Kijana yupo vizuri sana kiukweli, ni mtulivu akiwa na mpira na anajua afanye nini anapopata mpira, yaani anavyocheza utadhani alikuwa Madrid kwa kipndi kirefu. Ni matumaini yangu ataendelea na form hii kwa muda mrefu, Ana sehemu moja tu ya kufanyia kazi nayo ni upande wa physical fitness, hapo akisimama vyema basi atakuwa amepiga hatua kubwa sana