Chairman Lee
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,352
- 1,485
Wasalaaam, habarini za mchana wakuu?
Bila kupoteza muda nimeona niwashirikishe hili kwani kipindi cha mwanzo mliweza kunishauri vizuri sana, ukweli nilipenda sana ushauri wa kila mmoja wenu katika tatizo langu.
Huyu binti nilimpenda sana kama mlivyojua na nili tanabaisha hapa jamvini kuwa ananikosesha amani sana.
12/12/2020 naona ndio siku ambayo mapenzi yetu yamekwisha kwani aliweza kutamka ya moyoni japo mimi nilikuwa nafahamu nini atakacho sema, nilijaribu kumpa muda na kuvuta subira ili nione atasema nini kweli ametamka yaliyo sahihi kwake kamasintakuwa nimekosea.
Nitashare nanyi baadhi ya text zake na zangu kwa hatua zenu kama washauri wa hili swala , kwani mwanzo mliweza kunishauri vizuri na nikafuata ushauri wenu, nadhani tutafanikiwa kumaliza swala hilo wote.
Mwanamke huyu, nimejaribu kila njia chini ya jua kuwa nae baada ya kuhisi penzi letu limeingiliwa lakini imeshindikana , hasikii wala haelewi chochote , nimejidhalilisha sana kwake hata watu wengine wanashangaa ili kunusuru penzi langu lakini wapi, kama najaza maji kwenye gunia.
Nimejaribu kumshauri, kumlinda, kumuongoza kiroho na kimwili, lakini hamna kilichothaminiwa naweza nikasema hivyo, hakuna kitu sijafanya labda ambayo viko nje ya uwezo wangu lakini asilimia kuwa nimejitahidi sana.
Ili nisiwachoshe sana kutokana na uzi wangu wa mwanzo kuomba ushauri kwenu naleta mrejesho wa mwisho kwenu mpaka nilipofikia, ambapo naona ndio mwisho wa penzi langu japo roho inaniuma sana sina namna lazima nikubali matokeo.
12/12/ 2020 naona mwisho wetu hata hivyo sina kinyongo nae namtakia Maisha mema huko alikochagua kama ndio sahihi kwake, nimemwambia mimi nipo akitaka msaada wowote kwangu nipo tayari kumsaidia sina tatizo na yeye, nadhani haikuwa bahati yangu kuwa nae.
Najua hapa hayupo ila D, nakutakia maisha mema yenye furaha na amani, nimejaribu kuwa mtu mwema kwako kiasi cha kuuza na kudhalilisha utu wangu ili niwe na wewe lakini umeamua kuchagua njia yako. Mungu akubariki nashukuru kwa penzi lako nilifarijika sana na hata Mwanaume atakayekuwa na wewe atafaidi pia .
Asante kwa vyote na nadhamini mchango wako katika maisha yangu, nakupenda sana na utaendelea kuwa moyoni mwangu.
Nazileta kwenu baadhi ya text alizonitumia na niliyomjibu
Nawashukuru sana ndugu zangu kwa mchango na maoni yenu, hakika mmekuwa msaada mkubwa kwangu mpaka leo naamua kuagana na mwanamke niliyempenda katika maisha yangu .
Mungu awabariki sanaView attachment 1648854View attachment 1648856
Bila kupoteza muda nimeona niwashirikishe hili kwani kipindi cha mwanzo mliweza kunishauri vizuri sana, ukweli nilipenda sana ushauri wa kila mmoja wenu katika tatizo langu.
Huyu binti nilimpenda sana kama mlivyojua na nili tanabaisha hapa jamvini kuwa ananikosesha amani sana.
12/12/2020 naona ndio siku ambayo mapenzi yetu yamekwisha kwani aliweza kutamka ya moyoni japo mimi nilikuwa nafahamu nini atakacho sema, nilijaribu kumpa muda na kuvuta subira ili nione atasema nini kweli ametamka yaliyo sahihi kwake kamasintakuwa nimekosea.
Nitashare nanyi baadhi ya text zake na zangu kwa hatua zenu kama washauri wa hili swala , kwani mwanzo mliweza kunishauri vizuri na nikafuata ushauri wenu, nadhani tutafanikiwa kumaliza swala hilo wote.
Mwanamke huyu, nimejaribu kila njia chini ya jua kuwa nae baada ya kuhisi penzi letu limeingiliwa lakini imeshindikana , hasikii wala haelewi chochote , nimejidhalilisha sana kwake hata watu wengine wanashangaa ili kunusuru penzi langu lakini wapi, kama najaza maji kwenye gunia.
Nimejaribu kumshauri, kumlinda, kumuongoza kiroho na kimwili, lakini hamna kilichothaminiwa naweza nikasema hivyo, hakuna kitu sijafanya labda ambayo viko nje ya uwezo wangu lakini asilimia kuwa nimejitahidi sana.
Ili nisiwachoshe sana kutokana na uzi wangu wa mwanzo kuomba ushauri kwenu naleta mrejesho wa mwisho kwenu mpaka nilipofikia, ambapo naona ndio mwisho wa penzi langu japo roho inaniuma sana sina namna lazima nikubali matokeo.
12/12/ 2020 naona mwisho wetu hata hivyo sina kinyongo nae namtakia Maisha mema huko alikochagua kama ndio sahihi kwake, nimemwambia mimi nipo akitaka msaada wowote kwangu nipo tayari kumsaidia sina tatizo na yeye, nadhani haikuwa bahati yangu kuwa nae.
Najua hapa hayupo ila D, nakutakia maisha mema yenye furaha na amani, nimejaribu kuwa mtu mwema kwako kiasi cha kuuza na kudhalilisha utu wangu ili niwe na wewe lakini umeamua kuchagua njia yako. Mungu akubariki nashukuru kwa penzi lako nilifarijika sana na hata Mwanaume atakayekuwa na wewe atafaidi pia .
Asante kwa vyote na nadhamini mchango wako katika maisha yangu, nakupenda sana na utaendelea kuwa moyoni mwangu.
Nazileta kwenu baadhi ya text alizonitumia na niliyomjibu
Nawashukuru sana ndugu zangu kwa mchango na maoni yenu, hakika mmekuwa msaada mkubwa kwangu mpaka leo naamua kuagana na mwanamke niliyempenda katika maisha yangu .
Mungu awabariki sanaView attachment 1648854View attachment 1648856