Rashidi Mfaume Kawawa: Mtetezi Wanyonge aliyekuja kuwa Waziri Mkuu Na Alhaji Abdallah Tambaza

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,915
30,259
Shajara ya Mwana Mzizima
Rashidi Mfaume Kawawa

Mtetezi Wanyonge aliyekuja kuwa Waziri Mkuu
Na Alhaji Abdallah Tambaza


RASHIDI%2BKAWAWA%2BBOOK%2BCOVER.jpg


592E64A2-E65E-4496-8ADB-CE2498F9B879.jpeg

Raia Mwema Aprili 30 - May 1, 2018

UTAWALA dhalimu wa Kikoloni wa Ulaya Ingereza hapa kwetu, ulijaa uonevu, udhalilishaji na ukandamizaji katika utoaji wake wa huduma muhimu miongoni mwa wanajamii. Raia tuliwekwa kwa madaraja ambayo Wazungu walikuwa daraja 1; Wahindi daraja II; Waarabu daraja III na Watu weusi tukawa kwenye daraja la IV la mwisho.

Miongoni mwa mateso hayo ni pamoja na watu ‘mababa majitu mazima’, kuchapwa viboko Bomani na Ma-DC na PC (wote walikuwa Wazungu wanaotisha na masharubu yao mazito) pindi inapotokea ukawa umefanya kosa la aina fulani, ambalo kwa wakubwa itabidi upigwe viboko.

Tiba, makazi pamoja na elimu, ilikuwa kwa matabaka vilevile, hata ikawa kwa sisi wananchi wenyewe kutokuwa na sehemu bora ya kuishi; tukiumwa tiba yetu ni panadol tu; kujifungua ni kienyeji nyumbani ambako wengi wa wazazi walipoteza maisha; na shule zilikuwa chache tu za ‘Kayumba’, utake usitake. Katu, haikuwezekana watu weusi kuchanganywa na Wazungu ama Wahindi kwenye elimu hata kama baba yako anao uwezo wa kukulipia ada kubwa - afadhali ilikuwapo kidogo kwa watoto wa machifu.

Watesaji wakubwa kwenye ajira walikuwa ni Wahindi wakati huo, maana wao ndio waliokuwa wakilimiliki uchumi pamoja na nyenzo zake zote kuu (maduka, viwanda, mashamba, pamoja na ajira za nyumbani). Wenyewe wakituita ‘golo’, jina ambalo maana yake pengine ni fisi, sokwe au nyani mweusi - walitudharau sana hata ni aibu kuhadithia.

Malkia wa Uingereza, pamoja na kwamba alikuwa ni mkubwa wa Kanisa Anglikana duniani, alishindwa kutuona sisi kama binadamu kama alivyo yeye na watu wa kwao; na akashindwa kutufanyia uadilifu kwa miaka yote aliyoikalia nchi yetu.

Hali ikawa mbaya sana isiyovumilika kwa Waafrika wanyonge hata ikasababisha kuwaibua watetezi wengi wa haki waje kuongoza mapambano ya kupigania haki kwenye ajira na utumishi. Miongoni mwao alikuwamo mwanaharakati wa kukumbukwa na kupigiwa mfano, hayati Rashidi Mfaume Kawawa.

Hayati Mzee Kawawa, ambaye baadaye alikuja kuwa mpaka Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa nchi hii, alikuwa ni kiongozi asiyetetereka kwenye masuala ya utetesi wa Haki za Binadamu kwenye masuala ya wafanyakazi.

Alipambana vikali sana wakati huo wa ukoloni, kwani anasifika na kukumbukwa kwa kuandaa migomo bila woga pamoja na kwamba ilipigwa marufuku na Serikali ya Kikoloni. Habari zinasema, Kawawa alikuwa na sauti na nguvu kubwa kwa jamii ya wanyonge wakati huo kiasi kwamba alichokisema yeye basi kilitekelezwa mara moja.

Aliongoza muungano wa vyama vingi vya wafanyakazi hapa nchini wakati huo kikiwemo kile cha ‘Makuli’ (wapakiaji na wapakuaji mizigo melini) wa bandarini cha Dockworkers Union 1948, Tanganyika Railways African Union, African Cooks Union na Domestic Workers Union (Chama cha Watumishi wa Majumbani)

Wakati ule, ukiacha Serikali na Railways, mwajiri mwengine mkubwa alikuwa ni Bandari ya Dar es Salaam, ambapo kazi nyingi za Waafrika pale Pwani zilikuwa za ‘daily pay’, yaani ya malipo kila siku jioni. Iliwezekana kufanya hivyo kwa sababu kazi za bandarini ni za msimu maana kuna wakati meli zinakuwa nyingi na wakati mwengine zinaadimika; hivyo watu wachache sana walikuwa na ajira za mwezi hata mwezi.

Kazi zile za Bandari zilikuwa ni za kuhatarisha maisha sana. Wengi wa watu walipata vilema ama kupoteza maisha, hivyo kufanyishwa kazi za namna ile bila mikataba stahili ulikuwa ni uonevu mkubwa sana. Hali hiyo ilisababisha migomo isiyokwisha kutoka kwa wafanyakazi kwa kule kutotendewa ipasavyo.

‘’Katika miaka ile kazi ya bandarini ilikuwa ni hatari, ikishindana na kazi ya migodi.

“Lakini bado serikali ya kikoloni ilijifanya kutoelewa ukweli kwamba Mwafrika alikuwa mwanadamu kama alivyo Mzungu Muasia au Mwarabu …Serikali ilikuwa na dhana ya ajabu na wakati mwengine ya kusikitisha kuhusu Mwafrika kama binadamu,”anaandika Mohammed Said, Uk 64 katika kitabu chake mashuhuri cha Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes, kinachosambazwa na Kampuni ya Ibn Hazm Media Center, Dar es Salaam.

Wanaharakati wawili wakubwa ndio waliojitokeza mbele zaidi katika kuwapigania na kuwatetea Waafrika wenzao wakati huo. Abdulwahid Sykes akajikita kwenye Dockworkers Union na Rashidi Kawawa akiwa zaidi kule TRAU; huku wakisaidiwa kwa karibu na watetezi wengine shupavu wakati huo kama vile Kassanga Tumbo, Michael Kamaliza, Alfred Tandau na Jacob Namfua.

Vuguvugu hizi na mwamko huu mkubwa ukazaa chombo kikubwa zaidi kilichounganisha vyama vya wafanyakazi wote wakati huo kilichojulikana kama Tanganyika Federation of Labour na Rashidi Mfaume Kawawa akawa ndiye Katibu Mkuu wa mwanzo. Chama kingine machachari wakati huo ni kile cha madereva na hasa madereva Teksi, kilichoongozwa na kada mashuhuri wa CCM, Mustapha Songambele.

