Rita Mlaki hatarini kusimamishwa udiwani Dar

Sina hakika kama Wabongo tuna haki ya kudhihaki mtu mwenye hata basic certificate ya taaluma yoyote ile na kumwita kuwa hajasoma. Embu mtu atuletee takwimu za Watanzania na viwango vyao vya elimu, kama mimi na wewe sio tu tutakuwa kwenye kundi dogo sana la Watanzania na wengi wao watakuwa hao tunaowacheka ambao kwa kiasi kikubwa kutopata bahati hii ambayo mimi na wewe tumeipata kumesababishwa na wao bali na wabinafsi wachache wasiokuwa hata na dhima katika jamii yetu.
 
hebu acheni mambo ya ajabu........! yaani amesomea kuokota kuokota vichupa vya maji ya uhai?
yaani wale tunaowaona wamebeba mifuko huku wakiokota masalia ya plastiki ndo fildi yake?

Siyo hivo mzee. Umeambiwa ana masters in polychemistry. She is an expert in chemical and Polymer processing, especially Plastics. She can be a good industrial production manager especially for polymer(plastic) industries. Lakini hata hivo ni incompetent politician.
 
Huyu mama anaona aibu kutokea si alikuwa waziri zamani?
Anaona aibu kutokea.
 
..mara nyingine huyu Mama wanamshambulia kutokana na chuki dhidi ya kabila lake.

..sioni ajabu yoyote kwa yeye kushindwa kuhudhuria vikao vya madiwani. labda ametingwa na shughuli nyingine ambazo ni muhimu zaidi kwake.

..cha msingi hapa sheria na taratibu zifuatwe katika kushughulikia suala hili.

..zaidi, hivi Rita Mlaki ndiye diwani pekee nchi nzima,mkoa wa dsm,...asiyehudhuria vikao?

JokaKuu! Unatetea yasiyowezekana kutetewa. Hayo ya kabila lake au usomi wake( kama wengine wanavyojaribu kuingiza) au jinsia yake (kama wengine watakavyojaribu kuingiza) havina nafasi humu. Unapokubali cheo ina maana unakubali vile vile kufuata sheria na kanuni zinazohusu hiyo nafasi. Katika nafasi za uwakilishi kuna minimum namba ya vikao unavyotakiwa kuhudhuria. Hii ni kwa sababu upo katika nafasi hiyo kuchangia mawazo na wenzio na kuwasilisha na kutetea maslahi ya watu waliokutuma. Kutokuhudhuria (bila sababu maalum) ni kutowatendea haki hao anaowawakilisha. Uungwana ni kuwa kama hauwezi kuwawakilisha watu wako kikamilifu, bora uwaambie, uachie ngazi na umpishe mwingine. Kama haufanyi hivi, basi unastahili adhabu yeyote ambayo imeainishwa kwa mtu atendaye ulivyotenda. Kama ni kunyang'anywa hiyo dhamana, basi iwe hivyo! Kumtetea kuwa kuna wengine mbona wanafanya alivyofanya hakuna mantik! waswahili wasema " bahati ya mwenzio, usiilalie mlango wazi!"
 
Fundi Mchundo,

..ile kuonyesha fairness katika habari yake mwandishi alipaswa kueleza kama kuna wengine ambao hawahudhurii vikao.

..inawezekana kabisa diwani "mtoro" akawa ni Mama Mlaki peke yake, lakini mwandishi hajaeleza kama alifanya uchunguzi na kubaini hilo.

..nashauri Mama achukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu rasmi.

..pia nashauri zoezi hilo lisiishie kwa Mama Mlaki tu, bali kwa wale wote wenye tabia ya "utoro" kama yake.

..vilevile naomba baadhi yetu humu tupunguze chuki binafsi dhidi ya Wachaga.
 
