Hatimaye baada ya Ray C kuteseka kwa muda mrefu bila kupata mtu wa kumfadhali hela ya matibabu hatimaye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ajitosa kumfadhali. Akiongea katika viwanja vya Ikulu Ray C amemshukuru Rais Kikwete kwa moyo aliouonyesha wa kumsaidia matibabu na sasa hivi anaendelea vizuri.
SWALI:
1.Rais Kikwete ametambua sasa madhara ya madawa ya kulevya, Je, atawachukulia hatua sasa wote wanauzia madawa ya kulevya maana kuna tetesi kuwa anayo majina ya DRUG DEALERS?
2. Je, ni Ray C tu mwenye aliyekumbwa na tatizo la kuwa TEJA? Watanzania wengine tena nguvu kazi kubwa ambayo imeshadhirika na madawa ya kulevya ana mpango upi wa kuwasaidia? Ama wao hawastahili msaada?
AIDHA; Nampongeza Rais Kikwete kwa moyo wake wa kumuokoa Mtanzania huyu " RAY C" maana angepotea na talent yake ya uimbaji.