Rigath Gachagua aanzisha chama chake

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
52,024
Reaction score
101,745
Inawezekana kukawa na chaguzi ndogo maana wabunge wa sasa wanaweza kujiuzulu especially in Mount Kenya area kwa kujiunga na Gachagua na hivyo kuwepo na ulazima wa chaguzi ndogo.

My take:
1. Ukabila, maana anatokea Mt. Kenya na inaonekana wanamuunga mkono mwenzao...Ukabila ..ethinicity
2. Inaelekea kuanzisha chama kenya ni process rahisi sana siyo kama mizengwe ya Tanzania
3. Kenya is more demoratic comapred to the rest of eastern africa countries!

---
Aliyekuwa naibu wa rais wa Kenya, Rigathi Gachagua, ambaye kwa sasa ni mkosoaji mkubwa wa aliyekuwa bosi wake rais William Ruto, baadae hivi leo anatarajiwa kuzindua chama kipya ambacho anasema kitatumika kumng’oa Ruto madarakani katika uchaguzi ujao.

Kulingana na vyanzo vya karibu na Rigathi, chama atakachokizindua kitafahamika kama Democracy Citizens Party (DCP), ambacho hata hivyo kilisajiliwa mwezi Februari mwaka huu.

Licha ya kwamba jina la chama hicho halijawekwa wazi kwa umma, waliokaribu na shughuli zake wanasema kauli mbiu ni Kazi na Haki.

Jumanne ya wiki hii, Gachagua na washirika wake waliripotiwa kukutana faragha kupanga na kuamua uongozi wa chama hicho na namna ya kuzuia uuingiliaji wa serikali.

Gachagua na washirika wake wanamtuhumu rais William Ruto kwa uongozi mbaya wakiahidi kumshinda katika uchaguzi mkuu wa 2027.

Miongoni mwa wanasiasa tajika wanaohusishwa na chama cha Rigathi ni pamoja na Kalonzo Musyoka, aliyewahi pia kuwa makamu wa rais, Martha Karua, Eugene Wamalwa na Fred Matiang’i, waliohudumu katika serikali ya Uhuru Kenyatta.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema huenda serikali ikatumia rasilimali zake kuwavuta washirika wa Rigathi serikali pamoja na kuhujumu harakati zake.
 
Kenya wana msajili wa vyama vya siasa
mbona hasikiki akitumia rungu lake kama Jaji Mutungi
 
Africa ni kichwa Cha mwenda wazimu.

Gharama za uongozi ni kubwa kuliko gharama zinazotumika kwenye maendeleo,
 
Mbowe aanzishe Chama Cha Mlima Kilimanjaro 😁

Kenya ukihama chama unahama na Ubunge wako we Mangi πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Raila si alisema kuwa Ruto hakuchaguliwa na wananchi?
 
Mbowe aanzishe Chama Cha Mlima Kilimanjaro 😁

Kenya ukihama chama unahama na Ubunge wako we Mangi πŸ˜‚πŸ˜‚
Kilimanjaro kwa sasa hakuna mtu anakubalika kama Lissu , wachaga wameshtuka walikua wanauziwa mbuzi kwenye gunia , wapo kimya tu ila maamuzi yao huwa ni magumu.
 
Demokrasia hiyo ...
 
Kenya wana msajili wa vyama vya siasa
mbona hasikiki akitumia rungu lake kama Jaji Mutungi
huenda ni kwasababu hufuatilii siasa za Kenya vya kutosha gentleman,

Anaitwa Ann Nderitu,
ni mkaks zaidi ya msajili wa vyama vya siasa yeyote Africa Masharika, na kwa sasa ameteuliwa kua miongoni mwa wajumbe wa tume ya uchaguzi Kenya IEBC, mayowe ya vyama vya siasa kama yote
 
Nimekutana na habari jamaa wamefungia Free Mason Hall wanadai kodi ya ardhi na jengo Hawa jamaa yaani
 
muwakilishi wa wananchi atakae thubutu kujiuzulu nafasi yake kwaajili ya chama cha RiGy, uhakika wa kutetea nafasi yake tena ni 0%
 
muwakilishi wa wananchi atakae thubutu kujiuzulu nafasi yake kwaajili ya chama cha RiGy, uhakika wa kutetea nafasi yake tena ni 0%
Muwage mnasoma Katiba za nchi mbalimbali

Wabunge wanaounda chama cha Gachagua wanahamia na Ubunge wao

Kenya ni next level we mnyasa πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Muwage mnasoma Katiba za nchi mbalimbali

Wabunge wanaounda chama cha Gachagua wanahamia na Ubunge wao

Kenya ni next level we mnyasa πŸ˜‚πŸ˜‚
zingatia maelezo ya mtoa hoja bila kukurupuka gentleman,
ameeleza tu iwapo muwakilishi atajiuzulu,

hata hivyo,
kwa katiba ya kenya huwezi kua muwakilishi wa wananchi wa chama A, halafu ukahubiri sera na uelekeo wa chama B.Automatically unakua umejiondoa kwenye nafasi yako
 
Kenya πŸ‡°πŸ‡ͺ siyo Tanzania bwashee

Kenya wanalinda Haiti πŸ‡­πŸ‡Ή wewe kuendesha Lori Qatar πŸ‡ΆπŸ‡¦ umefeli mtihani πŸ˜‚
 
Kenya πŸ‡°πŸ‡ͺ siyo Tanzania bwashee

Kenya wanalinda Haiti πŸ‡­πŸ‡Ή wewe kuendesha Lori Qatar πŸ‡ΆπŸ‡¦ umefeli mtihani πŸ˜‚
Upinzani wa Kenya na Tanzania ni wa kilofa sana,
eti kachama kamoja tu tena ka mount kenya pekeyake au kachadema tu kana bwekabweka na kukoromea muungano wa chama tawala wenye vyama zaidi ya 10.
huo ni ulofa wa kisiasa wa gridi ya Taifa gentleman
 
Upinzani wa Kenya na Tanzania ni wa kilofa sana,
eti kachama kamoja tu tena ka mount kenya pekeyake au kachadema tu kana bwekabweka na kukoromea muungano wa chama tawala wenye vyama zaidi ya 10.
huo ni ulofa wa kisiasa wa gridi ya Taifa gentleman
Taifa lolote huanzia kwenye Clan kwa mfano TAIFA LA ISRAEL πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…