Angalia vizuri Sikonge ipo tena atarudi Tabora mara mbili na mgombea mwenza atafika huko.Hii RATIBA ina makosa. Waambie wasahihishe haraka sana. SIKONGE haipo kwenye RATIBA.
Dr Slaa uliahidi kufika SIKONGE. Hata kama hutapata kura za Wanyamwezi wenzangu, tafadhali UJE.
Inawezekana hatupo wengi, tafadhali ufike huko pia kwani sisi pia ni Watanzania.
Marais wote wamekuwa na tabia ya kuitembelea Sikonge kwenye kampeni tu.........
Usije na wewe ukafika Magogoni na ukatusahau Sikonge na sisi tukabaki na umbumbu wetu milele na milele
Wee Njoo tu hata kama kwa saa moja ukiwa juu ya Helcopiter. Unaweza kuamsha roho kadhaa zilizokata tamaa.
Angalia vizuri Sikonge ipo tena atarudi Tabora mara mbili na mgombea mwenza atafika huko.
Nimeangalia hata kwa Bwana Mapesa Bariadi haendi kamwachia mgombea mwenza, labda wana maana yao kutokwenda sehemu hizo kwa sababu huwezi kufika kila sehemu. Hebu angalia hizi sehemu hazijumuishi Sikonge.SIKONGE haipo Mkuu. Hii imenihuzunisha sana.
Nakubaliana kuwa hawezi kufika kila mahali. Ila walau kwenye WILAYA basi afike.
Nikisema aje Kijijini kwetu hapo itakuwa kweli inaleta mushkeli. Ila akifika walau Sikonge mjini basi kuna watu wengi tu watakuja kumuona na kumsikiliza Rais mtarajiwa. Akiwapa hope kuwa mambo yatakuwa mazuri wamchague na wasiendelee kusikiliza ahadi zilezile miaka nenda miaka rudi. Awaambie wenzao wanavyoendelea na wao wako nyuma saaana.
I hope watabadili ratiba ili walau aende kwa walau nusu saa. Helcopiter inaweza kwenda kwa muda mfupi na akakutana na wananchi na akiondoka hapo anaendelea na msafara wake majimbo mengine. La muhimu ni kuwa alifika na kuwaona Wa-Sikonge wakoje kabla hajawa Rais hapo Mwakani.