Wakati hali ikiwa hivyo kwa harakati za vyama vya wafanyakazi, kwenye harakati za kudai uhuru chama cha TANU kilikuwa kikihitaji sana kuungwa mkono na kila sekta ya wazalendo wa Tanganyika wakati huo. Rashidi Kawawa, haraka akaunganisha nguvu na TANU kwa kupeleka umma wote ule wa watumishi kutoka vyama vilivyoungana na kuwa wanachama wa rasmi wa TANU.

Kwa namna ile viongozi wote wale waandamizi kutoka TFL wakachukua nafasi za juu na kuwa na sauti kwenye masuala ya ukombozi wa taifa hili. Chama cha TANU kikawa hakishikiki kutokana na chachu mpya aliyoingiza Kawawa kwenye mapambano. Huo ukawa ndio mwanzo wa Kawawa kuwa karibu na Nyerere kiasi kile.

Nilimfahamu Rashidi Mfaume Kawawa, nikiwa bado kijana mdogo kabisa kwenye miaka ya mwanzo 1950s pale alipokuwa Ofisa kwenye Idara ya Ustawi wa Jamii (Community Development Department) ya Serikali ya Kikoloni, alipokuwa akicheza filamu za vichekesho. Filamu alizocheza hayati Mzee Kawawa zilikuwa zikitupa burudani tosha sisi vijana wadogo wa wakati huo, kwani filamu zile hazikuwa za kuburudisha peke yake, lakini pia kuelimisha jamii katika masuala mbalimbali. Jina lake la kwenye sinema lilikuwa ‘Muhogo Mchungu’.

Sinema nyingine maarufu aliyoicheza Mzee Kawawa ni ile iliyojulikana kama, ‘’Mgeni Mwema,’’ ambapo kila mwanzo wa mwezi kwa jiji la Dar es Salaam zilikuwa zikionyeshwa pale viwanja vya Mnazi Mmoja, Ilala na Magomeni na baadaye kuhamia sehemu nyengine mikoani. Pamoja na sinema za Muhogo Mchungu, usiku huohuo huonyeshwa pia sinema nyingine za wale Wazungu wawili wasanii, Stan Laurel na Oliver Hardy, hapa kwetu Dar es Salaam tukiwaita ‘Chale Ndute na Chale Mbwambwambwa’, ambao vichekesho vyao kwenye zile sinema vimekuwa kivutio mpaka leo duniani kote.

Kwa sababu ambazo hazikuelezwa sawasawa mpaka leo, jamii ya Watanzania wamenyimwa nafasi ya kuburudika na uhondo wa filamu za Mzee Rashidi Kawawa - hatujui zilipo, zimevichwa kama zilivyofichwa nyaraka nyingi za historia ya muhimu ya nchi yetu.

Katika miaka ile ya 50s, nikiwa mwanafunzi pale Shule ya Msingi Mnazi Mmoja, mjini Dar es Salaam kila mara nilikuwa namwona Mzee Kawawa akirandaranda nje ya nyumba ile ndogo iliyokuwa mkabala na shule yetu akiwa ama anatoka au kuingia mle ndani kukutana na wapigania uhuru wenzake. Pale Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya CCM, ndipo yalipokuwa makao makuu ya Chama TANU wakati wa kudai uhuru.

Hayati Mzee Kawawa, wakati ule alikuwa kijana mtanashati kwelikweli; kila mara akiwa amependeza kimavazi, hasa pale alipokuwa akivaa ile migolole ya vitenge vya Afrika Magharibi, hususan kutoka Ghana na Nigeria, iliyokuwa ikipendwa na wapigania uhuru wengi sana wakati ule, akiwamo Dk Kenneth Kaunda na Harry Chipembere wa Zambia; Kanyama Chiume na Yatuta Chisiza wa Malawi; na Nyerere, Kassanga Tumbo na Michael Kamaliza wa Tanganyika.

Mtoto mkubwa wa hayati Mzee Kawawa, dadangu Rehema, nilikuwa nasoma naye darasa moja pale shuleni Mnazi Mmoja pamoja na Silas Munanka mtoto wa Mzee Bhoke Munanka. Wengine waliokuwapo pale wakati ule ni pamoja na Wendo, mtoto wa Mzee Hamza Kibwana Mwapachu, Muharrami Kilongola na Mohammed Rashid Sisso, ambao baba zao walikuwa viongozi waandamizi pale Lumumba Makao Makuu.

Sasa asubuhi moja ya mwaka 1960, nchi ikiwa ndio kwanza imepata Utawala wa Ndani (Internal Government), ambayo hata maana yake hatukuijua ni nini siku hizo; tuliiona gari nyeusi aina ya Humber yenye kibao cha namba kilichosomeka MWP, kwa maana ya Minister Without Portfolio inaingia mpaka ndani mle shuleni. Dereva akiwa amevalia sare zinazomereta kabisa akashuka kuja kumfungulia mlango abiria wake. Abiria alikuwa ni Rehema Rashidi Kawawa, ambaye sasa hakuwa mwenzetu tena, kwani babake alikuwa amechaguliwa kuwa “Waziri Asiyekuwa na Wizara Maalumu’ katika Serikali ile ya Madaraka ya Ndani.

Kwetu sisi vijana wadogo siku zile, lile lilikuwa ni tukio kubwa la kukumbukwa, kwa sababu haikupata kutokea hata siku moja pale shuleni, mwenzetu au mwalimu, akaletwa na gari mpaka ndani.

Kama vile sinema ndoto usingizini! Tulianza kuona cheche za kuelekea uhuru kamili. ‘Golo mdogo’ anakuja shule na gari la aina yake! Ule ukawa ni wakati kutafakari na kusubiri lini na sisi wengine tutahamia kwenye magorofa ya Upanga na Uhindini wanakokaa Wahindi; kwani moja ya ilani au ahadi za wanasiasa siku zile ni kwamba huru utakapopatikana, basi sisi ‘makabwela’ tutachupa kutoka raia daraja la IV hadi la kwanza.

Tumesubiri sana; na mpaka leo bado tunaendelea kusubiri siku hiyo ifike. Ni mapambano ambayo bado yanaendelea mpaka leo tumefikisha miaka zaidi ya 60 ya uhuru wetu na bado hayajafikiwa kisawasawa.

Kwa sababu ambazo mpaka leo hazijawekwa hadharani, kipande hiki cha historia yetu hakitajwi, hakiadhimishwi na wala hakienziwi hata kidogo. Nilidhani, kuwa na madaraka ya ndani lilikuwa jambo zuri sana katika safari ya kuelekea kupata uhuru kamili. Pale nchini Kenya, ambako mwandishi huyu alipata kuishi zaidi ya miaka mitano kwenye miaka ya 1970s, Sikukuu ya Madaraka Day, husherehekewa kwa shangwe, nderemo na vifijo vikubwa sana pengine kuliko hata siku ya uhuru kamili mwaka 1962.

