review ya nokia lumia zinazotumia windows phone 7.5

review ya nokia lumia zinazotumia windows phone 7.5

Chief-Mkwawa

Platinum Member
Joined
May 25, 2011
Posts
32,229
Reaction score
44,261
nokia lumia ni series mpya ya simu za nokia ambazo zinatumia operating system ya windows phone. kwa sasa zipo zinazotumia windows phone 7.5 na nyengine zinatumia windows phone 8 ila kwa sasa sitazungumzia windows phone 8 kwa sababu hazijafika kwa wingi. nimepita maduka mbali mbali nimeziona simu za windows phone 7.5 nyingi tu nikaona niandae hii thread ili kuweza kuweka wazi zipoje hizi simu.





kwa kuanza kiujumla ni simu nzuri sana kwa perfomance maana zipo very fast kucompare na android na iphones sema tatizo kubwa ni kwamba zina uhaba wa application. so kama wewe si mtu wa kushughulika sana na simu unapenda simu ya kibiashara isiosumbua au matumizi ya kawaida hii ndo simu yako. pia simu hizi haziingii memory card so unapochagua phone memory uangalie na matumizi yako.





mpaka sasa nokia kwenye family yake ya windows 7.5 ana simu 6 nokia lumia 505, 510, 610, 710, 800 na 900 nitazigawanya makundi matatu ili uweze kuzielewa vizuri kuanzia kundi la chini hadi la juu.


KUNDI LA CHINI


hapa nazieka simu tatu, lumia 510, 610 na 505 hizi simu zinafanana kila kitu kasoro vitu vichache sana na ndio simu za bei rahisi kabisa za lumia. lumia 510 ikiwa na ukubwa wa screen 4 inch ikifuatiwa na lumia 610 na 505 zenye kioo 3.7 inch


nokia-lumia-505-ofic.jpg






general perfomance;


hizi simu 3 zina processor ya 800mhz ram 256mb wakati 505 na 510 zina phone memory 4gb 610 ina phone memory 8gb. kutokana na udogo wa specification battery yake ni nzuri kwa matumizi makubwa inakaa zaidi ya siku moja kwa matumizi ya nguvu na zaidi ya wiki kwa wasiotumia sana. zote utapewa 7gb free space online kwa ajili ya kuhifadhia vitu vyako. nguvu ya lumia 610 kushinda wenzake ni memory ya 8gb wakate wenzake ni 4gb. nguvu ya lumia 510 ni screen ya 4inch kucompare na wenzake 3.7. nweguvu ya lumia 505 ni camera ya 8mp compare na wenzake 5mp so hizi ndo zilivo





watu gani wanunue simu hii;


hii simu ni nzuri kwa watu wa makamo na wazee kwa sababu ya memory ndogo na ukubwa wa screen ili waone vizuri, ni nzuri kwa watu wasiopenda mambo mengi kwenye simu, wafanya biashara wanaotaka simu ya kukaa na charge, vijana wanaopenda miziki na kuangalia video fupifupi.





watu gani wasinunue simu hizi;


moja ya weakness ya simu hizi ni udogo wa processor na ram so kuna application nyingi haziingii humu utaambiwa incompatible so sitegemei vijana wa jf tuwe na simu hizi bali tununulie tu wazazi wetu tu. pia wale wanaopenda kustore vitu hizi simu sio type yao.





bei


lumia 505 na 510 sijaziona madukani lakini ni cheap kuliko 610 ila hii 610 dukani zipo laki 3 hadi 3 na nusu if ur lucky hadi 280,000 unapata.





kundi la katikati


hapa nitaziweka simu mbili lumia 710 na 800. zote hizi mbili zina award nyingi sana na naweza kusema ndio best phone za nokia of all time ukicompare price, design na perfomance.


nokia-lumia-800.jpg






general perfomance;


zote zina speed ya internet sawa 14.4mbps zinapowerfull processor ya 1.4 ghz scorpion, zote zina ram ya 512mb. lumia 800 imemzidi lumia 710 kwenye design ina curved screen, 8mp camera against 5mp, 16gb ya memory against 8gb, wakati lumia 710 amemzidi 800 interms of price.





nani anunue simu hizi;


lumia 800 kutokana na uzuri wa design yake (angalia picha juu) ni nzuri kwa wanawake, vijana wanaopenda kupendeza watu wanaopenda simu zenye perfomance kubwa na wafanyabiashara wanaotaka simu zisizosumbua. lumia 710 haina design nzuri lakini ina same perfomance ya nokia 800 ila kwa bei ya chini. so lumia 710 kwa bei na perfomance i think ndio best duniani i hope wengi msiojali umbo la simu mtaenda kwenye hii.





nani asinunue simu hizi;


wale wanaopenda kuhamisha kila kitu kwenye simu 16gb au 8gb haziwatoshi atleast 32 au 64gb zitahitajika so simu hizi haziwafai maana huwezi ongeza memory.





bei;


lumia 710 kama nilivosema kwa perfomance yake ni cheap bongo ni kama 350,000 (nokia wanauza 250,000 tamaa za wabongo) wakati lumia 800 ni around laki 4 hadi





KUNDI LA TATU


hili ndi kundi la mwisho lina simu moja tu





NOKIA LUMIA 900


hii ndo flagship ya nokia lumia zenye windows phone 7.5 ikiwa na vitu vingi vizuri zaidi ya wote bei ni around laki 6, siirecomend sana kuinunua maana kwa laki 6 unapata simu nyengine nzuri tu .


kama una tatizo lolote linalohusu nokia lumia series usisite kupost hapo chini
 
Hurecomend Lumia 900 kutokana na bei tu ama kuna critical prob na hiyo simu?
 
Hurecomend Lumia 900 kutokana na bei tu ama kuna critical prob na hiyo simu?

bei na operating system mkuu.

Nokia wamezindua simu inaitwa nokia 620 ina 8gb internal na uwezo wa memory card hadi 64 gb so total ni 72gb, ina processor s4 dual core against single core kila upande 620 imeizidi lumia 900 lakini reason sjaieka 620 ni kua inatumia windows phone 8 badala ya windows phone 7.5

hii 620 imeanzwa kuuzwa nchi kama malyasia kwa dola 269 kama laki 4 na 30 za kibongo. Nokia wenyewe wanaiuza dola 250. So ukiangalia 620 pia ni cheap so siwezi recomend 900 japo nayo ni simu nzuri
 
Kaka naomba unisaidie kwenye nokia lumia 920 na inaweza range kama ngapi kwa tanzania.naitamani sana hata kwa mil.
 
Kaka naomba unisaidie kwenye nokia lumia 920 na inaweza range kama ngapi kwa tanzania.naitamani sana hata kwa mil.

nependa sana kutumia price za india maana ndo tunafanana nazo mara nyingi kule ni dola 679 kwa change ya 1600 hapo ni kama milion 1 na elf 80 so nafkiri unaweza pata milion 1 na laki 1 kama utaagizia mtu.
 
Mkuu ninasimu ya Tecno T1 Android ni nouma aisee. Inaweza fanya v2 karibia vyote vya Samsung galaxy, kama tofauti ni ndogo mno. mf. Ina skype,inadownload video yeyote ya Youtube, double Camera, 34 GB total memory, 3.5"screen size inadownload programme yyt, ina watsapp, fb messanger, ina Office writer kama Ms-word,excel,powerpoint,adobe reader na flash player,fax appl,walls na ss zake ni sawa na zile za galaxy, ina game nyingi mno mf magari, draft nk. Inaweza kushoot picha nyingi at per mf 4,6,8 snaps pia inaflash na tochi kali sn. Ina GPS nzuri na inaweza recod mawasiliano ya mtu aliyekaribu ya mita 5(hacking). Hii simu naikubali sn. Naweza tumia internet ya simu kwenye Pc yangu pia. Mkuu unaifahamu hii simu? Je kwa uwezo huo itakuwa inalingana na ipi kati ya hizo ama nyingine? Ili nikitaka kubadili nifanye hivyo?
 
Na lumia 710 tunasumbuana sana upande wa blutooth nfanyaje,wngne wanaxema ni update kwenda wp7.8 ht km hio n solution hiw do i update,msaada plz
 
Too bad Windows Phone 7.5 hazi support USSD codes so hapo M-Pesa haito fanya kazi.
 
Yaani ni noma asa awaa jamaa kipind wanatngneza hzi cm hawakujua aya matatzo au ni makusudi,w utatoaje cm kbw hv af haisupport blututh au USSD codes
 
Msinunue Windows Phone 7,7.5 etc nunueni Windows Phone 8.

WP 7 haziwezi kuwa updated kwenda WP 8 na zinamiss feature nyingi kama USSD na Bluetooth kamili, basically ziletengenezwa fasta Microsoft kuingia market.
 
CHIEF MKWAWA Nimependa sana maelezo yako kuhusu Lumia 800 kwa Dar nitaipata wapi na kwa bei gani?
 
Na lumia 710 tunasumbuana sana upande wa blutooth nfanyaje,wngne wanaxema ni update kwenda wp7.8 ht km hio n solution hiw do i update,msaada plz

hii simu bluetooth yake sio kwa ajili ya FTP. Pitia hapa unaweza pata full specification. Nokia Lumia 710 Specifications - Nokia - UK

au hapa bluetooth in nokia lumia 710 - Nokia Support Discussions


Yaani ni noma asa awaa jamaa kipind wanatngneza hzi cm hawakujua aya matatzo au ni makusudi,w utatoaje cm kbw hv af haisupport blututh au USSD codes

sasa salio unaulizaje kama haisupport USSD!!! cdhani kama kuna cm ambayo haisupport USSD
 
1. Issue ya bluetooth ipo solved kwa lumia kwenye wp7.8 now zinasuport bluetooth

2. Yah hakuna ussd but zipo apps zinazofanya kazi kama ussd mfano emDIAL
 
Mkuu ninasimu ya Tecno T1 Android ni nouma aisee. Inaweza fanya v2 karibia vyote vya Samsung galaxy, kama tofauti ni ndogo mno. mf. Ina skype,inadownload video yeyote ya Youtube, double Camera, 34 GB total memory, 3.5"screen size inadownload programme yyt, ina watsapp, fb messanger, ina Office writer kama Ms-word,excel,powerpoint,adobe reader na flash player,fax appl,walls na ss zake ni sawa na zile za galaxy, ina game nyingi mno mf magari, draft nk. Inaweza kushoot picha nyingi at per mf 4,6,8 snaps pia inaflash na tochi kali sn. Ina GPS nzuri na inaweza recod mawasiliano ya mtu aliyekaribu ya mita 5(hacking). Hii simu naikubali sn. Naweza tumia internet ya simu kwenye Pc yangu pia. Mkuu unaifahamu hii simu? Je kwa uwezo huo itakuwa inalingana na ipi kati ya hizo ama nyingine? Ili nikitaka kubadili nifanye hivyo?

mkuu hivo vitu ulivovitaja ni features za android ambayo kila simu ya android inavyo
 
WIndows Phone 7 ilitengenezwa kwa ajili ya market ya US sana sana, ambapo watu wanalipia simu kwa contract so hakuna haja ya USSD kucheck balance na matumizi ya USSD ni madogo sana ndo maana haina. Pia jihadharini na 7.8 update nadhani Nokia tu ndo wamepromise kuleta Bluetooth file sharing.
 
Too bad Windows Phone 7.5 hazi support USSD codes so hapo M-Pesa haito fanya kazi.
Mkuu nakubaliana na wewe,ni kweli hili nalo ni tatizo kwa hizi simu zinazo-run window 7.5.Nilikua na HTC HD2 window phone niliyoi-upgrade, kwakweli ilibidi niipige chini hii window os, nikaweka android os, sasa hivi kila kitu kiko fine.
 
Mkuu nakubaliana na wewe,ni kweli hili nalo ni tatizo kwa hizi simu zinazo-run window 7.5.Nilikua na HTC HD2 window phone niliyoi-upgrade, kwakweli ilibidi niipige chini hii window os, nikaweka android os, sasa hivi kila kitu kiko fine.

Wakubwa nna samsung omnia i900 inatumia window 6.1 naweza kubadili niweke android?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Wakubwa nna samsung omnia i900 inatumia window 6.1 naweza kubadili niweke android?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
Kwa samsung omnia i900 sina hakika, ngoja tusubiri wenye kujua watoe ufafanuzi.

 
Back
Top Bottom