RFA na Utabiri wa mrithi wa Sheikh Yahya kuhusu CCM

RFA na Utabiri wa mrithi wa Sheikh Yahya kuhusu CCM

KAMP2015

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2013
Posts
281
Reaction score
69
Leo katika taarifa ya habari ya saa nne asubuhi Radio Free Africa imetangaza kuwa Alhaj Husein ambaye ni mrithi wa sheikh Yahya amekitabiria CCM ushindi wa 90% katika chaguzi zijazo eti kutokana na migogoro inayovikumba vyama vya upinzani. My take: kama RFA imeona kwamba hii ndo habari ya maana basi nasema yafuatayo:
1. Mmezidisha Mahaba kwa CCM (Mnatukera wasikilizaji)
2. Mnaamini vitu visivyo na scientific proof (ushirikina)
Ni bora mkaripoti hata habari za Balozi wa nyumba kumi kuhusu shida za watu wake kuliko huyo mshirikina.
 
Huyu Hassan ni tapeli tu la Kinondoni....ila swali hivi cheo cha utabiri huwa kinaridhishwa ?
 
Hii redio mimi huwa naiona kama Uhuru 2.
 
Hii redio mimi nikishasikilizaga headline za magazeti huwa ndio tunaagana mpaka siku inayofuata.
 
wapo sahihi kabisa kutangaza hizo habari,nadhani mtakua mlishasahau kwamba mmiliki wake (Diallo)ni mwenyekiti wa ccm mkoa wa Mwanza,yeye ni miongoni mwa wachahe wanaoitafuna hii nchi bila huruma.
 
Hivi inakuwaje ALHAJI anajihusisha na uchawi
 
Huyu hajarithi utabiri, amerithi kazi ya Baba yake ya kutumwa na watawala kutangaza kile wanachokifikiria kukifanya ili endapo itatokea, basi umma uaminishwe kwamba ilitabiriwa. Ujinga mtupu.

Tiba
 
Nafikiri ametoa maoni yake kutokana experience ya hayo yanayotokea.!!!! Ila niaibu na fedheha kwa chombo cha habari kama hicho kuitangaza hiyo taarifa!
 
Wewe unatofautishaje alhaji na mchawi?mbona zote ni sifa za binadamu?kipi kinashindikana?

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

kwangu kidini alhaji ni mtu anaeheshimika.. na sifa ya kuitwa hivyo ni kwenda kuhiji sehemu takatifu ya MAKKA. sasa iweje ajuhusishe na ushirikina tena
 
Hivi ni yule mtoto wa Sheikh Yahya? Alitokaje gerezani kwa tuhuma nzito vile au mmesahau alichofanya? Kumbe siku hizi ni Alhaji? Ipo kazi!

nchi yetu imeshafika kugumu... Kama chombo cha habari kinarely kwenye unreliable source kutoa habari zake, basi hata rais akitabiriwa na T B Joshua, vyombo vya aina hii vitapiga debe. watch out!
 
Huyu hajarithi utabiri, amerithi kazi ya Baba yake ya kutumwa na watawala kutangaza kile wanachokifikiria kukifanya ili endapo itatokea, basi umma uaminishwe kwamba ilitabiriwa. Ujinga mtupu.

Tiba

Halafu cha kushangaza yeye ni mwanachama wa Chadema, je alipogombea udiwani pale Magomeni na kupigwa chini na mgombea wa CCM alishindwaje kujitabiria yeye mwenyewe? Mnafki hawa ndio misukule ya Zitto.
 
Marehemu baba yake Sheikh Yahaya Hussen ,aliwahi kutabiri mpira kuwa Yanga itaifunga Simba matokeo yake Simba ikaifunga Yanga,nusra Mashabiki wa Simba wamfanye kama Mabina(walitaka kumdunda)
 
Sasa huu ni utabiri au uchambuzi wa kisiasa?
 
Baba yake alitabiri kuwa atakayeshindana na Kikwete katika kuwania nafasi ua Urais atakufa mwisho wa siku AKAFA YEYE.
 
Halafu cha kushangaza yeye ni mwanachama wa Chadema, je alipogombea udiwani pale Magomeni na kupigwa chini na mgombea wa CCM alishindwaje kujitabiria yeye mwenyewe? Mnafki hawa ndio misukule ya Zitto.

Unaona ehee? Huyu hana lolote anaisafishia njia CCM ili ije iibe kura. Eti utabiri na mbona Baba yake hakujitabiria atakufa lini?

Tiba
 
Back
Top Bottom