Binadamu wote wana uwezo wa kufikiri, hata hivyo kwa makusudi au kwa sababu za kimazingira; wakati fulani mtu anaweza kutofikiri.Ikiwa kuna watu zaidi ya wawili mahali na wote wanafikiri, kimsingi hawawezi kukubaliana kwenye kila kitu na hiyo ni kanuni ya kimaumbile.Unapoona kuna watu zaidi ya wawili na wanakubaliana kwa kila kitu na kila wakati; basi ujue kwamba lazima kutakuwa na baadhi ambao wameamua kuwaachia wenzao wawasaidie kufikiri kwa niaba yao.Katika mazingira ya kutofautiana fikra katika baadhi ya mambo, na kukubaliana katika baadhi ya mambo, maendeleo huweza kupatikana.Katika mazingira ya kukubaliana kwenye kila kitu, maendeleo hayawezi kupatikana.
Pamoja na kuwa kila mtu huamini kwamba mawazo na mitizamo yake ni sahihi!, ukweli ni kwamba wakati fulani tunakuwa hatuko sahihi, au hata tunapokuwa sahihi, kunakuwa kuna watu wengine tunao wajua au tusiowajua ambao wanakuwa wako sahihi zaidi.Kwa sababu hiyo basi;Ni vyema kuwa 'a bit flexible!' ili kuruhusu akili zetu kuingiza hewa na kupokea maarifa na mawazo mapya kila inapobidi.
Kama tutaamua kuwa 'Rigid' kwenye kila kitu na kila wakati, bongo zetu haziwezi kunasa ujuzi mpya kutoka kwa watu wengine na hivyo fikra zetu zitakuwa hazina uwezo wa kustawi na mwishowe tutakuwa na mawazo yale yale wakati wote hata kama watu na mazingira yanabadilika. Tukiichagua njia hii, wakati mwingi tutajikuta tukiwa katika hali ya 'Confusion' hasa katika zama hizi ambazo watu wengi wamechagua kuwa waliberali.
kama wakati fulani huwa kuna watu hasa wasomi ambao huwa wanatuchanganya kwa hoja zao, naamini inakuwa tunachanganyikiwa kwa bahati mbaya tu! lakini sidhani kama wanakuwa na nia ya kutuchanganya.Nadhani tunachoweza kufanya; ni kuing'amua na kuitia akilini, misingi niliyoisemea hapo juu na kisha kuifanyia kazi.Tukiweza kufanya hivyo, kidogo kidogo tutakuwa tunabadili utaratibu wetu wa kufikiri na kufikiri katika utaratibu sawia.Hata hivyo kuizingatia na kuifanyia kazi misingi hii, inabakia kuwa ni suala la utashi wa mtu.