Shermax Ngahemera, ni mhariri mwandamizi wa gazeti la Kiingereza la The African, linalochapishwa kila siku na Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, pale Sinza, Kijiweni. Siku moja wakati ilipotangazwa kwamba Rashidi Kawawa hatunaye tena hapa duniani; watu wakawa wanahaha kujaribu kumpamba na kumpembua ili wapate kuandika taazia iliyo bora kuhusu mwanamajumui yule shupavu. Shermax alisema hivi:

“Unajua huyu mzee ana mchango mkubwa sana katika kufanikisha kupatikana kwa haraka uhuru wa nchi hii pengine kuliko mtu mwengine Mwalimu, wakati fulani aliitwa na Gavana Sir Richard Turnbull na kuulizwa anafikiri lini tutakuwa tayari kujitawala ili maandalizi yaanze mara moja. Nyerere aliruka mita 100 juu akikataa kabisa kupewa uhuru kwa haraka hivyo kwa sababu nchi ilikuwa bado haina wasomi ambao wangeweza kusaidiana na Mwalimu kuendesha nchi,” anasimulia Shermax na kuendelea, ‘’ ”Siku kadhaa baadaye Nyerere aliulizwa na Kawawa juu ya safari yake kwa Gavana. Nyerere alimwambia Kawawa kwamba Gavana alikuwa anataka tumwambie kama tuko tayari kujitawala maana yeye alikuwa amechoka na anataka kurudi kwao,” amesema Shermax na kuendelea, “Nyerere alimwambia Kawawa kwamba hakutaka kupata uhuru wakati ule maana watu wa kuweza kufanya kazi nyeti za kisomi za Serikali hawakuwapo bado. Kawawa akamwambia Mwalimu akachukue nchi hata saa ile, maana tuko kwetu na kama tutaanguka basi lazima tutasimama tena. Hatuna wa kumwogopa hata kidogo. Nyerere alirudi tena kwa Gavana na kumwambia kwamba amefuta usemi wake yuko tayari kujitawala wenyewe!” alimaliza Ngahemera.

Uhuru ulipopatikana mwaka 1961, hayati Mzee Kawawa alikuwa Waziri wa Serikali za Mitaa na Maendeleo Vijijini, na ile Humber yake nyeusi iliendelea kumleta shuleni Rehema.

Habari zinasema, baada ya miezi kadhaa ya kuwa huru, hayati Mwalimu Nyerere alijiuzulu uwaziri mkuu na kumpisha Rashidi Kawawa aongoze serikali maana ni yeye aliyesema ‘tutaweza tu hatumwogopi mtu’. Mwalimu alirudi uraiani na kuzunguka nchi nzima kutafuta wasomi japo walikuwa wachache waje kuchukua nafasi kwenye serikali ifikapo 1962 tutakapokuwa Jamhuri, yaani mamlaka kamili.

Rashidi Kawawa, aliitumia vyema nafasi hii, kwani hakusita hata kidogo, pale alipoona kuna Mwafrika mwenye ujuzi wa kazi ambayo imeshikwa na Mzungu, basi mara moja alimpa mzalendo kazi hiyo. Kipindi hicho kilijulikana maarufu kama Afrikanizesheni (Africanisation). Watu wengi walipandishwa vyeo bila kutegemea. Mmoja wa watu hao alikuwa Mzee Mangara Tabu Mangara, aliyekuwa Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali (Government Printer), nafasi ambayo haikuwa inashikwa na Mwafrika kabla uhuru.

Nakumbuka pia shule za sekondari hapa jijini ambazo zikiongozwa na Wazungu siku zote wakapewa kuwa Headmasters wake akina Abdulrahman Mwalongo (Azania), Borry Lilla (Agha Khan), Rahma Mwapachu (Zanaki).

Huyo ndiye Rashidi Mfaume Kawawa; msanii wa filamu za maigizo; mtetezi wa wanyonge wakati wa ukoloni; kiongozi wa vyama vya wafanyakazi; Waziri Mkuu na Makamu wa Rais nchini; Waziri wa Ulinzi na ‘Simba wa Vita’; Mwanasiasa nguli aliyekuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa CCM.

Alamsiki!

atambaza@yahoo.com
 
Shajara ya Mwana Mzizima
Rashidi Mfaume Kawawa


Mtetezi Wanyonge aliyekuja kuwa Waziri Mkuu
Na Alhaji Abdallah Tambaza





Raia Mwema Aprili 30 - May 1, 2018

UTAWALA dhalimu wa Kikoloni wa Ulaya Ingereza hapa kwetu, ulijaa uonevu, udhalilishaji na ukandamizaji katika utoaji wake wa huduma muhimu miongoni mwa wanajamii. Raia tuliwekwa kwa madaraja ambayo Wazungu walikuwa daraja 1; Wahindi daraja II; Waarabu daraja III na Watu weusi tukawa kwenye daraja la IV la mwisho.

Miongoni mwa mateso hayo ni pamoja na watu ‘mababa majitu mazima’, kuchapwa viboko Bomani na Ma-DC na PC (wote walikuwa Wazungu wanaotisha na masharubu yao mazito) pindi inapotokea ukawa umefanya kosa la aina fulani, ambalo kwa wakubwa itabidi upigwe viboko.

Tiba, makazi pamoja na elimu, ilikuwa kwa matabaka vilevile, hata ikawa kwa sisi wananchi wenyewe kutokuwa na sehemu bora ya kuishi; tukiumwa tiba yetu ni panadol tu; kujifungua ni kienyeji nyumbani ambako wengi wa wazazi walipoteza maisha; na shule zilikuwa chache tu za ‘Kayumba’, utake usitake. Katu, haikuwezekana watu weusi kuchanganywa na Wazungu ama Wahindi kwenye elimu hata kama baba yako anao uwezo wa kukulipia ada kubwa - afadhali ilikuwapo kidogo kwa watoto wa machifu.

Watesaji wakubwa kwenye ajira walikuwa ni Wahindi wakati huo, maana wao ndio waliokuwa wakilimiliki uchumi pamoja na nyenzo zake zote kuu (maduka, viwanda, mashamba, pamoja na ajira za nyumbani). Wenyewe wakituita ‘golo’, jina ambalo maana yake pengine ni fisi, sokwe au nyani mweusi - walitudharau sana hata ni aibu kuhadithia.

Malkia wa Uingereza, pamoja na kwamba alikuwa ni mkubwa wa Kanisa Anglikana duniani, alishindwa kutuona sisi kama binadamu kama alivyo yeye na watu wa kwao; na akashindwa kutufanyia uadilifu kwa miaka yote aliyoikalia nchi yetu.

Hali ikawa mbaya sana isiyovumilika kwa Waafrika wanyonge hata ikasababisha kuwaibua watetezi wengi wa haki waje kuongoza mapambano ya kupigania haki kwenye ajira na utumishi. Miongoni mwao alikuwamo mwanaharakati wa kukumbukwa na kupigiwa mfano, hayati Rashidi Mfaume Kawawa.

Hayati Mzee Kawawa, ambaye baadaye alikuja kuwa mpaka Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa nchi hii, alikuwa ni kiongozi asiyetetereka kwenye masuala ya utetesi wa Haki za Binadamu kwenye masuala ya wafanyakazi.

