Je, shilingi bilioni 350 za Benki ya Dunia mmezipeleka wapi? Zimepeperuka kwenda wapi? Nani amezitafuna?

Song of Solomon

JF-Expert Member
Aug 5, 2021
2,733
5,490
Ukiingia katika tovuti ya Benki ya Dunia utaona Serikali ya Tanzania tarehe 22 September 2022 iliwasilisha na kuomba pesa ya mradi wa Mto msimbazi.

Mradi huo Benki ya Dunia (World Bank) uliusajiliwa kwa utambulisho wa namba P169425. Unaweza kutembelea na kuona. Mtasha hataki mambo ya gizani.

Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya OR-TAMISEMI iliomba Jumla ya Kiasi cha Tsh billioni 650 kwa ajili ya mradi wa Mto msimbazi wenye madhumuni

1. Kuzuia mafuriko ya Mto Jangwani.
2. Kufanya bonde la Msimbazi kuwa na uoto wa kijani
3. Kutengeneza maeneo ya kupumzika Mto msimbazi na Jangwani
4. Kujenga Daraja la Jangwani kutoka Magomeni kwenda kariakoo
5. Kujenga kingo na sakafu ya Mto msimbazi
6. Kujaza maji na kufanya usafirishaji katika mto msimbazi.

24 November 2022 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa barabara (TANROADS) Mhandisi Rogatus H. Mativila akatangazia Dunia kuwa Serikali ya Tanzania imesainia Makubaliano na Benki ya Dunia.

Makubaliano kuhusu mradi huo na kwamba hatua za awali za kumtafuta Mkandarasi mshauri zimeanza na michoro imeshaanza kamilika na akaonyesha waandishi wa Habari michoro ya Jangwani na Mto msimbazi.

Bwana weeeee! Mvua ya mwaka huu kuanza na mafuriko kutokea tena Serikali ya CCM na watoto wa UVCCM wametugeuka kabisa kama vile siyo wale wa mwaka Jana. Leo wanasema

1. Mradi wote ni shilingi Billioni 300
2. Hawazungumzii tena shughuli zingine za mradi kama uboreshaji wa mazingira, uoto wa kijani
3. Hawazungumzii ujenzi wa kingo za Mto msimbazi
4. MWISHO anasema mama ndiyo katoa pesa (ameidhinisha) wala siyo benki ya Dunia tena.

Wakati ukiingia katika tovuti ya Benki ya Dunia inasema pesa zimeidhinishwa na Benki hiyo tangu mwaka 2022 November na mradi ulitegemewa kuishia 2028

Je, shilingi bilioni 350 za Benki ya Dunia mmezipeleka wapi? Zimepeperuka kwenda wapi? Nani amezitafuna?

Nimesikiliza mawaziri wawili, Innocent Bashungwa na Mohammed Mchengerwa wote wanazungumzia shilingi billioni 300, Vijana wa CCM na wao wamebeba gharama za mradi ni shilingi billioni 300 na zinatolewa na mama..
 
Ukiingia katika tovuti ya Benki ya Dunia utaona Serikali ya Tanzania tarehe 22 September 2022 iliwasilisha na kuomba pesa ya mradi wa Mto msimbazi...
Mpaka hapo wewe ndio umelaaniwa na jambo dogo tuu inashindwa kuelewa.

Kuomba pesa ni jambo Moja na kupisha items za kwenye andiko ni jambo jingine.

Kama items walizo clear awamu ya kwanza Zina bil.300 wewe ulitaka wataje activities zingine Kwa pesa ipi sasa?

Hujaona hata kwenye Tactic kwamba pesa iliyotoka ni Kiduchu na hivyo wamepunguza volume ya kazi?

Shule mnaendaga kufanya nini Sasa kama jambo dogo kama hili huelewi?
 