Kwa kweli pamoja na kuwa huyu mama Mlaki ana matatizo makubwa, lakini tatizo ninaloliona hapa ni la muda mrefu ambalo ni tofauti kubwa walizonazo Londa na Mlaki. Kwanza Londa ana matatizo makubwa ya kiutendaji yeye na madiwani wake kadhaa wateule kama vile Diwani Rajabu na wengine. Hawa ni wezi wa wazi wazi na nina ushahidi mwingi sana. Na hapa Londa amempatia mahali adu yake mkubwa. Tofauti zao ni za kisiasa. Madiwani wengi sasa wamebaini udhaifu wa Londa na wameanza kumshughulikia na yeye anaamini kazi hiyo inafanywa na Mlaki. Tatizo la Coco Beach, uuzwaji holela wa maeneo, rushwa ya wazi kwa wafanyabiashara na watendaji na miundombinu duni katika manispaa hiyo hadi wanashindwa na manispaa ya Temeke ambayo miaka ya nyuma Temeke ilikua nyuma sana. Tuna kazi kubwa Watanzani lakini huo ndio mwanguko wa CCM, Londa, Mlaki, Iddi Azan, Keenja must go 2010
 
Halisi,

..ina maana wezi wanaachwa wakipeta badala yake anasumbuliwa huyo Rita Mlaki kwa kutohudhuria vikao?
 
Kama kawaida, tumekimbilia elimu yake, Kabila lake na soon tutazungumzia dini na ndoa yake.

Basic question, ni hii, kwa nini Mbunge anakuwa Diwani?

Ni Diwani wa kuteuliwa kupitia kata au ni Diwani maalum kwa kuwa ni Mbunge?

Kama ni diwani wa kuchaguliwa, swali lingine linakuja, kwa nini yeye kama Mwakilishi wa Jimbo alikwenda kugombea Uwakilishi wa Mtaa? Jee hii si uroho wa madaraka au conflict of interest? Je ni kipi alikipata kwanza Ubunge au Udiwani? kwa nini asishikilie kimoja na kuachana na kingine?

Kwa nini Sheria zetu na kanuni za uongozi zinaruhusu kuwepo na utata kama huu? Mbunge kuwa Diwani, kuwa mjumbe wa Bodi au Mwenyekiti wa Bodi wa Taasisi au Shirika?

Hamuoni kama aligombea Udiwani wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa 2004, tayari alikuwa ni Mbunge (Waziri pia kama sikukosea), basi ilikuwa ni rahisi kwake kutumia turufu ya Ubunge kupata hicho kiti cha Udiwani?

Kwa nini hajiondoi kwenye Udiwani akaachia wenye nafasi za kufanya kazi hiyo wafanye? je haoni kuwa kuendelea kwake kuwa Mbunge na Diwani kunaweza kuleta picha mbaya ya upendeleo kwa kata na mtaa wake kuliko maeneo mengine kwa kuwa yeye ni Mbunge?

Huko kushindwa kufanya kazi yake ya Udiwani hata kushiriki katika vikao ni kutokana na majukumu mengine aliyokuwa nayo. Ni Mbunge na aliwahi kuwa Waziri toka 2001 mpaka February 2008.

Sasa kama kila mara hutoa udhuru na kushindwa kushiriki kwenye vikao, ni kosa gani Londa kafanya kuomba Mlaki asimamishwe Udiwani?

Kama ningekuwa Rita Mlaki, ningejiuzulu Udiwani kama ni wa kuchaguliwa na si kutokana na wasifu wa kuwa Mbunge!

Lakini kama Udiwani wake ni kutokana na kuwa Mbunge, basi ama awajibike kwa kukiuka kanuni au sheria inayotaka Wabunge kuwa madiwani ifutwe!

Kama Sheria za TAMISEMI zinasema kuwa Mbunge ni Diwani, bado hapo kuna kosa. Haiwezekani akawa Diwani Maalumu halafu hapo hapo awe Mbunge.

Mbunge abakie Mbunge, shughuli za Maendeleo za Wilaya azifanyie kazi kupitia Mkuu wa Wilaya au Mkoa na si Halmashauri ya jiji.
 
Kama kawaida, tumekimbilia elimu yake, Kabila lake na soon tutazungumzia dini na ndoa yake.

Basic question, ni hii, kwa nini Mbunge anakuwa Diwani?

Ni Diwani wa kuteuliwa kupitia kata au ni Diwani maalum kwa kuwa ni Mbunge?

Kama ni diwani wa kuchaguliwa, swali lingine linakuja, kwa nini yeye kama Mwakilishi wa Jimbo alikwenda kugombea Uwakilishi wa Mtaa? Jee hii si uroho wa madaraka au conflict of interest? Je ni kipi alikipata kwanza Ubunge au Udiwani? kwa nini asishikilie kimoja na kuachana na kingine?

