Rejea Halmashauri Kuu ya CCM Kubariki mkataba wa Bandari yetu, Wananchi tushikamane

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,566
41,086
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa CCM siyo baba yangu wala siyo mama yangu.

Wazazi wako, hata ukisema kuwa kuanzia leo ninyi siyo wazazi wangu, ukweli hubakia palepale kuwa hao ni wazazi wako, huna wazazi wengine zaidi ya hao. Lakini hili halipo kwa vyama vya siasa au hata serikali, vitu ambavyo tumevikuta ukubwana, tukaungana navyo kwa sababu tunakubaliana na yale ambayo vyama hivyo vimekubali kuyasimamia.

Kama unaibiwa, ukaipata taasisi inayopigania kuzuia kuibiwa, utaungana nayo, lakini mpo kwenye mapambano ya kuzuia kuibiwa, ukaja kugundua taasisi ile imekengeuka na kuungana na anayekuibia, utaendelra kuwa naye? Wakati wewe unaimba zuia wizi, taasisi inasema linda wizi kwa nguvu zako zote, bado mtaweza kusimama kwenye behewa moja?

Wapo watu ndani ya CCM wanapambana kufa na kupona kuhakikisha bandari zote za Tanganyika zinaporwa na DP.

Wapo watu ndani ya CCM wanapinga kwa sauti kubwa na ya mwisho kulinda rasilimali zetu za bandari.

Wapo watu kwenye vyama vya upinzani, wanapinga kwa nguvu zao zote uporwaji wa bandari zetu.

Lakini wapo wapinzani pia, japo siyo kwa sauti ya juu, wanaunga mkono bandari za Tanganyika kuporwa.

Wananchi tuunganishwe kwa yale tunayoyasimamia.

WanaCCM, wapinzani na wasio na vyama, wasiokubali kuporwa kwa bandari zetu, uhuru wetu na heshima ya Taifa letu, tusimame pamoja kupambania kuzuia kuporwa kwa rasilimali zetu, utu wetu, na heshima ya Taifa letu. Itikadi zetu za kivyama, kidini, kikabila, maeneo, chuki kwa mambo madogo madogo, vikae pembeni, tuunganishwe na jambo moja pekee, ULINZI WA BANDARI ZETU, ULINZI WA HESHIMA YA TAIFA LETU.

Isijalishe lengo hili linafikiwa ndani ya mwezi, mwaka au miaka kadhaa, lakini kamwe tusikubali uhuru wa kufanya maamuzi yetu uliopiganiwa tangu babu zetu akina Mkwawa, Mirambo, Isike, Chabruma, Nyerere, Kawawa, na wengine wengi, leo ufikie kikomo kwa sababu tu DP ana pesa. Leo DP akitaka eneo kuanzia ikulu ya Dar, Azania Front, St Joseph, chuo Chang'ombe; DP akisema naitaka ardhi hii, eti sisi tuitikie 'hewala, tutatekeleza'. Hili kamwe lisikubalike, hata kama ni kwa mtutu wa bunduki.

Leo tukiona DP hatufai, maslahi ya Taifa ni madogo, tukimpata mwekezaji mwingine akawekeze Tanga, eti itabidi tukamwombe DP, akisema hapana, sisi tuseme, 'tumesikia bwana mkubwa, tutatii uamuzi wako'. Kamwe tusikubali.

Tanganyika siyo pori lisilo na mwenyewe,ni nchi ambayo ina watu kamili wenye ubinadamu uliokamilika, ulio sawa na wa mwarabu aliyewageuza babu zetu kuwa bidhaa kama shanga za kuvaa shingoni.

ULINZI WA RASILIMALI ZETU, HAKUNA MJAFALA, HAKUNA WA KUTUHADAA. DAIMA TUZILINDE, NAYE MWENYE KURUHUSU UPORAJI, NI ADUI WA TAIFA LETU.

Chama chetu kikuu cha siasa kwa sasa iwe RASILIMALI ZETU.

Moto zetu itakuwa:

ZIDUMU RASILIMALI ZETU, Tuzilinde milele.

PEOPLES,
Tuzilinde rasilimali zetu.

UHURU
Ni kulinda rasilimali zetu.
 
Wale ni wasaliti...
Fikiria katika jambo hili la uporwaji wa bandari, mtuhumiwa wa kwanza ni Rais, kwa sababu ndiye sahihi yake inaonekana kwenye mkataba. Halafu huyo huyo anayetuhimiwa nfiye mqenyekiti wa kamati kui na Halmashauri kuu ya CCM. Na kwa CCM, mkubwa hakosei. Je, utatarajia lolote kutoka kwenye vyombo hivyo viwili vya maamuzi vya CCM?

Kwa muundo wa CCM, tusitarajie chochote tofauti na matakwa ya Rais kwenye kutoka kwenye vikao vyote vya maamuzi. Zaidi tutarajie uzalendo wa mwanachama mmoja mmoja lakini uamuzi wa kitaasisi.
 
Fikiria katika jambo hili la uporwaji wa bandari, mtuhumiwa wa kwanza ni Rais, kwa sababu ndiye sahihi yake inaonekana kwenye mkataba. Halafu huyo huyo anayetuhimiwa nfiye mqenyekiti wa kamati kui na Halmashauri kuu ya CCM. Na kwa CCM, mkubwa hakosei. Je, utatarajia lolote kutoka kwenye vyombo hivyo viwili vya maamuzi vya CCM?

Kwa muundo wa CCM, tusitarajie chochote tofauti na matakwa ya Rais kwenye kutoka kwenye vikao vyote vya maamuzi. Zaidi tutarajie uzalendo wa mwanachama mmoja mmoja lakini uamuzi wa kitaasisi.
pale hamna kitu. ccm wana ujinga mwingi na viburi. dawa yao ni nguvu ya umma, tatizo ni usingizi wa wananchi wetu. wamelala sana.

YESU NI KRISTO
 
Wanafahamu kabisa wametufanyia jambo la kihuni, ndio maana limewashinda kulijibu mpaka leo, matokeo yake sasa ndio wameamua kujitoa akili makusudi, wanadiriki kubariki uhuni tuliofanyiwa na mkimbizi msaliti toka Zanzibar.

Hawa wanachochea moto wenyewe, ajabu ukikolea, wanaanza kutoa vitisho kwa wakosoaji wao na kuwafundisha matumizi ya lugha, wakati wao wanaobariki uhuni waliotufanyia hatujawafundisha popote matumizi ya uhuni wao kwetu, kwenye hili wacha wajitoe akili tu, lakini ujumbe watazidi kuupata hata kama wakiziba masikio.
 
Huyu Dp world anatumika tu lakini ukweli bandari inachukuliwa na zanzibar.

Matanganyika menzetu nayo bila kutumia akili yanashadadia huu uporaji kwa mgongo wa uwekezaji.

Ni Wakati wa Watanganyika Kuilinda Tanganyika Yetu kuliko wakati Wowote.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa CCM siyo baba yangu wala siyo mama yangu.

Wazazi wako, hata ukisema kuwa kuanzia leo ninyi siyo wazazi wangu, ukweli hubakia palepale kuwa hao ni wazazi wako, huna wazazi wengine zaidi ya hao. Lakini hili halipo kwa vyama vya siasa au hata serikali, vitu ambavyo tumevikuta ukubwana, tukaungana navyo kwa sababu tunakubaliana na yale ambayo vyama hivyo vimekubali kuyasimamia.

Kama unaibiwa, ukaipata taasisi inayopigania kuzuia kuibiwa, utaungana nayo, lakini mpo kwenye mapambano ya kuzuia kuibiwa, ukaja kugundua taasisi ile imekengeuka na kuungana na anayekuibia, utaendelra kuwa naye? Wakati wewe unaimba zuia wizi, taasisi inasema linda wizi kwa nguvu zako zote, bado mtaweza kusimama kwenye behewa moja?

Wapo watu ndani ya CCM wanapambana kufa na kupona kuhakikisha bandari zote za Tanganyika zinaporwa na DP.

Wapo watu ndani ya CCM wanapinga kwa sauti kubwa na ya mwisho kulinda rasilimali zetu za bandari.

Wapo watu kwenye vyama vya upinzani, wanapinga kwa nguvu zao zote uporwaji wa bandari zetu.

Lakini wapo wapinzani pia, japo siyo kwa sauti ya juu, wanaunga mkono bandari za Tanganyika kuporwa.

Wananchi tuunganishwe kwa yale tunayoyasimamia.

WanaCCM, wapinzani na wasio na vyama, wasiokubali kuporwa kwa bandari zetu, uhuru wetu na heshima ya Taifa letu, tusimame pamoja kupambania kuzuia kuporwa kwa rasilimali zetu, utu wetu, na heshima ya Taifa letu. Itikadi zetu za kivyama, kidini, kikabila, maeneo, chuki kwa mambo madogo madogo, vikae pembeni, tuunganishwe na jambo moja pekee, ULINZI WA BANDARI ZETU, ULINZI WA HESHIMA YA TAIFA LETU.

Isijalishe lengo hili linafikiwa ndani ya mwezi, mwaka au miaka kadhaa, lakini kamwe tusikubali uhuru wa kufanya maamuzi yetu uliopiganiwa tangu babu zetu akina Mkwawa, Mirambo, Isike, Chabruma, Nyerere, Kawawa, na wengine wengi, leo ufikie kikomo kwa sababu tu DP ana pesa. Leo DP akitaka eneo kuanzia ikulu ya Dar, Azania Front, St Joseph, chuo Chang'ombe; DP akisema naitaka ardhi hii, eti sisi tuitikie 'hewala, tutatekeleza'. Hili kamwe lisikubalike, hata kama ni kwa mtutu wa bunduki.

Leo tukiona DP hatufai, maslahi ya Taifa ni madogo, tukimpata mwekezaji mwingine akawekeze Tanga, eti itabidi tukamwombe DP, akisema hapana, sisi tuseme, 'tumesikia bwana mkubwa, tutatii uamuzi wako'. Kamwe tusikubali.

Tanganyika siyo pori lisilo na mwenyewe,ni nchi ambayo ina watu kamili wenye ubinadamu uliokamilika, ulio sawa na wa mwarabu aliyewageuza babu zetu kuwa bidhaa kama shanga za kuvaa shingoni.

ULINZI WA RASILIMALI ZETU, HAKUNA MJAFALA, HAKUNA WA KUTUHADAA. DAIMA TUZILINDE, NAYE MWENYE KURUHUSU UPORAJI, NI ADUI WA TAIFA LETU.

Chama chetu kikuu cha siasa kwa sasa iwe RASILIMALI ZETU.

Moto zetu itakuwa:

ZIDUMU RASILIMALI ZETU, Tuzilinde milele.

PEOPLES,
Tuzilinde rasilimali zetu.

UHURU
Ni kulinda rasilimali zetu.
Hili andiko lako lingekuwa na maana kama ungeorodhesha mikataba yote kuanzia ile ya madini hadi Swissport pale Uwanja wa Ndege wa JKN na kutaka Watanganyika waijadili na kuipinga. Lakini kwa kitendo chako cha kuitaja DP World pekee ilhali nchi ina mikataba kibao ya kifisadi toka enzi za Mkapa inaonyesha una chuki zako binafsi na kuna lililojificha nyuma yako.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa CCM siyo baba yangu wala siyo mama yangu.

Wazazi wako, hata ukisema kuwa kuanzia leo ninyi siyo wazazi wangu, ukweli hubakia palepale kuwa hao ni wazazi wako, huna wazazi wengine zaidi ya hao. Lakini hili halipo kwa vyama vya siasa au hata serikali, vitu ambavyo tumevikuta ukubwana, tukaungana navyo kwa sababu tunakubaliana na yale ambayo vyama hivyo vimekubali kuyasimamia.