Alipambana vikali sana wakati huo wa ukoloni, kwani anasifika na kukumbukwa kwa kuandaa migomo bila woga pamoja na kwamba ilipigwa marufuku na Serikali ya Kikoloni. Habari zinasema, Kawawa alikuwa na sauti na nguvu kubwa kwa jamii ya wanyonge wakati huo kiasi kwamba alichokisema yeye basi kilitekelezwa mara moja.

Aliongoza muungano wa vyama vingi vya wafanyakazi hapa nchini wakati huo kikiwemo kile cha ‘Makuli’ (wapakiaji na wapakuaji mizigo melini) wa bandarini cha Dockworkers Union 1948, Tanganyika Railways African Union, African Cooks Union na Domestic Workers Union (Chama cha Watumishi wa Majumbani)

Wakati ule, ukiacha Serikali na Railways, mwajiri mwengine mkubwa alikuwa ni Bandari ya Dar es Salaam, ambapo kazi nyingi za Waafrika pale Pwani zilikuwa za ‘daily pay’, yaani ya malipo kila siku jioni. Iliwezekana kufanya hivyo kwa sababu kazi za bandarini ni za msimu maana kuna wakati meli zinakuwa nyingi na wakati mwengine zinaadimika; hivyo watu wachache sana walikuwa na ajira za mwezi hata mwezi.

Kazi zile za Bandari zilikuwa ni za kuhatarisha maisha sana. Wengi wa watu walipata vilema ama kupoteza maisha, hivyo kufanyishwa kazi za namna ile bila mikataba stahili ulikuwa ni uonevu mkubwa sana. Hali hiyo ilisababisha migomo isiyokwisha kutoka kwa wafanyakazi kwa kule kutotendewa ipasavyo.

‘’Katika miaka ile kazi ya bandarini ilikuwa ni hatari, ikishindana na kazi ya migodi.

“Lakini bado serikali ya kikoloni ilijifanya kutoelewa ukweli kwamba Mwafrika alikuwa mwanadamu kama alivyo Mzungu Muasia au Mwarabu …Serikali ilikuwa na dhana ya ajabu na wakati mwengine ya kusikitisha kuhusu Mwafrika kama binadamu,”anaandika Mohammed Said, Uk 64 katika kitabu chake mashuhuri cha Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes, kinachosambazwa na Kampuni ya Ibn Hazm Media Center, Dar es Salaam.

Wanaharakati wawili wakubwa ndio waliojitokeza mbele zaidi katika kuwapigania na kuwatetea Waafrika wenzao wakati huo. Abdulwahid Sykes akajikita kwenye Dockworkers Union na Rashidi Kawawa akiwa zaidi kule TRAU; huku wakisaidiwa kwa karibu na watetezi wengine shupavu wakati huo kama vile Kassanga Tumbo, Michael Kamaliza, Alfred Tandau na Jacob Namfua.

Vuguvugu hizi na mwamko huu mkubwa ukazaa chombo kikubwa zaidi kilichounganisha vyama vya wafanyakazi wote wakati huo kilichojulikana kama Tanganyika Federation of Labour na Rashidi Mfaume Kawawa akawa ndiye Katibu Mkuu wa mwanzo. Chama kingine machachari wakati huo ni kile cha madereva na hasa madereva Teksi, kilichoongozwa na kada mashuhuri wa CCM, Mustapha Songambele.

Wakati hali ikiwa hivyo kwa harakati za vyama vya wafanyakazi, kwenye harakati za kudai uhuru chama cha TANU kilikuwa kikihitaji sana kuungwa mkono na kila sekta ya wazalendo wa Tanganyika wakati huo. Rashidi Kawawa, haraka akaunganisha nguvu na TANU kwa kupeleka umma wote ule wa watumishi kutoka vyama vilivyoungana na kuwa wanachama wa rasmi wa TANU.

Kwa namna ile viongozi wote wale waandamizi kutoka TFL wakachukua nafasi za juu na kuwa na sauti kwenye masuala ya ukombozi wa taifa hili. Chama cha TANU kikawa hakishikiki kutokana na chachu mpya aliyoingiza Kawawa kwenye mapambano. Huo ukawa ndio mwanzo wa Kawawa kuwa karibu na Nyerere kiasi kile.

Nilimfahamu Rashidi Mfaume Kawawa, nikiwa bado kijana mdogo kabisa kwenye miaka ya mwanzo 1950s pale alipokuwa Ofisa kwenye Idara ya Ustawi wa Jamii (Community Development Department) ya Serikali ya Kikoloni, alipokuwa akicheza filamu za vichekesho. Filamu alizocheza hayati Mzee Kawawa zilikuwa zikitupa burudani tosha sisi vijana wadogo wa wakati huo, kwani filamu zile hazikuwa za kuburudisha peke yake, lakini pia kuelimisha jamii katika masuala mbalimbali. Jina lake la kwenye sinema lilikuwa ‘Muhogo Mchungu’.

Sinema nyingine maarufu aliyoicheza Mzee Kawawa ni ile iliyojulikana kama, ‘’Mgeni Mwema,’’ ambapo kila mwanzo wa mwezi kwa jiji la Dar es Salaam zilikuwa zikionyeshwa pale viwanja vya Mnazi Mmoja, Ilala na Magomeni na baadaye kuhamia sehemu nyengine mikoani. Pamoja na sinema za Muhogo Mchungu, usiku huohuo huonyeshwa pia sinema nyingine za wale Wazungu wawili wasanii, Stan Laurel na Oliver Hardy, hapa kwetu Dar es Salaam tukiwaita ‘Chale Ndute na Chale Mbwambwambwa’, ambao vichekesho vyao kwenye zile sinema vimekuwa kivutio mpaka leo duniani kote.

Kwa sababu ambazo hazikuelezwa sawasawa mpaka leo, jamii ya Watanzania wamenyimwa nafasi ya kuburudika na uhondo wa filamu za Mzee Rashidi Kawawa - hatujui zilipo, zimevichwa kama zilivyofichwa nyaraka nyingi za historia ya muhimu ya nchi yetu.

Katika miaka ile ya 50s, nikiwa mwanafunzi pale Shule ya Msingi Mnazi Mmoja, mjini Dar es Salaam kila mara nilikuwa namwona Mzee Kawawa akirandaranda nje ya nyumba ile ndogo iliyokuwa mkabala na shule yetu akiwa ama anatoka au kuingia mle ndani kukutana na wapigania uhuru wenzake. Pale Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya CCM, ndipo yalipokuwa makao makuu ya Chama TANU wakati wa kudai uhuru.

Hayati Mzee Kawawa, wakati ule alikuwa kijana mtanashati kwelikweli; kila mara akiwa amependeza kimavazi, hasa pale alipokuwa akivaa ile migolole ya vitenge vya Afrika Magharibi, hususan kutoka Ghana na Nigeria, iliyokuwa ikipendwa na wapigania uhuru wengi sana wakati ule, akiwamo Dk Kenneth Kaunda na Harry Chipembere wa Zambia; Kanyama Chiume na Yatuta Chisiza wa Malawi; na Nyerere, Kassanga Tumbo na Michael Kamaliza wa Tanganyika.

