Rasmi Baba Levo Ajiunga na MEMKWA (TEWW)

Mhaya

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2023
Posts
2,563
Reaction score
7,321
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Mheshimiwa Clayton Revocatus Chipando maarufu kama Baba Levo , ametembelea Ofisi za Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) leo tarehe 28 Januari, 2026 Jijini Dodoma, kwa lengo la kujiunga na elimu ya Sekondari kwa njia mbadala.

Katika ziara hiyo, Mh. Chipando alipatiwa maelezo mahsusi pamoja na taratibu za kujiunga na masomo ya sekondari kupitia TEWW, na tayari amepewa control number kwa ajili ya kulipia ada ili aanze masomo yake mara moja. Hatua hiyo inaakisi dhamira yake ya kuthamini elimu kama nguzo ya maendeleo binafsi na ya jamii.

Mh. Chipando aliambatana na Mh. Asha Feruzi (MB), Mbunge wa Viti Maalum anayewakilisha vyuo na vyuo vikuu, ambaye kabla ya kuingia Bungeni alikuwa Mhadhiri Msaidizi wa TEWW.

Ikumbukwe kwamba, TEWW ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 12 ya mwaka 1975, pamoja na majukumu mengine, ikiwa na jukumu la kutoa elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi kwa rika zote, ili kuchochea maendeleo endelevu ya Watanzania.



 
Asaivi ndo wanaona umuhimu wa elim, kabla hawajaingia kwenye mfumo walikuwa wanazarau wenye elim Kwa vijisent vyao walivyokuwa wakivimiliki, ila baada ya kuingizwa kwenye mfumo ndo wanaona umuhimu wa elim, na ni Bado mammaaaae
 
Elimu aina mwisho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…