Ukiingia katika tovuti ya Benki ya Dunia utaona Serikali ya Tanzania tarehe 22 September 2022 iliwasilisha na kuomba pesa ya mradi wa Mto msimbaz...
Mkuu hawa viongozi wanaila hii nchi kwa sababu wanajua watanzania walio wengi hizi habari hawana time nazo wao wanafurahia kumwona mtu amepanda lori kwao ndio ishara ya uchapakazi na uadilifu wanasahau kuwa kaja na v8.

Hizi taarifa hawana time nazo.

Kujua mambo yanayoendelea nchi hii kuna muda unaumia unaamua uachane nayo maana wananchi wengi hawajui na hawana uelewa nayo.
 
Walishapewa viwanja mabwepande kawauza,wapambane na hali zao🤣🤣🤣
Habari ndo hiyooo
 
Ukiingia katika tovuti ya Benki ya Dunia utaona Serikali ya Tanzania tarehe 22 September 2022 iliwasilisha na kuomba pesa ya mradi wa Mto msimbazi.

Mradi huo Benki ya Dunia (World Bank) uliusajiliwa kwa utambulisho wa namba P169425. Unaweza kutembelea na kuona. Mtasha hataki mambo ya gizani.

Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya OR-TAMISEMI iliomba Jumla ya Kiasi cha Tsh billioni 650 kwa ajili ya mradi wa Mto msimbazi wenye madhumuni

1. Kuzuia mafuriko ya Mto Jangwani.
2. Kufanya bonde la Msimbazi kuwa na uoto wa kijani
3. Kutengeneza maeneo ya kupumzika Mto msimbazi na Jangwani
4. Kujenga Daraja la Jangwani kutoka Magomeni kwenda kariakoo
5. Kujenga kingo na sakafu ya Mto msimbazi
6. Kujaza maji na kufanya usafirishaji katika mto msimbazi.

24 November 2022 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa barabara (TANROADS) Mhandisi Rogatus H. Mativila akatangazia Dunia kuwa Serikali ya Tanzania imesainia Makubaliano na Benki ya Dunia.

Makubaliano kuhusu mradi huo na kwamba hatua za awali za kumtafuta Mkandarasi mshauri zimeanza na michoro imeshaanza kamilika na akaonyesha waandishi wa Habari michoro ya Jangwani na Mto msimbazi.

Bwana weeeee! Mvua ya mwaka huu kuanza na mafuriko kutokea tena Serikali ya CCM na watoto wa UVCCM wametugeuka kabisa kama vile siyo wale wa mwaka Jana. Leo wanasema

1. Mradi wote ni shilingi Billioni 300
2. Hawazungumzii tena shughuli zingine za mradi kama uboreshaji wa mazingira, uoto wa kijani
3. Hawazungumzii ujenzi wa kingo za Mto msimbazi
4. MWISHO anasema mama ndiyo katoa pesa (ameidhinisha) wala siyo benki ya Dunia tena.

Wakati ukiingia katika tovuti ya Benki ya Dunia inasema pesa zimeidhinishwa na Benki hiyo tangu mwaka 2022 November na mradi ulitegemewa kuishia 2028

Je, shilingi bilioni 350 za Benki ya Dunia mmezipeleka wapi? Zimepeperuka kwenda wapi? Nani amezitafuna?

Nimesikiliza mawaziri wawili, Innocent Bashungwa na Mohammed Mchengerwa wote wanazungumzia shilingi billioni 300, Vijana wa CCM na wao wamebeba gharama za mradi ni shilingi billioni 300 na zinatolewa na mama..
Mimi pia nimesikitika Sana kuona hivyo. Ni kichaa peke yake anaweza amini Serikali hii
 
Mpaka hapo wewe ndio umelaaniwa na jambo dogo tuu inashindwa kuelewa.

Kuomba pesa ni jambo Moja na kupisha items za kwenye andiko ni jambo jingine.

Kama items walizo clear awamu ya kwanza Zina bil.300 wewe ulitaka wataje activities zingine Kwa pesa ipi sasa?

Hujaona hata kwenye Tactic kwamba pesa iliyotoka ni Kiduchu na hivyo wamepunguza volume ya kazi?

