huku akijaribu kuwakwepa waandishi wa habari ambao walifika mapema sana baada ya kupata habari kuwa Bwana Thomas amekamatwa.
Wakati Kelvin akizidi kwenda mara ghafula alihisi kunamtu amemshika mkono kwa nyuma, haraka aligeuka kutazama.
Alishangaa kumuona mtoto mdogo wa kike mwenye umri wa miaka kama saba hivi akiwa ameung’ang’ania mkono wake wa kushoto, mtoto huyo alikuwa amevaa sare ya shule ya msingi akiwa na begi lake mgongoni.
Kelvin alimtazama yule mtoto kwa sekunde kazaa, yule mtoto nae alimtazama Kelvin huku akiachia tabasamu pana kisha akaingiza mkono kwenye mfuko wa sketi yake akatoa kitu fulani na kumpatia Kelvin.
“Unaitwa nani mtoto mzuri” Kelvin alipokea kile kitu alichopewa huku akimtupia swali yule mtoto, kisha akatazama ni kitu gani amepewa, ilikuwa ni saa nzuri ya kike yenye umbo la kopa.
Kelvin alishtuka kidogo baada ya kuiona ile saa, haraka aliigeuza upande wa nyuma na kuitazama kwa makini hapo alijikuta anashtuka zaidi
Kelvin aliikumbuka vizuri saa hiyo, ilikuwa ni zawadi pekee aliyompatia Catherine miaka mingi iliyopita baada ya Catherine kumaliza darasa la saba, nyuma ya saa hiyo kulikuwa na picha dogo iliyoonyesha sura Catherine
Ni saa ambayo Catherine allikuwa akiithamini kuliko kitu kingine chochote.
“umepata wapi hii saa?” Aliuliza Kelvin huku akigeuka kumuangalia yule mtoto lakini hakumuona tena, tayari alisha ondoka .
Aliangaza macho huku na huku kwa mbali alimuona yule mtoto anakimbia na kutokomea kwenye msongamano mkubwa wa watu.
Haraka Kelvin nae alianza kupiga hatua ndefu ndefu kumfuata, hakutaka kabisa kumuacha aende kwani alikuwa na maswali mengi sana ya kumuliza.
Yule mtoto alizidi kukimbia huku Kelvin nae akizidi kumfuata nyuma hali akimuangalia kwa makini asije kumpotea.
Ilikuwa hivyo kwa zaidi ya dakika 15, Mwisho Kelvin alimuona yule mtoto anaingia ndani ya jengo moja kubwa lenye ghorofa kadhaa.
Haraka Kelvin nae pasipo kuwa na wasiwasi wowote elienda moja kwa moja na kuingia ndani ya lile jengo,
Baada tu ya Kelvin kuingia ndani mara milango miwili ya jengo hilo akajifunga lakini Kelvin hakuona hilo.
**********
Ndani kulikuwa kimya kabisa, ilionekana ni eneo ambalo hutumiaka kama ukumbi wa starehe lakini hakukuwa na mtu hata mmoja wakati huo.
Kelvin aliendelea kuangaza macho huku na huku akijaribu kumtafuta yule mtoto kwani alikuwa na asilimia mia moja kwamba yupo mle ndani.
ni kweli baada ya muda alifanikiwa kumuona yule mtoto akiwa amepanda ngazi na kufika eneo la juu kabisa.
Baada ya yule mtoto kukutanisha macho na Kelvin alitabasamu na kumpungia mkono kisha akakimbia tena, hali hii ilimshangaza kidogo Kelvin lakini hakusita kuendelea kumfuata.
Alipandisha ngazi upesi upesi na hatimae alifika juu kabisa eneo alilomuona yule mtoto kwa mara ya mwisho, akafuata uelekeo ule alikokimbilia.
Kelvin aliendelea kupenya na kuingia ndani zaidi ya jengo hilo lilokuwa na utulivu wa ajabu, alionekana kuwa na ujasiri wa ajabu kutokana na kazi yake aliyokuwa akiifanya, tayari alishakutana na matukio mengi ya kutisha hivyo mazingira ya jengo hilo kwake aliyaona kawaida tu.
Alianza kunyata akifuata uelekeo wa korido moja ndefu.