Kwa nini Sheria zetu na kanuni za uongozi zinaruhusu kuwepo na utata kama huu? Mbunge kuwa Diwani, kuwa mjumbe wa Bodi au Mwenyekiti wa Bodi wa Taasisi au Shirika?

Hamuoni kama aligombea Udiwani wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa 2004, tayari alikuwa ni Mbunge (Waziri pia kama sikukosea), basi ilikuwa ni rahisi kwake kutumia turufu ya Ubunge kupata hicho kiti cha Udiwani?

Kwa nini hajiondoi kwenye Udiwani akaachia wenye nafasi za kufanya kazi hiyo wafanye? je haoni kuwa kuendelea kwake kuwa Mbunge na Diwani kunaweza kuleta picha mbaya ya upendeleo kwa kata na mtaa wake kuliko maeneo mengine kwa kuwa yeye ni Mbunge?

Huko kushindwa kufanya kazi yake ya Udiwani hata kushiriki katika vikao ni kutokana na majukumu mengine aliyokuwa nayo. Ni Mbunge na aliwahi kuwa Waziri toka 2001 mpaka February 2008.

Sasa kama kila mara hutoa udhuru na kushindwa kushiriki kwenye vikao, ni kosa gani Londa kafanya kuomba Mlaki asimamishwe Udiwani?

Kama ningekuwa Rita Mlaki, ningejiuzulu Udiwani kama ni wa kuchaguliwa na si kutokana na wasifu wa kuwa Mbunge!

Lakini kama Udiwani wake ni kutokana na kuwa Mbunge, basi ama awajibike kwa kukiuka kanuni au sheria inayotaka Wabunge kuwa madiwani ifutwe!

Kama Sheria za TAMISEMI zinasema kuwa Mbunge ni Diwani, bado hapo kuna kosa. Haiwezekani akawa Diwani Maalumu halafu hapo hapo awe Mbunge.

Mbunge abakie Mbunge, shughuli za Maendeleo za Wilaya azifanyie kazi kupitia Mkuu wa Wilaya au Mkoa na si Halmashauri ya jiji.

Unakubaliana na Waziri kuwa Mbunge?
 
Unakubaliana na Waziri kuwa Mbunge?

Sikubaliani!

Wabunge wabakie kuwa wabunge. Wabunge wasipewe Uwaziri, Ukuu wa Mikoa, Udiwani, Ujumbe wa Bodi au Uenyekiti wa Taasisi.

Ushiriki wao uwe kwenye Bunge na Majimbo yao. Kwenye Majimbo wawepo kwenye Vikao vya Maendeleo vya Majimbo na Mikoa kutokana na nafasi zao kama Wawakilishi.
 
Sikubaliani!

Wabunge wabakie kuwa wabunge. Wabunge wasipewe Uwaziri, Ukuu wa Mikoa, Udiwani, Ujumbe wa Bodi au Uenyekiti wa Taasisi.

Ushiriki wao uwe kwenye Bunge na Majimbo yao. Kwenye Majimbo wawepo kwenye Vikao vya Maendeleo vya Majimbo na Mikoa kutokana na nafasi zao kama Wawakilishi.
Naunga mkono hoja
 
Mimi nimekuwa nikisema huku bodini kwa muda sasa: huyu Mama Rita Mlaki hafai kwenye siasa...HAFAI kabisa..huyu mama namjua miaka mingi mpaka alipoenda kusoma Masters ya mambo ya kemikali za plastic na baadaye kuwa General Manager wa Teggy Plastic...huo Ubunge wa Kawe ni kwa kifua cha Ben Mkapa (kupitia urafiki wake na Mama Mkapa) la sivyo asingeambulia kitu huko Kawe.

Kutokuhudhuria hivyo vikao ni dharau zake tu hana sababu yoyote ya maana...huyo mwandishi alipoteza dola zake kumpigia simu. Wamfukuze kabisa....

Wapinzani kaeni tayari hili jimbo la kawe ni rahisi sana kulichukua iwapo CCM watamuweka Rita Mlaki kama mgombea 2010 (kitu ambacho nitashangaa sana).
Ni kweli jimbo lilichukuliwa mkuu phares
 
Back
Top Bottom