RC Gambo afiwa na dada yake

RC Gambo afiwa na dada yake

Mungu anaga upendeleo watu wengi mbona wanafiwa na ndugu zao Gambo ajikaze na pia nifundisho majivuno aliyokua nayo kwa Mungu tuanapita tu
 
pole dogo Gambo. ni njia yetu sote hiyo.
haichagui nani atangulie nani afuate.

kuna watu walitaka kumtanguliza ndugu Lissu. usijeshangaa kuona wanatangulia wao na/au ndugu zao. Mungu si Mrisho wala Daudi wala John.

kwikwikwi
 
Kwa masikitiko makubwa natangaza kifo Cha Dada yangu mpendwa Bi Mwajuma Gambo (akitoka yeye ni mimi) kilichotokea Jana tarehe 04/10/2018 kwenye Hospital ya Taifa Muhimbili Dar Es Salaam.

Mazishi yatakuwa siku ya Jumamosi tarehe 06/10/2018 Saa 6 Mchana kwenye makaburi ya MCHIKICHINI Ilala Dar Es Salaam.

Msiba upo nyumbani Kariakoo mtaa wa Mheza Karibu na Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa. Mwaka huu tumepata mtihani mwingine baada ya kumpoteza tena mama yetu mzazi. Kazi ya Mungu haina Makosa!

Mwenyezi Mungu amjalie dada yetu kauli thabiti kaburini.

View attachment 887247
Pole Gambo,,
 
Alale anapostahili...
Kila mtu apambane na hali yake
 
Mungu ibariki Tanzania, dumisha Uhuru na umoja.

Hapa kwenye umoja na Uhuru Mungu katutupa, hatuko wamoja tena, sasa tumejikwaa wapi?
 
Pole Mh Gambo kwa kufiwa na Dada.
Ni kipindi cha kujitazama na kutafakari nyendo "zenu".Hakika ukipitia comment nyingi,unaweza kujifunza kitu.
 
Kwa masikitiko makubwa natangaza kifo Cha Dada yangu mpendwa Bi Mwajuma Gambo (akitoka yeye ni mimi) kilichotokea Jana tarehe 04/10/2018 kwenye Hospital ya Taifa Muhimbili Dar Es Salaam.

POLE SANA KWA KUFIWA NA DADA YAKO. HATA HIVYO BILA KUJUA UMEJITAMBULUSHA KUWA WEWE NDIO MASIGA!! AKILI NDOGO HIYO KAKA SIKU NYINGINE UTULIE NDIO UENDE KWENYE KEYBOARD.
 
Binafsi, sio mnazi wa jinsi wanafanya siasa zao. Lakini kwa andiko lake nimejikutwa nikilengwa na mchozi. Ama kweli kifo hakichagui wa kumtoa. Ni muda muafaka wa kujitengenezea mapito mazuri hapa Duniani, ni muda mzuri wa kujirudi. Mwl wangu wa saikolojia aliwahi tuambia ukiona watu wanalia msibani, usidhani wanamlilia tu marehemu. Lasha! Wanafahamu kwamba wao ndio watafuata. Pole sana kiongozi kwa misiba mfululizo, iliyokupata. Mungu akupe nguvu ya kushinda machungu haya.
 
Kwa
Wahenga wanasema malipo ni hapa hapa Duniani,ahera kuhesabiwa tuu. Ilifika kipindi akajiona yeye ni mungu mtu hakuna lolote litakalomsumbua sio kifo wala magonjwa. Ni kipindi chake sasa cha kukaa chini na kutafakari na kutubu uovu wake wote aliowafanyia wenzake iwe kwa utashi wake au kwa maelekezo. Pole yake sana.
Una maanisha akitubu hatofiwa tena au?
Fafanua please.
 
Back
Top Bottom