Wakati anazidi kwenda mara ghafula taa zilizima na kuwaka, zikazima na kuwaka tena kisha kikazima tena jumla, kukawa na giza zito eneo lile.
Wakati Kelvin akizidi kutahamaki mara ghafula ukatokea mkikisiko mkubwa, kufumba na kufumbua eneo alilokuwa amesimama likaanza kushuka chini kwa kasi.
Hali hii ilimtisha sana Kelvin akatamani kupiga kelele za kuomba msada lakini akasita akalala chini na kujishikilia vizuri kwenye kile kitu kilichokuwa kikimpeleka chini kwa kasi.
Dakika tatu baadaen Kelvin alilushwa na kujikuta anadondoka chini kwenye ene.o lingine tofauti, mara hiyo taa zilianza kuwaka moja baada ya nyingine kukawa na mwanga tena.
Kelvin alijikuta yupo ndani ya chumba kimoja kikubwa sana, kwa mtazamo wa haraka haraka Kelvin aliweza kulifananisha eneo hilo kama eneo la bunge, lakini viti na meza vilikuwa wazi hakukuwa na mtu hata mmoja.
Akiwa katika hali ya kushangaa mara ghafula alisikia vyishindo mbele yake, haraka aliina macho yake kutazama.
kwa mbali aliwaona wanaume watano wanakuja upande wake taratibu. Wanne walikuwa wamevaa suti nadhifu zenye rangi nyekundu, mmoja alivaa suti nyeupe mkononi akiwa ameshikilia mkongojo wenye rangi nyeupe pia.
Kelvin alibaki amekaa palepale chini, hakuweza kurudi nyuma wala kusogea mbele.
Mwisho wale watu walifika na kusimama mbele yake.
Kelvin aliwatazama kwa zamu mmoja baada ya mwingine. Zilikuwa ni sura ngeni kabisa kwake.
“Kelvin Johnson, bila shaka upo hapa kwa ajili ya kumtafuta mtu humihu sana kwako, Catherine peter” Alisema yule mzee aliyevaa suti nyeupe hali akiachia tabasamu mwanana.
JE NINI KITAFUATA?
=>Kelvin yupo eneo salama?
=>Catherine je, yuko wapi?
Nini maana ya Dunia ndani ya Dunia mpya.
Huu ni mwanzo tu,
ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII YA KUSISIMUA.
(Dunia ndani ya dunia mpya).
SEHEMU YA…………………………01.
Mtunzi: Saul David
Tel: +255756862047
Email: Saulstewarty@gmail.com ******
Tarehe 29-09-2008. Dar es Salaam - Tanzania.
Hali ya sintofahamu iliendelea kutanda ndani ya jiji la Dar es salaam, ni baada ya mfuatano wa matukio mengi ya kustaajabisha yaliyomfanya kila mmoja kutoka sehemu mbalimbali nje na ndani ya Tanzania kuwa makini kufuatilia mambo yaliyokuwa yakiendelea ndani ya jiji hilo.
Ulikuwa ni mwezi mmoja sasa umepita tangu kupotea kwa binti mmoja mrembo kupindukia aliyejipatia umaarufu mkubwa baada ya kulitwaa taji la Miss Tanzania 2008, aliitwa CATHERINE PETER, binti mwenye umri yapata miaka 23.
Ikiwa ni siku mbili tu baada ya Catherine kutwaa taji hilo la miss Tanzania, alipotea ghafula na hakuna mtu aliyejua mahali alipokwenda, ilibidi wazazi wake watoe taarifa kituo cha polisi na hapo msako mkali wa kumtafuta Catherin ulianza mara moja.
Waandishi wa habari pamoja na watu wengine wengi bado walitamani kujua mawili matatu kumuhusu mlimbwende huyo ambaye ama kwa hakika alikuwa na sifa zote za kulitwaa taji hilo la Miss Tanzania 2008, lakini Catherine hakuwepo tena.
Taarifa za kupotea kwa binti huyo mrembo Catherine zilikuwa za ghafula na kushtusha mno, hali hii iliwafanya wapambe na mashabiki wake kuisisitiza serikali kuhakikisha wanampata Catherine mapema akiwa salama salmini.
****
KELVIN JOHNSON kijana mwenye umri wa miaka 25, alikuwa ni mmoja kati ya askari makini wa kitengo cha upelelezi waliopewa jukumu la kuifuatilia kesi ya kupotea kwa Catherine.
