tatum
JF-Expert Member
- Jan 16, 2018
- 5,786
- 4,490
Ukiamka asubuhi nchini Tanzania na kufungulia station mbalimbali za redio kitu ambacho utakuwa unasikia ni watangazi vijana wadogo wa kiume na kike kusoma habari za magezti na kuchekacheka tu huku wakileta na habari zao kiutani kila siku asubuhi.
Nimekuwa mpenzi wa kusikiliza sana Magic FM redio 92.9 kipindi cha asubuhi wakina Kawawu,Mary Edward na Kibwana Dachi bila kumsahau Salum Mkambala wakiwa wanapaka rangi na kuchambua baadhi ya habari zilizojiri jana yake na hasa anapokuwepo Kibwana Dachi huwa unapata mambo mengi sana ya maana watoto wa mjini wanasema madini
Pamoja na kusikiliza redio hiyo huwa najaribu kusikiliza redio zingine kiukweli ukiondoa TBC zingine nyingi wamekalia habari za kwenye magazeti tu mpaka haileti ile ladha ya kusikiliza redion.
Nina app moja kwenye simu yangu ambayo naweza kusikiliza redio zote za dunia hii ambazo zinatumia satelite kiukweli wenzetu wana mada nzuri sana ktk redio zao,
mfano mada za technology mbalimbali za kuvutia sana,elimu jinsi ya ufugaji wa kuku,mbuzi,nk..unaweza ukakuta wanachambua mambo magumu kabisa kuhusu Green Revolution,nuclear na atahri zake,au basi kuna vipindi za historia vizuri sana au jiografia utapata elimu kubwa sana humo na hata mambo ya afya mengi utayasikia na tamaduni.
Sijui kama kuna redio huwa zinaenda nchini ndani ndani kabisa kupata taarifa na kufanya tafiti jinsi makabila fulani wanavyoishi na mambo yao ya kimila zaidi ya TBC labda na Redio free africa kidogo.
Redio zetu ziwekeze kwenye kuelimisha jamii sio kutwa wao ni matangazo tu na habari muhimu unazisikia kwa uchache sana.
Nimekuwa mpenzi wa kusikiliza sana Magic FM redio 92.9 kipindi cha asubuhi wakina Kawawu,Mary Edward na Kibwana Dachi bila kumsahau Salum Mkambala wakiwa wanapaka rangi na kuchambua baadhi ya habari zilizojiri jana yake na hasa anapokuwepo Kibwana Dachi huwa unapata mambo mengi sana ya maana watoto wa mjini wanasema madini
Pamoja na kusikiliza redio hiyo huwa najaribu kusikiliza redio zingine kiukweli ukiondoa TBC zingine nyingi wamekalia habari za kwenye magazeti tu mpaka haileti ile ladha ya kusikiliza redion.
Nina app moja kwenye simu yangu ambayo naweza kusikiliza redio zote za dunia hii ambazo zinatumia satelite kiukweli wenzetu wana mada nzuri sana ktk redio zao,
mfano mada za technology mbalimbali za kuvutia sana,elimu jinsi ya ufugaji wa kuku,mbuzi,nk..unaweza ukakuta wanachambua mambo magumu kabisa kuhusu Green Revolution,nuclear na atahri zake,au basi kuna vipindi za historia vizuri sana au jiografia utapata elimu kubwa sana humo na hata mambo ya afya mengi utayasikia na tamaduni.
Sijui kama kuna redio huwa zinaenda nchini ndani ndani kabisa kupata taarifa na kufanya tafiti jinsi makabila fulani wanavyoishi na mambo yao ya kimila zaidi ya TBC labda na Redio free africa kidogo.
Redio zetu ziwekeze kwenye kuelimisha jamii sio kutwa wao ni matangazo tu na habari muhimu unazisikia kwa uchache sana.