Shule mnaendaga kufanya nini Sasa kama jambo dogo kama hili huelewi?

Tupunguze wizi. Bilioni 650 ni pesa nyingi Sana.
 
Nje kidogo ya mada
Walengwa: NDAGA UFIPA SUSA SUSA

Sio siku nyingi zimepita vilevile Mbowe nae akadai amekopesha fedha nyingi sana kwenda kwenye chama, na hivyo yuko hatihati kufilisika.

Kulingana na taarifa, kama chama waliona ili kuonrokana na kadhia hiyo basi wauze kadi za Uanachama na kuanza kampeni kabambe.

Nimesahau jina lake e bana Lucas mwashambwa, hivi iliitwa nini ile kusanya pesa?

Juzi kati yametokea mauwa hapa ya kumpamba Mwenyekiti kajenga hekalu, wakati huo huo wakiwasihi CCM wawajengee Wastaafu vijijini kwao kama alivyojenga Mh. Mbowe kijijini. Mmeku

....malizia mwenyewe

...milioni 300 zimeenda wapi?


hathivyo, tusubiri ripoti ya CAG novemba mwakani? wakati huo Tundu Lissu akiwa spika wa Bunge.
 
Shule mnaendaga kufanya nini Sasa kama jambo dogo kama hili huelewi?
Katika hili, shule yako ndiyo yenye mashaka. Hayo maelezo unayoyatoa wewe yako wapi. Kama unayafahamu wewe pekee; kwa nini usitoe ufafanuzi juu ya hilo badala ya kujifanya wewe ni mjuaji sana kuliko wengine.

Tueleze, hizo Bilioni 300 ni kwa mpango gani uliopitishwa na ni yapi yatakayo endelea baada ya hapo.

Mleta mada kajenga hoja inayo eleweka, wewe kwa ulevi wa kudhani ni mjuaji, unajirusha tu kilevilevi bila maelezo yanayojibu hoja.
Unayo matatizo wewe.
 
Tupunguze wizi. Bilioni 650 ni pesa nyingi Sana.
Kusema kweli, siyo pesa nyingi hiyo. Tukitaka sisi wenyewe kuufanya mradi huo inawezekana sana. Ni milioni kama 200 na ushee kidogo.
Sasa fikiria ni kiasi gani cha pesa kinachopotea serikalini kila mwaka. Kodi TRA wanakimbizana na machinga, mapapa ya wakwepa kodi hayasumbuliwi kabisa.

Tumekuwa watu wenye utamaduni wa kutegemea sana tufanyiwe kila kitu. Huku ni kulemaa ambako kutatufanya tuwe tegemezi milele.

Nikupe mfano: Lile bwawa kubwa la Ethiopia la kufua umeme, ambalo kila mara waMisri wanalalamika juu yake. Ethiopia waliamua kujichangisha kulijenga lile bwawa, na hatimae limekamilika.

Sijui hili letu la Mwalimu Nyerere, nalo tumekpa hela?
Lakini bila shaka Ikulu yetu ya Dodoma, na shughuli zote za kuhamia huko hatukusubiri tupate mkopo (nadhani).
Huo ndio uthubutu tunaoukosa sana ndani ya nchi yetu hii.
 
Mpaka hapo wewe ndio umelaaniwa na jambo dogo tuu inashindwa kuelewa.

Kuomba pesa ni jambo Moja na kupisha items za kwenye andiko ni jambo jingine.

Kama items walizo clear awamu ya kwanza Zina bil.300 wewe ulitaka wataje activities zingine Kwa pesa ipi sasa?

Hujaona hata kwenye Tactic kwamba pesa iliyotoka ni Kiduchu na hivyo wamepunguza volume ya kazi?

Shule mnaendaga kufanya nini Sasa kama jambo dogo kama hili huelewi?
Huyu hajaenda shule, ni mwalimu wa madrasa pale Msimbazi.....msamehe tu.
 
Back
Top Bottom