Kelvin akiwa ndio kwanza ana miaka miwili tu tangu aanze kazi hii ya upelelezi tayari alikuwa amejipatia sifa na umaarufu mkubwa kutokana na namna alivyokuwa akifanya kazi kwa kujituma na kwa usahihi,
pamoja na umri wake kuwa mdogo lakini Kelvin alikuwa akifanya kazi vizuri mno kuwazidi hata askari wengine waliokuwa na uzoefu.
hali hii ilimfanya Kelvin kuaminika zaidi na wakubwa wake na ndio sababu alikuwa miongoni mwa askari watano waliokabidhiwa jukumu la kuipeleleza kesi hii ya Miss Catherine.
Mara tu baada ya Kelvin kukabidhiwa kesi hii alianza upelelezi mara moja akishirikiana na askari wenzake wanne, lakini Kelvin alikuwa akitumia mda mwingi sana kuifuatilia kesi hii wakati mwingine alilazimika kufanya kazi hadi nyakati za usiku jambo lililomshangaza sana kiongozi wa timu yake waliyependa kumuita Chief Mark.
Ni kweli Chief Mark alielewa kuwa Kelvin ni askari bora anaefanya kazi kwa kujituma sana lakini katika kesi hii ya Catherine, Kelvin alionekana kuvuka mipaka.
alikuwa akiifanya kazi kwa nguvu kubwa sana wakati mwingine alisahau hata kula hali iliyomfanya Chief Mark amtilie shaka.
Waliendelea kufanya kazi kama kawaida lakini safari hii Chief mark alikuwa akifuatilia kila jambo aliloifanya Kelvin kwa siri.
Siku chache baadae Chief Mark alimuita Kelvin ofisini kwake.
“Kelvin unaweza kuniambia wewe na Catherine mnajuana kwa mda gani mpaka sasa hivi?” Aliuliza Chief Mark.
Swali hili lilimfanya Kelvin ashituke kidogo lakini akajitahidi kuficha mshtuko wake.
“Ca..catherine?, catherine yupi?” Kelvin alijibu kwa swali.
“Catherine peter, miss Tanzania 2008 aliyepotea mwezi mmoja uliopita, umejuana nae wapi na ni kwa mda gani mpaka sasa?” Chief Mark aliuliza tena kwa msisitizo zaidi.
Kelvin alitoa macho kwa mshangao, hakutegemea kabisa kama kiongozi wake wa kazi angemuliza swali hilo.
Ni kweli Kelvin anafahamiana vizuri sana Catherine lakini alifanya jambo hilio kuwa siri, hakutamani mtu yoyote wakiwemo polisi wenzake wajue.
Kelvin alibaki ametulia kimya huku akijaribu kumtafakari Chief mark akiwa haelewi ni vipi ameweza kugundua kama yeye na Catherine wanafahamiana.
“Kelvin mbona haunijibu swali langu, okay basi haina shida nakuuliza swali lingine,
Ni kwanini unatumia nguvu kubwa sana ukijaribu kumsaidia Catherine mwanamke ambaye alikuacha na kukutamkia wazi kuwa hakupendi?”
“Heee!! Chief umejuaje haya yote?”.
“Kumbuka mimi ni mpelelezi wa mda mrefu zaidi yako Kelvin na istoshe ni mkubwa wako wa kazi, huna haja ya kuendelea kunificha”.
Yalikuwa ni maneno yaliyomfanya Kelvin akabiki kimya kwa sekunde kadhaa,
“Ni kweli mimi na Catherine tunafahamiana, tulikuwa na mahusiano yaani eeeh! Mmh, tulikuwa tuna…” Kelvin alisita kidogo kueleza
“Kwa nini mlitengana?”
“Aaah! Ni hostoria ndefu sana chief, ila bado nampenda sana Cathe, naamini na yeye pia ananipenda japo ndio ni kweli kwa mara ya mwisho aliniambia kuwa hanipendi lakini……. ” Kelvin aliongea kwa masikitiko mwisho Chief Mark alinyoosha mkono akimtaka asiongee zaidi.
