RC Chalamila: Tunaweza kuwa na ‘Magufuli Ruling Party’ na mambo yakaenda vizuri kabisa

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,958
141,951
Nimeisikia hii kupitia ITV huko mkoani Mbeya wilayani Kyela.

Ngoja niitafakari kidogo hii kauli ya RC Chalamila....... Nijiridhishe alichomaanisha.

Maendeleo hayana vyama!

ALICHOJIBU RAIS:

Rais Magufuli amesema mkuu wa mkoa Albert Chalamila anatamani tuwe na mfumo wa chama kimoja lakini yeye (Dr Magufuli) matamanio yake ni kuwa na mfumo wa vyama vingi lakini CCM iendelee kupata ushindi.

Rais Magufuli Magufuli anasema katika hilo anatofautiana na Mkuu wa Mkoa na kwa maana hiyo kila mmoja wao abakie na msimamo wake.

Hongera Rais Magufuli kwa kulitolea ufafanuzi wa haraka sana swala hili!

====================

Habari zaidi kutoka kwa Mdau mwingine

Katika ziara ya Raisi inayofanyika leo hapa Kyela, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amesikika akisema "Natamani kuwe na Chama kimoja Magufuli Ruling Party".

Akifafanua kauli hiyo Mkuu wa mkoa amesema "Kila mwezi unatusaidia kuwalipa watumishi 2471 wanao lipwa zaidi ya bil.1, pesa ambazo wewe mh. raisi Magufuli unazileta katika mji wa Kyela.

Ninacho shangaa unapokuta tunaendeleza malumbano katika mazuri hayo unayoyafanya, ambayo hatuna mahali popote pakuyalinganisha. Sioni sababu ya kua na mfumo wa vyama vingi Kyela zaidi ya kua na chama kimoja kinachoitwa "Magufuli Ruling party katika mazuri"

Akijibu hoja hiyo mh: raisi amesema "Mkuu wa mkoa anatamani kuwa na chama kimoja, lakini mimi natamani kuwe na vyama vingi sana vitakavyoleta ushindani lakini siku zote Ccm ndio iwe inashinda kwasababu ni kwa mujibu wa katiba yetu".
 
Bado sina imani kama anakanusha serious.

Kama mwenyekiti wa Chama na mkuu wa nchi angekuwa tayari amekemea haya mambo juu ya subordinates wake.

Mambo mengi tu anakemea na hayazungumzwi tena.

Ila hili la utawala wa milele analikanusha kwa Kibaji, Chalamila analileta. Kuna jinsi hapa.

Itaenda hivi mwisho wa siku utasikia anasema basi wananchi wameamua niendelee japo nilikuwa sitaki, kama anavyosemaga alisukumiwa urais ata hili atasema alisukumiwa.
 
Katika ziara ya Raisi inayofanyika leo hapa Kyela, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amesikika akisema "Natamani kuwe na Chama kimoja Magufuli Ruling Party".

Akifafanua kauli hiyo Mkuu wa mkoa amesema "Kila mwezi unatusaidia kuwalipa watumishi 2471 wanao lipwa zaidi ya bil.1, pesa ambazo wewe mh. raisi Magufuli unazileta katika mji wa Kyela.

Ninacho shangaa unapokuta tunaendeleza malumbano katika mazuri hayo unayoyafanya, ambayo hatuna mahali popote pakuyalinganisha. Sioni sababu ya kua na mfumo wa vyama vingi Kyela zaidi ya kua na chama kimoja kinachoitwa "Magufuli Ruling party katika mazuri"

Akijibu hoja hiyo mh: raisi amesema "Mkuu wa mkoa anatamani kuwa na chama kimoja, lakini mimi natamani kuwe na vyama vingi sana vitakavyoleta ushindani lakini siku zote Ccm ndio iwe inashinda kwasababu ni kwa mujibu wa katiba yetu".

MY TAKE: viongozi wa Ccm acheni kujipendejeza hamumsaidii raisi wala nchi mnaharibu dhana zima ya uzalendo.
 
Nimeisikia hii kupitia ITV huko mkoani Mbeya wilayani Kyela.

Ngoja niitafakari kidogo hii kauli ya RC Chalamila....... Nijiridhishe alichomaanisha.

Maendeleo hayana vyama!

ALICHOJIBU RAIS:

Rais Magufuli amesema mkuu wa mkoa Albert Chalamila anatamani tuwe na mfumo wa chama kimoja lakini yeye (Dr Magufuli) matamanio yake ni kuwa na mfumo wa vyama vingi lakini CCM iendelee kupata ushindi.

Rais Magufuli Magufuli anasema katika hilo anatofautiana na Mkuu wa Mkoa na kwa maana hiyo kila mmoja wao abakie na msimamo wake.

Hongera Rais Magufuli kwa kulitolea ufafanuzi wa haraka sana swala hili!
Ukisikia Madaraka ya kulevya ujue ndiyo haya. Mtu keshavimbiwa madaraka hapo. Akili haina tena ushirikiano na mdomo
 
Back
Top Bottom