Mtoto mkubwa wa hayati Mzee Kawawa, dadangu Rehema, nilikuwa nasoma naye darasa moja pale shuleni Mnazi Mmoja pamoja na Silas Munanka mtoto wa Mzee Bhoke Munanka. Wengine waliokuwapo pale wakati ule ni pamoja na Wendo, mtoto wa Mzee Hamza Kibwana Mwapachu, Muharrami Kilongola na Mohammed Rashid Sisso, ambao baba zao walikuwa viongozi waandamizi pale Lumumba Makao Makuu.

Sasa asubuhi moja ya mwaka 1960, nchi ikiwa ndio kwanza imepata Utawala wa Ndani (Internal Government), ambayo hata maana yake hatukuijua ni nini siku hizo; tuliiona gari nyeusi aina ya Humber yenye kibao cha namba kilichosomeka MWP, kwa maana ya Minister Without Portfolio inaingia mpaka ndani mle shuleni. Dereva akiwa amevalia sare zinazomereta kabisa akashuka kuja kumfungulia mlango abiria wake. Abiria alikuwa ni Rehema Rashidi Kawawa, ambaye sasa hakuwa mwenzetu tena, kwani babake alikuwa amechaguliwa kuwa “Waziri Asiyekuwa na Wizara Maalumu’ katika Serikali ile ya Madaraka ya Ndani.

Kwetu sisi vijana wadogo siku zile, lile lilikuwa ni tukio kubwa la kukumbukwa, kwa sababu haikupata kutokea hata siku moja pale shuleni, mwenzetu au mwalimu, akaletwa na gari mpaka ndani.

Kama vile sinema ndoto usingizini! Tulianza kuona cheche za kuelekea uhuru kamili. ‘Golo mdogo’ anakuja shule na gari la aina yake! Ule ukawa ni wakati kutafakari na kusubiri lini na sisi wengine tutahamia kwenye magorofa ya Upanga na Uhindini wanakokaa Wahindi; kwani moja ya ilani au ahadi za wanasiasa siku zile ni kwamba huru utakapopatikana, basi sisi ‘makabwela’ tutachupa kutoka raia daraja la IV hadi la kwanza.

Tumesubiri sana; na mpaka leo bado tunaendelea kusubiri siku hiyo ifike. Ni mapambano ambayo bado yanaendelea mpaka leo tumefikisha miaka zaidi ya 60 ya uhuru wetu na bado hayajafikiwa kisawasawa.

Kwa sababu ambazo mpaka leo hazijawekwa hadharani, kipande hiki cha historia yetu hakitajwi, hakiadhimishwi na wala hakienziwi hata kidogo. Nilidhani, kuwa na madaraka ya ndani lilikuwa jambo zuri sana katika safari ya kuelekea kupata uhuru kamili. Pale nchini Kenya, ambako mwandishi huyu alipata kuishi zaidi ya miaka mitano kwenye miaka ya 1970s, Sikukuu ya Madaraka Day, husherehekewa kwa shangwe, nderemo na vifijo vikubwa sana pengine kuliko hata siku ya uhuru kamili mwaka 1962.

Shermax Ngahemera, ni mhariri mwandamizi wa gazeti la Kiingereza la The African, linalochapishwa kila siku na Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, pale Sinza, Kijiweni. Siku moja wakati ilipotangazwa kwamba Rashidi Kawawa hatunaye tena hapa duniani; watu wakawa wanahaha kujaribu kumpamba na kumpembua ili wapate kuandika taazia iliyo bora kuhusu mwanamajumui yule shupavu. Shermax alisema hivi:

“Unajua huyu mzee ana mchango mkubwa sana katika kufanikisha kupatikana kwa haraka uhuru wa nchi hii pengine kuliko mtu mwengine Mwalimu, wakati fulani aliitwa na Gavana Sir Richard Turnbull na kuulizwa anafikiri lini tutakuwa tayari kujitawala ili maandalizi yaanze mara moja. Nyerere aliruka mita 100 juu akikataa kabisa kupewa uhuru kwa haraka hivyo kwa sababu nchi ilikuwa bado haina wasomi ambao wangeweza kusaidiana na Mwalimu kuendesha nchi,” anasimulia Shermax na kuendelea, ‘’ ”Siku kadhaa baadaye Nyerere aliulizwa na Kawawa juu ya safari yake kwa Gavana. Nyerere alimwambia Kawawa kwamba Gavana alikuwa anataka tumwambie kama tuko tayari kujitawala maana yeye alikuwa amechoka na anataka kurudi kwao,” amesema Shermax na kuendelea, “Nyerere alimwambia Kawawa kwamba hakutaka kupata uhuru wakati ule maana watu wa kuweza kufanya kazi nyeti za kisomi za Serikali hawakuwapo bado. Kawawa akamwambia Mwalimu akachukue nchi hata saa ile, maana tuko kwetu na kama tutaanguka basi lazima tutasimama tena. Hatuna wa kumwogopa hata kidogo. Nyerere alirudi tena kwa Gavana na kumwambia kwamba amefuta usemi wake yuko tayari kujitawala wenyewe!” alimaliza Ngahemera.

Uhuru ulipopatikana mwaka 1961, hayati Mzee Kawawa alikuwa Waziri wa Serikali za Mitaa na Maendeleo Vijijini, na ile Humber yake nyeusi iliendelea kumleta shuleni Rehema.

Habari zinasema, baada ya miezi kadhaa ya kuwa huru, hayati Mwalimu Nyerere alijiuzulu uwaziri mkuu na kumpisha Rashidi Kawawa aongoze serikali maana ni yeye aliyesema ‘tutaweza tu hatumwogopi mtu’. Mwalimu alirudi uraiani na kuzunguka nchi nzima kutafuta wasomi japo walikuwa wachache waje kuchukua nafasi kwenye serikali ifikapo 1962 tutakapokuwa Jamhuri, yaani mamlaka kamili.

Rashidi Kawawa, aliitumia vyema nafasi hii, kwani hakusita hata kidogo, pale alipoona kuna Mwafrika mwenye ujuzi wa kazi ambayo imeshikwa na Mzungu, basi mara moja alimpa mzalendo kazi hiyo. Kipindi hicho kilijulikana maarufu kama Afrikanizesheni (Africanisation). Watu wengi walipandishwa vyeo bila kutegemea. Mmoja wa watu hao alikuwa Mzee Mangara Tabu Mangara, aliyekuwa Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali (Government Printer), nafasi ambayo haikuwa inashikwa na Mwafrika kabla uhuru.

Nakumbuka pia shule za sekondari hapa jijini ambazo zikiongozwa na Wazungu siku zote wakapewa kuwa Headmasters wake akina Abdulrahman Mwalongo (Azania), Borry Lilla (Agha Khan), Rahma Mwapachu (Zanaki).

