Ndugu wana JF, nimekuwa nilkisikia wanafunzi wa sheria wa Tanzania Law School wakisema wana ratiba tight kuanzia asubuhi hadi mchana. Kwa upande wangu, naona utaratibu huu unawanyima nafasi ya kusoma wanafunzi wa sheria wa Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania (Open University of Tanzania - OUT) kwa vile wengi wao ni wafanyakazi na wangetaka pia kupata nafasi ya kusoma Law School ili wale wanaotaka waweze kuwa mawakili pia.
Nasema haya kwa sababu si rahisi kwa hapa Tanzania, mfanyakazi aombe likizo isiyo ya malipo miezi tisa na ajilipie ada ya chuo na mahitaji mengine ya kila siku bila kuwa kwenye ajira. Na pia sina hakika kama kuna kampuni yoyote inayoweza kukubali kumlipa mshahara mfanyakazi asiyekazini kwa muda wa miezi 9 ili asome!
Kwa nini kusiwepo utaratibu wa masomo ya jioni kuanzia mfano saa 11 hadi saa 4 usiku kulingana na mahitaji ili wale wanafunzi wa OUT nao wapate nafasi ya kwenda kwenye mafunzo ya vitendo baada ya saa zao za kazi? Au Law School ina nia ya kuwanyima wanafunzi wa sheria wa OUT wasiwe mawakili kwa vile wao watashindwa kuhudhuria hayo masomo ya vitendo muda wa asubuhi hadi mchana na hakuna njia mbadala? Naomba maoni yenu.
Nasema haya kwa sababu si rahisi kwa hapa Tanzania, mfanyakazi aombe likizo isiyo ya malipo miezi tisa na ajilipie ada ya chuo na mahitaji mengine ya kila siku bila kuwa kwenye ajira. Na pia sina hakika kama kuna kampuni yoyote inayoweza kukubali kumlipa mshahara mfanyakazi asiyekazini kwa muda wa miezi 9 ili asome!
Kwa nini kusiwepo utaratibu wa masomo ya jioni kuanzia mfano saa 11 hadi saa 4 usiku kulingana na mahitaji ili wale wanafunzi wa OUT nao wapate nafasi ya kwenda kwenye mafunzo ya vitendo baada ya saa zao za kazi? Au Law School ina nia ya kuwanyima wanafunzi wa sheria wa OUT wasiwe mawakili kwa vile wao watashindwa kuhudhuria hayo masomo ya vitendo muda wa asubuhi hadi mchana na hakuna njia mbadala? Naomba maoni yenu.