Egnecious
JF-Expert Member
- Jul 8, 2015
- 875
- 960
RC HAPI ATEMA CHECHE IRINGA
*Asema hatovumilia watendaji wazembe wanaopuuza wananchi
*Apiga marufuku ufanyaji kazi wa mazoea, majungu, fitina
* Aeleza vipaumbele vyake
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Ally Hapi jana amekutana na kufanya kikao na watendaji mbalimbali wa Mkoa wa Iringa ambapo ameeleza msimamo na muelekeo wa uongozi wake.
RC Hapi alianza kwa kuwataka watendaji wote kuchapa kazi kwa uadilifu na kutatua changamoto za wananchi kwa wakati. Hapi ameonya kuwa hatovumilia mtendaji yeyote ambaye atakua mzembe na chanzo cha kuzalisha chuki kwa wananchi dhidi ya serikali yao.
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watendaji wote kuondokana na ugonjwa wa kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kuwa wabunifu katika kuwaletea wananchi maendeleo.
"Sitakuwa na huruma na mtendaji mzembe anayesababisha serikali na Chama tawala kuchukiwa. Watendaji wa aina hii hawana nafasi katika mkoa wa Iringa. Kila mmoja lazima ahakikishe changamoto zinazohusu Idara yake anazikabili na kuzipatia majawabu."
Aidha, RC Hapi amekemea tabia ya majungu na fitina kazini na hasa kwa viongozi wapya huku akiwataka kuchapa kazi kwa kumuogopa Mungu.
"Kiongozi ukiwa mgeni mahali kitu cha kwanza unachokutana nacho ni majungu na fitina. Huyu mzuri, yule mbaya, yule hivi; kwangu mimi sitaki majungu. Ukija kwangu uje na jambo lenye ukweli na maslahi ya nchi na wana Iringa." Alisema Hapi.
Mkuu wa Mkoa alianza kwa kutembelea ofisi ya CCM Mkoa wa Iringa na baadae kukabidhiwa ofisi na aliyekua Mkuu wa Mkoa huo Amina Masenza ambapo ameeleza vipaumbele vyake kuwa ni:-
•ulinzi na usalama,
•kuimarisha ukusanyaji na udhibiti wa mapato ya serikali,
•Kilimo (ghala la taifa)
•msukumo uanzishaji wa viwanda vipya
•utatuzi wa migogoro ya ardhi
•mikopo ya vinaja na kina mama kutoka katika mapato ya halmashauri.
*Asema hatovumilia watendaji wazembe wanaopuuza wananchi
*Apiga marufuku ufanyaji kazi wa mazoea, majungu, fitina
* Aeleza vipaumbele vyake
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Ally Hapi jana amekutana na kufanya kikao na watendaji mbalimbali wa Mkoa wa Iringa ambapo ameeleza msimamo na muelekeo wa uongozi wake.
RC Hapi alianza kwa kuwataka watendaji wote kuchapa kazi kwa uadilifu na kutatua changamoto za wananchi kwa wakati. Hapi ameonya kuwa hatovumilia mtendaji yeyote ambaye atakua mzembe na chanzo cha kuzalisha chuki kwa wananchi dhidi ya serikali yao.
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watendaji wote kuondokana na ugonjwa wa kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kuwa wabunifu katika kuwaletea wananchi maendeleo.
"Sitakuwa na huruma na mtendaji mzembe anayesababisha serikali na Chama tawala kuchukiwa. Watendaji wa aina hii hawana nafasi katika mkoa wa Iringa. Kila mmoja lazima ahakikishe changamoto zinazohusu Idara yake anazikabili na kuzipatia majawabu."
Aidha, RC Hapi amekemea tabia ya majungu na fitina kazini na hasa kwa viongozi wapya huku akiwataka kuchapa kazi kwa kumuogopa Mungu.
"Kiongozi ukiwa mgeni mahali kitu cha kwanza unachokutana nacho ni majungu na fitina. Huyu mzuri, yule mbaya, yule hivi; kwangu mimi sitaki majungu. Ukija kwangu uje na jambo lenye ukweli na maslahi ya nchi na wana Iringa." Alisema Hapi.
Mkuu wa Mkoa alianza kwa kutembelea ofisi ya CCM Mkoa wa Iringa na baadae kukabidhiwa ofisi na aliyekua Mkuu wa Mkoa huo Amina Masenza ambapo ameeleza vipaumbele vyake kuwa ni:-
•ulinzi na usalama,
•kuimarisha ukusanyaji na udhibiti wa mapato ya serikali,
•Kilimo (ghala la taifa)
•msukumo uanzishaji wa viwanda vipya
•utatuzi wa migogoro ya ardhi
•mikopo ya vinaja na kina mama kutoka katika mapato ya halmashauri.