“Okay inatosha, hayo ni mambo yako mwenyewe sitaki kufahamu zaidi kuhusu mahusiano yenu, ila pata muda wa kupumzika na usipende kufanya kazi peke yako, hii kazi ni ya timu nzima haijalishi tunamfahamu au hatumfahamu Catherine.” Alisema Chief Mark kisha akaondoka na kumuacha Kelvin ndani ya ofisi yake hali akiwa na mawazo mengi a akitafakari mambo kadhaa yalyotokea kipindi cha nyuma pindi alipokuwa pamoja na Catherine.
“Am so sorry Catherine, I miss you much”(Samahani sana Catherine, nimekukumbuka mno) Alisema Kelvin huku akisimama kwa unyonge na kuondoka.
*********
Upelelezi uliendelea huku safari hii Kelvin akijitahidi kushirikiana na timu yake kama alivyoelekezwa na Chief mark,
Baada ya upelelezi wa kina hatimae walifanikiwa kumbaini dereva taksi mmoja ambaye ndiye aliyembeba Miss Catherine kwa mara ya mwisho kabla ya kupotea.
Dereva huyu alijulikana kwa jina la Thomas Maziku, picha zake zilisambazwa katika maeneo mbalimbali huku Thomas akihusushwa moja kwa moja na tukio la kumteka Catherine.
Kwa msaada wa raia hatimae polisi walifankiwa kupajua eneo aliloishi Thomas nje kidogo na jiji la Dar es salaam, haraka walifika eneo hilo lakini haikuwa kazi rahisi kumkamata kwani Thomas alikuwa akiishi kama gaidi, alimiliki siraha nyingi za moto.
Baada ya purukushani nzito na ya aina yake hatimae askari walifanikiwa kumkamata bwana Thomas wakafika nae kituo cha polisi kwa ajili ya hamojiano zaidi ikiwa ni pamoja na kusema mahali alipompeleka Catherine.
********
Baada ya Kelvin kuhakikisha mtuhumiwa ameingizwa ndani ya kituo cha polisi aliondoka taratibu hali alionekana kuchoka sana baada ya purukushani nzito wakati wa kumkamata Bwana Thomas.
Alipiga hatua taratibu huku akijaribu kuwakwepa waandishi wa habari ambao walifika mapema sana baada ya kupata habari kuwa Bwana Thomas amekamatwa.
Wakati Kelvin akizidi kwenda mara ghafula alihisi kunamtu amemshika mkono kwa nyuma, haraka aligeuka kutazama.
Alishangaa kumuona mtoto mdogo wa kike mwenye umri wa miaka kama saba hivi akiwa ameung’ang’ania mkono wake wa kushoto, mtoto huyo alikuwa amevaa sare ya shule ya msingi akiwa na begi lake mgongoni.
Kelvin alimtazama yule mtoto kwa sekunde kazaa, yule mtoto nae alimtazama Kelvin huku akiachia tabasamu pana kisha akaingiza mkono kwenye mfuko wa sketi yake akatoa kitu fulani na kumpatia Kelvin.
“Unaitwa nani mtoto mzuri” Kelvin alipokea kile kitu alichopewa huku akimtupia swali yule mtoto, kisha akatazama ni kitu gani amepewa, ilikuwa ni saa nzuri ya kike yenye umbo la kopa.
Kelvin alishtuka kidogo baada ya kuiona ile saa, haraka aliigeuza upande wa nyuma na kuitazama kwa makini hapo alijikuta anashtuka zaidi
Kelvin aliikumbuka vizuri saa hiyo, ilikuwa ni zawadi pekee aliyompatia Catherine miaka mingi iliyopita baada ya Catherine kumaliza darasa la saba, nyuma ya saa hiyo kulikuwa na picha dogo iliyoonyesha sura Catherine
Ni saa ambayo Catherine allikuwa akiithamini kuliko kitu kingine chochote.
“umepata wapi hii saa?” Aliuliza Kelvin huku akigeuka kumuangalia yule mtoto lakini hakumuona tena, tayari alisha ondoka .
Aliangaza macho huku na huku kwa mbali alimuona yule mtoto anakimbia na kutokomea kwenye msongamano mkubwa wa watu.
Haraka Kelvin nae alianza kupiga hatua ndefu ndefu kumfuata, hakutaka kabisa kumuacha aende kwani alikuwa na maswali mengi sana ya kumuliza.