Huyo ndiye Rashidi Mfaume Kawawa; msanii wa filamu za maigizo; mtetezi wa wanyonge wakati wa ukoloni; kiongozi wa vyama vya wafanyakazi; Waziri Mkuu na Makamu wa Rais nchini; Waziri wa Ulinzi na ‘Simba wa Vita’; Mwanasiasa nguli aliyekuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa CCM.

Alamsiki!

atambaza@yahoo.com


Nawakubali sana Waislamu wa TZ ni wastaarabu na Waungwana sana siyo Mafisadi kama Shoo na KKKT!
 
Sijui kama hizo filamu za Kawawa bado zipo au zishaharibiwa. Kama zipo ni vema zikawepo ili watu waone ujuzi wa wazee wetu
 
Maa sha allah historia adhwiim hii..kuna haja ya kurejea vzuri mitaala zetu kuhusiana na historia ya nchi yetu katika harakati za kudai uhuru wa tanganyika...nahis kuna mambo mengi nje ya box..ahsante mzee wangu mohammed said.
 
Nimeshindwda kusoma dude refu lisilokuwa na uandishi wa mvuto.

Lakini kama kawaida ya mwandishi mwenye nia ovu mgongoni huficha ukwelil.

Kawawa angelikuwa mtetezi wa wanyonge asingesababisha mauaji ya wananchi walioliwa na simba kwa kuamuru nyumba zao zichomwe moto wakati wa operation vijiji 1974.

Tunaongea siku zote, elimu inaongeza sana upeo. Hakuwa kiwango.

Shajara ya Mwana Mzizima
Rashidi Mfaume Kawawa


Mtetezi Wanyonge aliyekuja kuwa Waziri Mkuu
Na Alhaji Abdallah Tambaza





Raia Mwema Aprili 30 - May 1, 2018

UTAWALA dhalimu wa Kikoloni wa Ulaya Ingereza hapa kwetu, ulijaa uonevu, udhalilishaji na ukandamizaji katika utoaji wake wa huduma muhimu miongoni mwa wanajamii. Raia tuliwekwa kwa madaraja ambayo Wazungu walikuwa daraja 1; Wahindi daraja II; Waarabu daraja III na Watu weusi tukawa kwenye daraja la IV la mwisho.

Miongoni mwa mateso hayo ni pamoja na watu ‘mababa majitu mazima’, kuchapwa viboko Bomani na Ma-DC na PC (wote walikuwa Wazungu wanaotisha na masharubu yao mazito) pindi inapotokea ukawa umefanya kosa la aina fulani, ambalo kwa wakubwa itabidi upigwe viboko.

Tiba, makazi pamoja na elimu, ilikuwa kwa matabaka vilevile, hata ikawa kwa sisi wananchi wenyewe kutokuwa na sehemu bora ya kuishi; tukiumwa tiba yetu ni panadol tu; kujifungua ni kienyeji nyumbani ambako wengi wa wazazi walipoteza maisha; na shule zilikuwa chache tu za ‘Kayumba’, utake usitake. Katu, haikuwezekana watu weusi kuchanganywa na Wazungu ama Wahindi kwenye elimu hata kama baba yako anao uwezo wa kukulipia ada kubwa - afadhali ilikuwapo kidogo kwa watoto wa machifu.

Watesaji wakubwa kwenye ajira walikuwa ni Wahindi wakati huo, maana wao ndio waliokuwa wakilimiliki uchumi pamoja na nyenzo zake zote kuu (maduka, viwanda, mashamba, pamoja na ajira za nyumbani). Wenyewe wakituita ‘golo’, jina ambalo maana yake pengine ni fisi, sokwe au nyani mweusi - walitudharau sana hata ni aibu kuhadithia.

Malkia wa Uingereza, pamoja na kwamba alikuwa ni mkubwa wa Kanisa Anglikana duniani, alishindwa kutuona sisi kama binadamu kama alivyo yeye na watu wa kwao; na akashindwa kutufanyia uadilifu kwa miaka yote aliyoikalia nchi yetu.

Hali ikawa mbaya sana isiyovumilika kwa Waafrika wanyonge hata ikasababisha kuwaibua watetezi wengi wa haki waje kuongoza mapambano ya kupigania haki kwenye ajira na utumishi. Miongoni mwao alikuwamo mwanaharakati wa kukumbukwa na kupigiwa mfano, hayati Rashidi Mfaume Kawawa.

Hayati Mzee Kawawa, ambaye baadaye alikuja kuwa mpaka Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa nchi hii, alikuwa ni kiongozi asiyetetereka kwenye masuala ya utetesi wa Haki za Binadamu kwenye masuala ya wafanyakazi.

Alipambana vikali sana wakati huo wa ukoloni, kwani anasifika na kukumbukwa kwa kuandaa migomo bila woga pamoja na kwamba ilipigwa marufuku na Serikali ya Kikoloni. Habari zinasema, Kawawa alikuwa na sauti na nguvu kubwa kwa jamii ya wanyonge wakati huo kiasi kwamba alichokisema yeye basi kilitekelezwa mara moja.

Aliongoza muungano wa vyama vingi vya wafanyakazi hapa nchini wakati huo kikiwemo kile cha ‘Makuli’ (wapakiaji na wapakuaji mizigo melini) wa bandarini cha Dockworkers Union 1948, Tanganyika Railways African Union, African Cooks Union na Domestic Workers Union (Chama cha Watumishi wa Majumbani)

Wakati ule, ukiacha Serikali na Railways, mwajiri mwengine mkubwa alikuwa ni Bandari ya Dar es Salaam, ambapo kazi nyingi za Waafrika pale Pwani zilikuwa za ‘daily pay’, yaani ya malipo kila siku jioni. Iliwezekana kufanya hivyo kwa sababu kazi za bandarini ni za msimu maana kuna wakati meli zinakuwa nyingi na wakati mwengine zinaadimika; hivyo watu wachache sana walikuwa na ajira za mwezi hata mwezi.

Kazi zile za Bandari zilikuwa ni za kuhatarisha maisha sana. Wengi wa watu walipata vilema ama kupoteza maisha, hivyo kufanyishwa kazi za namna ile bila mikataba stahili ulikuwa ni uonevu mkubwa sana. Hali hiyo ilisababisha migomo isiyokwisha kutoka kwa wafanyakazi kwa kule kutotendewa ipasavyo.

‘’Katika miaka ile kazi ya bandarini ilikuwa ni hatari, ikishindana na kazi ya migodi.

“Lakini bado serikali ya kikoloni ilijifanya kutoelewa ukweli kwamba Mwafrika alikuwa mwanadamu kama alivyo Mzungu Muasia au Mwarabu …Serikali ilikuwa na dhana ya ajabu na wakati mwengine ya kusikitisha kuhusu Mwafrika kama binadamu,”anaandika Mohammed Said, Uk 64 katika kitabu chake mashuhuri cha Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes, kinachosambazwa na Kampuni ya Ibn Hazm Media Center, Dar es Salaam.

