joseph1989
JF-Expert Member
- May 4, 2014
- 15,157
- 31,738
Naona una-assume upande wa WCB, haya wa Konde kama Jembe pamoja na Mjerumani wakiwa na hisa kubwa kuliko Konde, manake umeassume mtu anapata kubwa kwa idadi ya watu, haya turudi kwenye asilimia ya Konde unajua wanagawana ngapi Konde, Jembe ni Jembe na Mjerumani.Tuweke hesabu Sawa , harmonize huwez mfananisha na Rayvanny , Kondeboy ni fighter , ashampiga gap kubwa Sana Rayvanny huo ndo ukweli , Rayvanny amelala lala Sana , kupenda mademu kupitiliza na kusahau kazi , Rayvanny anabebwa na label ya WCB anategemea mbeleko za Diamond ambaye ndo chanzo cha nguvu Kwa wasanii waliopo na waliotokea WCB but Leo hii likitokea la kutokea Mwenyezi Mungu akamchukua Diamond ndo utajua Rayvanny ni boya... Badala atumie nguvu ya mond kujitengenezea empire anabaki kubweteka na madanga ya mjini ....
Kipind cha msuguano Kati yake na Harmonize Kwenye issue ya Paula ndo ilikuwa golden chance ya yeye kutembea sambamba na Harmonize , na hata Mond alilijua Hilo ndo mana alikuwa kimya kabisa ili kumpa mileage mshikaji , mana vyombo vyote vya habar viliwamulika watu wawili vanny boy Vs Harmonize...!! Cha ajabu jamaa likaaa kimya badala ya kutembea na hyo Kiki likalala kabisa kazi kupiga picha kwenye label yake, kujilamba midomo as nothing new ,mziki hautak ulale lazima uamshe , angetumia hyo chance kuinua next level na kutoa msanii juu Kwa kutoa Ngoma Kali , angeweza kuyumbisha upepo wa Konde gang , ukimya wake ulimpa nguvu konde boy kujijenga na kujipanga kuattack WCB, japo still he is too far to match lakini matokeo yake utayaona soon believe me .... !! Rayvanny hawezi kumkimbiza Harmonize now, too late na mwenzake kajijengea ngome , Leo hii konde boy akifanya chochote kundi kubwa linammulika Kwa nguvu zote na kumpa mileage , alichobakiza Kondeboy sa hv ni kutoa hitsong na kusubir mda umpe majibu mwanana ....!!
Rayvanny anajidanganya Tu kudai et anapendwa akitoa wimbo unatembea , akiendelea na huu msimamo wake yatamkuta ya Alli Kiba ,.... Hana power yyte nje ya WCB na pia WCB now Wana mengi ya kufanya hawawezi kumpigania yeye tuuu ....!! Endorsement Hana , show zenyewe anapata moja moja , label haina msanii yyte inaendelea Kula Tu fixed cost,...
Ni kweli sportfy anaongoza monthly streams akiwa nyuma ya Diamond na akiwa amempiga Kondeboy gap la Stream 100000 per month , swali linakuja yeye vannyboy anachukua ngap na konde boy anachukua ngapi??? Ndo hapo tunasema Kondeboy anapata kikubwa kuliko vanny boy japo Rayvanny number zake zpo juu kidogo..!! Tuchukulie Mimi hapa napata 8 lakini nagawana na watu kama watatu hvi , na mwenzagu anapata 6 lakini anachukua yote hyo sita , ni Nani anapata kikubwa ??
View attachment 1866880
View attachment 1866881
View attachment 1866882
Halafu kaa ukijua Jembe ni Jembe sio fala mtoto wa mjini plus ana PhD, we jidanganye HATUOMBEI ITOKEE ila siku ikitokea wamekosana kibiashara unaweza ukakuta anachopata Vanny kikubwa kuliko Konde,sema Vanny tokea zamani hanaga tabia ya kuanika anavyo miliki.