Heshima sana wanajamvi,
Dr Reginald Mengi ni mmoja wa wafanyabiashara wakubwa wazawa lakini jambo la kushangaza katika kampuni zake Bonite Bottlers top management yake yote kaajiri wahindi na si watanzania wenzake wazawa.
Nimeshangaa sana majuzi nilitembelea kiwanda chake za uzalishaji wa vinywaji baridi soda wahindi wamejazana ungfikiri uko Bombay je huu ni uzalendo ?.
Dr Mengi ebu tuambie umeshindwa kuwaamini watanzania wenzako katika ajira lakini hapo hapo unataka tuendelee kunywa soda za kampuni yako /.
kUANZIA LEO NIMESUSA KUNYWA SODA ZA BONITE BOTTLERS mpaka hali ya ajira itakabotazamwa upya,fikiria stores officer ni mhindi yaani huko Machame kwenu au Marangu Kibosho vijana wamejaa kibao bila ajira wewe unakwenda kutoa ajira Punjap
Dk. Mengi haamini katika ubaguzi anaamini katika tija, Naamini kazi zilitangazwa wenye sifa husika wakachaguliwa.