Ridhiwani akabidhi Ambulance Jimboni

Ridhiwani akabidhi Ambulance Jimboni

HAMY-D

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2011
Posts
7,146
Reaction score
3,830
WanaJF,

Moja ya vijana ambao taifa hili halina budi kuwatazama kwa jicho la tatu ni Ridhiwani Kikwete. Hii ni kwa kuwa ni kijana ambae yupo kwenye fungu la vijana 'asset' wa hii nchi na sio 'liability'.

Katika hatua ya kutimiza ahadi zake kwa wananchi wake wa jimboni Chalinze, Ridhiwani akabidhi ambulance ambayo ameahidi wakati wa kampeni kwenye hospital ya Chalinze siku ya jana.

Ahadi hii imetekelezwa kufuatia makabidhiano ya kompyuta katika shule takribani tano ambazo nazo zinapatikana katika jimbo lake hilo la Chalinze.

Aidha, mbunge huyo kijana alipohojiwa juu ya uwezo wake wa kutekeleza ahadi zake kwa kasi alieleza ripota wetu kuwa, yeye hawezi kungoja pesa za mfuko wa jimbo ili kufanya maendeleo kwa wananchi wake badala yake atajitahidi kutumia hata vyanzo vyake vya ziada ikiwemo pesa za tozo za uwakili na mapato yatokanayo na kodi ya nyumba yake ili kusukuma maendeleo jimboni kwake Chalinze.

Ndugu wanaJF, hii ndio aina ya vijana ambao hili taifa linahitaji. Sio wale wanywa viroba watembea na majeneza kutwa kucha huku wamama wajawazito wanakosa huduma bora za afya na mbunge amekazania tu, "eti mbunge sio kazi yangu kuboresha huduma ya afya, hiyo ni kazi ya serikali". Mawazo hayo yamepitwa na wakati na ndio yamefanya wakina Kafulila, Wenje, Mkosamali na yule Kiwia kupigwa chini vibaya na wananchi wao kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Tumuunge mkono Ridhiwani.

Screenshot_2015-11-30-14-07-09-1.png
 
Pesa sio za kustaafu kagawiwa fungu?

Anatumegea au za mini?


Tumuunge mkono awe waziri pia wa mambo ya nje China anapafahamu sana atakuza uhusiano
 
rich forever kwao ndo wanajiita hivyo

Hivi makongoro nyerere na ridhiwan nani tajiri
 
HAMY-D katika ubora wake......tunashukuru mkuu kwa post yako, ila muulize Riz hii Ambulance kweli inalingana na hela alizotupiga katika miaka kumi ya uongozi wa baba yake?
 
rich forever kwao ndo wanajiita hivyo

Hivi makongoro nyerere na ridhiwan nani tajiri

Hapo ndio utashangaa!Nyerere alikaa madarakani 23 yrs ila utajiri wa watoto wake ni wa kawaida,huyu mkwere miaka 10 tu ila utajiri wa wanae ni kufuru
 
Salient haulage na dili ya makontena, UDA na bandari kavu, Mkono wale lake oili, Ngada, et al.
 
Watu wanavichaa kwelikweli,riz ni asset?😀😀😀😀 utakuwa na laana!!! Huyo muuza unga ambaye ametumia madaraka ya baba yake kufanya chochote anachotaka huku akijipatia utajiri wa kutisha kwa muda mfupi ni asset? Me ni mwanaccm ila nataman riz anyongwe hata leo
 
Back
Top Bottom