Wanaharakati wawili wakubwa ndio waliojitokeza mbele zaidi katika kuwapigania na kuwatetea Waafrika wenzao wakati huo. Abdulwahid Sykes akajikita kwenye Dockworkers Union na Rashidi Kawawa akiwa zaidi kule TRAU; huku wakisaidiwa kwa karibu na watetezi wengine shupavu wakati huo kama vile Kassanga Tumbo, Michael Kamaliza, Alfred Tandau na Jacob Namfua.

Vuguvugu hizi na mwamko huu mkubwa ukazaa chombo kikubwa zaidi kilichounganisha vyama vya wafanyakazi wote wakati huo kilichojulikana kama Tanganyika Federation of Labour na Rashidi Mfaume Kawawa akawa ndiye Katibu Mkuu wa mwanzo. Chama kingine machachari wakati huo ni kile cha madereva na hasa madereva Teksi, kilichoongozwa na kada mashuhuri wa CCM, Mustapha Songambele.

Wakati hali ikiwa hivyo kwa harakati za vyama vya wafanyakazi, kwenye harakati za kudai uhuru chama cha TANU kilikuwa kikihitaji sana kuungwa mkono na kila sekta ya wazalendo wa Tanganyika wakati huo. Rashidi Kawawa, haraka akaunganisha nguvu na TANU kwa kupeleka umma wote ule wa watumishi kutoka vyama vilivyoungana na kuwa wanachama wa rasmi wa TANU.

Kwa namna ile viongozi wote wale waandamizi kutoka TFL wakachukua nafasi za juu na kuwa na sauti kwenye masuala ya ukombozi wa taifa hili. Chama cha TANU kikawa hakishikiki kutokana na chachu mpya aliyoingiza Kawawa kwenye mapambano. Huo ukawa ndio mwanzo wa Kawawa kuwa karibu na Nyerere kiasi kile.

Nilimfahamu Rashidi Mfaume Kawawa, nikiwa bado kijana mdogo kabisa kwenye miaka ya mwanzo 1950s pale alipokuwa Ofisa kwenye Idara ya Ustawi wa Jamii (Community Development Department) ya Serikali ya Kikoloni, alipokuwa akicheza filamu za vichekesho. Filamu alizocheza hayati Mzee Kawawa zilikuwa zikitupa burudani tosha sisi vijana wadogo wa wakati huo, kwani filamu zile hazikuwa za kuburudisha peke yake, lakini pia kuelimisha jamii katika masuala mbalimbali. Jina lake la kwenye sinema lilikuwa ‘Muhogo Mchungu’.

Sinema nyingine maarufu aliyoicheza Mzee Kawawa ni ile iliyojulikana kama, ‘’Mgeni Mwema,’’ ambapo kila mwanzo wa mwezi kwa jiji la Dar es Salaam zilikuwa zikionyeshwa pale viwanja vya Mnazi Mmoja, Ilala na Magomeni na baadaye kuhamia sehemu nyengine mikoani. Pamoja na sinema za Muhogo Mchungu, usiku huohuo huonyeshwa pia sinema nyingine za wale Wazungu wawili wasanii, Stan Laurel na Oliver Hardy, hapa kwetu Dar es Salaam tukiwaita ‘Chale Ndute na Chale Mbwambwambwa’, ambao vichekesho vyao kwenye zile sinema vimekuwa kivutio mpaka leo duniani kote.

Kwa sababu ambazo hazikuelezwa sawasawa mpaka leo, jamii ya Watanzania wamenyimwa nafasi ya kuburudika na uhondo wa filamu za Mzee Rashidi Kawawa - hatujui zilipo, zimevichwa kama zilivyofichwa nyaraka nyingi za historia ya muhimu ya nchi yetu.

Katika miaka ile ya 50s, nikiwa mwanafunzi pale Shule ya Msingi Mnazi Mmoja, mjini Dar es Salaam kila mara nilikuwa namwona Mzee Kawawa akirandaranda nje ya nyumba ile ndogo iliyokuwa mkabala na shule yetu akiwa ama anatoka au kuingia mle ndani kukutana na wapigania uhuru wenzake. Pale Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya CCM, ndipo yalipokuwa makao makuu ya Chama TANU wakati wa kudai uhuru.

Hayati Mzee Kawawa, wakati ule alikuwa kijana mtanashati kwelikweli; kila mara akiwa amependeza kimavazi, hasa pale alipokuwa akivaa ile migolole ya vitenge vya Afrika Magharibi, hususan kutoka Ghana na Nigeria, iliyokuwa ikipendwa na wapigania uhuru wengi sana wakati ule, akiwamo Dk Kenneth Kaunda na Harry Chipembere wa Zambia; Kanyama Chiume na Yatuta Chisiza wa Malawi; na Nyerere, Kassanga Tumbo na Michael Kamaliza wa Tanganyika.

Mtoto mkubwa wa hayati Mzee Kawawa, dadangu Rehema, nilikuwa nasoma naye darasa moja pale shuleni Mnazi Mmoja pamoja na Silas Munanka mtoto wa Mzee Bhoke Munanka. Wengine waliokuwapo pale wakati ule ni pamoja na Wendo, mtoto wa Mzee Hamza Kibwana Mwapachu, Muharrami Kilongola na Mohammed Rashid Sisso, ambao baba zao walikuwa viongozi waandamizi pale Lumumba Makao Makuu.

Sasa asubuhi moja ya mwaka 1960, nchi ikiwa ndio kwanza imepata Utawala wa Ndani (Internal Government), ambayo hata maana yake hatukuijua ni nini siku hizo; tuliiona gari nyeusi aina ya Humber yenye kibao cha namba kilichosomeka MWP, kwa maana ya Minister Without Portfolio inaingia mpaka ndani mle shuleni. Dereva akiwa amevalia sare zinazomereta kabisa akashuka kuja kumfungulia mlango abiria wake. Abiria alikuwa ni Rehema Rashidi Kawawa, ambaye sasa hakuwa mwenzetu tena, kwani babake alikuwa amechaguliwa kuwa “Waziri Asiyekuwa na Wizara Maalumu’ katika Serikali ile ya Madaraka ya Ndani.

Kwetu sisi vijana wadogo siku zile, lile lilikuwa ni tukio kubwa la kukumbukwa, kwa sababu haikupata kutokea hata siku moja pale shuleni, mwenzetu au mwalimu, akaletwa na gari mpaka ndani.

Kama vile sinema ndoto usingizini! Tulianza kuona cheche za kuelekea uhuru kamili. ‘Golo mdogo’ anakuja shule na gari la aina yake! Ule ukawa ni wakati kutafakari na kusubiri lini na sisi wengine tutahamia kwenye magorofa ya Upanga na Uhindini wanakokaa Wahindi; kwani moja ya ilani au ahadi za wanasiasa siku zile ni kwamba huru utakapopatikana, basi sisi ‘makabwela’ tutachupa kutoka raia daraja la IV hadi la kwanza.

