RC Anthony Mtaka ana sifa gani spesheli?

RC Anthony Mtaka ana sifa gani spesheli?

Lorenzo Samike

JF-Expert Member
Joined
Jun 18, 2021
Posts
1,184
Reaction score
1,914
Huyu anayeitwa Anthony Mtaka ni muda sasa nimeanza kumsikia lakini sikumtilia maanani kivile. Hata wakati wa Magufuli nilikuwa namsikia sikia tu kwamba ati ni Mkuu wa Mkoa bora. Akapewa sijui na tuzo!

Binafsi sikuwahi kumfuatilia kwa sababu sikuwahi kuvutika nae. Nilikuwa namsikia sikia tu kwa juu juu sana. Hivi majuzi alivyoteuliwa kuwa RC Dodoma nilimuona anazungumza akitoa hotuba fupi.

Kwanza ni wa kawaida sana na anaonekana ana majigambo ya ujuaji. Hata lugha yake ya mwili inaonesha anajidhania kwamba yeye ni mtaaluma na mjuvi kuliko wengine.

Jana tu hapa kamfokea Waziri wa elimu na kuyapuuza maagizo yake kwa kejeli na dhihaka. Hii kiprotokali sijui imekaaje?

Udhalilishaji wake dhidi ya Waziri umethibitisha yale yote niliyokuwa nayafikiri juu yake — Kwamba ni mjuaji juaji tu.

Na si ajabu anawalipa watu mitandaoni ili wamsifie sifie. Binafsi sioni kama ana ubora wowote au maajabu yoyote.

Kwani amefanya kitu gani hicho mpaka astahili misifa yote hiyo ninayoisikia mitandaoni kutoka kwa wafuasi wake pendwa?
 
Huwezi kumuelewa Mtaka kama umewehuka. Sifa yake ya kwanza ni muungwana na katika kuthibitisha hilo ameandika andiko lenye kuomba radhi kwa yote hayo yaliyotokea akiwa na Waziri.

Pili, juhudi za Mtaka na ufanisi wake zipo Simiyu siyo Dar, Arusha wala kwingineko, kama unataka kumjua ni nani nenda waulize Simiyu. Ndiye mkuu pekee wa mkoa enzi za JPM alipinga watu kuwekwa ndani na wakuu wa wilaya.

Haihitaji kamusi kumjua huyu jamaa.
 
Kama unahisi tunao muunga mkono huyo RC tumelipwa! Ni kwa nini na sisi tusiamini na wewe umelipwa pia kuja kumtetea huyo Waziri mwenye vyeti lukuki vya shule, huku akiwa ni bendera tu fuata upepo katika hiyo Wizara aliyo kabidhiwa?
 
Acha kuzingua JF. Mpigie - 0755300301
Huyu anayeitwa Anthony Mtaka ni muda sasa nimeanza kumsikia lakini sikumtilia maanani kivile.

Hata wakati wa Magufuli nilikuwa namsikia sikia tu kwamba ati ni Mkuu wa Mkoa bora. Akapewa sijui na tuzo!...
 
Huyu anayeitwa Anthony Mtaka ni muda sasa nimeanza kumsikia lakini sikumtilia maanani kivile.

Hata wakati wa Magufuli nilikuwa namsikia sikia tu kwamba ati ni Mkuu wa Mkoa bora. Akapewa sijui na tuzo!...
Mmeanza chokochoko wanaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom