Rich Mavoko anakwama wapi?

kombaME

JF-Expert Member
Aug 24, 2015
2,115
2,809
Kwa wapenzi wa mziki mzuri watakubaliana na mimi kwamba moja ya msanii aliyekuwa anatuburudisha vilivyo na kuyafanya masikio yetu yapate burudani ya kutosha ni huyu bwana mdogo, tulipokuwa tunasikia Mavoko anakwenda kutambulisha nyimbo mpya masikio yetu yalijawa na hamu kubwa kutaka kusikia safari hii amekujaje na alikuwa hatuangushi kwa kweli.

Ni mmoja kati ya wasanii ambao walitengeneza hit songs za kutosha enzi zake, kama vile; SILALI, ROHO YANGU, PACHA WANGU, MARRY ME n.k na pia amezipamba nyimbo nyingi na kuzifanya zisikilizike na zivutie masikioni mwa wengi kama lile song la KABWELA la bwana mdogo Stamina, Mavoko alilipambisha vilivyo na sauti yake kwenye chorus.Na nyinginezo nyingi.

Na hata alipoamua kujiunga na kijana mwenzake Diamond Platnumz katika label ya WCB, bado hakukosea sana japo wadau kadhaa wa mziki waliona kama amepoteza sana kuchukua uamuzi huo maana ni kama ameua upinzani ambao aliutengeneza na Platnumz, maana Ali kiba alianza kuonekana kupwaya na vita mpya mjini ikahamia kwa Mavoko na Platnumz. BTW pamoja na hayo yote bado Mavoko aliendelea kutuburudisha baada ya kutoa nyimbo kadhaa akiwa WCB kama vile KOKORO aliyeshirikiana na Platnumz, IMEBAKI STORI na SHOW ME aliyeimba na Harmonize msanii mwenza kutoka WCB.

Baada ya mgogoro ambao ukweli wa chanzo cha huo mgogoro anaujua vizuri mwenyewe Mavoko, akaamua kujitoa WCB na hapo ndipo ulipoanza mdororo wa huyu kijana, kuna nyimbo amezitoa toa lakini hajafikia hata robo ya uwezo aliouonesha mwanzo.

NINI TATIZO LA HUYU KIJANA WANABODI?
 
Kwa wapenzi wa mziki mzuri watakubaliana na mimi kwamba moja ya msanii aliyekuwa anatuburudisha vilivyo na kuyafanya masikio yetu yapate burudani ya kutosha ni huyu bwana mdogo, tulipokuwa tunasikia Mavoko anakwenda kutambulisha nyimbo mpya masikio yetu yalijawa na hamu kubwa kutaka kusikia safari hii amekujaje na alikuwa hatuangushi kwa kweli.

Ni mmoja kati ya wasanii ambao walitengeneza hit songs za kutosha enzi zake, kama vile; SILALI, ROHO YANGU, PACHA WANGU, MARRY ME n.k na pia amezipamba nyimbo nyingi na kuzifanya zisikilizike na zivutie masikioni mwa wengi kama lile song la KABWELA la bwana mdogo Stamina, Mavoko alilipambisha vilivyo na sauti yake kwenye chorus.Na nyinginezo nyingi.

Na hata alipoamua kujiunga na kijana mwenzake Diamond Platnumz katika label ya WCB, bado hakukosea sana japo wadau kadhaa wa mziki waliona kama amepoteza sana kuchukua uamuzi huo maana ni kama ameua upinzani ambao aliutengeneza na Platnumz, maana Ali kiba alianza kuonekana kupwaya na vita mpya mjini ikahamia kwa Mavoko na Platnumz. BTW pamoja na hayo yote bado Mavoko aliendelea kutuburudisha baada ya kutoa nyimbo kadhaa akiwa WCB kama vile KOKORO aliyeshirikiana na Platnumz, IMEBAKI STORI na SHOW ME aliyeimba na Harmonize msanii mwenza kutoka WCB.

Baada ya mgogoro ambao ukweli wa chanzo cha huo mgogoro anaujua vizuri mwenyewe Mavoko, akaamua kujitoa WCB na hapo ndipo ulipoanza mdororo wa huyu kijana, kuna nyimbo amezitoa toa lakini hajafikia hata robo ya uwezo aliouonesha mwanzo.

NINI TATIZO LA HUYU KIJANA WANABODI?
hivi Kings Empire nayo imeishia wapi?
 
Back
Top Bottom