Michael Amon
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 8,775
- 3,610
Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania imeamua kutoa mfumo mpya wa elimu ambapo imetoa rasimu ya mfumo mpya wa kutoa elimu kuanzia ngazi ya chekechea mpaka ngazi ya elimu ya juu.
Katika sera hiyo mpya ya Elimu kuna mambo na mabadiliko mengi yaliyopendekezwa ikiwemo yafuatayo:
Katika rasimu hii mpya ya elimu serikali imeruhusu wanafunzi wenye uja uzito kuendelea na masomo na kufupisha muda wa elimu ya msingi kutoka miaka saba hadi sita.
Aidha sera hiyo pia inaeleza kuwa wanafunzi wa awali watasoma kutwa nzima kwa mwaka mzima na kupatiwa huduma mbali mbali zinazostahili.
Pia sera hiyo inasema kuwa wanafunzi wa shule za msingi watakuwa wakisoma kwa miaka sita ikifuatiwa na elimu ya sekondari ambayo wataisoma hadi kidato cha nne. Baada ya kusoma hadi kidato cha nne, ambacho itakuwa ni lazima kufuatiwa na elimu ya juu (Kidato cha tano na sita) ambayo itaendelea kwa miaka miwili.
Kadhalika sera hiyo inaruhusu wanafunzi wenye vipaji kupandishwa madarasa na wanafunzi wanaojifunza pole pole wataruhusiwa kurudia darasa.
Kwa upande wa lugha sera hiyo inasema kuwa wanafunzi wa elimu ya msingi na sekondari watasoma kwa lugha ya kiswahili na kiingereza
Kwa upande wa ada sera hiyo inasema kuwa gharama halisi zitakuwa msingi wa kupanga ada za taasisi ya elimu.
Katika uchangiaji wa rasimu hiyo kati ya wabunge 30 waliochangia,10 wamepinga elimu ya msingi kwa miaka sita na kutaka iwe saba au nane huku waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Dk. Shukuru Kawambwa akiahidi swala hilo kuangaliwa kiundani.
Naye mbunge wa Makete (CCM) Dk. Benelith Mahenge, alisema elimu ya msingi iwe miaka nane na ya sekondari iwe miaka mitatu huku akiituhumu Wizara ya Elimu kuwa inaua ufundi na kutolea mfano wa Ujerumani imawesaidia katika kujikita kwenye ufundi.
Uamuzi wa kuwaruhusu wanafunzi waliopata uja uzito kuendelea na masomo ulipingwa na mbunge wa Nkenge (CCM) Assumpta Mshama ambaye alisema utaleta tatizo kwa sababu watoto wataona kuwa kupata mimba ni jambo la kawaida.
Na je wewe mdau mwenzangu wa Jamii Forums The Home of great thinkers una maoni gani, mapendekezo au ushauri kuhusiana na rasimu hii mpya ya elimu?
Katika sera hiyo mpya ya Elimu kuna mambo na mabadiliko mengi yaliyopendekezwa ikiwemo yafuatayo:
Katika rasimu hii mpya ya elimu serikali imeruhusu wanafunzi wenye uja uzito kuendelea na masomo na kufupisha muda wa elimu ya msingi kutoka miaka saba hadi sita.
Aidha sera hiyo pia inaeleza kuwa wanafunzi wa awali watasoma kutwa nzima kwa mwaka mzima na kupatiwa huduma mbali mbali zinazostahili.
Pia sera hiyo inasema kuwa wanafunzi wa shule za msingi watakuwa wakisoma kwa miaka sita ikifuatiwa na elimu ya sekondari ambayo wataisoma hadi kidato cha nne. Baada ya kusoma hadi kidato cha nne, ambacho itakuwa ni lazima kufuatiwa na elimu ya juu (Kidato cha tano na sita) ambayo itaendelea kwa miaka miwili.
Kadhalika sera hiyo inaruhusu wanafunzi wenye vipaji kupandishwa madarasa na wanafunzi wanaojifunza pole pole wataruhusiwa kurudia darasa.
Kwa upande wa lugha sera hiyo inasema kuwa wanafunzi wa elimu ya msingi na sekondari watasoma kwa lugha ya kiswahili na kiingereza
Kwa upande wa ada sera hiyo inasema kuwa gharama halisi zitakuwa msingi wa kupanga ada za taasisi ya elimu.
Katika uchangiaji wa rasimu hiyo kati ya wabunge 30 waliochangia,10 wamepinga elimu ya msingi kwa miaka sita na kutaka iwe saba au nane huku waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Dk. Shukuru Kawambwa akiahidi swala hilo kuangaliwa kiundani.
Naye mbunge wa Makete (CCM) Dk. Benelith Mahenge, alisema elimu ya msingi iwe miaka nane na ya sekondari iwe miaka mitatu huku akiituhumu Wizara ya Elimu kuwa inaua ufundi na kutolea mfano wa Ujerumani imawesaidia katika kujikita kwenye ufundi.
Uamuzi wa kuwaruhusu wanafunzi waliopata uja uzito kuendelea na masomo ulipingwa na mbunge wa Nkenge (CCM) Assumpta Mshama ambaye alisema utaleta tatizo kwa sababu watoto wataona kuwa kupata mimba ni jambo la kawaida.
Na je wewe mdau mwenzangu wa Jamii Forums The Home of great thinkers una maoni gani, mapendekezo au ushauri kuhusiana na rasimu hii mpya ya elimu?