mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,135
- 276
- Thread starter
-
- #21
SIMULIZI.. BALAA
MWANDISHI.. HALFANI SUDY
Simu ...0757 633010
SEHEMU YA NANE
Bibi harusi, Nasra, alirushwa kwa kasi kule nyuma alikokuwa amekaa, na kupenya pale panapokaa kioo cha mbele ambapo sasa kulikuwa na uwazi tu, kioo kilikuwa kimeshavunjika na vioo vyote viliishia usoni kwa dereva na kwa Mzee Mpaukha. Kule nje alikotokea Nasra kichwa chake kilikutana na jiwe kubwa sana. Jiwe lile lilikipasua vibaya sana kichwa kile na kuweka ufa mkubwa. Damu zilikuwa zinatiririka! Nasra alikuwa anatoa muungurumo wa ajabu sana huku akitapika madonge makubwa ya damu mdomoni.
Mpambe wa bibi harusi, Hasina, kona kali iliyokata ile gari ilikata na yeye. Alijigonga vibaya sana pale dirishani, kiasi cha kukibobaza kioo kile kigumu cha gari. Pigo la nguvu katika kioo kile kiliondoka na fahamu zake. kiwiliwili chake kisicho na fahamu kilirushwa mbele na kujipigiza vibaya sana katika boneti ya gari ile na kudondoka chini kikiwa nyang'anyang'a.
Mama Mpaukha ambaye nae alikuwa amekaa siti za nyuma za gari lile. Yeye hakupata athari yoyote ya mwili. Mkanda aliokuwa ameufunga ulimsaidia vizuri wa gari ulimsaidia. Yeye hakurushwa kama wenzake, alibaki palepale katika kiti lakini akiwa hana uhai, bila shaka presha ilimpeleka kuzimu.
Ilikuwa ajari kubwa sana. Iliyoacha majeruhi wanne na kuondoka na roho ya mtu mmoja, mama Mpaukha.
Ajari ilitokea usiku wa manane, na kusababisha msaada uchelewe sana kufika eneo lile. Eneo lote la ajari lilikuwa linanuka damu !
Mwanasheria, ni jina la utani la mlevi maarufu sana katika wilaya ya Kilwa. Hakuna mtu aliyekuwa analijua jina lake halisi. Watu wote walimtambua kwa jina la mwanasheria.
Walimwita mwanasheria kutokana na uongeaji wake uliopita kiasi anapokuwa amekunywa pombe. Akishalewa hujifanya anajua kila kitu, anaelewa kila kitu, yeye ndiye huwa muongeaji mkuu baada ya kunywa pombe chafu.
Ni kiongozi gani ndani ya Kilwa asiyemjua mwanasheria? Alikuwa na namba za viongozi wote kuthibitisha uanasheria wake.
Tarehe ile ya sherehe ya harusi ya Dokta Yusha, mwanasheria alikuwa kilabuni akipata ulabu. Saa tisa ya usiku alihisi pombe zilimtosha. Alirudi nyumbani kwake kwa mwendo wa kupepesuka, huku akiimba nyimbo zisizoeleweka kwa sauti kubwa, na kutupia tusi moja moja hapa na pale, kama ilivyo kawaida ya walevi.
Mwanasheria alifika pale konani, kona iliyomshinda dereva Musa muda mfupi uliopita. Alijitahidi kujikaza ili atembee bila kupepesuka, alishindwa. Kona ilimshinda kama ilivyomshinda dereva Musa, mlevi mwenzie.
Naye alipepesukia kwa nguvu na kuangukia kulekule kwenye mtaro, lilikoingia gari la Mzee Mpaukha muda mfupi uliopita..
ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
MWANDISHI.. HALFANI SUDY
Simu ...0757 633010
SEHEMU YA NANE
Bibi harusi, Nasra, alirushwa kwa kasi kule nyuma alikokuwa amekaa, na kupenya pale panapokaa kioo cha mbele ambapo sasa kulikuwa na uwazi tu, kioo kilikuwa kimeshavunjika na vioo vyote viliishia usoni kwa dereva na kwa Mzee Mpaukha. Kule nje alikotokea Nasra kichwa chake kilikutana na jiwe kubwa sana. Jiwe lile lilikipasua vibaya sana kichwa kile na kuweka ufa mkubwa. Damu zilikuwa zinatiririka! Nasra alikuwa anatoa muungurumo wa ajabu sana huku akitapika madonge makubwa ya damu mdomoni.
Mpambe wa bibi harusi, Hasina, kona kali iliyokata ile gari ilikata na yeye. Alijigonga vibaya sana pale dirishani, kiasi cha kukibobaza kioo kile kigumu cha gari. Pigo la nguvu katika kioo kile kiliondoka na fahamu zake. kiwiliwili chake kisicho na fahamu kilirushwa mbele na kujipigiza vibaya sana katika boneti ya gari ile na kudondoka chini kikiwa nyang'anyang'a.
Mama Mpaukha ambaye nae alikuwa amekaa siti za nyuma za gari lile. Yeye hakupata athari yoyote ya mwili. Mkanda aliokuwa ameufunga ulimsaidia vizuri wa gari ulimsaidia. Yeye hakurushwa kama wenzake, alibaki palepale katika kiti lakini akiwa hana uhai, bila shaka presha ilimpeleka kuzimu.
Ilikuwa ajari kubwa sana. Iliyoacha majeruhi wanne na kuondoka na roho ya mtu mmoja, mama Mpaukha.
Ajari ilitokea usiku wa manane, na kusababisha msaada uchelewe sana kufika eneo lile. Eneo lote la ajari lilikuwa linanuka damu !
Mwanasheria, ni jina la utani la mlevi maarufu sana katika wilaya ya Kilwa. Hakuna mtu aliyekuwa analijua jina lake halisi. Watu wote walimtambua kwa jina la mwanasheria.
Walimwita mwanasheria kutokana na uongeaji wake uliopita kiasi anapokuwa amekunywa pombe. Akishalewa hujifanya anajua kila kitu, anaelewa kila kitu, yeye ndiye huwa muongeaji mkuu baada ya kunywa pombe chafu.
Ni kiongozi gani ndani ya Kilwa asiyemjua mwanasheria? Alikuwa na namba za viongozi wote kuthibitisha uanasheria wake.
Tarehe ile ya sherehe ya harusi ya Dokta Yusha, mwanasheria alikuwa kilabuni akipata ulabu. Saa tisa ya usiku alihisi pombe zilimtosha. Alirudi nyumbani kwake kwa mwendo wa kupepesuka, huku akiimba nyimbo zisizoeleweka kwa sauti kubwa, na kutupia tusi moja moja hapa na pale, kama ilivyo kawaida ya walevi.
Mwanasheria alifika pale konani, kona iliyomshinda dereva Musa muda mfupi uliopita. Alijitahidi kujikaza ili atembee bila kupepesuka, alishindwa. Kona ilimshinda kama ilivyomshinda dereva Musa, mlevi mwenzie.
Naye alipepesukia kwa nguvu na kuangukia kulekule kwenye mtaro, lilikoingia gari la Mzee Mpaukha muda mfupi uliopita..
ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA