Mkuu SirChief, muda huwa ni mwalimu mzuri mno. Huwa tunabishana hapa na kupeana kejeli nyingi, lakini nadhani mwaka 2023 tumepata uzima ni vema tena tukaupitia huu mjadala kuhusu taifa la Uturuki.
Migogoro mikubwa duniani imethibitisha jinsi Uturuki ilivyojijenga kidiplomasia, kijeshi na kiuchumi. Hakuna mgogoro wowote ule mkubwa uliotokea Ulaya na Mashariki ya Kati ndani ya 2020-2022, taifa la Uturuki halijahusika.
Migogoro ya Nogorno-Karabakh, Ukraine, Iraq, Syria na Serbia serikali ya Uturuki imekuwa na ushawishi mkubwa kidiplomasia kuliko taifa lolote lile la NATO kwasababu za kijiografia, kihistoria na kitamaduni.
Dola la Ottoman lilifika eneo lote la Transcaucasia na Balkans, na miaka mia-moja baada ya kuanguka jamii za kituruki (Turkic People) ambazo ni waislamu utazikuta kwenye nchi kama Georgia, Azerbaijan, Armenia na Serbia/Kosovo. Taifa la Uturuki lina ushawishi mkubwa mno juu ya hizi jamii mpaka leo.
Kwenye mgogoro wa Ukraine, Uturuki kama taifa lisilofungamana na upande wowote (A Neutral State) limetumika na Urusi na NATO kama kitovu cha usafirishaji wa gesi kwenda Ulaya. Urusi siyo rafiki wa Uturuki, lakini anafahamu fika kwamba ni lazima ashirikiane naye, hasa kiuchumi kwa kuwekeza miundo-mbinu ya gesi nchini kwake ili kutanua uwanja wake wa usambazaji.
Nchi za Magharibi nazo zimefahamu kwamba Uturuki ndani ya NATO amekuwa na nguvu kubwa siyo kwasababu ni mwanachama. Lakini kwasababu za kihistoria na kijiografia ambazo ziko nje ya uwezo wa NATO, lakini bila hivyo Uturuki ingeshashughulikiwa na ingeshatolewa NATO kitambo mno.
Huu udhaifu NATO anaufahamu na Uturuki ameutumia kujipa manufaa kidiplomasia, kwa kula chakula Urusi na kulala Brussels. Muhimu pia ni kwamba Umoja wa Ulaya (EU) hauwezi kutatua migogoro mikubwa barani humo bila Uturuki, hata kama siyo mwanachama.
Ila pia tatizo la wahamiaji haramu kutoka Afrika na Mashariki ya Kati, ambako kuna migogoro mikubwa lango lake kubwa ni Uturuki.
Kule Mashariki ya Kati, nchi zenye nguvu kubwa kiushawishi ni Israel, Saudi-Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Iran na Uturuki. Kiufupi ukitaka kufanikisha chochote kwenye huu ukanda ambao umejaa mataifa ya kiislamu ni lazima uongee vizuri na ushirikiane na Iran, Saudi-Arabia, Uturuki na UAE.
Hili halijalishi wewe ni Marekani, Umoja wa Ulaya au Uchina. Huwezi kufanya lolote bila kuyashirikisha haya mataifa niliyoyataja. Ila sasa, Uturuki ni tofauti kidogo na mataifa mengine kama Iran, Saudi na UAE, kwasababu yeye ana kitu ambacho Israeli anacho: NGUVU KUBWA YA KIUSHAWISHI BARANI ULAYA kwasababu yeye ni taifa ambalo liko Mashariki ya Kati na Ulaya.
Wanazuoni wa sayansi na siasa, na mahusiano ya kimataifa kama Prof Graham T Alison, kutoka chuo cha Harvard wanasema kwenye ukanda wowote ule, yanapokuwepo mataifa mawili yenye nguvu basi tegemea mtafaruku mkubwa mno. Hili analiita The Thucydides-Trap.
Mashariki ya kati, wenye nguvu kubwa ni Uturuki na Israel. Hawa wawili watakuja kushindana mno huko mbeleni, tena katika kiwango kisicho cha kawaida. Siyo lazima wapigane kijeshi, lakini watafanyiana hujuma nyingi mno.
Mengine sitayasema, lakini miaka mingi ijayo tutashuhudia mengi mno. Tuombe uzima...
Mkuu
Consigliere tunaupitia huu uzi tena mwaka 2023, ili tujisahihishe pale ambapo tafakuri zetu zilijikwaa katika kuangalia mambo...