Yule mtoto alizidi kukimbia huku Kelvin nae akizidi kumfuata nyuma hali akimuangalia kwa makini asije kumpotea.
Ilikuwa hivyo kwa zaidi ya dakika 15, Mwisho Kelvin alimuona yule mtoto anaingia ndani ya jengo moja kubwa lenye ghorofa kadhaa.
Haraka Kelvin nae pasipo kuwa na wasiwasi wowote elienda moja kwa moja na kuingia ndani ya lile jengo,
Baada tu ya Kelvin kuingia ndani mara milango miwili ya jengo hilo akajifunga lakini Kelvin hakuona hilo.
**********
Ndani kulikuwa kimya kabisa, ilionekana ni eneo ambalo hutumiaka kama ukumbi wa starehe lakini hakukuwa na mtu hata mmoja wakati huo.
Kelvin aliendelea kuangaza macho huku na huku akijaribu kumtafuta yule mtoto kwani alikuwa na asilimia mia moja kwamba yupo mle ndani.
ni kweli baada ya muda alifanikiwa kumuona yule mtoto akiwa amepanda ngazi na kufika eneo la juu kabisa.
Baada ya yule mtoto kukutanisha macho na Kelvin alitabasamu na kumpungia mkono kisha akakimbia tena, hali hii ilimshangaza kidogo Kelvin lakini hakusita kuendelea kumfuata.
Alipandisha ngazi upesi upesi na hatimae alifika juu kabisa eneo alilomuona yule mtoto kwa mara ya mwisho, akafuata uelekeo ule alikokimbilia.
Kelvin aliendelea kupenya na kuingia ndani zaidi ya jengo hilo lilokuwa na utulivu wa ajabu, alionekana kuwa na ujasiri wa ajabu kutokana na kazi yake aliyokuwa akiifanya, tayari alishakutana na matukio mengi ya kutisha hivyo mazingira ya jengo hilo kwake aliyaona kawaida tu.
Alianza kunyata akifuata uelekeo wa korido moja ndefu.
Wakati anazidi kwenda mara ghafula taa zilizima na kuwaka, zikazima na kuwaka tena kisha kikazima tena jumla, kukawa na giza zito eneo lile.
Wakati Kelvin akizidi kutahamaki mara ghafula ukatokea mkikisiko mkubwa, kufumba na kufumbua eneo alilokuwa amesimama likaanza kushuka chini kwa kasi.
Hali hii ilimtisha sana Kelvin akatamani kupiga kelele za kuomba msada lakini akasita akalala chini na kujishikilia vizuri kwenye kile kitu kilichokuwa kikimpeleka chini kwa kasi.
Dakika tatu baadaen Kelvin alilushwa na kujikuta anadondoka chini kwenye ene.o lingine tofauti, mara hiyo taa zilianza kuwaka moja baada ya nyingine kukawa na mwanga tena.
Kelvin alijikuta yupo ndani ya chumba kimoja kikubwa sana, kwa mtazamo wa haraka haraka Kelvin aliweza kulifananisha eneo hilo kama eneo la bunge, lakini viti na meza vilikuwa wazi hakukuwa na mtu hata mmoja.
Akiwa katika hali ya kushangaa mara ghafula alisikia vyishindo mbele yake, haraka aliina macho yake kutazama.
kwa mbali aliwaona wanaume watano wanakuja upande wake taratibu. Wanne walikuwa wamevaa suti nadhifu zenye rangi nyekundu, mmoja alivaa suti nyeupe mkononi akiwa ameshikilia mkongojo wenye rangi nyeupe pia.
Kelvin alibaki amekaa palepale chini, hakuweza kurudi nyuma wala kusogea mbele.
Mwisho wale watu walifika na kusimama mbele yake.
Kelvin aliwatazama kwa zamu mmoja baada ya mwingine. Zilikuwa ni sura ngeni kabisa kwake.
“Kelvin Johnson, bila shaka upo hapa kwa ajili ya kumtafuta mtu humihu sana kwako, Catherine peter” Alisema yule mzee aliyevaa suti nyeupe hali akiachia tabasamu mwanana.
JE NINI KITAFUATA?
=>Kelvin yupo eneo salama?
=>Catherine je, yuko wapi?
Nini maana ya Dunia ndani ya Dunia mpya.
Huu ni mwanzo tu,
ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII YA KUSISIMUA.