Tumesubiri sana; na mpaka leo bado tunaendelea kusubiri siku hiyo ifike. Ni mapambano ambayo bado yanaendelea mpaka leo tumefikisha miaka zaidi ya 60 ya uhuru wetu na bado hayajafikiwa kisawasawa.

Kwa sababu ambazo mpaka leo hazijawekwa hadharani, kipande hiki cha historia yetu hakitajwi, hakiadhimishwi na wala hakienziwi hata kidogo. Nilidhani, kuwa na madaraka ya ndani lilikuwa jambo zuri sana katika safari ya kuelekea kupata uhuru kamili. Pale nchini Kenya, ambako mwandishi huyu alipata kuishi zaidi ya miaka mitano kwenye miaka ya 1970s, Sikukuu ya Madaraka Day, husherehekewa kwa shangwe, nderemo na vifijo vikubwa sana pengine kuliko hata siku ya uhuru kamili mwaka 1962.

Shermax Ngahemera, ni mhariri mwandamizi wa gazeti la Kiingereza la The African, linalochapishwa kila siku na Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, pale Sinza, Kijiweni. Siku moja wakati ilipotangazwa kwamba Rashidi Kawawa hatunaye tena hapa duniani; watu wakawa wanahaha kujaribu kumpamba na kumpembua ili wapate kuandika taazia iliyo bora kuhusu mwanamajumui yule shupavu. Shermax alisema hivi:

“Unajua huyu mzee ana mchango mkubwa sana katika kufanikisha kupatikana kwa haraka uhuru wa nchi hii pengine kuliko mtu mwengine Mwalimu, wakati fulani aliitwa na Gavana Sir Richard Turnbull na kuulizwa anafikiri lini tutakuwa tayari kujitawala ili maandalizi yaanze mara moja. Nyerere aliruka mita 100 juu akikataa kabisa kupewa uhuru kwa haraka hivyo kwa sababu nchi ilikuwa bado haina wasomi ambao wangeweza kusaidiana na Mwalimu kuendesha nchi,” anasimulia Shermax na kuendelea, ‘’ ”Siku kadhaa baadaye Nyerere aliulizwa na Kawawa juu ya safari yake kwa Gavana. Nyerere alimwambia Kawawa kwamba Gavana alikuwa anataka tumwambie kama tuko tayari kujitawala maana yeye alikuwa amechoka na anataka kurudi kwao,” amesema Shermax na kuendelea, “Nyerere alimwambia Kawawa kwamba hakutaka kupata uhuru wakati ule maana watu wa kuweza kufanya kazi nyeti za kisomi za Serikali hawakuwapo bado. Kawawa akamwambia Mwalimu akachukue nchi hata saa ile, maana tuko kwetu na kama tutaanguka basi lazima tutasimama tena. Hatuna wa kumwogopa hata kidogo. Nyerere alirudi tena kwa Gavana na kumwambia kwamba amefuta usemi wake yuko tayari kujitawala wenyewe!” alimaliza Ngahemera.

Uhuru ulipopatikana mwaka 1961, hayati Mzee Kawawa alikuwa Waziri wa Serikali za Mitaa na Maendeleo Vijijini, na ile Humber yake nyeusi iliendelea kumleta shuleni Rehema.

Habari zinasema, baada ya miezi kadhaa ya kuwa huru, hayati Mwalimu Nyerere alijiuzulu uwaziri mkuu na kumpisha Rashidi Kawawa aongoze serikali maana ni yeye aliyesema ‘tutaweza tu hatumwogopi mtu’. Mwalimu alirudi uraiani na kuzunguka nchi nzima kutafuta wasomi japo walikuwa wachache waje kuchukua nafasi kwenye serikali ifikapo 1962 tutakapokuwa Jamhuri, yaani mamlaka kamili.

Rashidi Kawawa, aliitumia vyema nafasi hii, kwani hakusita hata kidogo, pale alipoona kuna Mwafrika mwenye ujuzi wa kazi ambayo imeshikwa na Mzungu, basi mara moja alimpa mzalendo kazi hiyo. Kipindi hicho kilijulikana maarufu kama Afrikanizesheni (Africanisation). Watu wengi walipandishwa vyeo bila kutegemea. Mmoja wa watu hao alikuwa Mzee Mangara Tabu Mangara, aliyekuwa Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali (Government Printer), nafasi ambayo haikuwa inashikwa na Mwafrika kabla uhuru.

Nakumbuka pia shule za sekondari hapa jijini ambazo zikiongozwa na Wazungu siku zote wakapewa kuwa Headmasters wake akina Abdulrahman Mwalongo (Azania), Borry Lilla (Agha Khan), Rahma Mwapachu (Zanaki).

Huyo ndiye Rashidi Mfaume Kawawa; msanii wa filamu za maigizo; mtetezi wa wanyonge wakati wa ukoloni; kiongozi wa vyama vya wafanyakazi; Waziri Mkuu na Makamu wa Rais nchini; Waziri wa Ulinzi na ‘Simba wa Vita’; Mwanasiasa nguli aliyekuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa CCM.

Alamsiki!

atambaza@yahoo.com
 
Sijui kama hizo filamu za Kawawa bado zipo au zishaharibiwa. Kama zipo ni vema zikawepo ili watu waone ujuzi wa wazee wetu
Kwezisho,
Hizi senema za Mzee Rashid Kawawa zilikuwapo Audio Visual lakini
katika hali ambayo haziwezi kuwekwa katika ''projector,'' zikaoneshwa.

Lakini mimi nina hakika nakala za hizi senema zipo katika ''archives,''
za Waingereza.

Ikiwa tunazitaka ni wahusika kufanya juhudi zitapatikana.
 
Mohamed Said hivi kwenye maktaba yako hamna kabisa hero ambaye ni Mkristo?
Naomba uweke link ya shujaa ambaye siyo muislam kutoka kwenye makala zako
Bujibuji,
Sijui kwa nini unaniuliza swali hili.

Mimi nimeandika historia ya uhuru wa Tanganyika na Maktaba
yangu ina mengi kuhusu historia hii.

Kwani wewe huwajui mashujaa wa Tanganyika kiasi unitake
mie nikufahamishe?
 
Maa sha allah historia adhwiim hii..kuna haja ya kurejea vzuri mitaala zetu kuhusiana na historia ya nchi yetu katika harakati za kudai uhuru wa tanganyika...nahis kuna mambo mengi nje ya box..ahsante mzee wangu mohammed said.
Al Abry,
Ahsante sana kaka.
 
Wakubwa napenda kuomba kuujua mchango wa huyu mzee wetu maana kwa kweli kama vile hakuwahi kuwa mmojawapo wa watu waliopigana sana ktk hili taifa letu.
Tafadhali
 
Jambo la faraja sana kwa kuwajua hawa wanaharakati wetu ili kizazi kijacho kisije kosa kujua uhalisia wa taifa letu
 
Back
Top Bottom