Kama kawaida game dhidi ya Bilbao haswa San Memes huwa inakuwa ya speed sana., kila upande unashambulia, tunacheza chini muda mwingi., ninadhani ni tahadhari kwa kuwa wana wachezaji wenye speed sana.
Vijana walijitahid kiukweli, sio mbaya sana, ningependa kuona wanajitahidi kukaa na mpira zaidi na kutengeneza nafasi kutokea kati kati, kwasababu kwasasa hatuna full back wa kufanya hiyo kazi.,
Kituo kinachofuata ni Kombe la Mfalme dhidi ya Atletico Madrid pale Bernabéu., halafu Jumapili tena hapo hapo tunawakaribisha Real Sociedad., yaani ni bampa to bampa
Ancelotti bado anawaamini Modrić na Kroos, ila kiukweli kwasasa wapo slow sana., yaani licha ya kuwa na Valverde kama ziada katika kiungo ila jamaa bado wanacheza vizuri kati kati ya uwanja., shida nyingine tuliyonayo ni kuwa na watu wachache wakati tunashambulia.!
Ceballos ameingia acha tuone kama atafanya mabadiliko yoyote pale kati kati.
Tunahitaji vijana wenye kasi kwenye kiungo., hii itatusaidia wakati wa kushambulia kuwa tutakuwa na wachezaji wengi eneo la Atletico., so option zinakuwa nyingi pia., ila hii ya kuwa wa watu wawili ama watatu wakati tunashambulia wakati huo wao wakiwa wengi itatuwia ngumu sana kupata goli.