Kama unaibiwa, ukaipata taasisi inayopigania kuzuia kuibiwa, utaungana nayo, lakini mpo kwenye mapambano ya kuzuia kuibiwa, ukaja kugundua taasisi ile imekengeuka na kuungana na anayekuibia, utaendelra kuwa naye? Wakati wewe unaimba zuia wizi, taasisi inasema linda wizi kwa nguvu zako zote, bado mtaweza kusimama kwenye behewa moja?

Wapo watu ndani ya CCM wanapambana kufa na kupona kuhakikisha bandari zote za Tanganyika zinaporwa na DP.

Wapo watu ndani ya CCM wanapinga kwa sauti kubwa na ya mwisho kulinda rasilimali zetu za bandari.

Wapo watu kwenye vyama vya upinzani, wanapinga kwa nguvu zao zote uporwaji wa bandari zetu.

Lakini wapo wapinzani pia, japo siyo kwa sauti ya juu, wanaunga mkono bandari za Tanganyika kuporwa.

Wananchi tuunganishwe kwa yale tunayoyasimamia.

WanaCCM, wapinzani na wasio na vyama, wasiokubali kuporwa kwa bandari zetu, uhuru wetu na heshima ya Taifa letu, tusimame pamoja kupambania kuzuia kuporwa kwa rasilimali zetu, utu wetu, na heshima ya Taifa letu. Itikadi zetu za kivyama, kidini, kikabila, maeneo, chuki kwa mambo madogo madogo, vikae pembeni, tuunganishwe na jambo moja pekee, ULINZI WA BANDARI ZETU, ULINZI WA HESHIMA YA TAIFA LETU.

Isijalishe lengo hili linafikiwa ndani ya mwezi, mwaka au miaka kadhaa, lakini kamwe tusikubali uhuru wa kufanya maamuzi yetu uliopiganiwa tangu babu zetu akina Mkwawa, Mirambo, Isike, Chabruma, Nyerere, Kawawa, na wengine wengi, leo ufikie kikomo kwa sababu tu DP ana pesa. Leo DP akitaka eneo kuanzia ikulu ya Dar, Azania Front, St Joseph, chuo Chang'ombe; DP akisema naitaka ardhi hii, eti sisi tuitikie 'hewala, tutatekeleza'. Hili kamwe lisikubalike, hata kama ni kwa mtutu wa bunduki.

Leo tukiona DP hatufai, maslahi ya Taifa ni madogo, tukimpata mwekezaji mwingine akawekeze Tanga, eti itabidi tukamwombe DP, akisema hapana, sisi tuseme, 'tumesikia bwana mkubwa, tutatii uamuzi wako'. Kamwe tusikubali.

Tanganyika siyo pori lisilo na mwenyewe,ni nchi ambayo ina watu kamili wenye ubinadamu uliokamilika, ulio sawa na wa mwarabu aliyewageuza babu zetu kuwa bidhaa kama shanga za kuvaa shingoni.

ULINZI WA RASILIMALI ZETU, HAKUNA MJAFALA, HAKUNA WA KUTUHADAA. DAIMA TUZILINDE, NAYE MWENYE KURUHUSU UPORAJI, NI ADUI WA TAIFA LETU.

Chama chetu kikuu cha siasa kwa sasa iwe RASILIMALI ZETU.

Moto zetu itakuwa:

ZIDUMU RASILIMALI ZETU, Tuzilinde milele.

PEOPLES,
Tuzilinde rasilimali zetu.

UHURU
Ni kulinda rasilimali zetu.
Waaoo!
Hii ni mada ya maana kuwahi kutolewa!
"Uchama" ni ujinga na upumbafu unaobungua hadhi na haiba za watu hata walioonekana zamani katika jamii kuwa ni watu wa maana, lakini la uchama linawavua nguo na kuwaacha uchi!
Hivi kweli waTz wenye mrengo mmoja wa utaifa, tumeshindwa kuunganisha mawazo yetu na misimamo yetu kwa sababu ya uvyama?
Ilitakiwa tuondoe tofauti zetu za uchama, tuziweke pembeni kwanza linapokuja suala la utaifa!
 
Back
Top Bottom