- hivi kwa nini mwanmke ukimwonyesha mwananume unampenda anakutesa?
- unashuri tuwe tunafanya mapenzi kwa style ipi?
- kwenye mahusiano kusamehe mwisho mara ngapi?
- je kuna fomula ya kuishi na mpenzi?
- unafanyaje kujua kama mwenzio anacheat?
Miss Chaga, natumai u mzima wa afya, niwie radhi kwa kuchelewa kuleta majibu ya maswali yako tata sana. naomba nianze
Swali: hivi kwa nini mwanamke ukimwonyesha mwananume unampenda anakutesa?
Jibu: Hapa hili suala huenda kwa pande mbili na huwa linachangiwa sana na makuzi na mazingira ya mtu alipokulia kwa mfano: Mvulana wakati anakua hakua amepata malezi yanaonyesha maisha ya upendo (amekua kwenye familia ya mfumo dume) na akiwa mtaani na wenzake ni stori hizo kuwa mwanamke akikupenda anakua amekupenda moja kwa moja sasa ili kumteka jifanye kama hujali. Sasa malezi na makuzi haya lazima yataleta mkanganyiko kidogo linapokuja suala la kuelezea hisia za mapenzi kwa mwenzake, kitu cha pili ni utashi (ego) ambayo ipo kwa watu wote pia.
Swali: unashuri tuwe tunafanya mapenzi kwa style ipi?
Hili swali linategemea zaidi uwezo na maumbile ya mwili pamoja na via vya uzazi. kuna mitindo mbalimbali ya kujamiiana na inapendeza kama utashauriana na mwenzio nakujaribu mtindo ule utakaowafaa na kuwanya mjisikie huru bila mmoja kuumia.
Swali:kwenye mahusiano kusamehe mwisho mara ngapi?
Mahusiano ni njia mbili, mmoja asimzidi mwenzake kwa kutoa, hasa kihisia. Linapokuja suala la uaminifu ambalo ni tata sana inabaki kwa mtu husika kutolea maamuzi ambayo kwake yako sawa, maamuzi haya yanategemea zaidi upande uliokosa uko tayari kwa kiasi gani kubadilika na kujitoa zaidi kwa upande uliokosa. Lakini ni vyema kuzungumza na mwenzako ili kujua tofauti na kuona kama kuna mazoea yamejijenga au mitoko imepungua, zaidi kama wote mko tayari kujaribu kuupigania uhusiano wenu, na kama hamuwezi ni bora kila mtu akashika hamsini zake.
Swali: je kuna fomula ya kuishi na mpenzi?
Ndio, formula ipo na ni rahisi sana. Kuzungumza hisia zenu na kutojaribu kubadilika, kama mlikua mnatoka basi endeleeni kutoka au kama mlikua mnanunuliana maua na hakuna sababu ya kiuchumi inayozuia endelea kufanya hivyo. Na zaidi kumbuka mapenzi ni njia mbili sio moja, penda, amini na kujiaminisha; omba msamaha kwa dhati unapokosea. Zungumza tofauti zenu bila kuingiza watu wa pembeni kwanza.
Swali:unafanyaje kujua kama mwenzio anacheat?
Tafuta PE (aaah aaah, natania), Sumaku hupungua kwa kiasi kikubwa na ule ukaribu wa mwanzo na kuaminiana kunapungua au kupotea, kama alikua anakuacha kushika simu sasa hakutakua na hiyo kitu. Lakini pia sumaku huweza kupotea kwa mambo mengine sio lazima kudanganya na kuchochoroka, ni nzuri kuongea ili mambo yawe sawa. cha msingi ni kujitahidi kuwa na uhakika kwanza kwa namna nyingi tuu.
Miss chaga, natumani nimejitahidi kujibu maswali yako kwa maelezo ya haraka, sasa tunaweza anza kudadavua sehemu zenye utata.