Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Vin ana umachachari mwingi ila anapoingia kwenye 18 anakuwa siyo hatar...huwez kumpa hata 20% yakufunga goli akiingia kwenye 18...nakubaliana na wewe,ni either kocha abadilike au kocha aondoke yeye maana huu mfumo ni kila mtu anajichezea hakuna timu ila tuna wachezaji..

Sent from my SM-A336E using JamiiForums mobile app
 
Nilidhani angejirekebisha baada ya kufanya mambo hayo pre season ila bado hali ni ile ile., ni muda sasa Ancelloti kumwelekeza kijana kitu cha kufanya anapokuwa kwenye box la team pinzani.
Siamini kama vini ni mchezaji wa kuelekezwa kitu cha kufanya uwanjani kulingana na wakati.
Aletewe Rafael Leao ajifunze
 
Yah leo tupo uwanjani ugenini kucheza mchezo wa pili. Pasi na shaka leo ushindi ni muhimu ili kuendelea kuboost confidence ya timu.

Kila la kheri.
Game ni saa mbili na nusu usiku
Naam naam, baada ya kukosa mechi zetu nyingi, leo nipo tayari kuwashuhudia tena vijana wakisakata gozi, Tumaini ni moja tu., Ushindi
#HalaMadrid¡¡
 
Bado team haijachanganya ila kuna vitu ninaviona vizuri, upande wa kulia kuna maelewano mazuri kati ya Carvajal na Rodrygo, kati kati Toni anacheza vizuri sana na Tchouameni, Valverde ndio bado hajasomeka, huyu Fran ni mzuri sana kwenye kushambulia na ana speed nzuri tu, anaingia ndani ninadhani anajaribu kumtengenezea Vinicius nafasi kwenye wing, shida bado hawajaelewana kwenye mikimbio yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…