Tanzania ni moja nchi iliyochukua mkopo (US$ 951.00 million) ili kuboresha huduma ya maji kwa wananchi wake. Mradi huu unaogharimiwa na benki ya dunia umeshaanza kutekelezwa katika wilaya mbalimbali hapa nchini. Taarifa zilizopo ni kwamba hela hizi zimeshindwa kuonyesha matokeo yaliyotarajiwa kutokana na utekelezaji wake kuingiliwa na ufisadi. Mazingira ya ufisadi ni kama ifuatavyo.
1. Watu waliopewa tenda ya kuchimba visima virefu vya maji katika baadhi ya wilaya mfano Handeni, Babati, kibaha nk, hawakuchimba kulingana na ushauri wa kitaalamu, kwa kuchimba urefu wa mita zinazotakiwa, hivyo maji hayajaoneka! mfano sehemu ambayo wanatakiwa/walitakiwa kuchimba mita 120 wao wamechimba mita 60 au pungufu.
2. Kuna baadhi ya sehemu mtu aliyepewa tenda anajenga tanki la maji kabla maji hayajapatika, hivyo baada ya kuchimba kisima na hakuna maji tenki linakuwa hakuna kazi.
3. Baadhi ya waliokuwa wafanyakazi wa wizara ya maji walijianzishia makampuni ya kuchimba maji ambayo hayana uwezo wa kutosha. Lenge lao ni kuzengea hiyo hela. Inasemekana wengine waliacha kabisa kazi.
4. Baadhi ya tenda walipewa wanasiasa au makada (CCM) wa vyama vya siasa. Baadaye wao/yeye akaanza kutafuta mtu wa kufanya kazi kwa niaba yake.
5. Baadhi ya maeneo machache ambapo maji yamepatikana kwa bahati njema, miradi imeshindwa kukamilika kama Dare es salaam maana fedha za kumalizia hakuna.
Jana nimeona wizara ya Maji imewasilisha bajeti yake nilitegemea huu ufisadi ungeibuliwa. Tunawashauri PCCB wafanye uchunguzi wa hili jambo.
Ukitaka kufahamu zaidi kuhusu hii project soma hii link.
Projects : Water Sector Support Project*|*The World Bank
1. Watu waliopewa tenda ya kuchimba visima virefu vya maji katika baadhi ya wilaya mfano Handeni, Babati, kibaha nk, hawakuchimba kulingana na ushauri wa kitaalamu, kwa kuchimba urefu wa mita zinazotakiwa, hivyo maji hayajaoneka! mfano sehemu ambayo wanatakiwa/walitakiwa kuchimba mita 120 wao wamechimba mita 60 au pungufu.
2. Kuna baadhi ya sehemu mtu aliyepewa tenda anajenga tanki la maji kabla maji hayajapatika, hivyo baada ya kuchimba kisima na hakuna maji tenki linakuwa hakuna kazi.
3. Baadhi ya waliokuwa wafanyakazi wa wizara ya maji walijianzishia makampuni ya kuchimba maji ambayo hayana uwezo wa kutosha. Lenge lao ni kuzengea hiyo hela. Inasemekana wengine waliacha kabisa kazi.
4. Baadhi ya tenda walipewa wanasiasa au makada (CCM) wa vyama vya siasa. Baadaye wao/yeye akaanza kutafuta mtu wa kufanya kazi kwa niaba yake.
5. Baadhi ya maeneo machache ambapo maji yamepatikana kwa bahati njema, miradi imeshindwa kukamilika kama Dare es salaam maana fedha za kumalizia hakuna.
Jana nimeona wizara ya Maji imewasilisha bajeti yake nilitegemea huu ufisadi ungeibuliwa. Tunawashauri PCCB wafanye uchunguzi wa hili jambo.
Ukitaka kufahamu zaidi kuhusu hii project soma hii link.
Projects : Water Sector Support Project*|*The World Bank