Bibianna
JF-Expert Member
- Jun 6, 2025
- 400
- 135
==
Akiongea na wanahabari, Katika Sekta ya Huduma ya Maji Mijini na Vijijini, jumla ya Tshs bilioni 184.8 zimetolewa kwa ajili ya kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama, ambapo hali ya upatikanaji imeongezeka kutoka asilimia 85 hadi asilimia 93 mijini na kutoka asilimia 76 hadi asilimia 83 vijijini.
Jumla ya miradi 41 ya maji imetekelezwa, ikijumuisha miradi 23 vijijini na 18 mijini, yenye thamani ya Tshs bilioni 164.7. Miongoni mwa miradi mikubwa iliyotekelezwa ni pamoja na upanuzi wa mradi wa maji Bukoba Mjini TZS3.1bn na mradi wa maji Kyaka–Bunazi wilayani Missenyi TZS15.71bil, ambayo yote imekamilika. Miradi mingine ni ule wa Miji ya Kayanga–Omurushaka (Karagwe) wenye thamani ya TZS64.2bn na umefikia asilimia 64 ya utekelezaji, pamoja na mradi wa maji wa Kemondo (Bukoba Vijijini) ambao umetumia TZS4.57bn na umekamilika kwa asilimia 100 kwa mujibu wa mkuu wa Mkoa Jumla ya TZS 184.8bn zimetolewa kwa ajili ya miradi ya maji mkoani Kagera chini ya Rais Samia.
| Eneo | 2020 (%) | 2025 (%) | Ongezeko |
|---|---|---|---|
| Mijini | 85% | 93% | +8% |
| Vijijini | 76% | 83% | +7% |
Utekelezaji wa Miradi
- Jumla ya miradi minne (41) imetekelezwa:
- Mijini: 18 miradi
- Vijijini: 23 miradi
- Thamani ya jumla: Tshs Bilioni 164.7
Baadhi ya Miradi Mikubwa ya Maji na halzi zao,
| Mradi | Mahali | Thamani (Tshs Bil.) | Utekelezaji |
|---|---|---|---|
| Upanuzi wa mradi wa maji Bukoba Mjini | Bukoba Mjini | 3.1 | 100 |
| Mradi wa maji Kyaka – Bunazi | Missenyi | 15.71 | 100 |
| Mradi wa maji wa Miji ya Kayanga – Omurushaka | Karagwe | 64.2 | 64% |
| Mradi wa maji wa Kemondo | Bukoba Vijijini | 4.57 | 100 |